< Kutoka 37 >

1 Bezaleli akafanya Sanduku la mbao za mshita. Mikono miwili na nusu urefu wake, na mkono mmoja na nusu upana wake, na mkono mmoja na nusu kimo chake.
And Bezalel made the ark of acacia wood; two cubits and a half was the length of it, and a cubit and a half the breadth of it, and a cubit and a half the height of it.
2 Kisha akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje na kulifanyia ukingo wa dhahabu kulizunguka pande zote.
And he overlaid it with pure gold inside and outside, and made a crown of gold to it round about.
3 Kisha akalitengenezea pete nne za dhahabu, za juu ya miguu yake minne, pete mbili upande wake mmoja na pete mbili upande wake mwingine
And he cast four rings of gold for it, in the four feet of it, even two rings on the one side of it, and two rings on the other side of it.
4 Kisha akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
And he made staves of acacia wood, and overlaid them with gold.
5 Halafu akaitia miti hiyo kwenye zile pete zilizo pande za Sanduku ili kulibeba Sanduku.
And he put the staves into the rings on the sides of the ark, to bear the ark.
6 Naye akafanya kifuniko cha dhahabu safi. Mikono miwili na nusu urefu wake, na mkono mmoja na nusu upana wake.
And he made a mercy-seat of pure gold, two cubits and a half the length of it, and a cubit and a half the breadth of it.
7 Bezaleli akafanya makerubi wawili wa dhahabu. Kwa kazi ya kufua akawafanya kwenye miisho yote miwili ya kifuniko.
And he made two cherubim of gold, of beaten work he made them, at the two ends of the mercy-seat,
8 Kerubi mmoja kwenye mwisho ule, na yule kerubi mwingine kwenye mwisho huu. Aliwafanya makerubi juu ya kifuniko kwenye miisho yote miwili.
one cherub at the one end, and one cherub at the other end, of one piece with the mercy-seat. He made the cherubim at the two ends of it.
9 Nao wakawa makerubi wanaonyoosha mabawa yao mawili kuelekea juu, wakisitiri kifuniko kwa mabawa yao, nazo nyuso zao zilikuwa zikielekeana. Nyuso za makerubi hao zilielekea kifuniko hicho.
And the cherubim spread out their wings on high, covering the mercy-seat with their wings, with their faces one to another. The faces of the cherubim were toward the mercy-seat.
10 Bezaleli akafanya meza ya mbao za mshita. Mikono miwili urefu wake, na mkono mmoja upana wake, na mkono mmoja na nusu kimo chake.
And he made the table of acacia wood, two cubits the length of it, and a cubit the breadth of it, and a cubit and a half the height of it.
11 Halafu akaifunika kwa dhahabu safi na kufanya ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
And he overlaid it with pure gold, and made thereunto a crown of gold round about.
12 Kisha akafanya mzingo wa upana wa kiganja kuizunguka na kufanya ukingo wa dhahabu kwa ajili ya mzingo wake kuizunguka pande zote.
And he made to it a border of a handbreadth round about, and made a golden crown to the border of it round about.
13 Tena, akatengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili yake na kuziweka pete hizo kwenye zile pembe nne zilizokuwa kwa ajili ya ile miguu minne.
And he cast four rings of gold for it, and put the rings in the four corners that were on the four feet of it,
14 Pete hizo zilikuwa karibu na ule mzingo, ili kutegemeza ile miti ya kuibeba meza hiyo.
close by the border were the rings, the places for the staves to bear the table.
15 Halafu akafanya ile miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu ili kuibeba ile meza.
And he made the staves of acacia wood, and overlaid them with gold, to bear the table.
16 Baada ya hilo akafanya kutokana na dhahabu safi vile vyombo vilivyo juu ya meza, sahani zake na vikombe vyake na mabakuli yake na mitungi yake iliyotumiwa kumimina matoleo ya kinywaji.
And he made the vessels which were upon the table, the dishes of it, and the spoons of it, and the bowls of it, and the flagons of it, with which to pour out, of pure gold.
17 Kisha akafanya kinara cha taa cha dhahabu safi. Kwa kazi ya kufua akakifanya kinara cha taa. Pande zake na matawi yake, vikombe vyake, mafundo yake na maua yake vikatokea kwake.
And he made the lampstand of pure gold. He made the lampstand of beaten work, even its base, and its shaft, its cups, its knobs, and its flowers, were of one piece with it.
18 Na matawi sita yalikuwa yakitoka kwenye pande zake, matawi matatu ya kinara cha taa kutoka kwenye upande wake mmoja na matawi mengine matatu ya kinara cha taa kutoka kwenye ule upande wake mwingine.
And there were six branches going out of the sides of it, three branches of the lampstand out of the one side of it, and three branches of the lampstand out of the other side of it,
19 Vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi vilikuwa kwenye kikundi kimoja cha matawi, vifundo na maua yakifuatana; na vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi vilikuwa kwenye kile kikundi kingine cha matawi, vifundo na maua yakifuatana. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa yale matawi sita yaliyokuwa yakitoka katika kile kinara cha taa.
three cups made like almond-blossoms in one branch, a knob and a flower, and three cups made like almond-blossoms in the other branch, a knob and a flower, so for the six branches going out of the lampstand.
20 Na kwenye kile kinara cha taa kulikuwa na vikombe vinne vyenye umbo la maua ya mlozi, vifundo vyake na maua yake yakifuatana.
And in the lampstand were four cups made like almond-blossoms, the knobs of it, and the flowers of it,
21 Na kile kifundo chini ya matawi mawili kilitoka kwake, na kifundo kilicho chini ya yale matawi mengine mawili kilitoka kwake, na kifundo kingine kilicho chini ya matawi mengine mawili zaidi kilitoka kwake, kwa ajili ya matawi sita yanayotoka katika kinara.
and a knob under two branches of one piece with it, and a knob under two branches of one piece with it, and a knob under two branches of one piece with it, for the six branches going out of it.
22 Vifundo vyake na matawi yake vilitoka kwake, vyote vilikuwa kitu kimoja cha kazi ya kufua, cha dhahabu safi.
Their knobs and their branches were of one piece with it. The whole of it was one beaten work of pure gold.
23 Kisha akafanya taa zake saba na mikasi ya tambi zake na vyetezo vyake kutokana na dhahabu safi.
And he made the lamps of it, seven, and the snuffers of it, and the snuff dishes of it, of pure gold.
24 Alikifanya kwa talanta ya dhahabu safi, hicho pamoja na vyombo vyake vyote.
He made it of a talent of pure gold, and all the vessels of it.
25 Sasa akafanya madhabahu ya uvumba kutokana na mbao za mshita. Mkono mmoja urefu wake na mkono mmoja upana wake, ikiwa mraba, na mikono miwili kimo chake. Pembe zake zilitoka kwake.
And he made the altar of incense of acacia wood: a cubit was the length of it, and a cubit the breadth of it, foursquare, and two cubits was the height of it. The horns of it were of one piece with it.
26 Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, upande wake wa juu na pande zake za kando kuizunguka na pembe zake, naye akafanya ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
And he overlaid it with pure gold, the top of it, and the sides of it round about, and the horns of it. And he made to it a crown of gold round about.
27 Naye akaifanyia pete mbili za dhahabu chini ya ukingo wake kwenye pande zake mbili, kwenye pande zake mbili zinazoelekeana, za kutegemeza ile miti ya kuibeba.
And he made for it two golden rings under the crown of it, upon the two ribs of it, upon the two sides of it, for places for staves with which to bear it.
28 Kisha akafanya ile miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
And he made the staves of acacia wood, and overlaid them with gold.
29 Tena akafanya yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na ule uvumba safi uliotiwa manukato, kazi ya mtengenezaji wa marhamu.
And he made the holy anointing oil, and the pure incense of sweet spices, after the art of the perfumer.

< Kutoka 37 >