< Kutoka 34 >
1 Yahweh akamwabia Musa, “Kata mbao mbili za mawe kama zile za awali. Nitaandika kwenye hizi mbao za mawe maneno yaliyo kuwa kwenye mbao za mawe za mwanzo, mbao za mawe ulizo zivunja.
Yahweh said to Moses, “Cut two tablets of stone like the first tablets. I will write on these tablets the words that were on the first tablets, the tablets that you broke.
2 Kuwa tayari asubui na uje Mlima Sinai, na uje mbele zangu juu ya mlima.
Be ready by morning and come up Mount Sinai, and present yourself there to me on the mountain top.
3 Hakuna atakaye kuja nawe. Usiruhusu mtu yeyote aonekana popote kwenye mlima. Hakuna kundi la mifugo wanao ruhusiwa ata kula mbele ya mlima.”
No one is to come up with you. Do not let anyone else be seen anywhere on the mountain. No flocks or herds are even to graze in front of the mountain.”
4 Hivyo Musa akakata mbao mbili za mawe kama za mwanzo, na akaamka asubui mapema na kwenda juu ya Mlima Sinai, kama Yahweh alivyo muelekeza. Musa alibeba mbao za mawe mikononi mwake.
So Moses cut two tablets of stone like the first ones, and he got up early in the morning and went up Mount Sinai, as Yahweh had instructed him. Moses carried the tablets of stone in his hand.
5 Yahweh akaja chini katika wingu na akasima mbele za Musa, na akatamka jina “Yahweh.”
Yahweh came down in the cloud and stood with Moses there, and he pronounced the name “Yahweh.”
6 Yahweh akapita kwake na kukiri, “Yahweh, Yahweh, Mungu ni wa rehema na wa neema, sio mwepesi wa hasira, na anadumu katika uwaminifu wa agano na uadilifu,
Yahweh passed by before him and proclaimed, “Yahweh, Yahweh, God is merciful and gracious, slow to anger, and abounding in covenant faithfulness and trustworthiness,
7 ukishika uaminifu wa agano kwa vizazi maelfu, ukisamehe maasi, makosa, na dhambi. Lakini hamsafishi mwenye hatia. Ataleta adhabu ya dhambi za baba kwa watoto wao na watoto wa watoto wao, kwa kizazi cha tatu na hadi cha nne.”
keeping covenant faithfulness for thousands of generations, forgiving iniquities, transgressions, and sins. But he will by no means clear the guilty. He will bring the punishment for the fathers' sin on their children and on their children's children, as far as the third and fourth generations.”
8 Musa haraka akainamisha kichwa chake kwenye ardhi na kuabudu.
Moses quickly bowed his head to the ground and worshiped.
9 Kisha akasema, “Kama sasa nimepata upendeleo machoni pako, Bwana wangu, tafadhali nenda pamoja nasi, kwa kuwa hawa watu ni wa korofi. Samehe maasi yetu na dhambi zetu, na utuchukuwe kama urithi wako.”
Then he said, “If now I have found favor in your eyes, my Lord, please go among us, for this people is stubborn. Pardon our iniquity and our sin, and take us as your inheritance.”
10 Yahweh akasema, “Ona, ninakaribu kufanya agano. Mbele za watu wako, nitafanya maajabu ambayo hayajawai kufanywa duniani kote wala kwenye taifa lote. Watu wote miongoni mwako wataona matendo yangu, kwa kuwa ni kitu cha hofu ninacho fanya kwako.
Yahweh said, “See, I am about to make a covenant. Before all your people, I will do marvels such as have not been done in all the earth nor in any nation. All the people among you will see my deeds, for it is a fearful thing that I am doing with you.
11 Tii amri zangu leo. Ninawaondoa mbele yako Waamori, Wakanani, Wahivi, Wahiti, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.
Obey what I command you today. I am about to drive out before you the Amorites, Canaanites, Hittites, Perizzites, Hivites, and Jebusites.
12 Kuwa mwanglifu usifanye agano na wakazi wa nchi unayo kwenda, au wata kuwa mtego kwako.
Be careful not to make a covenant with the inhabitants of the land where you are going, or they will become a trap among you.
13 Badala yake, lazima uvunje madhabahu zao, ponda nguzo zao za mawe, na kukata nguzo zao za Ashera.
Instead, you must break down their altars, smash their stone pillars, and cut down their Asherah poles.
14 Kwa kuwa wewe haupaswi kumuabudu mungu mwingine, maana Yahweh, ambaye jina lake ni Uwivu, ni Mungu wa uwivu.
For you must worship no other god, for Yahweh, whose name is Jealous, is a jealous God.
15 Hivyo kuwa mwangalifu usifanye agano na wakazi wa nchi, kwa kuwa wanajifanyia ukahaba kwa miungu yao, na wanatoa dhabihu kwa miungu yao. Kisha mmoja wao ata kukaribisha na wewe utakula baadhi ya dhabihu zake,
So be careful not to make a covenant with the inhabitants of the land, for they prostitute themselves to their gods, and they sacrifice to their gods. Then one of them will invite you and you will eat some of his sacrifice,
16 na kisha utachukuwa baadhi ya mabinti zake kwa wanao, na mabinti wake watafanya ukahaba kwa miungu yao, na watafanya wanao kufanya ukahaba kwa miungu yao.
and then you will even take some of his daughters for your sons, and his daughters will prostitute themselves to their gods, and they will make your sons prostitute themselves to their gods.
17 Usifanye Miungu ya chuma ya kuyayusha.
Do not make for yourselves gods of molten metal.
18 Laziam ushike Sherehe ya Mkate Usiotiwachachu. Kama nilivyo kuamuru, lazima ule mkate usio na hamira kwa siku saba kwa muda uliotengwa wa mwezi wa Abibu, maana nikatika mwezi wa Abibu ulitoka Misri.
You must keep the Festival of Unleavened Bread. As I commanded you, you must eat bread without yeast for seven days at the fixed time in the month of Aviv, for it was in the month of Aviv you came out from Egypt.
19 Wazaliwa wote ni mwangu, ata mzaliwa wa kwanza wa kiume wa mifugo, yote ya ng'ombe na kondoo.
All the firstborn are mine, even every male firstborn of your cattle, both of oxen and sheep.
20 Lazima umnunue tena mzaliwa kwanza wa punda kwa kondoo, lakini usipo mnunua tena, kisha uivunje shingo yake. Lazima ununue tena wazaliwa wa kwanza wote wa wanao. Hakuna ata mmoja atakye kuja kwangu mikono mitupu.
You must buy back the firstborn of a donkey with a lamb, but if you do not buy it back, then you must break its neck. You must buy back all the firstborn of your sons. No one may appear before me empty-handed.
21 Utafanya kazi kwa siku sita, lakini siku ya saba utapumzika. Ata wakati wakilimo na wa mavuno, lazima upumzike.
You may work for six days, but on the seventh day you must rest. Even at plowing time and in harvest, you must rest.
22 Lazima uadhimishe Sherehe ya Majuma kwa mazao ya kwanza ya mavuno ya ngano, na lazima uadhimishe Sherehe ya Makusanyo mwisho wa mwaka.
You must observe the Festival of Weeks with the first yield of the wheat harvest, and you must observe the Festival of Ingathering at the year's end.
23 Mara tatu kwa mwaka wanaume wenu wote watajitokeza kwa Bwana Yahweh, Mungu wa Israeli.
Three times a year all your men must appear before Lord Yahweh, the God of Israel.
24 Kwa kuwa nitaondoa mataifa mbele yenu na kutanua mipika. Hakuna atakaye tamani kuwa na ardhi yenu kama yao utakapo toka mbele za Yahweh mara tatu kwa mwaka.
For I will drive out nations before you and expand your borders. No one will desire to have your land as their own when you go up to appear before Yahweh your God three times in a year.
25 Hautatoa damu ya dhabihu yangu na hamira yeyote, wala nyama yeyote kutoka dhabihu za Sherehe ya Pasaka kubaki hadi asubui.
You must not offer the blood of my sacrifice with any yeast, nor may any meat from the sacrifice at the Festival of the Passover be left over to the morning.
26 Lazima ulete matunda ya kwanza yalio bora kutoka nyumbani kwako. Usimchemshe mbuzi mtoto katika maziwa ya mama yake.”
You must bring the best of the firstfruits from your fields to my house. You must not boil a young goat in its mother's milk.”
27 Yahweh akamwabia Musa, “Andika chini haya maneno, kwa kuwa nimejiahidi haya maneno niliyo yasema, na nimefanya agano kwako na Israeli.”
Yahweh said to Moses, “Write down these words, for in accordance with these words I have made a covenant with you and with Israel.”
28 Musa alikuwa huko na Yahweh kwa siku arobaini na usiku; hakula chakula chochote wala kunywa maji yeyote. Aliandika katika mbao maneno ya agano, Amri kumi.
Moses was there with Yahweh for forty days and nights; he did not eat any food nor drink any water. He wrote on the tablets the words of the covenant, the Ten Commandments.
29 Musa alipo shuka chini ya Mlima Sinai na mbao mbili za agano za ushuhuda mikononi mwake, hakujua kuwa ngozi ya kuwa uso wake ulikuwa wa'ngaa akizungumza na Mungu.
When Moses came down from Mount Sinai with the two tablets of the covenant decrees in his hand, he did not know that the skin of his face had become radiant while speaking with God.
30 Wakati Aruni na Waisraeli walipo muona Musa, ngozi ya uso wake ulikuwa wa ng'aa, na waliogopa kuja karibu yake.
When Aaron and the Israelites saw Moses, the skin of his face was shining, and they were afraid to come near him.
31 Lakini Musa aliwaita, na Aruni na viongozi wa jamii wakaja kwake. Kisha Musa akasema nao.
But Moses called to them, and Aaron and all the leaders of the community came up to him. Then Moses spoke with them.
32 Baada ya haya, watu wote wa Israeli wakaja kwa Musa, na akawambia amri zote Yahweh alizo mpa katika Mlima Sinai.
After this, all the people of Israel came up to Moses, and he told them all the commands that Yahweh had given him on Mount Sinai.
33 Musa alipo maliza kuzungumza nao, alifunika uso wake kwa kitambaa.
When Moses had finished speaking with them, he put a veil over his face.
34 Wakati Musa alipoenda mbele za Yahweh kusema naye, aliondoa kitambaa, hadi alipo toka. Alipo toka, aliwaambia Waisraeli alicho amriwa kusema.
Whenever Moses went before Yahweh to speak with him, he would remove the veil, until he came out. When he came out, he would tell the Israelites what he was commanded to say.
35 Waisraeli walipo muona Musa ana'ngaa uso, alirudisha kitambaa tena usoni mpaka alipokuwa anaenda kuongea na Yahweh.
When the Israelites saw Moses' face shining, he would put the veil over his face again until he went back in to speak with Yahweh.