< Kutoka 32 >
1 Hata watu walipoona ya kuwa Musa amekawia kushuka katika mlima, wakakusanyana wakamwendea Aruni, wakamwambia, “Njoo, katufanyizie sanamu itakayokwenda mbele yetu, kwa maana Musa huyo aliyetutoa katika nchi ya Misri hatujui yaliyompata.”
Cependant le peuple voyant le retard que mettait Moïse à descendre de la montagne, et s’étant assemblé contre Aaron, dit: Lève-toi, fais-nous des dieux qui nous précèdent; car pour Moïse, cet homme qui nous a retirés de la terre d’Egypte, nous ignorons ce qui lui est arrivé.
2 Hivyo Aruni akawaambia, “Zitoeni pete za dhahabu zilizo katika masikio ya wake zenu, na wana wenu, na binti zenu, mkaniletee.”
Et Aaron leur répondit: Otez les pendants d’or des oreilles de vos femmes, de vos fils et de vos filles, et apportez-les-moi.
3 Watu wote wakavua pete za dhahabu zilizo katika masikio yao, na wakamletea Aruni.
Et le peuple fit ce qu’il avait commandé, portant les pendants d’oreilles à Aaron.
4 Akapoke mikononi mwao akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha. Nao wakasema, “Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.”
Lorsque celui-ci les eut reçus, il les jeta en fonte, et il en fit un veau de fonte: alors ils dirent: Voici tes dieux, ô Israël, qui t’ont retiré de la terre d’Egypte.
5 Naye Haruni alipoona jambo hili, akajenga madhabahu mbele yake; Aruni akatangaza akasema,
Ce qu’ayant vu Aaron, il bâtit un autel devant le veau, et il cria par la voix d’un héraut: Demain est une solennité du Seigneur.
6 “Kesho itakuwa sikukuu kwa Yahweh.” Wakaondoka asubuhi na mapema, wakatoa dhabihu, wakaleta sadaka za amani, watu wakaketi kula na kunywa, wakaondoka wacheze.
Et, se levant le matin, ils offrirent des holocaustes et des hosties pacifiques, et le peuple s’assit pour manger et pour boire, et ils se levèrent pour jouer.
7 Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Shuka upesi, kwa maana watu wako uliowatoa katika nchi ya Misri wamejiharibu nafsi zao.
Mais le Seigneur parla à Moïse, disant: Va, descends: il a péché, ton peuple que tu as retiré de la terre d’Egypte.
8 Wamepotoka upesi kuiacha ile njia niliyowaamuru, wamejifanyizia ndama ya kuyeyusha wakaiabudu na kuitolea dhabihu. Wakasema, 'Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.
Ils se sont bientôt écartés de la voie que tu leur as montrée: ils se sont fait un veau de fonte, et ils l’ont adoré; puis lui immolant des hosties, ils ont dit: Voici tes dieux, ô Israël, qui t’ont retiré de la terre d’Egypte.
9 Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu.
Et de nouveau le Seigneur dit à Moïse; Je vois que ce peuple est d’un cou roide;
10 Basi sasa usinizuie. Ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize. Nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.”
Laisse-moi, afin que ma fureur s’irrite contre eux, et que je les extermine; et je te ferai chef d’une grande nation.
11 Musa akamsihi sana Yahweh Mungu wake, na kusema,”Yahweh, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu?
Mais Moïse priait le Seigneur son Dieu, disant: Pourquoi, Seigneur, votre fureur s’indigne-telle contre votre peuple que vous avez retiré de la terre d’Egypte, avec une grande puissance, et une main forte?
12 Kwa nini Wamisri kusema, 'Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi?' Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako.
Que les Egyptiens, je vous prie, ne disent pas: C’est par ruse qu’il les a retirés, afin de les tuer sur les montagnes, et les exterminer de la terre: que votre colère s’apaise et laissez-vous fléchir sur la méchanceté de votre peuple.
13 Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, 'Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele.'”
Souvenez-vous d’Abraham, d’Isaac et d’Israël vos serviteurs auxquels vous avez juré par vous-même, disant: Je multiplierai votre postérité comme les étoiles du ciel; et toute cette terre dont je vous ai parlé, je la donnerai à votre postérité, et vous la posséderez toujours.
14 Na Yahweh akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake.
Et le Seigneur s’apaisa, et il ne fit pas à son peuple le mal qu’il avait dit.
15 Kisha Musa akageuka akashuka katika mlima, na zile mbao mbili za mawe mikononi mwake. Mbao zilizoandikwa pande zote mbili, upande huu na upande huu ziliandikwa.
Ainsi, Moïse retourna de la montagne, portant en sa main les deux tables du témoignage écrites des deux côtés,
16 Na zile mbao zilikuwa kazi ya Mungu nayo maandiko yalikuwa maandiko ya Mungu, yaliyochorwa katika zile mbao.
Et faites par l’œuvre de Dieu; l’écriture aussi, gravée sur les tables, était de Dieu.
17 Na Yoshua aliposikia kelele za watu walipokuwa wakipiga kelele, akamwambia Musa, “Kuna kelele ya vita kambini.
Or, Josué entendant le tumulte du peuple qui vociférait, dit à Moïse: On entend des cris de combat dans le camp.
18 “Lakini Musa akasema, “Hiyo si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushinda vitani, wala si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushindwa; bali kelele za watu waimbao ndizo ninazozisikia mimi.”
Moïse répondit: Ce n’est point là le cri de ceux qui s’exhortent au combat, ni les vociférations de ceux qui poussent leurs ennemis à la fuite; mais c’est la voix de gens qui chantent, que moi j’entends.
19 Hata alipoyakaribia kambini akaiona ile ndama, na watu wakicheza. Hasira ya Musa ikawaka. Akazitupa zile mbao mikononi mwake, akazivunja chini ya mlima.
Et lorsqu’il se fut approché du camp, il vit le veau et les danses; alors très irrité, il jeta les tables qu’il tenait à la main, et les rompit au pied de la montagne;
20 Akaitwaa ile ndama waliyoifanya, akaichoma moto, akaisaga hata ikawa mavumbi, akainyunyiza juu ya maji. Akawanywesha wana wa Israeli.
Puis saisissant le veau qu’ils avaient fait, il le brûla, et le brisa jusqu’à le réduire en poudre, qu’il répandit dans l’eau, et il donna de cette poudre à boire aux enfants d’Israël.
21 Musa akamwambia Aruni, “Watu hawa wamekufanyani hata ukaleta dhambi hii kuu juu yao?
Il dit ensuite à Aaron: Que t’a fait ce peuple, pour que tu attirasses sur lui un très grand péché?
22 Aruni akasema, “Hasira yako isiwake, bwana wangu. Wewe unawajua watu hawa, ya kuwa wamejielekeza kwa mabaya.
Aaron lui répondit: Que mon Seigneur ne soit pas indigné; car tu connais ce peuple; tu sais qu’il est porté au mal:
23 Maana waliniambia, 'Katufanyie miungu, itakayokwenda mbele yetu. Kwa maana mtu huyo Musa, aliyetutoa katika nchi ya Misri, hatujui yaliyompata.'
Ils m’ont dit: Fais-nous des dieux qui nous précèdent; car pour ce Moïse qui nous a retirés de la terre d’Egypte, nous ne savons ce qui lui est arrivé.
24 Nikawaambia, 'Mtu ye yote aliye na dhahabu na aivue; basi wakanipa, nami nikaitupa ndani ya moto, akatoka ndama huyu.”
Moi, je leur ai dit: Qui de vous a de l’or? Ils l’ont apporté et me l’ont donné; et je l’ai jeté dans le feu, et il en est sorti ce veau.
25 Basi Musa alipoona ya kuwa watu hawa wameasi (maana Haruni amewaacha waasi, ili wawe dhihaka kati ya adui zao)
Moïse voyant donc que le peuple avait été mis nu (car Aaron l’avait dépouillé pour une ignominie d’ordure, et l’avait mis nu au milieu de ses ennemis),
26 Ndipo Musa akasimama katika mlango wa marago, akasema, “Mtu awaye yote aliye upande wa Yahweh na aje kwangu.” Wana wa Lawi wote wakamkusanyikia.
Et se tenant à la porte du camp, dit: Si quelqu’un est au Seigneur, qu’il se joigne à moi. Et tous les enfants de Lévi se réunirent auprès de lui;
27 Akawaambia, Yahweh, Mungu wa Israeli, asema hivi, 'Kila mtu na ajifunge upanga wake pajani mwake, akapite huko na huko toka mlango hata mlango kati ya marago, mkamchinje kila mtu ndugu yake, na kila mtu mwenziwe na kila mtu jirani yake.'”
Il leur dit: Voici ce que dit le Seigneur Dieu d’Israël: Que chaque homme mette un glaive sur sa cuisse: allez et revenez d’une porte à l’autre au travers du camp, et que chacun lue son frère, son ami, et celui qui lui est le plus proche.
28 Na hao wana wa Lawi wakafanya kama vile alivyosema Musa, wakaanguka siku ile kama watu elfu tatu.
Et les fils de Lévi firent selon la parole de Moïse, et il tomba en ce jour-là environ vingt-trois mille hommes.
29 Musa akasema, Jiwekeni wakfu kwa Yahweh leo, kila mtu juu ya mwanawe na juu ya ndugu yake; ili Yahweh awape baraka leo.”
Alors Moïse dit: Vous avez consacré aujourd’hui vos mains au Seigneur, chacun sur son fils et sur son frère, afin que vous soit donnée une bénédiction.
30 Hata asubuhi yake Musa akawaambia watu, “Mmetenda dhambi kuu. Sasa nitakwenda juu kwa Yahweh. Labda nitafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu.”
Mais le jour suivant arrivé, Moïse parla au peuple, disant: Vous avez commis un très grand péché; je monterai vers le Seigneur, pour voir si je pourrai en quelque manière détourner le châtiment de votre crime.
31 Musa akarejea kwa Yahweh akasema,” Oh! Watu hawa wametenda dhambi kuu wamejifanyia miungu ya dhahabu.
Et étant retourné vers le Seigneur, il dit: Je vous conjure, ce peuple a commis un très grand péché, ils se sont fait des dieux d’or: ou remettez-leur cette faute,
32 Walakini sasa, ikiwa utawasamehe dhambi yao – na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichoandika.”
Ou, si vous ne le faites pas, effacez-moi de votre livre que vous avez écrit.
33 Yahweh akamwambia Musa, “Mtu ye yote aliyenitenda dhambi ndiye nitakayemfuta katika kitabu changu.
Le Seigneur lui répondit: Celui qui aura péché contre moi, je l’effacerai de mon livre:
34 Basi sasa uende ukawaongoze watu hawa mpaka mahali pale ambapo nimekwambia habari zake. Tazama, malaika wangu atakutangulia. Lakini pamoja na hayo siku nitakayowajilia nitawapatiliza kwa ajili ya dhambi yao.”
Mais toi, va, et conduis ce peuple où je t’ai dit: mon ange te précédera. Pour moi, au jour de la vengeance, je visiterai ce péché qu’ils ont commis.
35 Kisha Yahweh akawapiga hao watu, kwa walivyoifanya ile ndama, ambayo Aruni aliifanya.
Le Seigneur frappa donc le peuple pour le crime du veau qu’avait fait Aaron.