< Kutoka 40 >

1 Kisha Yahweh akasema na Musa na kumwambia,
Y él Señor dijo a Moisés:
2 “Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka lazima wewe uandae hema la kukutania.
El primer día del primer mes debes colocar el santuario de la Tienda de reunión.
3 Utaweka sanduku la ushuhuda ndani yake, na utaziba sanduku kwa pazia.
Y en su interior pon el cofre del pacto, colgando el velo delante de ella.
4 Utaleta ndani meza na kuandaa kwa mpangilio vitu vyake. Kisha utaleta kinara cha taa na kuandaa taa.
Y pon la mesa dentro, colocando todas las cosas en orden; y pongan el candelabro, y coloca al candelabro sus lámparas.
5 Nawe utaweka madhabahu ya dhahabu ya uvumba mbele ya sanduku la ushuhuda, na utaweka pazia katika mwingilio wa hema la kukutania.
Y pon el altar de oro para él incienso delante del cofre del pacto, y cuelga la cortina sobre la entrada del santuario.
6 Utaweka madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa mbele ya mwingilio wa hema ya kukutania.
Y pondrás el altar de las ofrendas quemadas delante de la puerta de la Tienda de reunión.
7 Utaweka ile saani kubwa katikati ya hema la kukutania na madhabahu na utaweka maji ndani yake.
Y que el vaso para lavatorio, con agua en él, se ponga entre la Tienda de reunión y el altar.
8 Uandae nyuani inayoizunguka, na utundike pazia katika mwingilio wa nyuani.
Y pon las cortinas que forman el atrio alrededor de ella, con la cortina sobre su entrada.
9 Lazima uchukuwe mafuta ya upako na upake hema la kukutania na kila kitu kilichopo ndani yake. Lazima uitenge na samani zake kwangu; kisha itakuwa takatifu.
Y toma el aceite santo, y ungirás el tabernáculo todo lo que hay en él, y ungirás todos los utensilios; porque lo que está en él es santo;
10 Lazima upake mafuta madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake. Lazima utenge madhabhu kwa ajili yangu na itakuwa takatifu kwangu.
Y ungirás como aceite el altar de la ofrenda quemada, y lo santificarás con todos sus vasos; este altar debe ser santísimo.
11 Upake mafuta beseni la shaba na sakafu yake na uitenge kwa ajili yangu.
Y ungirás la vasija de lavar y su base, y santifícalos.
12 Umlete Aruni na wanae kwa mwingilio wa hema la kukutania na uwaoshe wote kwa maji.
Entonces Aarón y sus hijos vayan a la puerta de la Tienda de reunión; y después de lavarlos con agua,
13 Utamfunika Aruni kwa mavazi yaliyo tengwa kwa ajili yangu, mpake mafuta na umtenge ili anitumikie kama kuhani.
Debes vestir a Aarón con las vestiduras sagradas; y lo ungirás con aceite, y lo santificarás, para que sea mi sacerdote.
14 Utawaleta wana wake na kuwafunika kwa nguo nzito.
Y lleven sus hijos con él, y vístanlos con las túnicas;
15 Utawapaka mafuta kama ulivyo mpaka baba yao ili wanitumikie kama makuhani. Upako wao utawafanya makuhani wa kudumu vizazi vyote vya watu wao.”
Y y los ungirás con aceite como lo hiciste con su padre, para que sean mis sacerdotes; con la unción del aceite los convertirás en sacerdotes para siempre, de generación en generación.
16 Hivi ndivyo Musa alivyo sema; alifuata yote Yahweh aliyo muamuru. Alifanya vitu vyote hivi.
Y Moisés hizo esto; como el Señor le dio órdenes, así lo hizo.
17 Hivyo hema la kukutania liliandaliwa siku ya kwanza ya mwezi wa mwaka wa pili.
Así que en el primer día del primer mes en el segundo año el santuario fue levantado.
18 Musa alianda hema la kukutania, akaeka sakafu zake sehemu yake, akaanda fremu zake, akashikisha chuma zake, na akaanda minara na nguzo zake.
Moisés levantó el santuario; colocando sus bases en posición y levantando sus montantes, colocando las varillas y plantando los pilares en su lugar;
19 Alitandaza mfuniko juu ya hema la kukutania na kuweka hema juu yake, kama Yahweh alivyo muamuru.
Extendiendo la tienda exterior sobre ella, y cubriéndola, como el Señor le había dado órdenes.
20 Alichukuwa amri za agano na kuweka kwenye sanduku. Pia aliweka nguzo kwenye sanduku na kuweka mfuniko wa kiti cha rehema.
Y él tomó la ley y la puso dentro del arca, y puso las varas a su lado y la cubierta sobre ella;
21 Aliichukuwa sanduku na kuweka ndani ya hema la kukutania. Aliandaa pazia ili lizibe sanduku la ushuhuda, kama Yahweh alivyo muamuru.
Y llevó el cofre del pacto al santuario, colgando el velo delante de él, como el Señor le había dado órdenes.
22 Alieka meza kwenye hema la kukutania, kwa upande wa kaskazini mwa hema la kukutania, nje ya pazia.
Y él puso la mesa en la Tienda de reunión, en el lado norte fuera del velo.
23 Alieka mkate kwa mpangilio katika meza ya Yahweh, kama Yahweh alivyo amuru.
Y puso el pan delante del Señor, como él Señor lo había dicho.
24 Alieka kinara cha taa kwenye hema la kukutania, upande wa pili wa meza, kusini mwa hema la kukutani.
El candelabro lo puso en la Tienda de reunión, frente a la mesa, en el lado sur:
25 Aliwasha taa mbele za Yahweh, kama Yahweh alivyo muamuru.
Encendiendo las luces delante del Señor, como el Señor le había dado órdenes.
26 Aliweka madhabahu ya dhahabu ya uvumba ndani ya hema la kukutania mbele ya pazia.
Y puso el altar de oro en la Tienda de reunión, delante del velo:
27 Alichoma uvumba wa manukato hapo, kama Yahweh alivyo muamuru.
Y quemó sobre él el incienso aromático, como el Señor le había dado órdenes.
28 Alitundika pazia katika hema ya kukutania.
Y él puso la cortina en la puerta del santuario.
29 Aliweka madhabahu ya sadaka ya kuteketeza katika hema ya kukutania. Aliitolea sadaka ya kuteketeza na sadaka ya unga, kama Yahweh alivyo muamuru.
Y a la puerta del santuario de la Tienda de reunión, él puso el altar de las ofrendas quemadas, ofreciendo en él las ofrendas quemadas y las ofrendas de cereales, como el Señor le había dado las órdenes.
30 Aliweka beseni katikati ya hema ya kukutunia na madhabahu, na maji ya kuoshea.
Y entre el altar y la Tienda de reunión, puso el recipiente con agua para lavar.
31 Musa, Aruni, na wanae waliosha mikono yao na miguu kwenye beseni
En él se lavaron las manos y los pies de Moisés, Aarón y sus hijos,
32 muda wowote walipoenda kwenye hema ya kukutania na muda wowote walipoenda kwenye madhabahu. Walijisafisha, kama Yahweh alivyo muamuru Musa.
Cada vez que entraban en la Tienda de reunión, y cuando se acercaban al altar, como el Señor le había dado órdenes a Moisés.
33 Musa alianda nyuani nyuma ya hema ya kukutania na madhabahu. Alianda pazia katika mwingilio wa nyuani. Katika hili, Musa alimaliza kazi.
Y él puso las cortinas que forman el atrio alrededor del santuario y el altar, y puso la cortina sobre la entrada. Entonces Moisés hizo el trabajo completo.
34 Kisha wingu likafunika hema ya kukutania, na utukufu wa Yahweh ukafunika hema ya kukutania.
Entonces la nube descendió y cubrió la tienda de reunión, y la casa estaba llena de la gloria del Señor;
35 Musa hakuweza kuingia hema ya kukutania kwasababu wingu lilikuwa juu yake, na kwasababu utukufu wa Yahweh ulijaza hema ya kukutania.
De modo que Moisés no pudo entrar en la Tienda de reunión, porque la nube descansaba sobre ella, porque él santuario estaba lleno de la gloria del Señor.
36 Muda wowote wingu lilipo chukuliwa juu kutoka hema ya kukutania, watu wa Israeli waliendelea na safari yao.
Y cuando la nube se levantaba de la Casa, los hijos de Israel continuaban su viaje:
37 Lakini kama wingu haliku nyanyuka juu kutoka hema ya kukutania, kisha basi watu hawaku safiri. Walibaki hadi siku lilipo nyanyuliwa juu.
Pero mientras la nube estaba allí, no hicieron ningún movimiento hasta que la nube se levantaba, tampoco ellos levantaban su campamento.
38 Kwa kuwa wingu la Yahweh lilikuwa juu ya hema ya kukutania mchana, na moto wake ulikuwa juu yake usiku, wazi kwa watu wote wa Israeli kipindi chote cha safari yao.
Porque la nube del Señor estaba descansando en él santuario de día, y en la noche había fuego en la nube, ante los ojos de todo el pueblo de Israel, y así fue en todos sus viajes.

< Kutoka 40 >