< Kutoka 4 >

1 Musa akajibu, “Lakini itakuwaje wasiponiamini mimi au wasiponisikiliza na kusema, 'Yahwe hajakutokea wewe?”
Then responded Moses, and said, And lo! they will not believe me, neither hearken to my voice, —for they will say, Yahweh, hath not appeared unto thee.
2 Yahwe akamwambia, “Hicho ni nini mkononi mwako?” Musa aksema, “Ni fimbo.”
And Yahweh said unto him—What is this in thy hand? And he said—A staff.
3 Yahwe akasema, “Itupe chini.” Musa akaitupa chini ile fimbo, nayo ikageuka na kuwa nyoka. Musa akarudi nyumba.
Then said he—Cast it to the earth. And he cast it to the earth, and it became a serpent, —and Moses fled from the face thereof.
4 Yahwe akamwambia Musa, “Mchukue kwa kumshikia mkia wake.” Hivyo alimchukua yule nyoka. Mara ikaggeuka na kuwa fimbo mkononi mwake tena.
And Yahweh said unto Moses, Put forth thy hand, and take it by its tail: So he put forth his hand, and laid hold of it, and it became a staff in his hand: —
5 “Hii ni ili wapate kuamini ya kuwa Yahwe, Mungu wa baba zao, Mungu wa wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo amekutokea wewe.”
that they may believe that Yahweh, God of their fathers, —God of Abraham, God of Isaac, and God of Jacob hath appeared unto thee.
6 Yahwe pia alimwambia, “Sasaingiza mkono wako ndani ya vazi lako.” Hivyo Musa akaingiza mkono wake ndani ya vazi lake. Na alipoutoa nje, tazama, mkono wake ulikuwa na ukoma, mweupe kama theluji.
Then said Yahweh unto him, yet again—Bring, I pray thee, thy hand, into thy bosom. So he brought his hand, into his bosom, —and then took it out, and lo! his hand, was leprous, —like snow,
7 Yahwe akasema, “Ingiza mkono wako ndani ya vazi lako tena.” Hivyo akaingiza mkono wake ndani ya vazi lake, na alipoutoa nje aliona ukiwa mzima tena kama ulivyo mwili wake wote.
And he said—Put back thy hand into thy bosom: So he put back his hand into his bosom, —and then took it out of his bosom, and lo it had come again like his own flesh:
8 Yahwe akasema, “Kama hawatakuamini wewe - kama hawatazingatia ishara yanggu ya kwanza ya nguvu zangu au kuziamini, basi wataamini ishara ya pili.
thus shall it come to pass, if they will not believe thee, nor hearken to the voice of the first sign, then will they believe the voice of the next sign;
9 Na ikiwa hawataamini hata ishara hizi zote mbili za nguvu zangu, au wasipokusikiliza wewe, basi chota maji kutoka katika mto na uyamwage katika nchi kavu. Maji utakayoyamwaga yatakuwa damu katika nchi kavu.”
and it shall come to pass if they will not believe even these two signs nor hearken to thy voice, then shalt thou take of the water of the river, and pour it out on the dry land, —so shall the water which thou hast taken from the river, become, yea it shall become, blood, on the dry land.
10 Ndipo Musa akamwambia Yahwe, “Bwana, mimi ni mzuri wa kuongea, si hapo kwanza au hata baada ya kuwa umeongea na mtumishi wako. Mimi ni mdhaifu wa kuongea na nina kigugumizi.”
And Moses said unto Yahweh—Pardon, O My Lord! not a man of words, am I, neither heretofore, nor since thou hast spoken unto thy servant, —for heavy of mouth and heavy of tongue, I am.
11 Yahwe akamwambia, “Ni nani anayeumba mdomo wa mwanadamu? Ni nani amfanyaye mwanadamu kuwa bubu au aone au kipofu? Je si mimi Yahwe?
Then Yahweh said unto him—Who appointed a mouth for man, or who appointeth him to be dumb, or deaf, or seeing or blind? Is it not I, Yahweh?
12 Sasa nenda, nami nitauongoza mdomo wako na nitakufundisha cha kusema.”
Now, therefore go, —and, I, will be with thy mouth, so will I direct thee, what thou shalt speak.
13 Lakini Musa akasema, “Bwana, tafadhali mtume mtu mwingine, yeyote unayependa kumtuma.”
And he said—Pardon, O My Lord! send, I pray thee by the hand of him whom thou wilt send—
14 Kisha Yahwe akamkasirikia Musa. Akasema, “Vipi kuhusu Aroni kaka yako yule Mlawi? Najua ya kuwa anaweza kuongea vizuri. Hata hivyo, anakuja kukutana na wewe, na atakapokuona moyo wake utajawa na furaha.
Then was kindled the anger of Yahweh against Moses, and he said—Is there not Aaron, thy brother, the Levite? I know that he, can speak. Moreover also lo! he himself is coming forth to meet thee, as surely as he seeth thee, so surely will he rejoice in his heart.
15 Wewe utaongea naye na utaweka maneno ya kusema kinywani mwake. Nami nitakiongoza kinywa chako na kinywa chake pia, nami nitaonesha ninyi nyote yawapasayo kutenda.
Then shalt thou speak unto him, and shalt put the words in his mouth, —and, I, will be with thy mouth and with his mouth, so will I direct you what ye shall do.
16 Yeye ataongea na watu kwa niaba yako. Yeye atakuwa msemaji wako, na wewe utakuwa kama Mungu kwake.
And, he, shall speak for thee unto the people, —so shall it come to pass that he shall become thy mouth, and thou shalt become to him as God.
17 Utachukua hii fimbo pamoja nawe mkononi mwako. Kwa fimbo hii utafanya ishara.”
And this staff, take thou in thy hand, —wherewith thou shalt do the signs.
18 Hivyo Musa alirudi kwa Yethro - baba mkwe wake na kumwambia, “Niruhusu nipate kurudi kwa ndugu zangu walioko Misri ili niweze kuona kama bado wako hai.” Yethro akwambia Musa, “Nenda kwa amani.”
So Moses went and returned unto Jethro his father-in-law and said to him—Let me go, I pray thee, and return unto my brethren who are in Egypt, that I may see whether they are yet alive. And Jethro said to Moses: Go and prosper.
19 Yahwe akamwambia Musa kule Midiani, “Nenda, rudi Misri, kwa kuwa watu wote waliotaka kukuua wameshakufa.”
Then said Yahweh unto Moses in Midian, Go, return to Egypt, —for all the men are dead who were seeking thy life.
20 Musa akamchukua mke wake na watoto wake wa kiume na kuwapandisha kwenye punda. Akarudi mpaka nchi ya Misri, naye alichukua fimbo ya Mungu pamoja naye mkononi mwake.
So Moses took his wife and his sons, and caused them to ride upon the ass, and he returned to the land of Egypt, —and Moses took the staff of God in his hand.
21 Yahwe akamwambia Musa, “Utakaporudi Misri, jitahidi kufanya ishara zote nilizokupa kufanya mbele ya Farao. Lakini nitaufanya moyo wake kuwa mgumu, naye hawatawaacha watu waende.
And Yahweh said unto Moses, When thou goest to return to Egypt, see as touching all the wonders which I have put in thy hand, that thou do them before Pharaoh—but, I, will let his heart wax bold, and he will not suffer the people to go.
22 Lazima umwambie Farao, 'Hivi ndivyo asemavyo Yahwe: Israeli ni mtoto wangu, mzaliwa wa kwanza wangu,
Then shalt thou say unto Pharaoh, Thus, saith Yahweh—My son—my firstborn, is Israel;
23 nami nakuamuru, “Mwache mwanangu aende ili apate kuniabudu mimi.” Lakini kwa kuwa umekataa kumwachia, hakika nitamuua mtoto wako wa kiume, mzaliwa wa kwanza wako.”'
Therefore I say unto thee, Let my son go, that he may serve me, But if thou refuse to let him go, behold, I, am going to slay, thy son, thy firstborn.
24 Sasa wakiwa njiani, wakati wa usiku walipopumzika, Yahwe alikutana na Musa na kutaka kumuua.
And it came to pass, on the way, in the resting-place for the night, that Yahweh fell upon him, and sought to kill him.
25 Kisha Zipora akachukua kisu kikali na kukata govi la mtoto wake wa kiume na kuligusisha miguuni pake. Kisha akasema, “Hakika wewe ni bwana harusi wangu kwa njia ya damu.”
So Zipporah took a sharp stone and cut off the foreskin of her son, and cast it down at his feet, —and said—Surely, a bridegroom by rites of blood, art thou to me!
26 Hivyo Yahwe akamwachia. Akasema, “Wewe ni bwana harusi wa damu” kwa sababu ya kutahiriwa.
So he let him go, Then, it was that she said, A bridegroom by rites of blood—with regard to the rites of circumcision.
27 Yahwe akamwambia Aroni, “Nenda nyikani ukutane na Musa.” Aroni akaenda na kukutana naye katika mlima wa Mungu, na kumbusu.
And Yahweh said unto Aaron, Go thy way to meet Moses, towards the desert. So he went his way, and fell in with him in the mountain of God and kissed him.
28 Musa akwambia Aroni maneno yote ya Yahwe ambayo alimtuma kusema na kwa habari za ishara zote za nguvu za Yahwe ambazo alimwagiza kutenda.
And Moses told Aaron, all the words of Yahweh wherewith he had sent him, —and all the signs wherewith he had charged him.
29 Kisha Musa na Aroni wakaenda na kuwakusanya wazee wote wa Israeli.
So Moses and Aaron went their way, —and gathered together all the elders of the sons of Israel.
30 Aroni akawaambia maneno yote ambayo Yahwe alimwambia Musa. Pia alionesha ishara na miujiza ya nguvu za Yahwe mbele ya watu.
And Aaron spake all the words which Yahweh had spoken unto Moses, —and did the signs before the eyes of the people,
31 Watu waliamini. Waliposikia ya kuwa Yahwe aliwaona Waisraeli na ya kwamba aliyaona mateso yao, waliinamisha vichwa vyao na kumwabudu.
And the people believed, —and when they heard that Yahweh had concerned himself for the sons of Israel, and that he had looked upon their humiliation, then bent they their heads and bowed themselves down.

< Kutoka 4 >