< Kutoka 37 >
1 Bezaleli akafanya Sanduku la mbao za mshita. Mikono miwili na nusu urefu wake, na mkono mmoja na nusu upana wake, na mkono mmoja na nusu kimo chake.
И начини Веселеило ковчег од дрвета ситима, два и по лакта дуг и подруг лакта широк и подруг лакта висок.
2 Kisha akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje na kulifanyia ukingo wa dhahabu kulizunguka pande zote.
И покова га чистим златом изнутра и споља; и начини му златан венац унаоколо.
3 Kisha akalitengenezea pete nne za dhahabu, za juu ya miguu yake minne, pete mbili upande wake mmoja na pete mbili upande wake mwingine
И сали му четири биочуга од злата на четири угла његова: два биочуга с једне стране а два с друге.
4 Kisha akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
И начини полуге од дрвета ситима, и окова их златом.
5 Halafu akaitia miti hiyo kwenye zile pete zilizo pande za Sanduku ili kulibeba Sanduku.
И провуче полуге кроз биочуге с обе стране ковчегу, да се може носити ковчег.
6 Naye akafanya kifuniko cha dhahabu safi. Mikono miwili na nusu urefu wake, na mkono mmoja na nusu upana wake.
И начини заклопац од чистог злата, у дужину од два и по лакта, а у ширину од подруг лакта.
7 Bezaleli akafanya makerubi wawili wa dhahabu. Kwa kazi ya kufua akawafanya kwenye miisho yote miwili ya kifuniko.
И начини два херувима од злата, једноставне начини их, на два краја заклопцу,
8 Kerubi mmoja kwenye mwisho ule, na yule kerubi mwingine kwenye mwisho huu. Aliwafanya makerubi juu ya kifuniko kwenye miisho yote miwili.
Једног херувима на крају одовуд, а другог херувима на крају одонуд; заклопцу на оба краја начини херувиме.
9 Nao wakawa makerubi wanaonyoosha mabawa yao mawili kuelekea juu, wakisitiri kifuniko kwa mabawa yao, nazo nyuso zao zilikuwa zikielekeana. Nyuso za makerubi hao zilielekea kifuniko hicho.
И у херувима беху крила раширена у вис, и заклањаху крилима својим заклопац, и лицем беху окренути један другом, и гледаху према заклопцу херувими.
10 Bezaleli akafanya meza ya mbao za mshita. Mikono miwili urefu wake, na mkono mmoja upana wake, na mkono mmoja na nusu kimo chake.
И начини сто од дрвета ситима, у дужину од два лакта а у ширину од лакта, и од подруг лакта у висину.
11 Halafu akaifunika kwa dhahabu safi na kufanya ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
И покова га чистим златом, и начини му венац златан унаоколо.
12 Kisha akafanya mzingo wa upana wa kiganja kuizunguka na kufanya ukingo wa dhahabu kwa ajili ya mzingo wake kuizunguka pande zote.
И начини му оплату с подланице унаоколо, и начини венац златан уз оплату унаоколо.
13 Tena, akatengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili yake na kuziweka pete hizo kwenye zile pembe nne zilizokuwa kwa ajili ya ile miguu minne.
И сали му четири биочуга од злата, и метну биочуге на четири угла, који му беху на четири ноге.
14 Pete hizo zilikuwa karibu na ule mzingo, ili kutegemeza ile miti ya kuibeba meza hiyo.
Према оплати беху биочузи, а у њима полуге, да се може носити сто.
15 Halafu akafanya ile miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu ili kuibeba ile meza.
А полуге начини од дрвета ситима, и окова их златом, да се може носити сто.
16 Baada ya hilo akafanya kutokana na dhahabu safi vile vyombo vilivyo juu ya meza, sahani zake na vikombe vyake na mabakuli yake na mitungi yake iliyotumiwa kumimina matoleo ya kinywaji.
И начини од чистог злата посуђе што се меће на сто: зделе и чаше и котлиће и ведра, којим ће се преливати.
17 Kisha akafanya kinara cha taa cha dhahabu safi. Kwa kazi ya kufua akakifanya kinara cha taa. Pande zake na matawi yake, vikombe vyake, mafundo yake na maua yake vikatokea kwake.
И начини свећњак од чистог злата, једноставан начини свећњак; ступ му и гране, чашице и јабуке и цветови излажаху из њега.
18 Na matawi sita yalikuwa yakitoka kwenye pande zake, matawi matatu ya kinara cha taa kutoka kwenye upande wake mmoja na matawi mengine matatu ya kinara cha taa kutoka kwenye ule upande wake mwingine.
Шест грана излажаху му са страна; три гране свећњака с једне стране а три гране свећњака с друге стране;
19 Vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi vilikuwa kwenye kikundi kimoja cha matawi, vifundo na maua yakifuatana; na vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi vilikuwa kwenye kile kikundi kingine cha matawi, vifundo na maua yakifuatana. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa yale matawi sita yaliyokuwa yakitoka katika kile kinara cha taa.
Три чашице као бадем на једној грани и јабука и цвет, а три чашице као бадем на другој грани и јабука и цвет; тако на свих шест грана које излажаху из свећњака.
20 Na kwenye kile kinara cha taa kulikuwa na vikombe vinne vyenye umbo la maua ya mlozi, vifundo vyake na maua yake yakifuatana.
А на самом свећњаку беху четири чашице као бадем са својим јабукама и цветовима,
21 Na kile kifundo chini ya matawi mawili kilitoka kwake, na kifundo kilicho chini ya yale matawi mengine mawili kilitoka kwake, na kifundo kingine kilicho chini ya matawi mengine mawili zaidi kilitoka kwake, kwa ajili ya matawi sita yanayotoka katika kinara.
Једна јабука беше под две гране из њега, и једна јабука под друге две гране из њега, и једна јабука под друге две гране из њега; тако под шест грана које излажаху из њега.
22 Vifundo vyake na matawi yake vilitoka kwake, vyote vilikuwa kitu kimoja cha kazi ya kufua, cha dhahabu safi.
Јабуке њихове и гране им излажаху из њега, све беше од чистог злата једноставно.
23 Kisha akafanya taa zake saba na mikasi ya tambi zake na vyetezo vyake kutokana na dhahabu safi.
И начини му седам жижака и усекаче и спремице за гар од чистог злата.
24 Alikifanya kwa talanta ya dhahabu safi, hicho pamoja na vyombo vyake vyote.
Од таланта чистог злата начини га са свим справама његовим.
25 Sasa akafanya madhabahu ya uvumba kutokana na mbao za mshita. Mkono mmoja urefu wake na mkono mmoja upana wake, ikiwa mraba, na mikono miwili kimo chake. Pembe zake zilitoka kwake.
И начини олтар кадиони од дрвета ситима у дужину од једног лакта, и у ширину од једног лакта, четвороугласт, и од два лакта у висину; из њега излажаху му рогови.
26 Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, upande wake wa juu na pande zake za kando kuizunguka na pembe zake, naye akafanya ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
И покова га чистим златом озго и са стране унаоколо, и рогове; и начини му венац од злата унаоколо.
27 Naye akaifanyia pete mbili za dhahabu chini ya ukingo wake kwenye pande zake mbili, kwenye pande zake mbili zinazoelekeana, za kutegemeza ile miti ya kuibeba.
И два биочуга од злата начини му испод венца на два угла његова с обе стране, да у њима стоје полуге да се може носити о њима.
28 Kisha akafanya ile miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
А полуге начини од дрвета ситима, и окова их златом.
29 Tena akafanya yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na ule uvumba safi uliotiwa manukato, kazi ya mtengenezaji wa marhamu.
И начини уље за свето помазање и чисти кад мирисни вештином апотекарском.