< Kutoka 4 >
1 Musa akajibu, “Lakini itakuwaje wasiponiamini mimi au wasiponisikiliza na kusema, 'Yahwe hajakutokea wewe?”
Odpověděl pak Mojžíš, a řekl: Aj, neuvěří mi, ani uposlechnou hlasu mého; nebo řeknou: Neukázalť se tobě Hospodin.
2 Yahwe akamwambia, “Hicho ni nini mkononi mwako?” Musa aksema, “Ni fimbo.”
Tedy řekl jemu Hospodin: Co jest to v ruce tvé? Odpověděl: Hůl.
3 Yahwe akasema, “Itupe chini.” Musa akaitupa chini ile fimbo, nayo ikageuka na kuwa nyoka. Musa akarudi nyumba.
I řekl: Vrz ji na zem. I povrhl ji na zem, a obrácena jest v hada; a utíkal Mojžíš před ním.
4 Yahwe akamwambia Musa, “Mchukue kwa kumshikia mkia wake.” Hivyo alimchukua yule nyoka. Mara ikaggeuka na kuwa fimbo mkononi mwake tena.
Tedy řekl Hospodin Mojžíšovi: Vztáhni ruku svou, a chyť ho za ocas. Kterýžto vztáh ruku svou, chytil jej, a obrácen jest v hůl v rukou jeho.
5 “Hii ni ili wapate kuamini ya kuwa Yahwe, Mungu wa baba zao, Mungu wa wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo amekutokea wewe.”
Aby věřili, že se ukázal tobě Hospodin, Bůh otců jejich, Bůh Abrahamův, Bůh Izákův a Bůh Jákobův.
6 Yahwe pia alimwambia, “Sasaingiza mkono wako ndani ya vazi lako.” Hivyo Musa akaingiza mkono wake ndani ya vazi lake. Na alipoutoa nje, tazama, mkono wake ulikuwa na ukoma, mweupe kama theluji.
Potom zase řekl jemu Hospodin: Vlož nyní ruku svou za ňadra svá. I vložil ruku svou za ňadra svá; a vyňal ji, a aj, ruka jeho byla malomocná, bílá jako sníh.
7 Yahwe akasema, “Ingiza mkono wako ndani ya vazi lako tena.” Hivyo akaingiza mkono wake ndani ya vazi lake, na alipoutoa nje aliona ukiwa mzima tena kama ulivyo mwili wake wote.
Řekl opět: Vlož ruku svou zase v ňadra svá. Kterýž vložil ruku svou zase v ňadra svá; a vyňal ji z ňader svých, a aj, učiněna jest zase jako jiné tělo jeho.
8 Yahwe akasema, “Kama hawatakuamini wewe - kama hawatazingatia ishara yanggu ya kwanza ya nguvu zangu au kuziamini, basi wataamini ishara ya pili.
I budeť, jestliže neuvěří tobě, a neposlechnou hlasu a znamení prvního, uvěří hlasu a znamení druhému.
9 Na ikiwa hawataamini hata ishara hizi zote mbili za nguvu zangu, au wasipokusikiliza wewe, basi chota maji kutoka katika mto na uyamwage katika nchi kavu. Maji utakayoyamwaga yatakuwa damu katika nchi kavu.”
A pakli neuvěří ani těm dvěma znamením, a neuposlechnou hlasu tvého, tedy nabereš vody z řeky, a vyliješ ji na zem; a promění se vody, kteréž vezmeš z řeky, a obrátí se v krev na zemi.
10 Ndipo Musa akamwambia Yahwe, “Bwana, mimi ni mzuri wa kuongea, si hapo kwanza au hata baada ya kuwa umeongea na mtumishi wako. Mimi ni mdhaifu wa kuongea na nina kigugumizi.”
I řekl Mojžíš Hospodinu: Prosím, Pane, nejsem muž výmluvný, aniž prvé, ani jakž jsi mluvil s služebníkem svým; nebo zpozdilých úst a neohbitého jazyku jsem.
11 Yahwe akamwambia, “Ni nani anayeumba mdomo wa mwanadamu? Ni nani amfanyaye mwanadamu kuwa bubu au aone au kipofu? Je si mimi Yahwe?
Jemuž odpověděl Hospodin: Kdo dal ústa člověku? Aneb kdo může učiniti němého, neb hluchého, vidoucího, neb slepého? Zdali ne já Hospodin?
12 Sasa nenda, nami nitauongoza mdomo wako na nitakufundisha cha kusema.”
Nyní tedy jdi, a já budu v ústech tvých, a naučím tě, co bys mluviti měl.
13 Lakini Musa akasema, “Bwana, tafadhali mtume mtu mwingine, yeyote unayependa kumtuma.”
I řekl: Slyš mne, Pane, pošli, prosím, toho, kteréhož poslati máš.
14 Kisha Yahwe akamkasirikia Musa. Akasema, “Vipi kuhusu Aroni kaka yako yule Mlawi? Najua ya kuwa anaweza kuongea vizuri. Hata hivyo, anakuja kukutana na wewe, na atakapokuona moyo wake utajawa na furaha.
A rozhněvav se velmi Hospodin na Mojžíše, řekl: Zdaliž nemáš Arona bratra svého z pokolení Léví? Vím, že on výmluvný jest; ano aj, sám vyjde v cestu tobě, a vida tebe, radovati se bude v srdci svém.
15 Wewe utaongea naye na utaweka maneno ya kusema kinywani mwake. Nami nitakiongoza kinywa chako na kinywa chake pia, nami nitaonesha ninyi nyote yawapasayo kutenda.
Ty mluviti budeš k němu, a vložíš slova v ústa jeho; a já budu v ústech tvých a v ústech jeho, a naučím vás, co byste měli činiti.
16 Yeye ataongea na watu kwa niaba yako. Yeye atakuwa msemaji wako, na wewe utakuwa kama Mungu kwake.
A on mluviti bude za tebe k lidu; a bude tobě on za ústa, a ty budeš jemu za Boha.
17 Utachukua hii fimbo pamoja nawe mkononi mwako. Kwa fimbo hii utafanya ishara.”
Hůl pak tuto vezmeš v ruku svou, kterouž činiti budeš ta znamení.
18 Hivyo Musa alirudi kwa Yethro - baba mkwe wake na kumwambia, “Niruhusu nipate kurudi kwa ndugu zangu walioko Misri ili niweze kuona kama bado wako hai.” Yethro akwambia Musa, “Nenda kwa amani.”
Tedy odšed Mojžíš, navrátil se k Jetrovi tchánu svému, a řekl jemu: Nechť jdu nyní, a navrátím se k bratřím svým, kteříž jsou v Egyptě, a pohledím, jsou-li ještě živi. I řekl Jetro Mojžíšovi: Jdi v pokoji.
19 Yahwe akamwambia Musa kule Midiani, “Nenda, rudi Misri, kwa kuwa watu wote waliotaka kukuua wameshakufa.”
Nebo řekl byl Hospodin Mojžíšovi v zemi Madianské: Jdi, navrať se do Egypta; nebo zemřeli jsou všickni muži, kteříž hledali bezživotí tvého.
20 Musa akamchukua mke wake na watoto wake wa kiume na kuwapandisha kwenye punda. Akarudi mpaka nchi ya Misri, naye alichukua fimbo ya Mungu pamoja naye mkononi mwake.
A vzav Mojžíš ženu svou, a syny své, vsadil je na osla, aby se navrátil do země Egyptské; vzal také Mojžíš hůl Boží v ruku svou.
21 Yahwe akamwambia Musa, “Utakaporudi Misri, jitahidi kufanya ishara zote nilizokupa kufanya mbele ya Farao. Lakini nitaufanya moyo wake kuwa mgumu, naye hawatawaacha watu waende.
I řekl Hospodin Mojžíšovi: Když půjdeš a navrátíš se do Egypta, hleď, abys všecky zázraky, kteréž jsem složil v ruce tvé, činil před Faraonem. Jáť pak zatvrdím srdce jeho, aby nepropustil lidu.
22 Lazima umwambie Farao, 'Hivi ndivyo asemavyo Yahwe: Israeli ni mtoto wangu, mzaliwa wa kwanza wangu,
Protož díš Faraonovi: Toto praví Hospodin: Syn můj, prvorozený můj jest Izrael.
23 nami nakuamuru, “Mwache mwanangu aende ili apate kuniabudu mimi.” Lakini kwa kuwa umekataa kumwachia, hakika nitamuua mtoto wako wa kiume, mzaliwa wa kwanza wako.”'
I řekl jsem tobě: Propusť syna mého, ať slouží mi; a nechtěl jsi ho propustiti. Aj, já zabiji syna tvého, prvorozeného tvého.
24 Sasa wakiwa njiani, wakati wa usiku walipopumzika, Yahwe alikutana na Musa na kutaka kumuua.
I stalo se, když byl Mojžíš na cestě v hospodě, že se obořil na něj Hospodin, a hledal ho usmrtiti.
25 Kisha Zipora akachukua kisu kikali na kukata govi la mtoto wake wa kiume na kuligusisha miguuni pake. Kisha akasema, “Hakika wewe ni bwana harusi wangu kwa njia ya damu.”
Tedy vzala Zefora nůž ostrý, a obřezala neobřízku syna svého, kteroužto vrhla k nohám jeho, řkuci: Zajisté ženich krví jsi mi.
26 Hivyo Yahwe akamwachia. Akasema, “Wewe ni bwana harusi wa damu” kwa sababu ya kutahiriwa.
I nechal ho. Ona pak nazvala ho tehdáž ženichem krví pro obřezání.
27 Yahwe akamwambia Aroni, “Nenda nyikani ukutane na Musa.” Aroni akaenda na kukutana naye katika mlima wa Mungu, na kumbusu.
Řekl také Hospodin Aronovi: Jdi vstříc Mojžíšovi na poušť. I šel a potkal se s ním na hoře Boží, a políbil ho.
28 Musa akwambia Aroni maneno yote ya Yahwe ambayo alimtuma kusema na kwa habari za ishara zote za nguvu za Yahwe ambazo alimwagiza kutenda.
A vypravoval Mojžíš Aronovi všecka slova Hospodinova, kterýž ho poslal, i o všech znameních, kteráž přikázal jemu.
29 Kisha Musa na Aroni wakaenda na kuwakusanya wazee wote wa Israeli.
Tedy šel Mojžíš s Aronem, a shromáždili všecky starší synů Izraelských.
30 Aroni akawaambia maneno yote ambayo Yahwe alimwambia Musa. Pia alionesha ishara na miujiza ya nguvu za Yahwe mbele ya watu.
I mluvil Aron všecka slova, kteráž byl mluvil Hospodin k Mojžíšovi, a činil znamení před očima lidu.
31 Watu waliamini. Waliposikia ya kuwa Yahwe aliwaona Waisraeli na ya kwamba aliyaona mateso yao, waliinamisha vichwa vyao na kumwabudu.
A uvěřil lid, když uslyšeli, že navštívil Hospodin syny Izraelské, a že viděl ssoužení jejich. A sklonivše se, poklonu učinili.