< Kutoka 29 >

1 Sasa Hivi ndivyo wapaswa kufanya kuwatenga ili wanitumikie kama makuhani. Chukuwa mtoto wa ng'ombe dume na kondoo bila lawama,
« Voici ce que tu leur feras pour les sanctifier, afin qu'ils soient à mon service dans le sacerdoce: prends un jeune taureau et deux béliers sans défaut,
2 mkate bila hamira, na keki bila hamira iliyo changanywa na mafuta. Pia chukuwa maandazi bila hamira yalio pakwa mafuta. Fanya maandazi kwa unga mzuri wa ngano.
des pains sans levain, des gâteaux sans levain mélangés à de l'huile et des galettes sans levain ointes d'huile. Tu les feras avec de la fine farine de froment.
3 Lazima uweke kwenye ndoo moja, leta kwenye ndoo, na kuleta pamoja na ng'ombe dume na wana kondoo wawili.
Tu les mettras dans un panier, et tu les apporteras dans le panier, avec le taureau et les deux béliers.
4 Lazima nawe umlete Aruni na wana wake wawili katika lango la kuingilia hema la kukutania. Lazima uwasafishe Aruni na wana wake kwenye maji.
Tu feras venir Aaron et ses fils à l'entrée de la tente de la Rencontre, et tu les laveras avec de l'eau.
5 Kisha twaa hayo mavazi na kumvika Haruni; itie kanzu, na joho ya naivera, na naivera, na kifuko cha kifuani, na kumkaza kwa huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi.
Tu prendras les vêtements et tu revêtiras Aaron de la tunique, de la robe de l'éphod, de l'éphod et du pectoral, et tu le revêtiras de la bande de l'éphod habilement tissée.
6 Nawe mvike kile kilemba kichwani, na ile taji takatifu utaitia katika kile kilemba.
Tu placeras le turban sur sa tête, et tu mettras la couronne sacrée sur le turban.
7 Ndipo utakapotwaa hayo mafuta ya kutiwa, na kummiminia kichwani mwake, na kumtia mafuta.
Tu prendras ensuite l'huile d'onction, tu la verseras sur sa tête et tu l'oindras.
8 Kisha walete hao wanawe na kuwavika kanzu.
Tu feras venir ses fils, et tu les revêtiras de tuniques.
9 Nawe uwakaze mishipi, Aruni na wanawe, na kuwavika kofia. Nao watakuwa na huo ukuhani kwa amri ya milele. Nawe utawaweka Haruni na wanawe kwa kazi takatifu.
Tu les revêtiras de ceintures, Aaron et ses fils, et tu leur attacheras des bandeaux. Ils auront le sacerdoce par un statut perpétuel. Tu consacreras Aaron et ses fils.
10 Kisha utamleta huyo ng’ombe mbele ya hema ya kukutania; na Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo ng’ombe.
« Tu amèneras le taureau devant la tente de la Rencontre; Aaron et ses fils poseront leurs mains sur la tête du taureau.
11 Kisha utamchinja huyo ng’ombe mbele ya Yahweh pa hema ya kukutania. BWANA,
Tu égorgeras le taureau devant Yahvé, à l'entrée de la tente de la Rencontre.
12 Kisha twaa baadhi ya damu ya ng’ombe, uitie katika pembe za madhabahu kwa kidole chako; na kuimimina damu yote chini ya madhabahu.
Tu prendras du sang du taureau, tu en mettras sur les cornes de l'autel avec ton doigt, et tu verseras tout le sang au pied de l'autel.
13 Kisha chukuwa mafuta yote yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo juu yake, uyateketeze yote juu ya madhabahu.
Tu prendras toute la graisse qui recouvre les entrailles, la couverture du foie, les deux rognons et la graisse qui les recouvre, et tu les brûleras sur l'autel.
14 Lakini nyama yake huyo ng’ombe, na ngozi yake, na mavi yake, utayachoma kwa moto nje ya marago; ni sadaka kwa ajili ya dhambi.
Mais la viande du taureau, sa peau et ses excréments, tu les brûleras au feu en dehors du camp. C'est un sacrifice pour le péché.
15 Pia mtwae kondoo mume mmoja; na Aruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake huyo kondoo mume.
« Tu prendras aussi un bélier, et Aaron et ses fils poseront leurs mains sur la tête du bélier.
16 Kisha utamchinja huyo kondoo mume, na kuitwaa damu yake, na kuinyunyiza katika madhabahu kuizunguka kando-kando.
Tu égorgeras le bélier, tu prendras son sang, et tu en feras l'aspersion autour de l'autel.
17 Kisha utamkata-kata kondoo vipande vyake, na kuyaosha matumbo yake na miguu yake, na kuiweka pamoja na vipande vyake na kichwa chake,
Tu couperas le bélier en morceaux, tu laveras ses entrailles et ses jambes, et tu les mettras avec ses morceaux et avec sa tête.
18 nawe mteketeze kondoo mzima juu ya madhabahu. Ni sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yaYahweh; ni harufu nzuri, sadaka iliyosongezwa kwa Yahweh kwa njia ya moto.
Tu brûleras le bélier tout entier sur l'autel: c'est un holocauste à l'Éternel; c'est une odeur agréable, un sacrifice par le feu à l'Éternel.
19 Kisha mtwae huyo kondoo mwingine; na Aruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake huyo kondoo.
« Tu prendras l'autre bélier, et Aaron et ses fils poseront leurs mains sur la tête du bélier.
20 Kisha utamchinja kondoo, na kuitwaa damu yake, na kuitia katika ncha ya sikio la Aruni la upande wa kuume, na katika ncha za masikio ya kuume ya wanawe, na katika vyanda vya gumba vya mikono yao ya kuume, na katika vidole vikuu vya miguu yao ya kuume, na kuinyunyiza hiyo damu katika madhabahu kuizunguka kando-kando.
Tu égorgeras le bélier, tu prendras de son sang, tu en mettras sur le lobe de l'oreille droite d'Aaron et sur le lobe de l'oreille droite de ses fils, sur le pouce de leur main droite et sur le gros orteil de leur pied droit, et tu aspergeras le sang tout autour de l'autel.
21 Kisha twaa katika hiyo damu iliyo juu ya madhabahu, na katika hayo mafuta ya kutiwa, na kumnyunyizia Aruni, juu ya mavazi yake, na wanawe, na mavazi yao pia, pamoja naye; naye atatakaswa, na mavazi yake, na wanawe, na mavazi ya wanawe, pamoja naye.
Tu prendras du sang qui est sur l'autel et de l'huile d'onction, et tu en feras l'aspersion sur Aaron, sur ses vêtements, sur ses fils et sur les vêtements de ses fils avec lui; il sera sanctifié, ainsi que ses vêtements, ses fils et les vêtements de ses fils avec lui.
22 Tena yatwae mafuta ya huyo kondoo mume, na mkia wake wa mafuta, na mafuta yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo katika hizo figo, na paja la kuume; kwani ni kondoo ambaye ni wa kuwekwa kwa kazi takatifu.
Tu prendras aussi de la graisse du bélier, la queue, la graisse qui recouvre les entrailles, la couverture du foie, les deux rognons, la graisse qui les recouvre, et la cuisse droite (car c'est un bélier de consécration),
23 Utwae na mkate mmoja wa unga, na mkate mmoja ulioandaliwa kwa mafuta, na kaki moja katika kile kikapu cha mikate isiyotiwa chachu, kilichowekwa mbele ya Yahweh.
et un pain, un gâteau de pain huilé et une galette de la corbeille de pains sans levain qui est devant l'Éternel.
24 Nawe utavitia hivi vyote katika mikono ya Aruni, na katika mikono ya wanawe; nawe utavitikisa-tikisa viwe sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.
Tu mettras tout cela dans les mains d'Aaron et dans les mains de ses fils, et tu les agiteras en offrande par élévation devant l'Éternel.
25 Kisha uvitwae vile vitu mikononi mwao, na kuviteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa, viwe harufu nzuri mbele yangu; ni sadaka iliyotengenezwa kwangu kwa njia ya moto.
Tu les prendras de leurs mains et tu les brûleras sur l'autel, sur l'holocauste, comme une odeur agréable devant l'Éternel: c'est une offrande faite par feu à l'Éternel.
26 Kisha twaa kidari cha huyo kondoo wa kuwekwa kwake Haruni kwa kazi takatifu, na kukitikisa-tikisa kiwe sadaka ya kutikiswa mbele za Yahwe nacho kitakuwa ni sehemu yako.
« Tu prendras la poitrine du bélier de consécration d'Aaron et tu l'agiteras en signe d'offrande devant Yahvé. Ce sera ta part.
27 Nawe kitakase kile kidari cha ile sadaka ya kutikiswa, na lile paja la sadaka ya kuinuliwa, lililotikiswa, na lililoinuliwa juu, vya yule kondoo wa kuwekwa kwa kazi takatifu, huyo aliyekuwa kwa ajili ya Aruni na wanawe.
Tu sanctifieras la poitrine de l'offrande par agitation et la cuisse de l'offrande par agitation, qu'on agitera et qu'on élèvera, du bélier de consécration, de celle qui est pour Aaron et de celle qui est pour ses fils.
28 Navyo vitakuwa vya Haruni na wanawe posho ya lazima sikuzote itokayo kwa hao wana wa Israeli; kwa kuwa ni sadaka ya kuinuliwa; nayo itakuwa ni sadaka ya kuinuliwa itokayo kwa hao wana wa Israeli katika dhabihu zao za sadaka za amani, ni sadaka yao ya kuinuliwa kwa ajili ya Yahweh.
Ce sera pour Aaron et ses fils, comme leur part à perpétuité parmi les enfants d'Israël, car c'est une offrande par ondulation. C'est une offrande ondulée des enfants d'Israël, parmi les sacrifices de leurs sacrifices de communion, leur offrande ondulée à Yahvé.
29 Na hayo mavazi matakatifu ya Aruni yatakuwa ya wanawe baada yake, wayavae watakapotiwa mafuta, na watakapowekwa kwa kazi takatifu.
« Les vêtements sacrés d'Aaron seront destinés à ses fils après lui, pour qu'ils y soient oints et qu'ils y soient consacrés.
30 Huyo mwanawe atakayekuwa kuhani badala yake atayavaa muda wa siku saba, hapo atakapoingia ndani ya hiyo hema ya kukutania, ili atumike ndani ya mahali patakatifu.
Le fils qui sera prêtre à sa place les revêtira pendant sept jours, lorsqu'il entrera dans la tente de la Rencontre pour faire le service dans le lieu saint.
31 Nawe twaa huyo kondoo mume aliyekuwa wa kuwekwa kwa kazi takatifu, na kuitokosa nyama yake katika mahali patakatifu.
« Tu prendras le bélier de consécration et tu feras bouillir sa viande dans un lieu saint.
32 Na Aruni na wanawe wataila ile nyama ya kondoo, na mikate iliyo katika kile kikapu, hapo mbele ya mlango wa hema ya kukutania.
Aaron et ses fils mangeront la viande du bélier et le pain qui est dans la corbeille, à l'entrée de la tente d'assignation.
33 Nao watakula vile vitu ambavyo upatanisho ulifanywa kwa hivyo, ili kuwaweka kwa kazi takatifu na kuwatakasa; lakini mgeni asivile, maana, ni vitu vitakatifu.
Ils mangeront ces choses avec lesquelles on a fait l'expiation, pour les consacrer et les sanctifier; mais l'étranger n'en mangera pas, car elles sont saintes.
34 Na kwamba kitu cho chote cha ile nyama, iliyo kwa ajili ya kuweka kwa kazi takatifu, au cho chote cha hiyo mikate, kikisalia hata asubuhi, ndipo utavichoma kwa moto hivyo vilivyosalia; havitaliwa, maana, ni vitu vitakatifu
S'il reste quelque chose de la viande de la consécration ou du pain jusqu'au matin, vous brûlerez au feu ce qui restera. On n'en mangera pas, car c'est une chose sainte.
35 Ni hivyo utakavyowatendea Aruni na wanawe kama nilivyo kuagiza. Utawaweka kwa kazi takatifu siku saba.
« Tu feras ainsi à Aaron et à ses fils, selon tout ce que je t'ai ordonné. Tu les consacreras pendant sept jours.
36 Kila siku utamtoa ng’ombe wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho; nawe utaisafisha hiyo madhabahu, hapo utakapofanya upatanisho kwa ajili ya hiyo madhabahu; nawe utaitia mafuta, ili kuitakasa.
Chaque jour, tu offriras le taureau du sacrifice pour le péché en expiation. Tu purifieras l'autel lorsque tu en feras l'expiation. Tu l'oindras, pour le sanctifier.
37 Utafanya upatanisho kwa ajili ya hiyo madhabahu muda wa siku saba, na kuitakasa; ndipo madhabahu itakapokuwa takatifu sana; kila kitu kiigusacho madhabahu kitakuwa kitakatifu.
Pendant sept jours, tu feras des expiations sur l'autel et tu le sanctifieras; l'autel sera très saint. Tout ce qui touchera l'autel sera saint.
38 Lazima utoe kwenye madhabahu wana-kondoo wa mwaka mmoja wawili siku baada ya siku
« Voici ce que tu offriras sur l'autel: deux agneaux d'un an, jour par jour, continuellement.
39 daima. Mwana-kondoo mmoja utamchinja asubuhi; na mwana-kondoo wa pili utamchinja jioni
Tu offriras l`un des agneaux le matin, et l`autre agneau le soir;
40 Pamoja na mwana-kondoo mmoja utatoa vibaba vitatu vya unga mzuri uliochanganyika na mafuta yenye kupondwa, kiasi cha kibaba na robo kibaba; na divai kiasi cha kibaba na robo kibaba, iwe sadaka ya kinywaji.
tu offriras avec l`un des agneaux un dixième d`épha de fleur de farine mélangé à un quart de hin d`huile battue, et un quart de hin de vin, comme libation.
41 Na huyo mwana-kondoo wa pili utamchinja wakati wa jioni. Nawe utamfanyia vivyo kama ile sadaka ya unga ya asubuhi, na kama ile sadaka yake ya kinywaji. Hii itatoa harufu nzuri, ni dhabihu ya kusongezwa kwangu kwa njia ya moto.
Tu offriras l'autre agneau le soir, et tu lui feras selon l'offrande du matin et selon sa libation, un sacrifice consumé par le feu, d'une agréable odeur à l'Éternel.
42 Itakuwa ni sadaka ya kuteketezwa milele katika vizazi vyenu vyote mlangoni pa ile hema ya kukutania mbele ya Yahweh, hapo nitakapokutana nanyi, ili niseme na wewe hapo.
Ce sera un holocauste perpétuel, de génération en génération, à l'entrée de la tente d'assignation, devant l'Éternel, là où je me réunirai avec vous pour vous parler.
43 Nami nitakutana na wana wa Israeli hapo; na hiyo hema itafanywa takatifu na utukufu wangu. Nami nitaitakasa hiyo hema ya kukutania, na hiyo madhabahu.
C'est là que je rencontrerai les enfants d'Israël, et le lieu sera sanctifié par ma gloire.
44 Pia Aruni na wanawe nitawatakasa, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Je sanctifierai la tente de la Rencontre et l'autel. Je sanctifierai aussi Aaron et ses fils pour qu'ils soient à mon service dans le sacerdoce.
45 Na mimi nitakaa kati ya wana wa Israeli, nami nitakuwa Mungu wao.
J'habiterai au milieu des enfants d'Israël et je serai leur Dieu.
46 Nao watanijua kuwa mimi ndimi Yahweh, Mungu wao, niliyewaleta watoke katika nchi ya Misri, nipate kukaa kati yao. Ni mimi Yahweh, Mungu wao.
Ils sauront que je suis Yahvé leur Dieu, qui les a fait sortir du pays d'Égypte, pour habiter au milieu d'eux: Je suis Yahvé, leur Dieu.

< Kutoka 29 >