< Kutoka 39 >

1 Na kutokana na ule uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili wakafanya mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Basi wakafanya yale mavazi matakatifu yaliyokuwa kwa ajili ya Aruni, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
Babaen iti asul, maris ube ken nalabbaga a de lana ket nangaramidda iti kasayaatan ti pannakaabelna a pagan-anay para iti panagserbi iti nasantoan a disso. Inaramidda ti pagan-anay ni Aaron para iti nasantoan a disso, kas imbilin ni Yahweh kenni Moises.
2 Basi akaifanya ile naivera ya dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.
Inaramid ni Bezalel ti efod iti balitok, iti asul, maris ube ken nalabbaga a de lana, ken iti tinali a napino a lino.
3 Kisha wakafua mabamba ya dhahabu yawe mabamba membamba, naye akakata nyuzi za kufuma pamoja na ule uzi wa bluu na ile sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kile kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kile kitani bora, kama kazi ya mjenzi.
Nangpitpida kadagiti pidaso iti balitok ket rinagasda a pinagbalin a kasla kaingpis ti sinulid tapno mainayon dagitoy kadagiti asul, maris ube ken nalabbaga a de lana, ken iti napino a lino, ti aramid iti maysa a batido a trabahador.
4 Wakaifanyia vipande vya begani vilivyounganishwa. Iliunganishwa kwenye miisho yake miwili.
Nangaramidda kadagiti terante para iti efod, a naikapet iti dua nga akinngato a sulina.
5 Nao mshipi, uliokuwa juu yake ili kuifunga, ulikuwa wa kitambaa kilekile kulingana na ufundi wake, wa dhahabu, uzi wa bluu, na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
Ti napintas ti pannakaabelna a barikes ket kasla met laeng iti efod; naaramid daytoy a sangsangkamaysa a karaman ti efod, naaramid iti tinali a napino a lino a balitok, asul, maris ube ken nalabbaga, kas imbilin ni Yahweh kenni Moises.
6 Kisha wakafanya mawe ya shohamu yaliyopangwa kwenye mapambo ya dhahabu, yaliyochongwa kwa michoro ya muhuri kulingana na majina ya wana wa Israeli.
Tinabasda dagiti onyx a bato sada impabugas iti balitok a pagsaadanna, naisaad nga addaan naikitikit a kas pangselio, ken naikitikit dagiti nagan dagiti sangapulo ket dua nga annak a lallaki ni Israel.
7 Bezaleli akayaweka kwenye vile vipande vya begani vya naivera yawe mawe ya ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
Inkabil ni Bezalel dagitoy iti terante ti efod, a kas batbato a mangipalagip kenni Yahweh kadagiti sangapulo ket dua nga annak a lallaki ni Israel, kas imbilin ni Yahweh kenni Moises.
8 Kisha akafanya kile kifuko cha kifuani kwa ufundi wa mjenzi, kama ule ufundi wa naivera, kutokana na dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.
Inaramidna ti pektoral, ti aramid ti maysa a batido a trabahador, naaramid a kas iti efod. Inaramidna daytoy manipud iti balitok, iti asul, maris ube ken nalabbaga a de lana, ken napino a lino.
9 Kilikuwa mraba kilipokunjwa. Walikifanya kile kifuko cha kifuani, kinapokunjwa, shubiri moja urefu wake na shubiri moja upana wake.
Kuadrado daytoy. Inkulpida ti pektoral iti namindua. Maysa a dangan ti kaatiddogna ken maysa a dangan ti kalawana.
10 Kisha wakakijaza kwa mistari minne ya mawe. Mstari wa zabarijadi, topazi na zumaridi ulikuwa mstari wa kwanza.
Nangaramidda iti daytoy iti uppat nga intar dagiti napapateg a bato. Ti umuna nga intar ket addaan iti maysa a rubi, maysa a topasio ken maysa a granate.
11 Nao mstari wa pili ulikuwa feruzi, yakuti na yaspi.
Ti maikadua nga intar ket addaan iti maysa nga esmeralda, maysa a safiro ken maysa a diamante.
12 Nao mstari wa tatu ulikuwa jiwe la leshemi, akiki na amethisti.
Ti maikatlo nga intar ket addaan iti maysa a jasinto, maysa nga agata ken maysa nga amatista.
13 Nao mstari wa nne ulikuwa krisolito na shohamu na yashefi. Yaliwekwa katika mapambo ya dhahabu katika mahali pake.
Ti maikapat nga intar ket addaan iti maysa a berrilio, maysa nga onyx ken maysa a jaspe. Naimontar dagiti bato kadagiti balitok a pagsaadan.
14 Na mawe hayo yalikuwa kulingana na majina ya wana wa Israeli. Yalikuwa kumi na mawili kulingana na majina yao, kwa michongo ya muhuri, kila moja kulingana na jina lake kwa ajili ya yale makabila kumi na mawili.
Naiyurnos dagiti bato babaen kadagiti nagan dagiti sangapulo ket dua nga annak a lallaki ni Israel, babaen iti panagsisinnaruno ti nagan. Maipada dagitoy kadagiti naikitikit iti singsing a pangselio, itaktakder ti tunggal nagan ti maysa kadagiti sangapulo ket dua a tribu.
15 Nao wakafanya juu ya kile kifuko cha kifuani minyororo yenye mashada, msokoto wa kamba, wa dhahabu safi.
Iti pektoral nangaramidda iti kawar a kasla tali, a nasallapid a puro a balitok.
16 Kisha wakafanya mapambo mawili ya dhahabu na pete mbili za dhahabu na kuziweka hizo pete mbili kwenye ile miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani.
Nangaramidda iti dua a balitok a pagimontaran ken dua a balitok a singsing, ket inkapetda dagiti dua a singsing iti dua a suli ti pektoral.
17 Baada ya hilo wakapitisha zile kamba mbili za dhahabu kwenye zile pete mbili zilizo kwenye miisho ya kile kifuko cha kifuani.
Inkabilda dagiti dua a nasallapid a kawar a balitok iti dua a singsing kadagiti suli ti pektoral.
18 Nao wakapitisha ile miisho miwili ya zile kamba mbili kwenye yale mapambo mawili. Halafu wakaiweka juu ya vile vipande vya begani vya naivera, mbele yake.
Inkapetda dagiti sabali a dua a murdong ti nasallapid a kawar iti dua a pagimontaran. Inkapetda dagitoy iti terante ti efod iti sangoananna.
19 Kisha wakafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka kwenye ile miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani kwenye upindo wake ulio upande unaoelekea ile efodi upande wa ndani.
Nangaramidda iti dua a singsing a balitok ken inkapetda dagitoy iti dua a sabali pay a suli ti pektoral, iti akinbaba nga igid ti akin-uneg a gayadanna.
20 Halafu wakafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka juu ya vile vipande viwili vya begani vya efodi upande wake wa chini, sehemu yake ya mbele, karibu na mahali pake pa kuungania, juu ya ule mshipi wa naivera.
Nangaramidda pay iti dua a balitok a singsing ken inkapetda dagitoy iti akinbaba iti dua a terante iti sangoanan ti efod, nga asideg iti nagdaitan iti ngatoen ti nasayaat ti pannakaabelna a barikes ti efod.
21 Mwishowe wakakifunga kile kifuko cha kifuani kwa pete zake kwenye zile pete za efodi kwa uzi wa bluu, ili kipate kuwa juu ya mshipi wa efodi na kile kifuko cha kifuani kisiondoke juu ya efodi, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
Inggalotda ti pektoral babaen kadagiti singsingna kadagiti singsing ti efod iti asul a tali, tapno mabalin a maikapet daytoy iti ngatoen laeng ti nasayaat ti pannakaabelna a barikes ti efod. Daytoy ket tapno ti pektoral ket saan a maikkat manipud iti efod. Naaramid daytoy a kas imbilin ni Yahweh kenni Moises.
22 Bezaleli akafanya lile koti la naivera, lote la uzi wa zambarau, kazi ya mshonaji.
Inaramid ni Bezalel ti kagay ti efod a pasig a maris ube a lupot, ti aramid iti maysa nga umaabel.
23 Na sehemu wazi ya hilo koti ilikuwa katikati yake, kama sehemu wazi ya vazi la chuma. Sehemu hiyo iliyo wazi ilikuwa na ukingo kuizunguka pande zote ili isiraruke.
Addaan daytoy iti pangiyusokan ti ulo iti tengngana. Naabel ti igid ti pangiyusokan tapno saan a mapigis.
24 Halafu wakafanya kwenye upindo wa hilo koti makomamanga ya uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, vilivyosokotwa pamoja.
Iti gayadan, nangaramidda kadagiti sinan granada babaen iti asul, maris ube ken nalabbaga a sinulid, ken iti napino a lino.
25 Wakafanya kengele za dhahabu safi na kuziweka kengele hizo katikati ya makomamanga kwenye upindo wa lile koti kuzunguka pande zote, katikati ya makomamanga;
Nangaramidda kadagiti kampanilia a puro a balitok, ken inkabilda dagiti kampanilia iti nagbaetan dagiti sinan-granada iti amin nga aglawlaw ti gayadan ti kagay, iti nagbaetan dagiti sinan-granada—
26 kengele na komamanga, kengele na komamanga kwenye upindo wa hilo koti kuzunguka pande zote, kwa ajili ya kuhudumu, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
maysa a kampanilia ken maysa a sinan-granada, maysa a kampanilia ken maysa a sinan-granada—iti igid ti kagay tapno makapagserbi ni Aaron. Daytoy ket kas iti imbilin ni Yahweh kenni Moises.
27 Kisha wakafanya zile kamba za kitani bora, kwa ajili ya Haruni na wanawe.
Inaramidda dagiti tunika manipud iti napino a lino para kenni Aaron ken para kadagiti annakna a lallaki.
28 Na kile kilemba cha kitani bora na yale mavalio ya kichwani ya mapambo ya kitani bora na zile suruali za kitani bora kilichosokotwa,
Inaramidda ti turban manipud iti napino a lino, ti naarkusan a baredbed ti ulo manipud iti napino a lino, ti akin-uneg a pagan-anay manipud iti napino a lino,
29 na ule ukumbuu wa kitani bora kilichosokotwa na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, kazi ya mfumaji, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
ken ti barikes iti napino a lino ken asul, maris ube, ken nalabbaga a sinulid, ti aramid ti maysa a bumuborda. Daytoy ket kas imbilin ni Yahweh kenni Moises.
30 Mwishowe wakafanya lile bamba linalong’aa, ishara takatifu ya wakfu, kutokana na dhahabu safi na kuandika juu yake maandishi kwa mchongo wa muhuri: “Utakatifu kwa Yahweh.”
Inaramidda ti insignia ti nasantoan a korona iti puro a balitok; inkitikitda iti daytoy, kasla iti naikitikit iti singsing nga adda timbrena, NAIDATON KENNI YAHWEH.
31 Kisha wakalitia uzi wa bluu ili waliweke juu ya kile kilemba upande wa juu. Kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
Inkapetda iti turban ti maysa nga asul a tali iti rabaw ti turban. Daytoy ket kas imbilin ni Yahweh kenni Moises.
32 Basi kazi ya ile maskani ya hema la mkutano ikafikia mwisho wake. Kwa maana wana wa Israeli waliendelea kufanya kulingana na yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa.
Isu a ti trabaho iti tabernakulo, nga isu ti sagrado a tolda ket nalpas. Inaramid dagiti Israelita dagiti amin a banag. Sinurotda dagiti amin a bilin nga inted ni Yahweh kenni Moises.
33 Nao wakaileta maskani kwa Musa, lile hema pamoja na vyombo vyake vyote, kulabu zake, viunzi vyake vya mbao, miti yake na nguzo zake na vikalio vyake,
Impanda ti tabernakulo kenni Moises—ti tolda ken amin dagiti alikamenna, dagiti pagsab-itanna, dagiti tabla, dagiti balunet, dagiti poste, ken dagiti batay;
34 na kifuniko chake cha ngozi za kondoo-dume zilizotiwa rangi nyekundu na kifuniko chake cha ngozi za sili na pazia la kisitiri,
ti pangabbong a lalat ti kalakian a karnero a namarisan iti nalabbaga, ti pangabbong a lalat ti dugong ken dagiti kurtina a panglinged
35 na sanduku la ushuhuda na miti yake na kifuniko.
iti lakasa ti tulag, kasta met dagiti assiw ken ti kalub a mangipakita iti pannakakalub iti basol.
36 Wakaleta meza, vyombo vyake vyote, na ule mkate wa wonyesho,
Impanda ti lamisaan, dagiti amin nga alikamenna, ken ti tinapay iti presensia;
37 kile kinara cha taa cha dhahabu safi, taa zake, ule mstari wa taa, na vyombo vyake vyote na yale mafuta ya kuangazia taa,
ti kandelero a puro a balitok ken dagiti pagsilawanna a nakaintar, agraman dagiti alikamenna ken ti lana para kadagiti pagsilawan;
38 na madhabahu ya dhahabu na yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na ule uvumba uliotiwa manukato na kile kisitiri kwa ajili ya mwingilio wa hema,
ti altar a balitok, ti pangpulot a lana ken ti nabanglo nga insenso; ti maibitin para iti pagserkan ti tabernakulo;
39 ile madhabahu ya shaba na kile kiunzi chake cha shaba, miti yake na vyombo vyake vyote, ile beseni na kinara chake,
ti bronse nga altar agraman dagiti barandiliasna a bronse, dagiti assiwna ken dagiti alikamenna, ken ti dakkel a palanggana agraman ti batayna.
40 Wakaleta mapazia ya ua, nguzo zake na vikalio vyake na kile kisitiri kwa ajili ya lango la ua, kamba zake za hema na misumari yake ya hema na vyombo vyote kwa ajili ya utumishi wa maskani, kwa ajili ya hema ya kukutania.
Impanda dagiti maibitin para iti paraangan ken dagiti poste ken dagiti batayna, ken ti kurtina para iti pagserkan ti paraangan; dagiti talina ken dagiti pasok ti tolda; ken dagiti amin nga alikamen para iti panagserbi iti tabernakulo, ti sagrado a tolda.
41 Wakaleta yale mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika patakatifu, yale mavazi matakatifu kwa ajili ya Aruni kuhani na mavazi ya wanawe ya kutumikia wakiwa makuhani.
Impanda dagiti nasayaat a naabel a pagan-anay para iti panagserbi iti nasantoan a disso, dagiti nasantoan a pagan-anay ni Aaron a padi ken dagiti annakna a lallaki, tapno makapagserbida a kas papadi.
42 Kulingana na yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa, hivyo ndivyo wana wa Israeli walivyoufanya utumishi wote.
Inaramid ngarud dagiti Israelita ti amin a trabaho kas imbilin ni Yahweh kenni Moises.
43 Naye Musa akaiona ile kazi yote, na, tazama, walikuwa wameifanya kama vile Yahweh alivyokuwa ameamuru. Hivyo ndivyo walivyokuwa wamefanya. Basi Musa akawabariki.
Sinukimat ni Moises ti amin a trabaho, ket, adtoy, naaramidda daytoy. Kas imbilin ni Yahweh, iti dayta a wagas ket naaramidda daytoy. Kalpasanna, binendisionan ida ni Moises.

< Kutoka 39 >