< Kutoka 32 >

1 Hata watu walipoona ya kuwa Musa amekawia kushuka katika mlima, wakakusanyana wakamwendea Aruni, wakamwambia, “Njoo, katufanyizie sanamu itakayokwenda mbele yetu, kwa maana Musa huyo aliyetutoa katika nchi ya Misri hatujui yaliyompata.”
When the people realized how long Moses was taking before he came back down the mountain, they went together to see Aaron. They told him, “Get up! Make some gods for us who can lead us because this man Moses who brought us out of the land of Egypt—we don't know what's happened to him!”
2 Hivyo Aruni akawaambia, “Zitoeni pete za dhahabu zilizo katika masikio ya wake zenu, na wana wenu, na binti zenu, mkaniletee.”
“Bring to me the gold earrings that your wives, sons, and daughters are wearing,” Aaron replied.
3 Watu wote wakavua pete za dhahabu zilizo katika masikio yao, na wakamletea Aruni.
So everyone took off the gold earrings they were wearing and brought them to Aaron.
4 Akapoke mikononi mwao akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha. Nao wakasema, “Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.”
He took what they gave him and using a molding tool cast an idol in the shape of a bull calf. They shouted out, “Israel, these are the gods that brought you out of the land of Egypt.”
5 Naye Haruni alipoona jambo hili, akajenga madhabahu mbele yake; Aruni akatangaza akasema,
When Aaron saw this, he built an altar in front of the golden calf and shouted out, “Tomorrow will be a festival to honor the Lord!”
6 “Kesho itakuwa sikukuu kwa Yahweh.” Wakaondoka asubuhi na mapema, wakatoa dhabihu, wakaleta sadaka za amani, watu wakaketi kula na kunywa, wakaondoka wacheze.
Early the next day they sacrificed burnt offerings and presented peace offerings. Then they sat down to celebrate with eating and drinking. Then they got up to dance, and it became like an orgy.
7 Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Shuka upesi, kwa maana watu wako uliowatoa katika nchi ya Misri wamejiharibu nafsi zao.
Then the Lord told Moses, “Get back down, because your people that you brought out of Egypt are acting immorally.
8 Wamepotoka upesi kuiacha ile njia niliyowaamuru, wamejifanyizia ndama ya kuyeyusha wakaiabudu na kuitolea dhabihu. Wakasema, 'Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri.
They have been so quick to abandon the way I ordered them to follow. They have made a metal bull calf idol for themselves, bowing before it in worship and offering sacrifices to it. They're saying, ‘These are the gods that brought you out of the land of Egypt.’”
9 Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu.
“I know what these people are like,” the Lord continued saying to Moses. “They are so rebellious!
10 Basi sasa usinizuie. Ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize. Nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.”
Now leave me! I am angry with them—let me finish them off! I will make you into a great nation.”
11 Musa akamsihi sana Yahweh Mungu wake, na kusema,”Yahweh, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu?
But Moses pleaded with the Lord his God, saying, “Why are you angry with the people you brought out of the land of Egypt with tremendous power and great strength?
12 Kwa nini Wamisri kusema, 'Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi?' Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako.
Why should the Egyptians be able to say, ‘He brought them out with the evil purpose of killing them in the mountains, wiping them off the face of the earth’? Turn from your fierce anger. Please change your mind over the threat against your people.
13 Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, 'Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele.'”
Remember you swore a promise your servants Abraham, Isaac, and Jacob, telling them, ‘I will make your descendants as numerous as the stars of heaven, and give you all the land I promised to them, and they shall own it forever.’”
14 Na Yahweh akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake.
The Lord changed his mind over the disaster he threatened to cause his people.
15 Kisha Musa akageuka akashuka katika mlima, na zile mbao mbili za mawe mikononi mwake. Mbao zilizoandikwa pande zote mbili, upande huu na upande huu ziliandikwa.
Moses turned and went down the mountain, carrying the two stone tablets of the Law written on both sides.
16 Na zile mbao zilikuwa kazi ya Mungu nayo maandiko yalikuwa maandiko ya Mungu, yaliyochorwa katika zile mbao.
God had made the tablets, and God had engraved the writing himself.
17 Na Yoshua aliposikia kelele za watu walipokuwa wakipiga kelele, akamwambia Musa, “Kuna kelele ya vita kambini.
When Joshua heard all the shouting from the camp, he said to Moses, “It sounds like fighting in the camp!”
18 “Lakini Musa akasema, “Hiyo si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushinda vitani, wala si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushindwa; bali kelele za watu waimbao ndizo ninazozisikia mimi.”
But Moses replied, “These are not the shouts of victory or of defeat. What I'm hearing is people partying!”
19 Hata alipoyakaribia kambini akaiona ile ndama, na watu wakicheza. Hasira ya Musa ikawaka. Akazitupa zile mbao mikononi mwake, akazivunja chini ya mlima.
As he approached the camp he saw the bull calf idol and the dancing. He got so angry that he threw down the stone tablets and smashed them there at the foot of the mountain.
20 Akaitwaa ile ndama waliyoifanya, akaichoma moto, akaisaga hata ikawa mavumbi, akainyunyiza juu ya maji. Akawanywesha wana wa Israeli.
He took the bull calf and burned it, and ground it into powder. Then he mixed this with water and made the Israelites drink it.
21 Musa akamwambia Aruni, “Watu hawa wamekufanyani hata ukaleta dhambi hii kuu juu yao?
Then Moses asked Aaron, “What did these people do to you that you made them sin so badly?”
22 Aruni akasema, “Hasira yako isiwake, bwana wangu. Wewe unawajua watu hawa, ya kuwa wamejielekeza kwa mabaya.
“Please don't get angry with me, my lord,” Aaron replied, “You yourself know how liable these people are to do evil.
23 Maana waliniambia, 'Katufanyie miungu, itakayokwenda mbele yetu. Kwa maana mtu huyo Musa, aliyetutoa katika nchi ya Misri, hatujui yaliyompata.'
They told me, ‘Make some gods for us who can lead us because this man Moses who brought us out of the land of Egypt—we don't know what's happened to him!’
24 Nikawaambia, 'Mtu ye yote aliye na dhahabu na aivue; basi wakanipa, nami nikaitupa ndani ya moto, akatoka ndama huyu.”
So I said to them, ‘Anybody who has gold jewelry, take it off and give it to me.’ I threw the gold into the furnace and out came this bull calf.”
25 Basi Musa alipoona ya kuwa watu hawa wameasi (maana Haruni amewaacha waasi, ili wawe dhihaka kati ya adui zao)
Moses saw the people going completely wild because Aaron had let them, and that this had brought ridicule on them from their enemies.
26 Ndipo Musa akasimama katika mlango wa marago, akasema, “Mtu awaye yote aliye upande wa Yahweh na aje kwangu.” Wana wa Lawi wote wakamkusanyikia.
So he went and stood at the entrance to the camp, and shouted out, “Whoever is on the Lord's side, come and join me!” All the Levites gathered around him.
27 Akawaambia, Yahweh, Mungu wa Israeli, asema hivi, 'Kila mtu na ajifunge upanga wake pajani mwake, akapite huko na huko toka mlango hata mlango kati ya marago, mkamchinje kila mtu ndugu yake, na kila mtu mwenziwe na kila mtu jirani yake.'”
Moses told them, “This is what the Lord, the God of Israel says: Each of you strap on a sword. Then go all through the camp from one end to the other and kill your brothers, friends, and neighbors.”
28 Na hao wana wa Lawi wakafanya kama vile alivyosema Musa, wakaanguka siku ile kama watu elfu tatu.
The Levites did what Moses had told them, and that day around 3,000 men were killed.
29 Musa akasema, Jiwekeni wakfu kwa Yahweh leo, kila mtu juu ya mwanawe na juu ya ndugu yake; ili Yahweh awape baraka leo.”
Moses told the Levites, “Today you have dedicated yourselves to the Lord because you took action against your sons and brothers. Today you have gained a blessing for yourselves.”
30 Hata asubuhi yake Musa akawaambia watu, “Mmetenda dhambi kuu. Sasa nitakwenda juu kwa Yahweh. Labda nitafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu.”
The following day Moses spoke to the people, saying, “You have sinned very badly. But now I will go up to the Lord. Maybe I can get him to forgive your sin.”
31 Musa akarejea kwa Yahweh akasema,” Oh! Watu hawa wametenda dhambi kuu wamejifanyia miungu ya dhahabu.
So Moses went back to the Lord. He said, “Please—the people have sinned very badly by making gods of gold for themselves.
32 Walakini sasa, ikiwa utawasamehe dhambi yao – na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichoandika.”
But now, if you will, forgive their sin. Otherwise just blot me out of the scroll in which you keep your records.”
33 Yahweh akamwambia Musa, “Mtu ye yote aliyenitenda dhambi ndiye nitakayemfuta katika kitabu changu.
But the Lord replied to Moses, “It's those who sinned against me who will be blotted out of my scroll.
34 Basi sasa uende ukawaongoze watu hawa mpaka mahali pale ambapo nimekwambia habari zake. Tazama, malaika wangu atakutangulia. Lakini pamoja na hayo siku nitakayowajilia nitawapatiliza kwa ajili ya dhambi yao.”
Now go and lead the people to the place I told you about. Look, my angel will go before you, but at the time I decide to punish, I will punish them for their sin.”
35 Kisha Yahweh akawapiga hao watu, kwa walivyoifanya ile ndama, ambayo Aruni aliifanya.
The Lord brought a plague on the people because they made Aaron make the bull calf.

< Kutoka 32 >