< Kutoka 40 >
1 Kisha Yahweh akasema na Musa na kumwambia,
And Jehovah spoke to Moses, saying,
2 “Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka lazima wewe uandae hema la kukutania.
On the day of the first month, on the first of the month, shalt thou set up the tabernacle of the tent of meeting.
3 Utaweka sanduku la ushuhuda ndani yake, na utaziba sanduku kwa pazia.
And thou shalt put in it the ark of the testimony, and shalt cover the ark with the veil.
4 Utaleta ndani meza na kuandaa kwa mpangilio vitu vyake. Kisha utaleta kinara cha taa na kuandaa taa.
And thou shalt bring in the table, and set in order the things that are to be set in order upon it. And thou shalt bring in the candlestick and light its lamps.
5 Nawe utaweka madhabahu ya dhahabu ya uvumba mbele ya sanduku la ushuhuda, na utaweka pazia katika mwingilio wa hema la kukutania.
And thou shalt set the golden altar for the incense before the ark of the testimony; and hang up the curtain of the entrance to the tabernacle.
6 Utaweka madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa mbele ya mwingilio wa hema ya kukutania.
And thou shalt set the altar of burnt-offering before the entrance of the tabernacle of the tent of meeting.
7 Utaweka ile saani kubwa katikati ya hema la kukutania na madhabahu na utaweka maji ndani yake.
And thou shalt set the laver between the tent of meeting and the altar, and shalt put water in it.
8 Uandae nyuani inayoizunguka, na utundike pazia katika mwingilio wa nyuani.
And thou shalt fix the court round about, and hang up the curtain at the gate of the court.
9 Lazima uchukuwe mafuta ya upako na upake hema la kukutania na kila kitu kilichopo ndani yake. Lazima uitenge na samani zake kwangu; kisha itakuwa takatifu.
And thou shalt take the anointing oil, and anoint the tabernacle, and all that is in it, and shalt hallow it, and all its utensils; and it shall be holy.
10 Lazima upake mafuta madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake. Lazima utenge madhabhu kwa ajili yangu na itakuwa takatifu kwangu.
And thou shalt anoint the altar of burnt-offering, and all its utensils; and thou shalt hallow the altar, and the altar shall be most holy.
11 Upake mafuta beseni la shaba na sakafu yake na uitenge kwa ajili yangu.
And thou shalt anoint the laver and its stand, and hallow it.
12 Umlete Aruni na wanae kwa mwingilio wa hema la kukutania na uwaoshe wote kwa maji.
And thou shalt bring Aaron and his sons near, at the entrance of the tent of meeting, and bathe them with water.
13 Utamfunika Aruni kwa mavazi yaliyo tengwa kwa ajili yangu, mpake mafuta na umtenge ili anitumikie kama kuhani.
And thou shalt clothe Aaron with the holy garments, and anoint him, and hallow him, that he may serve me as priest.
14 Utawaleta wana wake na kuwafunika kwa nguo nzito.
And thou shalt bring his sons near, and clothe them with vests.
15 Utawapaka mafuta kama ulivyo mpaka baba yao ili wanitumikie kama makuhani. Upako wao utawafanya makuhani wa kudumu vizazi vyote vya watu wao.”
And thou shalt anoint them, as thou didst anoint their father, that they may serve me as priests. And their anointing shall be to them an everlasting priesthood throughout their generations.
16 Hivi ndivyo Musa alivyo sema; alifuata yote Yahweh aliyo muamuru. Alifanya vitu vyote hivi.
And Moses did so: as Jehovah had commanded him, so did he.
17 Hivyo hema la kukutania liliandaliwa siku ya kwanza ya mwezi wa mwaka wa pili.
And it came to pass in the first month in the second year, on the first of the month, that the tabernacle was set up.
18 Musa alianda hema la kukutania, akaeka sakafu zake sehemu yake, akaanda fremu zake, akashikisha chuma zake, na akaanda minara na nguzo zake.
And Moses set up the tabernacle, and put in its bases, and fixed its boards, and put in its bars, and set up its pillars.
19 Alitandaza mfuniko juu ya hema la kukutania na kuweka hema juu yake, kama Yahweh alivyo muamuru.
And he spread the tent over the tabernacle, and put the covering of the tent above over it; as Jehovah had commanded Moses.
20 Alichukuwa amri za agano na kuweka kwenye sanduku. Pia aliweka nguzo kwenye sanduku na kuweka mfuniko wa kiti cha rehema.
And he took and put the testimony into the ark, and put the staves in the ark, and put the mercy-seat above on the ark.
21 Aliichukuwa sanduku na kuweka ndani ya hema la kukutania. Aliandaa pazia ili lizibe sanduku la ushuhuda, kama Yahweh alivyo muamuru.
And he brought the ark into the tabernacle, and hung up the veil of separation, and covered the ark of the testimony; as Jehovah had commanded Moses.
22 Alieka meza kwenye hema la kukutania, kwa upande wa kaskazini mwa hema la kukutania, nje ya pazia.
And he put the table in the tent of meeting, on the side of the tabernacle northward, outside the veil,
23 Alieka mkate kwa mpangilio katika meza ya Yahweh, kama Yahweh alivyo amuru.
and arranged the bread in order upon it before Jehovah; as Jehovah had commanded Moses.
24 Alieka kinara cha taa kwenye hema la kukutania, upande wa pili wa meza, kusini mwa hema la kukutani.
And he put the candlestick in the tent of meeting, opposite to the table, on the side of the tabernacle southward.
25 Aliwasha taa mbele za Yahweh, kama Yahweh alivyo muamuru.
And he lighted the lamps before Jehovah; as Jehovah had commanded Moses.
26 Aliweka madhabahu ya dhahabu ya uvumba ndani ya hema la kukutania mbele ya pazia.
And he put the golden altar in the tent of meeting before the veil.
27 Alichoma uvumba wa manukato hapo, kama Yahweh alivyo muamuru.
And he burnt on it fragrant incense; as Jehovah had commanded Moses.
28 Alitundika pazia katika hema ya kukutania.
And he hung up the curtain of the entrance to the tabernacle.
29 Aliweka madhabahu ya sadaka ya kuteketeza katika hema ya kukutania. Aliitolea sadaka ya kuteketeza na sadaka ya unga, kama Yahweh alivyo muamuru.
And he put the altar of burnt-offering at the entrance to the tabernacle of the tent of meeting, and offered on it the burnt-offering and the oblation; as Jehovah had commanded Moses.
30 Aliweka beseni katikati ya hema ya kukutunia na madhabahu, na maji ya kuoshea.
And he set the laver between the tent of meeting and the altar, and put water in it for washing.
31 Musa, Aruni, na wanae waliosha mikono yao na miguu kwenye beseni
And Moses and Aaron and his sons washed their hands and their feet out of it:
32 muda wowote walipoenda kwenye hema ya kukutania na muda wowote walipoenda kwenye madhabahu. Walijisafisha, kama Yahweh alivyo muamuru Musa.
when they went into the tent of meeting, and when they drew near to the altar, they washed; as Jehovah had commanded Moses.
33 Musa alianda nyuani nyuma ya hema ya kukutania na madhabahu. Alianda pazia katika mwingilio wa nyuani. Katika hili, Musa alimaliza kazi.
And he set up the court round about the tabernacle and the altar, and hung up the curtain of the gate of the court. And so Moses finished the work.
34 Kisha wingu likafunika hema ya kukutania, na utukufu wa Yahweh ukafunika hema ya kukutania.
And the cloud covered the tent of meeting, and the glory of Jehovah filled the tabernacle.
35 Musa hakuweza kuingia hema ya kukutania kwasababu wingu lilikuwa juu yake, na kwasababu utukufu wa Yahweh ulijaza hema ya kukutania.
And Moses could not enter into the tent of meeting, for the cloud abode on it, and the glory of Jehovah filled the tabernacle.
36 Muda wowote wingu lilipo chukuliwa juu kutoka hema ya kukutania, watu wa Israeli waliendelea na safari yao.
And when the cloud was taken up from over the tabernacle, the children of Israel journeyed in all their journeys.
37 Lakini kama wingu haliku nyanyuka juu kutoka hema ya kukutania, kisha basi watu hawaku safiri. Walibaki hadi siku lilipo nyanyuliwa juu.
And if the cloud were not taken up, then they did not journey until the day that it was taken up.
38 Kwa kuwa wingu la Yahweh lilikuwa juu ya hema ya kukutania mchana, na moto wake ulikuwa juu yake usiku, wazi kwa watu wote wa Israeli kipindi chote cha safari yao.
For the cloud of Jehovah was on the tabernacle by day, and fire was in it by night, before the eyes of all the house of Israel, throughout all their journeys.