< Kutoka 4 >

1 Musa akajibu, “Lakini itakuwaje wasiponiamini mimi au wasiponisikiliza na kusema, 'Yahwe hajakutokea wewe?”
Then Moses answered, and said, But lo, they will not beleeue me, nor hearken vnto my voyce: for they will say, The Lord hath not appeared vnto thee.
2 Yahwe akamwambia, “Hicho ni nini mkononi mwako?” Musa aksema, “Ni fimbo.”
And the Lord said vnto him, What is that in thine hande? And he answered, A rod.
3 Yahwe akasema, “Itupe chini.” Musa akaitupa chini ile fimbo, nayo ikageuka na kuwa nyoka. Musa akarudi nyumba.
Then said he, Cast it on the ground. So he cast it on the grounde, and it was turned into a serpent: and Moses fled from it.
4 Yahwe akamwambia Musa, “Mchukue kwa kumshikia mkia wake.” Hivyo alimchukua yule nyoka. Mara ikaggeuka na kuwa fimbo mkononi mwake tena.
Againe the Lord saide vnto Moses, Put foorth thine hand, and take it by the tayle. Then he put foorth his hande and caught it, and it was turned into a rod in his hand.
5 “Hii ni ili wapate kuamini ya kuwa Yahwe, Mungu wa baba zao, Mungu wa wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo amekutokea wewe.”
Do this that they may beleeue, that the Lord God of their fathers, the God of Abraham, the God of Izhak, and the God of Iaakob hath appeared vnto thee.
6 Yahwe pia alimwambia, “Sasaingiza mkono wako ndani ya vazi lako.” Hivyo Musa akaingiza mkono wake ndani ya vazi lake. Na alipoutoa nje, tazama, mkono wake ulikuwa na ukoma, mweupe kama theluji.
And the Lord saide furthermore vnto him, Thrust nowe thine hand into thy bosome. And he thrust his hand into his bosome, and when he tooke it out againe, behold, his hand was leprous as snowe.
7 Yahwe akasema, “Ingiza mkono wako ndani ya vazi lako tena.” Hivyo akaingiza mkono wake ndani ya vazi lake, na alipoutoa nje aliona ukiwa mzima tena kama ulivyo mwili wake wote.
Moreouer he said, Put thine hand into thy bosome againe. So he put his hande into his bosome againe, and pluckt it out of his bosome, and behold, it was turned againe as his other flesh.
8 Yahwe akasema, “Kama hawatakuamini wewe - kama hawatazingatia ishara yanggu ya kwanza ya nguvu zangu au kuziamini, basi wataamini ishara ya pili.
So shall it be, if they wil not beleeue thee, neither obey the voyce of ye first signe, yet shall they beleeue for the voyce of the seconde signe.
9 Na ikiwa hawataamini hata ishara hizi zote mbili za nguvu zangu, au wasipokusikiliza wewe, basi chota maji kutoka katika mto na uyamwage katika nchi kavu. Maji utakayoyamwaga yatakuwa damu katika nchi kavu.”
But if they will not yet beleeue these two signes, neither obey vnto thy voyce, then shalt thou take of the water of the riuer, and powre it vpon the drie lande: so the water which thou shalt take out of the riuer, shalbe turned to blood vpon the drie land.
10 Ndipo Musa akamwambia Yahwe, “Bwana, mimi ni mzuri wa kuongea, si hapo kwanza au hata baada ya kuwa umeongea na mtumishi wako. Mimi ni mdhaifu wa kuongea na nina kigugumizi.”
But Moses said vnto the Lord, Oh my Lord, I am not eloquent, neither at any time haue bene, nor yet since thou hast spoken vnto thy seruant: but I am slowe of speach and slowe of tongue.
11 Yahwe akamwambia, “Ni nani anayeumba mdomo wa mwanadamu? Ni nani amfanyaye mwanadamu kuwa bubu au aone au kipofu? Je si mimi Yahwe?
Then the Lord said vnto him, Who hath giuen the mouth to man? or who hath made the domme, or the deafe, or him that seeth, or the blinde? haue not I the Lord?
12 Sasa nenda, nami nitauongoza mdomo wako na nitakufundisha cha kusema.”
Therefore goe nowe, and I will be with thy mouth, and will teach thee what thou shalt say.
13 Lakini Musa akasema, “Bwana, tafadhali mtume mtu mwingine, yeyote unayependa kumtuma.”
But he saide, Oh my Lord, sende, I pray thee, by the hande of him, whome thou shouldest sende.
14 Kisha Yahwe akamkasirikia Musa. Akasema, “Vipi kuhusu Aroni kaka yako yule Mlawi? Najua ya kuwa anaweza kuongea vizuri. Hata hivyo, anakuja kukutana na wewe, na atakapokuona moyo wake utajawa na furaha.
Then the Lord was verie angrie with Moses, and said, Doe not I know Aaron thy brother the Leuite, that he himselfe shall speake? for loe, he commeth also foorth to meete thee, and when he seeth thee, he will be glad in his heart.
15 Wewe utaongea naye na utaweka maneno ya kusema kinywani mwake. Nami nitakiongoza kinywa chako na kinywa chake pia, nami nitaonesha ninyi nyote yawapasayo kutenda.
Therefore thou shalt speake vnto him, and put the wordes in his mouth, and I will be with thy mouth, and with his mouth, and will teach you what ye ought to doe.
16 Yeye ataongea na watu kwa niaba yako. Yeye atakuwa msemaji wako, na wewe utakuwa kama Mungu kwake.
And he shall be thy spokesman vnto the people: and he shall be, euen he shall be as thy mouth, and thou shalt be to him as God.
17 Utachukua hii fimbo pamoja nawe mkononi mwako. Kwa fimbo hii utafanya ishara.”
Moreouer thou shalt take this rod in thine hand, wherewith thou shalt do miracles.
18 Hivyo Musa alirudi kwa Yethro - baba mkwe wake na kumwambia, “Niruhusu nipate kurudi kwa ndugu zangu walioko Misri ili niweze kuona kama bado wako hai.” Yethro akwambia Musa, “Nenda kwa amani.”
Therefore Moses went and returned to Iethro his father in lawe, and said vnto him, I pray thee, let me goe, and returne to my brethren, which are in Egypt, and see whether they be yet aliue. Then Iethro said to Moses, Go in peace.
19 Yahwe akamwambia Musa kule Midiani, “Nenda, rudi Misri, kwa kuwa watu wote waliotaka kukuua wameshakufa.”
(For the Lord had said vnto Moses in Midian, Goe, returne to Egypt: for they are all dead which went about to kill thee)
20 Musa akamchukua mke wake na watoto wake wa kiume na kuwapandisha kwenye punda. Akarudi mpaka nchi ya Misri, naye alichukua fimbo ya Mungu pamoja naye mkononi mwake.
Then Moses tooke his wife, and his sonnes, and put them on an asse, and returned towarde the lande of Egypt, and Moses tooke the rod of God in his hand.
21 Yahwe akamwambia Musa, “Utakaporudi Misri, jitahidi kufanya ishara zote nilizokupa kufanya mbele ya Farao. Lakini nitaufanya moyo wake kuwa mgumu, naye hawatawaacha watu waende.
And the Lord saide vnto Moses, When thou art entred and come into Egypt againe, see that thou doe all the wonders before Pharaoh, which I haue put in thine hand: but I will harden his heart, and he shall not let the people goe.
22 Lazima umwambie Farao, 'Hivi ndivyo asemavyo Yahwe: Israeli ni mtoto wangu, mzaliwa wa kwanza wangu,
Then thou shalt say to Pharaoh, Thus saith the Lord, Israel is my sonne, euen my first borne.
23 nami nakuamuru, “Mwache mwanangu aende ili apate kuniabudu mimi.” Lakini kwa kuwa umekataa kumwachia, hakika nitamuua mtoto wako wa kiume, mzaliwa wa kwanza wako.”'
Wherefore I say to thee, Let my sonne go, that he may serue me: if thou refuse to let him goe, beholde, I will slay thy sonne, euen thy first borne.
24 Sasa wakiwa njiani, wakati wa usiku walipopumzika, Yahwe alikutana na Musa na kutaka kumuua.
And as he was by the waye in the ynne, the Lord met him, and would haue killed him.
25 Kisha Zipora akachukua kisu kikali na kukata govi la mtoto wake wa kiume na kuligusisha miguuni pake. Kisha akasema, “Hakika wewe ni bwana harusi wangu kwa njia ya damu.”
Then Zipporah tooke a sharpe knife, and cut away the foreskinne of her sonne, and cast it at his feete, and said, Thou art indeede a bloody husband vnto me.
26 Hivyo Yahwe akamwachia. Akasema, “Wewe ni bwana harusi wa damu” kwa sababu ya kutahiriwa.
So he departed from him. Then she saide, O bloodie husband (because of the circumcision)
27 Yahwe akamwambia Aroni, “Nenda nyikani ukutane na Musa.” Aroni akaenda na kukutana naye katika mlima wa Mungu, na kumbusu.
Then the Lord saide vnto Aaron, Goe meete Moses in the wildernesse. And he went and mette him in the Mount of God, and kissed him.
28 Musa akwambia Aroni maneno yote ya Yahwe ambayo alimtuma kusema na kwa habari za ishara zote za nguvu za Yahwe ambazo alimwagiza kutenda.
Then Moses tolde Aaron all the wordes of the Lord, who had sent him, and all the signes wherewith he had charged him.
29 Kisha Musa na Aroni wakaenda na kuwakusanya wazee wote wa Israeli.
So went Moses and Aaron, and gathered all the Elders of the children of Israel.
30 Aroni akawaambia maneno yote ambayo Yahwe alimwambia Musa. Pia alionesha ishara na miujiza ya nguvu za Yahwe mbele ya watu.
And Aaron told all the wordes, which the Lord had spoken vnto Moses, and he did the miracles in the sight of the people,
31 Watu waliamini. Waliposikia ya kuwa Yahwe aliwaona Waisraeli na ya kwamba aliyaona mateso yao, waliinamisha vichwa vyao na kumwabudu.
And the people beleeued, and when they heard that the Lord had visited the children of Israel, and had looked vpon their tribulation, they bowed downe, and worshipped.

< Kutoka 4 >