< Kutoka 40 >

1 Kisha Yahweh akasema na Musa na kumwambia,
Locutusque est Dominus ad Moysen, dicens:
2 “Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka lazima wewe uandae hema la kukutania.
Mense primo, prima die mensis, eriges tabernaculum testimonii,
3 Utaweka sanduku la ushuhuda ndani yake, na utaziba sanduku kwa pazia.
et pones in eo arcam, dimittesque ante illam velum:
4 Utaleta ndani meza na kuandaa kwa mpangilio vitu vyake. Kisha utaleta kinara cha taa na kuandaa taa.
et illata mensa, pones super eam quæ rite præcepta sunt. Candelabrum stabit cum lucernis suis,
5 Nawe utaweka madhabahu ya dhahabu ya uvumba mbele ya sanduku la ushuhuda, na utaweka pazia katika mwingilio wa hema la kukutania.
et altare aureum, in quo adoletur incensum, coram arca testimonii. Tentorium in introitu tabernaculi pones,
6 Utaweka madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa mbele ya mwingilio wa hema ya kukutania.
et ante illud altare holocausti:
7 Utaweka ile saani kubwa katikati ya hema la kukutania na madhabahu na utaweka maji ndani yake.
labrum inter altare et tabernaculum, quod implebis aqua.
8 Uandae nyuani inayoizunguka, na utundike pazia katika mwingilio wa nyuani.
Circumdabisque atrium tentoriis, et ingressum ejus.
9 Lazima uchukuwe mafuta ya upako na upake hema la kukutania na kila kitu kilichopo ndani yake. Lazima uitenge na samani zake kwangu; kisha itakuwa takatifu.
Et assumpto unctionis oleo unges tabernaculum cum vasis suis, ut sanctificentur:
10 Lazima upake mafuta madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake. Lazima utenge madhabhu kwa ajili yangu na itakuwa takatifu kwangu.
altare holocausti et omnia vasa ejus,
11 Upake mafuta beseni la shaba na sakafu yake na uitenge kwa ajili yangu.
labrum cum basi sua: omnia unctionis oleo consecrabis, ut sint Sancta sanctorum.
12 Umlete Aruni na wanae kwa mwingilio wa hema la kukutania na uwaoshe wote kwa maji.
Applicabisque Aaron et filios ejus ad fores tabernaculi testimonii, et lotos aqua
13 Utamfunika Aruni kwa mavazi yaliyo tengwa kwa ajili yangu, mpake mafuta na umtenge ili anitumikie kama kuhani.
14 Utawaleta wana wake na kuwafunika kwa nguo nzito.
15 Utawapaka mafuta kama ulivyo mpaka baba yao ili wanitumikie kama makuhani. Upako wao utawafanya makuhani wa kudumu vizazi vyote vya watu wao.”
indues sanctis vestibus, ut ministrent mihi, et unctio eorum in sacerdotium sempiternum proficiat.
16 Hivi ndivyo Musa alivyo sema; alifuata yote Yahweh aliyo muamuru. Alifanya vitu vyote hivi.
Fecitque Moyses omnia quæ præceperat Dominus.
17 Hivyo hema la kukutania liliandaliwa siku ya kwanza ya mwezi wa mwaka wa pili.
Igitur mense primo anni secundi, prima die mensis, collocatum est tabernaculum.
18 Musa alianda hema la kukutania, akaeka sakafu zake sehemu yake, akaanda fremu zake, akashikisha chuma zake, na akaanda minara na nguzo zake.
Erexitque Moyses illud, et posuit tabulas ac bases et vectes, statuitque columnas,
19 Alitandaza mfuniko juu ya hema la kukutania na kuweka hema juu yake, kama Yahweh alivyo muamuru.
et expandit tectum super tabernaculum, imposito desuper operimento, sicut Dominus imperaverat.
20 Alichukuwa amri za agano na kuweka kwenye sanduku. Pia aliweka nguzo kwenye sanduku na kuweka mfuniko wa kiti cha rehema.
Posuit et testimonium in arca, subditis infra vectibus, et oraculum desuper.
21 Aliichukuwa sanduku na kuweka ndani ya hema la kukutania. Aliandaa pazia ili lizibe sanduku la ushuhuda, kama Yahweh alivyo muamuru.
Cumque intulisset arcam in tabernaculum, appendit ante eam velum ut expleret Domini jussionem.
22 Alieka meza kwenye hema la kukutania, kwa upande wa kaskazini mwa hema la kukutania, nje ya pazia.
Posuit et mensam in tabernaculo testimonii ad plagam septentrionalem extra velum,
23 Alieka mkate kwa mpangilio katika meza ya Yahweh, kama Yahweh alivyo amuru.
ordinatis coram propositionis panibus, sicut præceperat Dominus Moysi.
24 Alieka kinara cha taa kwenye hema la kukutania, upande wa pili wa meza, kusini mwa hema la kukutani.
Posuit et candelabrum in tabernaculo testimonii e regione mensæ in parte australi,
25 Aliwasha taa mbele za Yahweh, kama Yahweh alivyo muamuru.
locatis per ordinem lucernis, juxta præceptum Domini.
26 Aliweka madhabahu ya dhahabu ya uvumba ndani ya hema la kukutania mbele ya pazia.
Posuit et altare aureum sub tecto testimonii contra velum,
27 Alichoma uvumba wa manukato hapo, kama Yahweh alivyo muamuru.
et adolevit super eo incensum aromatum, sicut jusserat Dominus Moysi.
28 Alitundika pazia katika hema ya kukutania.
Posuit et tentorium in introitu tabernaculi testimonii,
29 Aliweka madhabahu ya sadaka ya kuteketeza katika hema ya kukutania. Aliitolea sadaka ya kuteketeza na sadaka ya unga, kama Yahweh alivyo muamuru.
et altare holocausti in vestibulo testimonii, offerens in eo holocaustum, et sacrificia, ut Dominus imperaverat.
30 Aliweka beseni katikati ya hema ya kukutunia na madhabahu, na maji ya kuoshea.
Labrum quoque statuit inter tabernaculum testimonii et altare, implens illud aqua.
31 Musa, Aruni, na wanae waliosha mikono yao na miguu kwenye beseni
Laveruntque Moyses et Aaron ac filii ejus manus suas et pedes,
32 muda wowote walipoenda kwenye hema ya kukutania na muda wowote walipoenda kwenye madhabahu. Walijisafisha, kama Yahweh alivyo muamuru Musa.
cum ingrederentur tectum fœderis, et accederent ad altare, sicut præceperat Dominus Moysi.
33 Musa alianda nyuani nyuma ya hema ya kukutania na madhabahu. Alianda pazia katika mwingilio wa nyuani. Katika hili, Musa alimaliza kazi.
Erexit et atrium per gyrum tabernaculi et altaris, ducto in introitu ejus tentorio. Postquam omnia perfecta sunt,
34 Kisha wingu likafunika hema ya kukutania, na utukufu wa Yahweh ukafunika hema ya kukutania.
operuit nubes tabernaculum testimonii, et gloria Domini implevit illud.
35 Musa hakuweza kuingia hema ya kukutania kwasababu wingu lilikuwa juu yake, na kwasababu utukufu wa Yahweh ulijaza hema ya kukutania.
Nec poterat Moyses ingredi tectum fœderis, nube operiente omnia, et majestate Domini coruscante, quia cuncta nubes operuerat.
36 Muda wowote wingu lilipo chukuliwa juu kutoka hema ya kukutania, watu wa Israeli waliendelea na safari yao.
Siquando nubes tabernaculum deserebat, proficiscebantur filii Israël per turmas suas:
37 Lakini kama wingu haliku nyanyuka juu kutoka hema ya kukutania, kisha basi watu hawaku safiri. Walibaki hadi siku lilipo nyanyuliwa juu.
si pendebat desuper, manebant in eodem loco.
38 Kwa kuwa wingu la Yahweh lilikuwa juu ya hema ya kukutania mchana, na moto wake ulikuwa juu yake usiku, wazi kwa watu wote wa Israeli kipindi chote cha safari yao.
Nubes quippe Domini incubabat per diem tabernaculo, et ignis in nocte, videntibus cunctis populis Israël per cunctas mansiones suas.

< Kutoka 40 >