< Kutoka 31 >
1 Yahweh akasema na Musa,
And YHWH speaks to Moses, saying,
2 “Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda
“See, I have called by name Bezaleel, son of Uri, son of Hur, of the tribe of Judah,
3 Nami nimemjaza Bezaleli na roho ya Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya kila aina,
and I fill him [with] the Spirit of God, in wisdom, and in understanding, and in knowledge, and in all work,
4 ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa fedha, na wa shaba,
to devise inventions to work in gold, and in silver, and in bronze,
5 na kukata vito kwa kutiwa mahali, na kuchora miti, na kufanya kazi ya ustadi iwayo yote.
and in a carving of stone for settings, and in a carving of wood to work in all work.
6 Tena, nimemchagua, awe pamoja naye Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila ya Dani. Nami nimetia hekima katika mioyo ya wote wenye moyo wa hekima, ili wapate kufanya vyote nilivyokuagiza. Hii ni,
And I, behold, have given with him Aholiab, son of Ahisamach, of the tribe of Dan, and I have given wisdom in the heart of every wise-hearted one, and they have made all that which I have commanded you.
7 hema ya kukutania na sanduku la ushuhuda, na kiti cha rehema kilicho juu yake, na vyombo vyote vya Hema;
The Tent of Meeting, and the Ark of Testimony, and the propitiatory covering which [is] on it, and all the vessels of the tent,
8 na meza, na vyombo vyake, na kinara cha taa safi pamoja na vyombo vyake vyote,
and the table and its vessels, and the pure lampstand and all its vessels, and the altar of the incense,
9 na madhabahu ya kufukizia uvumba; na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote, na birika na tako lake.
and the altar of the burnt-offering and all its vessels, and the laver and its base,
10 Pia mavazi yenye kufumwa kwa uzuri, na mavazi matakatifu ya Haruni kuhani, na mavazi ya wanawe, ili kutumika katika kazi ya ukuhani.
and the colored garments, and the holy garments for Aaron the priest, and the garments of his sons, for acting as priests in;
11 Pia mafuta ya kutiwa, na uvumba wa manukato mazuri, kwa ajili ya mahali patakatifu; sawasawa na yote niliyokuagiza ndivyo watakavyofanya wao.
and the anointing oil, and the incense of the spices for the holy place; according to all that I have commanded you—they do.”
And YHWH speaks to Moses, saying,
13 “Waambie wana wa Israeli, 'Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi BWANA niwatakasaye ninyi.
“And you, speak to the sons of Israel, saying, Surely you keep My Sabbaths, for it [is] a sign between Me and you throughout your generations, to know that I, YHWH, am sanctifying you;
14 Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake.
and you have kept the Sabbath, for it [is] holy to you, he who is defiling it is certainly put to death—for any who does work in it—that person has even been cut off from the midst of his people.
15 Kazi itafanywa siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, takatifu kwa BWANA; kila mtu atakayefanya kazi yo yote katika siku ya Sabato, hakika yake atauawa.
[For] six days work is done, and in the seventh day [is] a Sabbath of holy rest to YHWH; any who does work in the Sabbath day is certainly put to death,
16 Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli wataishika Sabato. Kuiangalia sana hiyo Sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele.
and the sons of Israel have observed the Sabbath; to keep the Sabbath throughout their generations [is] a perpetual covenant—
17 Ni ishara kati ya mimi na wana wa Israeli milele; kwani kwa siku sita Yahweh alifanya mbingu na nchi, akastarehe kwa siku ya saba na kupumzika.
it [is] a sign between Me and the sons of Israel for all time; for [in] six days YHWH made the heavens and the earth, and in the seventh day He has ceased and is refreshed.”
18 Hapo Mungu alipokuwa amekwisha zungumza na Musa katika mlima wa Sinai, akampa hizo mbao mbili za ushuhuda, mbao mbili za mawe, zilizoandikwa kwa mkono wake.
And He gives to Moses, when He finishes speaking with him in Mount Sinai, two tablets of the Testimony, tablets of stone, written by the finger of God.