< Kutoka 36 >

1 Hivyo Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Yahweh aliye mpa ustadi na uwezo kujua jinsi ya kufanya kazi katika ujenzi wa sehemu takatifu wafanye kazi kadiri ya yote Yahweh aliyo amuru.”
Then wrought Bezaleel, and Aholiab, and all cunning men, to whome the Lord gaue wisedome, and vnderstanding, to knowe howe to worke all maner worke for the seruice of the Sanctuarie, according to all that the Lord had commanded.
2 Musa akamuita Bezaleli, Oholiabu, na kila mtu mwenye ujuzi ambaye Yahweh kampa ujuzi, na ambaye moyoni mwake ulichochewa kuja na kufanya kazi.
For Moses had called Bezaleel, and Aholiab, and all the wise hearted men, in whose heartes the Lord had giuen wisedome, euen as many as their hearts encouraged to come vnto that worke to worke it.
3 Walipokea kutoka kwa Musa sadaka zote ambazo Waisraeli walizo leta kwa ujenzi ya sehemu takatifu. Watu walikuwa bado wanaleta sadaka za hiari kila asubui kwa Musa.
And they receiued of Moses all the offering which the children of Israel had brought for the worke of the seruice of the Sanctuary, to make it: also they brought still vnto him free giftes euery morning.
4 Hivyo watu wote walikuwa na ujuzi walikuwa wakifanya kazi sehemu takatifu walikuja kutoka kwenye kazi walikuwa wakifanya.
So all the wise men, that wrought all the holy worke, came euery man from his worke which they wrought,
5 Wachonga mawe walimwabia Musa, “Watu wanaleta zaidi sana ya yanayo itajika kufanya kazi Yahweh aliyo tuamuru.”
And spake to Moses, saying, The people bring too much, and more then ynough for the vse of the worke, which the Lord hath commanded to be made.
6 Hivyo Musa akaamuru mtu yeyote asilete tena kwa ujenzi wa sehemu takatifu. Kisha watu wakaacha kuleta hivi vitu.
Then Moses gaue a commandement, and they caused it to be proclaymed throughout the hoste, saying, Let neither man nor woman prepare any more worke for the oblation of the Sanctuarie. So the people were stayed from offring.
7 Walikuwa na zaidi ya vitu vya ujenzi.
For the stuffe they had, was sufficient for all the worke to make it, and too much.
8 Hivyo wachonga mawe miongoni mwao wakajenga lile hema la kuabudia kwa mapazia kumi yaliyo jengwa kitamba kizuri na buluu, zambarau, na sufu nyekundu kwa aina ya kerubi. Hii ni kazi ya Bezaleli, mjenzi mwenye ujuzi sana.
All the cunning men therefore among the workemen, made for the Tabernacle ten curtaines of fine twined linnen, and of blewe silke, and purple, and skarlet: Cherubims of broydred worke made they vpon them.
9 Urefu wa kila pazia ulikuwa mikono ishirini na nane, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono minne. Vitambaa vyote hivyo vilikuwa na kipimo kimoja.
The length of one curtaine was twentie and eight cubits, and the breadth of one curtaine foure cubites: and the curtaines were all of one cise.
10 Bezaleli akaunganisha vitambaa vitano pamoja, na vile vitambaa vingine vitano akaviunganisha pamoja.
And he coupled fiue curtaines together, and other fiue coupled he together.
11 Kisha akafanya vitanzi vya uzi wa bluu kwenye upindo wa kitambaa kilicho mahali pa kuungania. Akafanya vivyo hivyo kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pale pengine pa kuungania.
And he made strings of blewe silke by the edge of one curtaine, in the seluedge of the coupling: likewise he made on the side of the other curtaine in the seluedge in the second coupling.
12 Akafanya vitanzi hamsini kwenye kitambaa kimoja, akafanya vitanzi hamsini kwenye mwisho wa kitambaa kilichokuwa mahali pale pengine pa kuungania, vitanzi hivyo vikiwa vinaelekeana.
Fiftie strings made he in the one curtaine, and fiftie strings made he in the edge of the other curtaine, which was in the second coupling: the strings were set one against another.
13 Mwishowe akafanya kulabu hamsini za dhahabu na kuviunganisha vitambaa hivyo pamoja kwa kulabu hizo, hivi kwamba hiyo ikawa maskani moja.
After, he made fiftie taches of golde, and coupled the curtaines one to another with the taches: so was it one Tabernacle.
14 Bezaleli akafanya vitambaa vya mahema vya manyoya ya mbuzi kwa ajili ya hema lililo juu ya maskani. Vitambaa kumi na moja ndivyo alivyofanyiza.
Also he made curtaines of goates heare for the couering vpon the Tabernacle: he made them to the nomber of eleuen curtaines.
15 Urefu wa kila kitambaa ulikuwa mikono thelathini, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono minne. Vitambaa hivyo kumi na moja vilikuwa na kipimo kimoja.
The length of one curtaine had thirtie cubites, and the bredth of one curtaine foure cubites: the eleuen curtaines were of one cise.
16 Kisha akaunganisha vitambaa vitano pamoja na vile vitambaa vingine sita pamoja.
And hee coupled fiue curtaines by themselues, and sixe curtaines by themselues:
17 Kisha akafanya vitanzi hamsini kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pa kuungania, naye akafanya vitanzi hamsini kwenye upindo wa kile kitambaa kingine kilichoungana nacho.
Also he made fiftie strings vpon the edge of one curtaine in the seluedge in the coupling, and fiftie strings made hee vpon the edge of the other curtaine in the second coupling.
18 Bezaleli akafanya kulabu hamsini za shaba kwa ajili ya kuliunganisha hilo hema pamoja liwe kipande kimoja.
He made also fiftie taches of brasse to couple the couering that it might be one.
19 Naye akafanya kifuniko cha hema kutokana na ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu na kifuniko kutokana na ngozi za sili, upande wa juu.
And he made a couering vpon the pauilion of rams skinnes dyed red, and a couering of badgers skinnes aboue.
20 Bezaleli akafanya viunzi vya mbao vya hema ya kukutani kutokana na mbao za mshita.
Likewise he made the boards for the Tabernacle, of Shittim wood to stand vp.
21 Urefu wa kiunzi ulikuwa mikono kumi, nao upana wa kila kiunzi ulikuwa mkono mmoja na nusu.
The length of a board was ten cubites, and the bredth of one board was a cubite, and an halfe.
22 Kila kiunzi kilikuwa na ndimi mbili zilizounganishwa. Hivyo ndivyo alivyofanya viunzi vyote vya maskani.
One board had two tenons, set in order as the feete of a ladder, one against another: thus made he for all the boardes of the Tabernacle.
23 Basi akafanya viunzi vya maskani, viunzi ishirini kwa ajili ya upande kuelekea kusini.
So he made twentie boardes for the South side of the Tabernacle, euen full South.
24 Bezaleli akafanya vikalio arobaini vya fedha viwe chini ya vile viunzi ishirini, vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja pamoja na ndimi zake mbili na vikalio vingine viwili chini ya kiunzi kingine pamoja na ndimi zake mbili.
And fourtie sockets of siluer made he vnder the twentie boardes, two sockets vnder one board for his two tenons, and two sockets vnder another board for his two tenons.
25 Na kwa ajili ya ule upande mwingine wa maskani, upande wa kaskazini, akafanya viunzi ishirini
Also for the other side of the Tabernacle toward the North, he made twentie boards,
26 na vikalio vyake arobaini vya fedha. Vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja na vikalio viwili chini ya kiunzi kingine
And their fourtie sockets of siluer, two sockets vnder one board, and two sockets vnder another boarde.
27 Na kwa ajili ya zile pande za nyuma za maskani kuelekea magharibi akafanya viunzi sita.
Likewise toward the Westside of the Tabernacle he made sixe boardes.
28 Naye akafanya viunzi viwili vya pembeni ya maskani kwenye pande zake mbili za nyuma
And two boardes made he in the corners of the Tabernacle, for either side,
29 Hizi zilikuwa pacha upande wa chini, lakini juu ya kila moja kwenye pete ya kwanza. Hivyo ndivyo alivyoifanya yote miwili, ile miimo ya pembeni.
And they were ioyned beneath, and likewise were made sure aboue with a ring: thus he did to both in both corners.
30 Basi vikajumlika kuwa viunzi vinane na vikalio vyake kumi na sita vya fedha, vikalio viwili kando ya vikalio viwili chini ya kila kiunzi.
So there were eight boards and their sixteene sockets of siluer, vnder euery board two sockets.
31 Bezaleli akafanya miti ya mshita, mitano kwa ajili ya viunzi vya upande mmoja wa maskani,
After, he made barres of Shittim wood, fiue for the boards in ye one side of ye Tabernacle,
32 na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya upande ule mwingine wa maskani na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya maskani kwa ajili ya zile pande mbili za nyuma za magharibi.
And fiue barres for the boardes in the other side of the Tabernacle, and fiue barres for the boards of the Tabernacle on the side toward the West.
33 Kisha akafanya mti wa katikati upitie katikati ya vile viunzi toka mwisho mmoja mpaka ule mwingine.
And he made the middest barre to shoote through the boards, from the one end to ye other.
34 Naye akavifunika vile viunzi kwa dhahabu, akafanyiza pete zake za dhahabu ziwe vitegemezo kwa ajili ya ile miti, akaifunika ile miti kwa dhahabu.
He ouerlayd also the boards with gold, and made their rings of gold for places for the barres, and couered the barres with golde.
35 Bezaleli akafanya pazia, la uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa cha rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kalitia makerubi kwa kazi ya mjenzi.
Moreouer he made a vaile of blew silke, and purple, and of skarlet, and of fine twined linen: with Cherubims of broydred worke made he it:
36 Kisha akalifanyia nguzo nne za mshita na kuzifunika kwa dhahabu, vibanio vyake vikiwa vya dhahabu, na kutengeneza vikalio vinne vya fedha kwa ajili yake.
And made thereunto foure pillars of Shittim, and ouerlayd them with golde: whose hookes were also of golde, and hee cast for them foure sockets of siluer.
37 Naye akafanya kisitiri kwa ajili ya mwingilio wa hema kutokana na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kazi ya mfumaji.
And he made an hanging for the Tabernacle doore, of blew silke, and purple, and skarlet, and fine twined linnen, and needle worke,
38 Pia akafanya na nguzo zake tano na vibanio vyake. Naye akavifunika vilele vyake na viungo vyake kwa dhahabu, lakini vile vikalio vyake vitano vilikuwa vya shaba.
And the fiue pillars of it with their hookes, and ouerlayde their chapiters and their filets with golde, but their fiue sockets were of brasse.

< Kutoka 36 >