< Kutoka 32 >
1 Hata watu walipoona ya kuwa Musa amekawia kushuka katika mlima, wakakusanyana wakamwendea Aruni, wakamwambia, “Njoo, katufanyizie sanamu itakayokwenda mbele yetu, kwa maana Musa huyo aliyetutoa katika nchi ya Misri hatujui yaliyompata.”
And when the people saw that Moses delayed to come down from the mount, the people assembled themselves together around Aaron, and they said unto him, Up, make us gods, that shall go before us; for of this man Moses, who hath brought us up out of the land of Egypt, we know not what is become of him.
2 Hivyo Aruni akawaambia, “Zitoeni pete za dhahabu zilizo katika masikio ya wake zenu, na wana wenu, na binti zenu, mkaniletee.”
And Aaron said unto them, Take out the golden earrings, which are in the ears of your wives, of your sons, and of your daughters, and bring them unto me.
3 Watu wote wakavua pete za dhahabu zilizo katika masikio yao, na wakamletea Aruni.
And all the people took out the golden earrings, which were in their ears, and brought them unto Aaron.
4 Akapoke mikononi mwao akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha. Nao wakasema, “Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.”
And he took them from their hand, and fashioned it in a mould, and he made of it a molten calf; and they said, These are thy gods, O Israel, that have brought thee up out of the land of Egypt.
5 Naye Haruni alipoona jambo hili, akajenga madhabahu mbele yake; Aruni akatangaza akasema,
And when Aaron saw this, he built an altar before it; and Aaron called out, and said, A feast unto the Lord is tomorrow.
6 “Kesho itakuwa sikukuu kwa Yahweh.” Wakaondoka asubuhi na mapema, wakatoa dhabihu, wakaleta sadaka za amani, watu wakaketi kula na kunywa, wakaondoka wacheze.
And they rose up early on the morrow, and offered burnt-offerings, and brought near peace-offerings; and the people sat down to eat and to drink, and rose up to play.
7 Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Shuka upesi, kwa maana watu wako uliowatoa katika nchi ya Misri wamejiharibu nafsi zao.
And the Lord spoke unto Moses, Go, get thee down; for thy people, which thou hast brought up out of the land of Egypt, hath become corrupt:
8 Wamepotoka upesi kuiacha ile njia niliyowaamuru, wamejifanyizia ndama ya kuyeyusha wakaiabudu na kuitolea dhabihu. Wakasema, 'Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.
They have turned aside quickly from the way which I have commanded them; they have made themselves a molten calf: and they have bowed themselves to it, and have sacrificed unto it, and have said, These are thy gods, O Israel, that have brought thee up out of the land of Egypt.
9 Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu.
And the Lord said unto Moses, I have seen this people, and, behold, it is a stiffnecked people.
10 Basi sasa usinizuie. Ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize. Nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.”
And now let me alone, and my wrath shall wax hot against them, and I will make an end of them; and I will make of thee a great nation.
11 Musa akamsihi sana Yahweh Mungu wake, na kusema,”Yahweh, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu?
Thereupon Moses besought the Lord his God, and said, Why, O Lord, shall thy wrath wax hot against thy people, that thou hast brought forth out of the land of Egypt, with great power and with a mighty hand?
12 Kwa nini Wamisri kusema, 'Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi?' Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako.
Wherefore should the Egyptians say thus, For mischief did he bring them out, to slay them in the mountains, and to destroy them from the face of the earth? Turn from thy fierce wrath, and repent thee of the evil decreed against thy people.
13 Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, 'Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele.'”
Remember Abraham, Isaac, and Israel, thy servants, to whom thou didst swear by thy own self, and speak unto them, I will multiply your seed as the stars of heaven; and all this land that I have spoken of will I give unto your seed, and they shall inherit it for ever.
14 Na Yahweh akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake.
And the Lord bethought himself of the evil which he had spoken to do unto his people.
15 Kisha Musa akageuka akashuka katika mlima, na zile mbao mbili za mawe mikononi mwake. Mbao zilizoandikwa pande zote mbili, upande huu na upande huu ziliandikwa.
And Moses turned about, and went down from the mount with the two tables of the testimony in his hand: tables inscribed on both their sides; on the one side and on the other were they inscribed.
16 Na zile mbao zilikuwa kazi ya Mungu nayo maandiko yalikuwa maandiko ya Mungu, yaliyochorwa katika zile mbao.
And the tables were the work of God, and the writing was the writing of God, engraved upon the tables.
17 Na Yoshua aliposikia kelele za watu walipokuwa wakipiga kelele, akamwambia Musa, “Kuna kelele ya vita kambini.
And Joshua heard the noise of the people in its shouting, and he said unto Moses, There is a noise of war in the camp.
18 “Lakini Musa akasema, “Hiyo si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushinda vitani, wala si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushindwa; bali kelele za watu waimbao ndizo ninazozisikia mimi.”
And he said, It is not the voice of a shout for mastery, neither is it the voice of a cry for defeat; the noise of singing do I hear.
19 Hata alipoyakaribia kambini akaiona ile ndama, na watu wakicheza. Hasira ya Musa ikawaka. Akazitupa zile mbao mikononi mwake, akazivunja chini ya mlima.
And it came to pass, when he came nigh unto the camp, and he saw the calf, and the dancing: that the anger of Moses waxed hot, and he cast from his hands the tables, and broke them at the foot of the mount.
20 Akaitwaa ile ndama waliyoifanya, akaichoma moto, akaisaga hata ikawa mavumbi, akainyunyiza juu ya maji. Akawanywesha wana wa Israeli.
And he took the calf which they had made, and burnt it in fire, and ground it to a powder, and he strewed it upon the water, and made the children of Israel drink of it.
21 Musa akamwambia Aruni, “Watu hawa wamekufanyani hata ukaleta dhambi hii kuu juu yao?
And Moses said unto Aaron, What hath this people done unto thee, that thou hast brought upon it so great a sin?
22 Aruni akasema, “Hasira yako isiwake, bwana wangu. Wewe unawajua watu hawa, ya kuwa wamejielekeza kwa mabaya.
And Aaron said, Let not the anger of my Lord wax hot: thou knowest the people, that it is bent on mischief.
23 Maana waliniambia, 'Katufanyie miungu, itakayokwenda mbele yetu. Kwa maana mtu huyo Musa, aliyetutoa katika nchi ya Misri, hatujui yaliyompata.'
And they said unto me, Make us gods that shall go before us; for of this man Moses, who brought us up out of the land of Egypt, we know not what hath become of him.
24 Nikawaambia, 'Mtu ye yote aliye na dhahabu na aivue; basi wakanipa, nami nikaitupa ndani ya moto, akatoka ndama huyu.”
And I said unto them, Who hath any gold? They took it off themselves and gave it to me, and I cast it into the fire, and there came out this calf.
25 Basi Musa alipoona ya kuwa watu hawa wameasi (maana Haruni amewaacha waasi, ili wawe dhihaka kati ya adui zao)
And Moses saw the people that it had become unruly; for Aaron had made it unruly for a disgrace among their opponents.
26 Ndipo Musa akasimama katika mlango wa marago, akasema, “Mtu awaye yote aliye upande wa Yahweh na aje kwangu.” Wana wa Lawi wote wakamkusanyikia.
Moses then placed himself in the gate of the camp, and said, Whoever is on the Lord's side, let him come unto me! and there assembled themselves unto him all the sons of Levi.
27 Akawaambia, Yahweh, Mungu wa Israeli, asema hivi, 'Kila mtu na ajifunge upanga wake pajani mwake, akapite huko na huko toka mlango hata mlango kati ya marago, mkamchinje kila mtu ndugu yake, na kila mtu mwenziwe na kila mtu jirani yake.'”
And he said unto them, Thus hath said the Eternal, the God of Israel, Put ye every man his sword by his side, and go ye hither and thither, from gate to gate in the camp, and slay ye every man his brother, and every man his companion, and every man his relative.
28 Na hao wana wa Lawi wakafanya kama vile alivyosema Musa, wakaanguka siku ile kama watu elfu tatu.
And the children of Levi did according to the word of Moses: and there fell of the people on that day about three thousand men.
29 Musa akasema, Jiwekeni wakfu kwa Yahweh leo, kila mtu juu ya mwanawe na juu ya ndugu yake; ili Yahweh awape baraka leo.”
And Moses said, Consecrate yourselves today to the Lord, yea even every man on his son, and on his brother; and to bestow upon you this day a blessing.
30 Hata asubuhi yake Musa akawaambia watu, “Mmetenda dhambi kuu. Sasa nitakwenda juu kwa Yahweh. Labda nitafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu.”
And it came to pass on the morrow, that Moses said unto the people, Ye have sinned a great sin: and now I will go up unto the Lord; peradventure I may obtain an atonement for your sin.
31 Musa akarejea kwa Yahweh akasema,” Oh! Watu hawa wametenda dhambi kuu wamejifanyia miungu ya dhahabu.
And Moses returned unto the Lord, and said, Oh, this people hath sinned a great sin, and they have made themselves gods of gold.
32 Walakini sasa, ikiwa utawasamehe dhambi yao – na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichoandika.”
Yet now, if thou wilt forgive their sin—; but if not, blot me out, I pray thee, from thy book which thou hast written.
33 Yahweh akamwambia Musa, “Mtu ye yote aliyenitenda dhambi ndiye nitakayemfuta katika kitabu changu.
And the Lord said unto Moses, Whosoever hath sinned against me, him will I blot out from my book.
34 Basi sasa uende ukawaongoze watu hawa mpaka mahali pale ambapo nimekwambia habari zake. Tazama, malaika wangu atakutangulia. Lakini pamoja na hayo siku nitakayowajilia nitawapatiliza kwa ajili ya dhambi yao.”
And now go, lead the people unto the place of which I have spoken unto thee; behold, my angel shall go before thee; but on the day when I visit I will visit their sin upon them.
35 Kisha Yahweh akawapiga hao watu, kwa walivyoifanya ile ndama, ambayo Aruni aliifanya.
And the Lord sent a plague among the people, because that they had made the calf which Aaron made.