< Kutoka 31 >

1 Yahweh akasema na Musa,
I mluvil Hospodin k Mojžíšovi, řka:
2 “Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda
Hle, povolal jsem ze jména Bezeleele, syna Uri, syna Hur, z pokolení Judova.
3 Nami nimemjaza Bezaleli na roho ya Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya kila aina,
A naplnil jsem ho duchem Božím, moudrostí a rozumností, i uměním všelijakého řemesla,
4 ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa fedha, na wa shaba,
Aby vtipně smysliti uměl, což by koli řemeslně uděláno býti mohlo z zlata a z stříbra i z mědi.
5 na kukata vito kwa kutiwa mahali, na kuchora miti, na kufanya kazi ya ustadi iwayo yote.
I v řezání kamení drahého k vsazování, i v umělém vysazování na dřevě aby dělal všelijaké dílo.
6 Tena, nimemchagua, awe pamoja naye Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila ya Dani. Nami nimetia hekima katika mioyo ya wote wenye moyo wa hekima, ili wapate kufanya vyote nilivyokuagiza. Hii ni,
A aj, já přidal jsem jemu Aholiaba, syna Achisamechova, z pokolení Dan. A v srdci každého vtipného složil jsem moudrost, aby spravili vše, což jsem přikázal tobě:
7 hema ya kukutania na sanduku la ushuhuda, na kiti cha rehema kilicho juu yake, na vyombo vyote vya Hema;
Stánek úmluvy a truhlu svědectví, a slitovnici, kteráž má býti na ní, i všelijaké nádobí stánku;
8 na meza, na vyombo vyake, na kinara cha taa safi pamoja na vyombo vyake vyote,
Stůl také a nádoby k němu, i svícen čistý se všemi nádobami jeho, a oltář pro kadění;
9 na madhabahu ya kufukizia uvumba; na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote, na birika na tako lake.
Též oltář k zápalům se všemi nádobami jeho, a umyvadlo s podstavkem jeho;
10 Pia mavazi yenye kufumwa kwa uzuri, na mavazi matakatifu ya Haruni kuhani, na mavazi ya wanawe, ili kutumika katika kazi ya ukuhani.
I roucha k službě, i roucha svatá Aronovi knězi, i roucha synů jeho, aby mi úřad kněžský konali;
11 Pia mafuta ya kutiwa, na uvumba wa manukato mazuri, kwa ajili ya mahali patakatifu; sawasawa na yote niliyokuagiza ndivyo watakavyofanya wao.
I olej pomazání a kadidlo vonné do svatyně. Všecko tak, jakž jsem přikázal tobě, udělají.
12 akasema na Musa,
Mluvil také Hospodin k Mojžíšovi, řka:
13 “Waambie wana wa Israeli, 'Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi BWANA niwatakasaye ninyi.
Ty pak mluv k synům Izraelským a rci: A však sobot mých ostříhati budete. Nebo to znamením jest mezi mnou a vámi po rodech vašich, aby známo bylo, že já jsem Hospodin, kterýž vás posvěcuji.
14 Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake.
Protož ostříhati budete soboty, nebo svatá jest vám. Kdož by ji poškvrnil, smrtí umře; a kdo by koli dělal v ní dílo, vyhlazena bude ta duše z prostředku lidu svého.
15 Kazi itafanywa siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, takatifu kwa BWANA; kila mtu atakayefanya kazi yo yote katika siku ya Sabato, hakika yake atauawa.
Šest dní děláno bude dílo, ale v den sedmý sobota odpočinutí jest, svatost Hospodinu. Každý, kdož by dělal dílo v den sobotní, smrtí umře.
16 Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli wataishika Sabato. Kuiangalia sana hiyo Sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele.
Protož ostříhati budou synové Izraelští soboty, tak aby světili sobotu po rodech svých smlouvou věčnou.
17 Ni ishara kati ya mimi na wana wa Israeli milele; kwani kwa siku sita Yahweh alifanya mbingu na nchi, akastarehe kwa siku ya saba na kupumzika.
Mezi mnou a syny Izraelskými za znamení jest na věčnost; nebo šest dní činil Hospodin nebe i zemi, v den pak sedmý přestal a odpočinul.
18 Hapo Mungu alipokuwa amekwisha zungumza na Musa katika mlima wa Sinai, akampa hizo mbao mbili za ushuhuda, mbao mbili za mawe, zilizoandikwa kwa mkono wake.
I dal Pán Mojžíšovi po dokonání těchto řečí s ním na hoře Sinai dvě dsky svědectví, dsky kamenné, psané prstem Božím.

< Kutoka 31 >