< Kutoka 37 >

1 Bezaleli akafanya Sanduku la mbao za mshita. Mikono miwili na nusu urefu wake, na mkono mmoja na nusu upana wake, na mkono mmoja na nusu kimo chake.
Bezalel hizo el arca de madera de acacia. Su longitud era de dos codos y medio, y su anchura de codo y medio, y su altura de codo y medio.
2 Kisha akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje na kulifanyia ukingo wa dhahabu kulizunguka pande zote.
La recubrió de oro puro por dentro y por fuera, y le hizo una moldura de oro alrededor.
3 Kisha akalitengenezea pete nne za dhahabu, za juu ya miguu yake minne, pete mbili upande wake mmoja na pete mbili upande wake mwingine
Le fundió cuatro anillos de oro en sus cuatro pies: dos anillos en un lado y dos anillos en el otro.
4 Kisha akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
Hizo varas de madera de acacia y las recubrió de oro.
5 Halafu akaitia miti hiyo kwenye zile pete zilizo pande za Sanduku ili kulibeba Sanduku.
Colocó las varas en los anillos a los lados del arca, para transportarla.
6 Naye akafanya kifuniko cha dhahabu safi. Mikono miwili na nusu urefu wake, na mkono mmoja na nusu upana wake.
Hizo un propiciatorio de oro puro. Su longitud era de dos codos y medio, y su anchura de codo y medio.
7 Bezaleli akafanya makerubi wawili wa dhahabu. Kwa kazi ya kufua akawafanya kwenye miisho yote miwili ya kifuniko.
Hizo dos querubines de oro. Los hizo de obra batida, en los dos extremos del propiciatorio:
8 Kerubi mmoja kwenye mwisho ule, na yule kerubi mwingine kwenye mwisho huu. Aliwafanya makerubi juu ya kifuniko kwenye miisho yote miwili.
un querubín en un extremo, y un querubín en el otro extremo. Hizo los querubines de una sola pieza con el propiciatorio en sus dos extremos.
9 Nao wakawa makerubi wanaonyoosha mabawa yao mawili kuelekea juu, wakisitiri kifuniko kwa mabawa yao, nazo nyuso zao zilikuwa zikielekeana. Nyuso za makerubi hao zilielekea kifuniko hicho.
Los querubines extendían sus alas por encima, cubriendo el propiciatorio con sus alas, con sus rostros uno hacia el otro. Los rostros de los querubines estaban hacia el propiciatorio.
10 Bezaleli akafanya meza ya mbao za mshita. Mikono miwili urefu wake, na mkono mmoja upana wake, na mkono mmoja na nusu kimo chake.
Hizo la mesa de madera de acacia. Su longitud era de dos codos, su anchura de un codo y su altura de codo y medio.
11 Halafu akaifunika kwa dhahabu safi na kufanya ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
La recubrió de oro puro y le hizo una moldura de oro alrededor.
12 Kisha akafanya mzingo wa upana wa kiganja kuizunguka na kufanya ukingo wa dhahabu kwa ajili ya mzingo wake kuizunguka pande zote.
Hizo un borde de un palmo de ancho a su alrededor, e hizo una moldura de oro a su alrededor.
13 Tena, akatengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili yake na kuziweka pete hizo kwenye zile pembe nne zilizokuwa kwa ajili ya ile miguu minne.
Le fundió cuatro anillos de oro y los puso en las cuatro esquinas que estaban sobre sus cuatro pies.
14 Pete hizo zilikuwa karibu na ule mzingo, ili kutegemeza ile miti ya kuibeba meza hiyo.
Los anillos estaban cerca del borde, los lugares para las varas para llevar la mesa.
15 Halafu akafanya ile miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu ili kuibeba ile meza.
Hizo las varas de madera de acacia y las recubrió de oro para transportar la mesa.
16 Baada ya hilo akafanya kutokana na dhahabu safi vile vyombo vilivyo juu ya meza, sahani zake na vikombe vyake na mabakuli yake na mitungi yake iliyotumiwa kumimina matoleo ya kinywaji.
Hizo los recipientes que estaban sobre la mesa, sus platos, sus cucharas, sus tazones y sus cántaros para servir, de oro puro.
17 Kisha akafanya kinara cha taa cha dhahabu safi. Kwa kazi ya kufua akakifanya kinara cha taa. Pande zake na matawi yake, vikombe vyake, mafundo yake na maua yake vikatokea kwake.
Hizo el candelabro de oro puro. Hizo el candelabro de obra batida. Su base, su fuste, sus copas, sus capullos y sus flores eran de una sola pieza.
18 Na matawi sita yalikuwa yakitoka kwenye pande zake, matawi matatu ya kinara cha taa kutoka kwenye upande wake mmoja na matawi mengine matatu ya kinara cha taa kutoka kwenye ule upande wake mwingine.
Había seis brazos que salían de sus lados: tres brazos del candelabro salían de un lado, y tres brazos del candelabro salían del otro lado:
19 Vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi vilikuwa kwenye kikundi kimoja cha matawi, vifundo na maua yakifuatana; na vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi vilikuwa kwenye kile kikundi kingine cha matawi, vifundo na maua yakifuatana. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa yale matawi sita yaliyokuwa yakitoka katika kile kinara cha taa.
tres copas hechas como flores de almendro en un brazo, un capullo y una flor, y tres copas hechas como flores de almendro en el otro brazo, un capullo y una flor; así para los seis brazos que salían del candelabro.
20 Na kwenye kile kinara cha taa kulikuwa na vikombe vinne vyenye umbo la maua ya mlozi, vifundo vyake na maua yake yakifuatana.
En el candelabro había cuatro copas hechas como flores de almendro, sus capullos y sus flores;
21 Na kile kifundo chini ya matawi mawili kilitoka kwake, na kifundo kilicho chini ya yale matawi mengine mawili kilitoka kwake, na kifundo kingine kilicho chini ya matawi mengine mawili zaidi kilitoka kwake, kwa ajili ya matawi sita yanayotoka katika kinara.
y un capullo bajo dos ramas de una pieza con él, y un capullo bajo dos ramas de una pieza con él, y un capullo bajo dos ramas de una pieza con él, para las seis ramas que salían de él.
22 Vifundo vyake na matawi yake vilitoka kwake, vyote vilikuwa kitu kimoja cha kazi ya kufua, cha dhahabu safi.
Sus brotes y sus ramas eran de una sola pieza con él. Todo el conjunto era una sola pieza batida de oro puro.
23 Kisha akafanya taa zake saba na mikasi ya tambi zake na vyetezo vyake kutokana na dhahabu safi.
Hizo sus siete lámparas, sus apagadores y sus tabaqueras de oro puro.
24 Alikifanya kwa talanta ya dhahabu safi, hicho pamoja na vyombo vyake vyote.
Lo hizo de un talento de oro puro, con todos sus recipientes.
25 Sasa akafanya madhabahu ya uvumba kutokana na mbao za mshita. Mkono mmoja urefu wake na mkono mmoja upana wake, ikiwa mraba, na mikono miwili kimo chake. Pembe zake zilitoka kwake.
Hizo el altar del incienso de madera de acacia. Era cuadrado: su longitud era de un codo, y su anchura de un codo. Su altura era de dos codos. Sus cuernos eran de una sola pieza.
26 Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, upande wake wa juu na pande zake za kando kuizunguka na pembe zake, naye akafanya ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
Lo recubrió de oro puro: su parte superior, sus lados alrededor y sus cuernos. Hizo una moldura de oro a su alrededor.
27 Naye akaifanyia pete mbili za dhahabu chini ya ukingo wake kwenye pande zake mbili, kwenye pande zake mbili zinazoelekeana, za kutegemeza ile miti ya kuibeba.
Le hizo dos anillos de oro debajo de la corona de la moldura, en sus dos costillas, en sus dos lados, para los lugares de las varas con las que se transportaba.
28 Kisha akafanya ile miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
Hizo las varas de madera de acacia y las recubrió de oro.
29 Tena akafanya yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na ule uvumba safi uliotiwa manukato, kazi ya mtengenezaji wa marhamu.
Hizo el aceite santo de la unción y el incienso puro de especias dulces, según el arte del perfumista.

< Kutoka 37 >