< Kutoka 4 >
1 Musa akajibu, “Lakini itakuwaje wasiponiamini mimi au wasiponisikiliza na kusema, 'Yahwe hajakutokea wewe?”
And he answered Moses and he said and here! not they will believe me and not they will listen to voice my for they will say not he appeared to you Yahweh.
2 Yahwe akamwambia, “Hicho ni nini mkononi mwako?” Musa aksema, “Ni fimbo.”
And he said to him Yahweh (what [is] this? *Q(K)*) [is] in hand your and he said a staff.
3 Yahwe akasema, “Itupe chini.” Musa akaitupa chini ile fimbo, nayo ikageuka na kuwa nyoka. Musa akarudi nyumba.
And he said throw it [the] ground towards and he threw it [the] ground towards and it became a snake and he fled Moses from before it.
4 Yahwe akamwambia Musa, “Mchukue kwa kumshikia mkia wake.” Hivyo alimchukua yule nyoka. Mara ikaggeuka na kuwa fimbo mkononi mwake tena.
And he said Yahweh to Moses stretch out hand your and hold on tail its and he stretched out hand his and he took hold on it and it became a staff in hand his.
5 “Hii ni ili wapate kuamini ya kuwa Yahwe, Mungu wa baba zao, Mungu wa wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo amekutokea wewe.”
So that they may believe that he appeared to you Yahweh [the] God ancestors their [the] God of Abraham [the] God of Isaac and [the] God of Jacob.
6 Yahwe pia alimwambia, “Sasaingiza mkono wako ndani ya vazi lako.” Hivyo Musa akaingiza mkono wake ndani ya vazi lake. Na alipoutoa nje, tazama, mkono wake ulikuwa na ukoma, mweupe kama theluji.
And he said Yahweh to him again put please hand your in bosom your and he put hand his in bosom his and he brought out it and there! hand his [was] leprous like snow.
7 Yahwe akasema, “Ingiza mkono wako ndani ya vazi lako tena.” Hivyo akaingiza mkono wake ndani ya vazi lake, na alipoutoa nje aliona ukiwa mzima tena kama ulivyo mwili wake wote.
And he said return hand your into bosom your and he returned hand his into bosom his and he brought out it from bosom his and there! it had turned back like flesh his.
8 Yahwe akasema, “Kama hawatakuamini wewe - kama hawatazingatia ishara yanggu ya kwanza ya nguvu zangu au kuziamini, basi wataamini ishara ya pili.
And it will be if not they will believe you and not they will listen to [the] voice of the sign former and they will believe [the] voice of the sign latter.
9 Na ikiwa hawataamini hata ishara hizi zote mbili za nguvu zangu, au wasipokusikiliza wewe, basi chota maji kutoka katika mto na uyamwage katika nchi kavu. Maji utakayoyamwaga yatakuwa damu katika nchi kavu.”
And it will be if not they will believe also [the] two the signs these and not they will listen! to voice your and you will take some of [the] water of the River and you will pour [it] out the dry ground and they will become the waters which you will take from the River and they will become blood on the dry ground.
10 Ndipo Musa akamwambia Yahwe, “Bwana, mimi ni mzuri wa kuongea, si hapo kwanza au hata baada ya kuwa umeongea na mtumishi wako. Mimi ni mdhaifu wa kuongea na nina kigugumizi.”
And he said Moses to Yahweh pardon me O Lord not [am] a man of words I neither from yesterday nor from three days ago nor from then speaking you to servant your for [am] heavy of mouth and heavy of tongue I.
11 Yahwe akamwambia, “Ni nani anayeumba mdomo wa mwanadamu? Ni nani amfanyaye mwanadamu kuwa bubu au aone au kipofu? Je si mimi Yahwe?
And he said Yahweh to him who? did he make a mouth of person or who? does he make dumb or deaf or seeing or blind ¿ not [do] I Yahweh.
12 Sasa nenda, nami nitauongoza mdomo wako na nitakufundisha cha kusema.”
And therefore go and I I will be with mouth your and I will teach you [that] which you will say.
13 Lakini Musa akasema, “Bwana, tafadhali mtume mtu mwingine, yeyote unayependa kumtuma.”
And he said pardon me O Lord send please by [the] hand of [whoever] you will send.
14 Kisha Yahwe akamkasirikia Musa. Akasema, “Vipi kuhusu Aroni kaka yako yule Mlawi? Najua ya kuwa anaweza kuongea vizuri. Hata hivyo, anakuja kukutana na wewe, na atakapokuona moyo wake utajawa na furaha.
And it burned [the] anger of Yahweh on Moses and he said ¿ not [is] Aaron brother your the Levite I know that well he speaks he and also there! he [is] coming out to meet you and he will see you and he will be glad in heart his.
15 Wewe utaongea naye na utaweka maneno ya kusema kinywani mwake. Nami nitakiongoza kinywa chako na kinywa chake pia, nami nitaonesha ninyi nyote yawapasayo kutenda.
And you will speak to him and you will put the words in mouth his and I I will be with mouth your and with mouth his and I will teach you [that] which you will do!
16 Yeye ataongea na watu kwa niaba yako. Yeye atakuwa msemaji wako, na wewe utakuwa kama Mungu kwake.
And he will speak he for you to the people and it will be he he will become of you a mouth and you you will become of him a god.
17 Utachukua hii fimbo pamoja nawe mkononi mwako. Kwa fimbo hii utafanya ishara.”
And the staff this you will take in hand your which you will do with it the signs.
18 Hivyo Musa alirudi kwa Yethro - baba mkwe wake na kumwambia, “Niruhusu nipate kurudi kwa ndugu zangu walioko Misri ili niweze kuona kama bado wako hai.” Yethro akwambia Musa, “Nenda kwa amani.”
And he went Moses and he returned - to Jethro father-in-law his and he said to him let me go please so I may return to relatives my who [are] in Egypt so I may see ¿ [are] still they living and he said Jethro to Moses go to peace.
19 Yahwe akamwambia Musa kule Midiani, “Nenda, rudi Misri, kwa kuwa watu wote waliotaka kukuua wameshakufa.”
And he said Yahweh to Moses in Midian go return Egypt for they have died all the men who sought life your.
20 Musa akamchukua mke wake na watoto wake wa kiume na kuwapandisha kwenye punda. Akarudi mpaka nchi ya Misri, naye alichukua fimbo ya Mungu pamoja naye mkononi mwake.
And he took Moses wife his and sons his and he made ride them on the donkey and he returned [the] land of towards Egypt and he took Moses [the] staff of God in hand his.
21 Yahwe akamwambia Musa, “Utakaporudi Misri, jitahidi kufanya ishara zote nilizokupa kufanya mbele ya Farao. Lakini nitaufanya moyo wake kuwa mgumu, naye hawatawaacha watu waende.
And he said Yahweh to Moses when going you to return Egypt towards see all the wonders which I have put in hand your and you will do them before Pharaoh and I I will make strong heart his and not he will let go the people.
22 Lazima umwambie Farao, 'Hivi ndivyo asemavyo Yahwe: Israeli ni mtoto wangu, mzaliwa wa kwanza wangu,
And you will say to Pharaoh thus he says Yahweh [is] son my firstborn my Israel.
23 nami nakuamuru, “Mwache mwanangu aende ili apate kuniabudu mimi.” Lakini kwa kuwa umekataa kumwachia, hakika nitamuua mtoto wako wa kiume, mzaliwa wa kwanza wako.”'
And I said to you let go son my so he may serve me and you refused to let go him here! I [am] about to kill son your firstborn your.
24 Sasa wakiwa njiani, wakati wa usiku walipopumzika, Yahwe alikutana na Musa na kutaka kumuua.
And it was on the journey at the lodging place and he met him Yahweh and he sought to kill him.
25 Kisha Zipora akachukua kisu kikali na kukata govi la mtoto wake wa kiume na kuligusisha miguuni pake. Kisha akasema, “Hakika wewe ni bwana harusi wangu kwa njia ya damu.”
And she took Zipporah a flint and she cut off [the] foreskin of son her and she made [it] touch feet his and she said that [are] a bridegroom of blood you to me.
26 Hivyo Yahwe akamwachia. Akasema, “Wewe ni bwana harusi wa damu” kwa sababu ya kutahiriwa.
And he withdrew from him then she said a bridegroom of blood to the circumcision.
27 Yahwe akamwambia Aroni, “Nenda nyikani ukutane na Musa.” Aroni akaenda na kukutana naye katika mlima wa Mungu, na kumbusu.
And he said Yahweh to Aaron go to meet Moses the wilderness towards and he went and he met him at [the] mountain of God and he kissed him.
28 Musa akwambia Aroni maneno yote ya Yahwe ambayo alimtuma kusema na kwa habari za ishara zote za nguvu za Yahwe ambazo alimwagiza kutenda.
And he told Moses to Aaron all [the] words of Yahweh which he had sent him and all the signs which he had commanded him.
29 Kisha Musa na Aroni wakaenda na kuwakusanya wazee wote wa Israeli.
And he went Moses and Aaron and they gathered all [the] elders of [the] people of Israel.
30 Aroni akawaambia maneno yote ambayo Yahwe alimwambia Musa. Pia alionesha ishara na miujiza ya nguvu za Yahwe mbele ya watu.
And he spoke Aaron all the words which he had spoken Yahweh to Moses and he did the signs to [the] eyes of the people.
31 Watu waliamini. Waliposikia ya kuwa Yahwe aliwaona Waisraeli na ya kwamba aliyaona mateso yao, waliinamisha vichwa vyao na kumwabudu.
And it believed the people and they heard that he had observed Yahweh [the] people of Israel and that he had seen affliction their and they bowed low and they bowed down.