< Kutoka 35 >

1 Musa akawakusanya jamii yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndio mambo Yahweh aliyo waamuru mfanye.
And all the multitude of the children of Israel being gathered together, he said to them: These are the things which the Lord hath commanded to be done.
2 Kwa siku sita kazi ya weza fanywa, lakini kwako, siku ya saba lazima iwe siku takatifu, siku ya Sabato ya mapumziko, takatifu kwa Yahweh. Yeyote atakaye fanya kazi hiyo siku lazima auawe.
Six days you shall do work: the seventh day shall be holy unto you, the sabbath, and the rest of the Lord: he that shall do any work on it, shall be put to death.
3 Haupaswi kuwasha moto kwenye nyumba zenu siku ya Sabato.”
You shall kindle no fire in any of your habitations on the sabbath day.
4 Musa akasema na jamii yote ya Waisraeli, kwa kusema, “Hichi ndicho kitu Yahweh alicho amuru.
And Moses said to all the assembly of the children of Israel: This is the word the Lord hath commanded, saying:
5 Chukuwa sadaka kwa ajili ya Yahweh, wote wenye moyo mkunjufu. Leta sadaka kwa Yahweh - dhahabu, fedha, shaba,
Set aside with you firstfruits to the Lord. Let every one that is willing and hath a ready heart, offer them to the Lord: gold, and silver, and brass,
6 buluu, zambarau, sufu nyekundu na kitambaa kizuri; nywele za mbuzi;
Violet and purple, and scarlet twice dyed, and fine linen, goats’ hair,
7 ngozi za kondoo zilizotiwa rangi nyekundu na ngozi za pomboo; na mbao za mshita;
And rams’ skins dyed red, and violet coloured skins, setim wood,
8 mafuta ya taa kwa pahali patakatifu, viungo vya manukato kwa hayo mafuta ya kutiwa,
And oil to maintain lights, and to make ointment, and most sweet incense.
9 kwa uvumba mzuri na vito vya shohamu na vito vya kutiwa kwa hiyo naivera, na kwa hicho kifuko cha kifuani.
Onyx stones, and precious stones, for the adorning of the ephod and the rational.
10 Kila mwanaume mwenye ustadi kati yenu aje na afanye kila kitu ambacho Yahweh aliyaamuru —
Whosoever of you is wise, let him come, and make that which the Lord hath commanded:
11 hema la kuabudia, na kifuniko chake, na vifungo vyake, na mbao zake, nguzo, na sakafu;
To wit, the tabernacle and the roof thereof, and the cover, the rings, and the board work with the oars, the pillars, and the sockets:
12 pia sanduku na nguzo zake, kiti cha rehema, na pazia la kusitiri.
The ark and the staves, the propitiatory, and the veil that is drawn before it:
13 Walileta meza na miguu yake, vyombo vyake vyote, na mkate wa wonyesho;
The table with the bars and the vessels, and the loaves of proposition:
14 kinara cha taa, vyombo vyake, taa, na mafuta ya zile taa;
The candlestick to bear up the lights, the vessels thereof and the lamps, and the oil for the nourishing of fires:
15 ile madhabahu ya uvumba na nguzo zake, mafuta ya upako na uvumba ulitiwa maukato; kishikizo cha mwingilio wa hema ya kuabudia;
The altar of incense, and the bars, and the oil of unction and the incense of spices: the hanging at the door of the tabernacle:
16 madhabahu ya sadaka ya kuteketeza na kitunzi cha shaba na nguzo na vyombo; na ile beseni kubwa na sakafu yake.
The altar of holocaust, and its grate of brass, with the bars and vessels thereof: the laver and its foot:
17 Walileta vishikizo kwa ajili ya nyuani na nguzo zake na sakafu yake, na pazia kwa ajili mwingilio wa nyauni;
The curtains of the court with the pillars and the sockets, the hanging in the doors of the entry,
18 na ile misumari ya hema la kuabudia na nyuani, pamoja na kamba zake.
The pins of the tabernacle and of the court with their little cords:
19 Walileta mavazi yaliyofumwa kutumikia sehemu takatifu, mavazi takatifu ya Aruni kuhani na wanae, kwa wao kutumika kama makuhani.”
The vestments that are to be used in the ministry of the sanctuary, the vesture of Aaron the high priest, and of his sons, to do the office of priesthood to me.
20 Kisha makabila yote ya Israeli yakaondoka na kwenda kutoka uweponi mwa Musa.
And all the multitude of the children of Israel going out from the presence of Moses,
21 Kila mtu moyo wake ulimchochea na aliye andaliwa na roho yake alikuja na kuleta sadaka kwa Yahweh kwa matengenezo ya hema ya kuabudia, kwa vitu vyote kwajili ya huduma ndani yake, na kwa vazi takatifu.
Offered firstfruits to the Lord with a most ready and devout mind, to make the work of the tabernacle of the testimony. Whatsoever was necessary to the service, and to the holy vestments,
22 Walikuja, wote wanaume kwa wanawake, wote waliokuwa na moyo wa utayari. Walileta madini, hereni, pete, na vitu vya thamani, vitu vyote tofauti vyenye madini ya dhahabu. Waliwasilisha sadaka za dhahabu kama sadaka ya kupunga kwa Yahweh.
Both men and women gave bracelets and earrings, rings and tablets: every vessel of gold was set aside to be offered to the Lord.
23 Kila mmoja alikuwa na sufu ya buluu, dhambarau, au nyekundu, nguo nzuri, singa za mbuzi, ngozi za kondoo zilizobadili kuwa nyekundu, na ngozi ya pomboo walivileta.
If any man had violet, and purple, and scarlet twice dyed, fine linen and goats’ hair, rams’ skins dyed red, and violet coloured skins,
24 kila mmoja alitengeneza sadaka ya fedha au shaba walizileta kama sadaka kwa Yahweh, na kila mmoja aliyekuwa na mti wa mshita kwa matumizi ya kazi aliuleta.
Metal of silver and brass, they offered it to the Lord, and setim wood for divers uses.
25 kila mwanamke mwenye ustadi walisokota sufu kwa mikono yao na walileta sufu walizosokota za buluu, dhambarau, au sufu nyekundu, au nguo nzuri.
The skillful women also gave such things as they had spun, violet, purple, and scarlet, and fine linen,
26 Wanawake wote wenye mioyo iliyochochewa na walio na ustadi walisokota singa za mbuzi.
And goats’ hair, giving all of their own accord.
27 Viongozi walileta mawe ya shohamu na mawe mengine kwaajili ya kuwekwa kwenye hiyo naivera na hicho kifuko cha kifuani;
But the princes offered onyx stone, and precious stones, for the ephod and the rational,
28 walileta viungo na mafuta kwaajili ya taa, kwa mafuta ya upako, na kwa uvumba wa manukato.
And spices and oil for the lights, and for the preparing of ointment, and to make the incense of most sweet savour.
29 Waisraeli walileta sadaka ya hiyari kwa Yahweh; kila mwanaume na mwanamke ambao mioyo yao ilikuwa tayari walileta vifaa kwaajili kazi zote ambazo Yahweh aliamuru kupitia Musa zifanyike.
All both men and women with devout mind offered gifts, that the works might be done which the Lord had commanded by the hand of Moses. All the children of Israel dedicated voluntary offerings to the Lord.
30 Musa alisema kwa waisraeli, “Tazama, Yahweh ameita kwa jina juu ya Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huri, kutoka kabila la Yuda.
And Moses said to the children of Israel: Behold the Lord hath called by name Beseleel the son of Uri the son of Hur of the tribe of Juda.
31 Aliijaza Bezaleli kwa Roho yake, kumpa hekima, uwelewa, na maarifa, kwa aina zote za ujenzi,
And hath filled him with the spirit of God, with wisdom and understanding and knowledge and all learning.
32 kufanya sanaa ya ubunifu na kufanya kazi za dhahabu, shaba, na shaba;
To devise and to work in gold and silver and brass,
33 pia kukata na kupanga mawe na mbao iliochongwa- kufanya kazi za aina zote kwa ubunifu na ujenzi.
And in engraving stones, and in carpenters’ work. Whatsoever can be devised artificially,
34 Aliiweka kufundisha ndani ya moyo wake, yeye pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, kutoka kabila la Dani.
He hath given in his heart: Ooliab also the son of Achisamech of the tribe of Dan:
35 Aliwajaza kwa ustadi wa kufanya kazi za aina zote, kufanya kazi ya kama kuchora mawe, kama mwerevu, kama mtia taraza katika nyuzi za rangu ya buluu, dhambarau, na nyekundu na nguo nzuri, na kama washonaji. Walikuwa wachonga mawe wa kazi zote, na walikuwa wabunifu wa sanaa.
Both of them hath he instructed with wisdom, to do carpenters’ work and tapestry, and embroidery in blue and purple, and scarlet twice dyed, and fine linen, and to weave all things, and to invent all new things.

< Kutoka 35 >