< Kutoka 4 >

1 Musa akajibu, “Lakini itakuwaje wasiponiamini mimi au wasiponisikiliza na kusema, 'Yahwe hajakutokea wewe?”
Moïse répondit, en disant: « Ils ne me croiront pas et ils n’écouteront pas ma voix; mais ils diront: Yahweh ne t’est pas apparu. »
2 Yahwe akamwambia, “Hicho ni nini mkononi mwako?” Musa aksema, “Ni fimbo.”
Yahweh lui dit: « Qu’y a-t-il dans ta main? » Il répondit: « Un bâton. »
3 Yahwe akasema, “Itupe chini.” Musa akaitupa chini ile fimbo, nayo ikageuka na kuwa nyoka. Musa akarudi nyumba.
Et Yahweh dit: « Jette-le à terre. » Il le jeta à terre, et ce bâton devint un serpent, et Moïse s’enfuyait devant lui.
4 Yahwe akamwambia Musa, “Mchukue kwa kumshikia mkia wake.” Hivyo alimchukua yule nyoka. Mara ikaggeuka na kuwa fimbo mkononi mwake tena.
Yahweh dit à Moïse: « Etends ta main, et saisis-le par la queue, — et il étendit la main et le saisit, et le serpent redevint un bâton dans sa main, —
5 “Hii ni ili wapate kuamini ya kuwa Yahwe, Mungu wa baba zao, Mungu wa wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo amekutokea wewe.”
afin qu’ils croient que Yahweh, le Dieu de leurs pères, t’est apparu, le Dieu d’Abraham, le Dieu d’Isaac et le Dieu de Jacob. »
6 Yahwe pia alimwambia, “Sasaingiza mkono wako ndani ya vazi lako.” Hivyo Musa akaingiza mkono wake ndani ya vazi lake. Na alipoutoa nje, tazama, mkono wake ulikuwa na ukoma, mweupe kama theluji.
Yahweh lui dit encore: « Mets ta main dans ton sein. » Il mit sa main dans son sein, puis il l’en retira et voici qu’elle était couverte de lèpre, blanche comme la neige.
7 Yahwe akasema, “Ingiza mkono wako ndani ya vazi lako tena.” Hivyo akaingiza mkono wake ndani ya vazi lake, na alipoutoa nje aliona ukiwa mzima tena kama ulivyo mwili wake wote.
Yahweh dit: « Remets ta main dans ton sein, — et il remit sa main dans son sein, puis il la retira de son sein, et voici qu’elle était redevenue semblable à sa chair. —
8 Yahwe akasema, “Kama hawatakuamini wewe - kama hawatazingatia ishara yanggu ya kwanza ya nguvu zangu au kuziamini, basi wataamini ishara ya pili.
S’ils ne te croient pas, et s’ils n’écoutent pas la voix du premier signe, ils croiront à la voix du second.
9 Na ikiwa hawataamini hata ishara hizi zote mbili za nguvu zangu, au wasipokusikiliza wewe, basi chota maji kutoka katika mto na uyamwage katika nchi kavu. Maji utakayoyamwaga yatakuwa damu katika nchi kavu.”
Et s’ils ne croient pas même à ces deux signes, et n’écoutent pas ta voix, tu prendras de l’eau du fleuve, et tu la répandras sur le sol, et l’eau que tu auras prise du fleuve deviendra du sang sur le sol. »
10 Ndipo Musa akamwambia Yahwe, “Bwana, mimi ni mzuri wa kuongea, si hapo kwanza au hata baada ya kuwa umeongea na mtumishi wako. Mimi ni mdhaifu wa kuongea na nina kigugumizi.”
Moïse dit à Yahweh: « Ah! Seigneur, je ne suis pas un homme à la parole facile, et cela dès hier et dès avant-hier, et même encore depuis que vous parlez à votre serviteur; j’ai la bouche et la langue embarrassées. »
11 Yahwe akamwambia, “Ni nani anayeumba mdomo wa mwanadamu? Ni nani amfanyaye mwanadamu kuwa bubu au aone au kipofu? Je si mimi Yahwe?
Yahweh lui dit: « Qui a donné la bouche à l’homme, et qui rend muet ou sourd, voyant ou aveugle? N’est-ce pas moi, Yahweh?
12 Sasa nenda, nami nitauongoza mdomo wako na nitakufundisha cha kusema.”
Va donc, je serai avec ta bouche et je t’enseignerai ce que tu devras dire. »
13 Lakini Musa akasema, “Bwana, tafadhali mtume mtu mwingine, yeyote unayependa kumtuma.”
Moïse dit: « Ah! Seigneur, envoyez votre message par qui vous voudrez l’envoyer. »
14 Kisha Yahwe akamkasirikia Musa. Akasema, “Vipi kuhusu Aroni kaka yako yule Mlawi? Najua ya kuwa anaweza kuongea vizuri. Hata hivyo, anakuja kukutana na wewe, na atakapokuona moyo wake utajawa na furaha.
Alors la colère de Yahweh s’enflamma contre Moïse, et il dit: « N’y a-t-il pas Aaron, ton frère, le Lévite? Je sais qu’il parlera facilement, lui. Et même, voici qu’il vient à ta rencontre et, en te voyant, il se réjouira dans son cœur.
15 Wewe utaongea naye na utaweka maneno ya kusema kinywani mwake. Nami nitakiongoza kinywa chako na kinywa chake pia, nami nitaonesha ninyi nyote yawapasayo kutenda.
Tu lui parleras et tu mettras les paroles dans sa bouche, et moi je serai avec ta bouche et avec sa bouche, et je vous enseignerai ce que vous aurez à faire.
16 Yeye ataongea na watu kwa niaba yako. Yeye atakuwa msemaji wako, na wewe utakuwa kama Mungu kwake.
C’est lui qui parlera pour toi au peuple; il te servira de bouche, et tu lui seras un Dieu.
17 Utachukua hii fimbo pamoja nawe mkononi mwako. Kwa fimbo hii utafanya ishara.”
Quant à ce bâton, prends-le dans ta main; c’est avec quoi tu feras les signes. »
18 Hivyo Musa alirudi kwa Yethro - baba mkwe wake na kumwambia, “Niruhusu nipate kurudi kwa ndugu zangu walioko Misri ili niweze kuona kama bado wako hai.” Yethro akwambia Musa, “Nenda kwa amani.”
Moïse s’en alla. De retour auprès de Jéthro, son beau-père, il lui dit: « Laisse-moi partir, je te prie, et retourner auprès de mes frères qui sont en Égypte, pour voir s’ils sont encore vivants. » Jéthro dit à Moïse: « Va en paix. »
19 Yahwe akamwambia Musa kule Midiani, “Nenda, rudi Misri, kwa kuwa watu wote waliotaka kukuua wameshakufa.”
Yahweh dit à Moïse, en Madian: « Va, retourne en Égypte, car tous ceux qui en voulaient à ta vie sont morts. »
20 Musa akamchukua mke wake na watoto wake wa kiume na kuwapandisha kwenye punda. Akarudi mpaka nchi ya Misri, naye alichukua fimbo ya Mungu pamoja naye mkononi mwake.
Moïse prit donc sa femme et ses fils, et, les ayant fait monter sur des ânes, il retourna au pays d’Égypte; Moïse prit dans sa main le bâton de Dieu.
21 Yahwe akamwambia Musa, “Utakaporudi Misri, jitahidi kufanya ishara zote nilizokupa kufanya mbele ya Farao. Lakini nitaufanya moyo wake kuwa mgumu, naye hawatawaacha watu waende.
Yahweh dit à Moïse: « En partant pour retourner en Égypte, considère tous les prodiges que j’ai mis dans ta main: tu les feras devant Pharaon. Et moi, j’endurcirai son cœur, et il ne laissera pas aller le peuple.
22 Lazima umwambie Farao, 'Hivi ndivyo asemavyo Yahwe: Israeli ni mtoto wangu, mzaliwa wa kwanza wangu,
Tu diras à Pharaon: Ainsi parle Yahweh: « Israël est mon fils, mon premier-né.
23 nami nakuamuru, “Mwache mwanangu aende ili apate kuniabudu mimi.” Lakini kwa kuwa umekataa kumwachia, hakika nitamuua mtoto wako wa kiume, mzaliwa wa kwanza wako.”'
Je te dis: Laisse aller mon fils, pour qu’il me serve; si tu refuses de le laisser aller, je ferai périr ton fils, ton premier-né. »
24 Sasa wakiwa njiani, wakati wa usiku walipopumzika, Yahwe alikutana na Musa na kutaka kumuua.
Sur la route, dans un lieu où Moïse passa la nuit, Yahweh vint à sa rencontre et voulut le faire mourir.
25 Kisha Zipora akachukua kisu kikali na kukata govi la mtoto wake wa kiume na kuligusisha miguuni pake. Kisha akasema, “Hakika wewe ni bwana harusi wangu kwa njia ya damu.”
Séphora prit une pierre tranchante, coupa le prépuce de son fils, et en toucha les pieds de Moïse, en disant: « Tu es pour moi un époux de sang! »
26 Hivyo Yahwe akamwachia. Akasema, “Wewe ni bwana harusi wa damu” kwa sababu ya kutahiriwa.
Et Yahweh le laissa. C’est alors qu’elle dit: « Epoux de sang », à cause de la circoncision.
27 Yahwe akamwambia Aroni, “Nenda nyikani ukutane na Musa.” Aroni akaenda na kukutana naye katika mlima wa Mungu, na kumbusu.
Yahweh dit à Aaron: « Va au-devant de Moïse dans le désert. » Aaron partit et, ayant rencontré Moïse à la montagne de Dieu, il le baisa.
28 Musa akwambia Aroni maneno yote ya Yahwe ambayo alimtuma kusema na kwa habari za ishara zote za nguvu za Yahwe ambazo alimwagiza kutenda.
Moïse fit connaître à Aaron toutes les paroles avec lesquelles Yahweh l’avait envoyé, et tous les signes qu’il lui avait ordonné de faire.
29 Kisha Musa na Aroni wakaenda na kuwakusanya wazee wote wa Israeli.
Moïse et Aaron poursuivirent leur chemin, et ils assemblèrent tous les anciens des enfants d’Israël.
30 Aroni akawaambia maneno yote ambayo Yahwe alimwambia Musa. Pia alionesha ishara na miujiza ya nguvu za Yahwe mbele ya watu.
Aaron rapporta toutes les paroles que Yahweh avait dites à Moïse, et il fit les signes sous les yeux du peuple.
31 Watu waliamini. Waliposikia ya kuwa Yahwe aliwaona Waisraeli na ya kwamba aliyaona mateso yao, waliinamisha vichwa vyao na kumwabudu.
Et le peuple crut; ils apprirent que Yahweh avait visité les enfants d’Israël et qu’il avait vu leur souffrance; et, s’étant inclinés, ils adorèrent.

< Kutoka 4 >