< Kutoka 29 >
1 Sasa Hivi ndivyo wapaswa kufanya kuwatenga ili wanitumikie kama makuhani. Chukuwa mtoto wa ng'ombe dume na kondoo bila lawama,
This thing also shalt thou do vnto them whe thou consecratest them to be my Priestes, Take a yong calfe, and two rams without blemish,
2 mkate bila hamira, na keki bila hamira iliyo changanywa na mafuta. Pia chukuwa maandazi bila hamira yalio pakwa mafuta. Fanya maandazi kwa unga mzuri wa ngano.
And vnleauened bread and cakes vnleauened tempered with oyle, and wafers vnleauened anoynted with oyle: (of fine wheate flowre shalt thou make them)
3 Lazima uweke kwenye ndoo moja, leta kwenye ndoo, na kuleta pamoja na ng'ombe dume na wana kondoo wawili.
Then thou shalt put them in one basket, and present them in the basket with the calfe and the two rammes,
4 Lazima nawe umlete Aruni na wana wake wawili katika lango la kuingilia hema la kukutania. Lazima uwasafishe Aruni na wana wake kwenye maji.
And shalt bring Aaron and his sonnes vnto the doore of the Tabernacle of the Congregation, and wash them with water.
5 Kisha twaa hayo mavazi na kumvika Haruni; itie kanzu, na joho ya naivera, na naivera, na kifuko cha kifuani, na kumkaza kwa huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi.
Also thou shalt take the garments, and put vpon Aaron the tunicle, and the robe of the Ephod, and the Ephod, and the brest plate, and shalt close them to him with the broidred garde of the Ephod.
6 Nawe mvike kile kilemba kichwani, na ile taji takatifu utaitia katika kile kilemba.
Then thou shalt put the miter vpon his head, and shalt put the holy crowne vpon ye miter.
7 Ndipo utakapotwaa hayo mafuta ya kutiwa, na kummiminia kichwani mwake, na kumtia mafuta.
And thou shalt take the anoynting oyle, and shalt powre vpon his head, and anoynt him.
8 Kisha walete hao wanawe na kuwavika kanzu.
And thou shalt bring his sonnes, and put coates vpon them,
9 Nawe uwakaze mishipi, Aruni na wanawe, na kuwavika kofia. Nao watakuwa na huo ukuhani kwa amri ya milele. Nawe utawaweka Haruni na wanawe kwa kazi takatifu.
And shalt girde them with girdles, both Aaron and his sonnes: and shalt put the bonets on them, and the Priestes office shalbe theirs for a perpetuall lawe: thou shalt also fill the hands of Aaron, and the hands of his sonnes.
10 Kisha utamleta huyo ng’ombe mbele ya hema ya kukutania; na Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo ng’ombe.
After, thou shalt present the calfe before the Tabernacle of the Congregation, and Aaron and his sonnes shall put their handes vpon the head of the calfe.
11 Kisha utamchinja huyo ng’ombe mbele ya Yahweh pa hema ya kukutania. BWANA,
So thou shalt kill the calfe before the Lord, at the doore of the Tabernacle of the Congregation.
12 Kisha twaa baadhi ya damu ya ng’ombe, uitie katika pembe za madhabahu kwa kidole chako; na kuimimina damu yote chini ya madhabahu.
Then thou shalt take of the blood of the calfe, and put it vpon the hornes of the altar with thy finger, and shalt powre al the rest of the blood at the foote of the altar.
13 Kisha chukuwa mafuta yote yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo juu yake, uyateketeze yote juu ya madhabahu.
Also thou shalt take all the fat that couereth the inwardes, and the kall, that is on the liuer, and the two kidneis, and the fat that is vpon them, and shalt burne them vpon the altar.
14 Lakini nyama yake huyo ng’ombe, na ngozi yake, na mavi yake, utayachoma kwa moto nje ya marago; ni sadaka kwa ajili ya dhambi.
But the flesh of the calfe, and his skin, and his doung shalt thou burne with fire without the hoste: it is a sinne offring.
15 Pia mtwae kondoo mume mmoja; na Aruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake huyo kondoo mume.
Thou shalt also take one ramme, and Aron and his sonnes shall put their hands vpon the head of the ramme.
16 Kisha utamchinja huyo kondoo mume, na kuitwaa damu yake, na kuinyunyiza katika madhabahu kuizunguka kando-kando.
Then thou shalt kill the ramme, and take his blood, and sprinkle it round about vpon the altar,
17 Kisha utamkata-kata kondoo vipande vyake, na kuyaosha matumbo yake na miguu yake, na kuiweka pamoja na vipande vyake na kichwa chake,
And thou shalt cut the ramme in pieces, and wash the inwards of him and his legges, and shalt put them vpon the pieces thereof, and vpon his head.
18 nawe mteketeze kondoo mzima juu ya madhabahu. Ni sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yaYahweh; ni harufu nzuri, sadaka iliyosongezwa kwa Yahweh kwa njia ya moto.
So thou shalt burne the whole ram vpon the altar: for it is a burnt offering vnto the Lord for a sweete sauour: it is an offering made by fire vnto the Lord.
19 Kisha mtwae huyo kondoo mwingine; na Aruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake huyo kondoo.
And thou shalt take the other ramme, and Aaron and his sonnes shall put their handes vpon the head of the ramme.
20 Kisha utamchinja kondoo, na kuitwaa damu yake, na kuitia katika ncha ya sikio la Aruni la upande wa kuume, na katika ncha za masikio ya kuume ya wanawe, na katika vyanda vya gumba vya mikono yao ya kuume, na katika vidole vikuu vya miguu yao ya kuume, na kuinyunyiza hiyo damu katika madhabahu kuizunguka kando-kando.
Then thou shalt kill the ramme, and take of his blood and put it vpon the lappe of Aarons eare, and vpon the lappe of the right eare of his sonnes, and vpon the thumbe of their right hand, and vpon the great toe of their right foote, and shalt sprinkle the blood vpon ye altar roud about.
21 Kisha twaa katika hiyo damu iliyo juu ya madhabahu, na katika hayo mafuta ya kutiwa, na kumnyunyizia Aruni, juu ya mavazi yake, na wanawe, na mavazi yao pia, pamoja naye; naye atatakaswa, na mavazi yake, na wanawe, na mavazi ya wanawe, pamoja naye.
And thou shalt take of the blood that is vpon the altar, and of the anoynting oyle, and shalt sprinkle it vpon Aaron, and vpon his garments, and vpon his sonnes, and vpon the garments of his sonnes with him: so he shall be halowed, and his clothes, and his sonnes, and the garments of his sonnes with him.
22 Tena yatwae mafuta ya huyo kondoo mume, na mkia wake wa mafuta, na mafuta yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo katika hizo figo, na paja la kuume; kwani ni kondoo ambaye ni wa kuwekwa kwa kazi takatifu.
Also thou shalt take of the rammes ye fatte and the rumpe, euen the fat that couereth the inwards, and the kall of the liuer, and the two kidneis, and the fat that is vpon them, and the right shoulder, (for it is the ramme of consecration)
23 Utwae na mkate mmoja wa unga, na mkate mmoja ulioandaliwa kwa mafuta, na kaki moja katika kile kikapu cha mikate isiyotiwa chachu, kilichowekwa mbele ya Yahweh.
And one loafe of bread, and one cake of bread tempered with oyle, and one wafer, out of the basket of the vnleauened bread that is before the Lord.
24 Nawe utavitia hivi vyote katika mikono ya Aruni, na katika mikono ya wanawe; nawe utavitikisa-tikisa viwe sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.
And thou shalt put al this in the handes of Aaron, and in the handes of his sonnes, and shalt shake them to and from before the Lord.
25 Kisha uvitwae vile vitu mikononi mwao, na kuviteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa, viwe harufu nzuri mbele yangu; ni sadaka iliyotengenezwa kwangu kwa njia ya moto.
Againe, thou shalt receyue them of their handes, and burne them vpon the altar besides the burnt offring for a sweete sauour before ye Lord: for this is an offering made by fire vnto the Lord.
26 Kisha twaa kidari cha huyo kondoo wa kuwekwa kwake Haruni kwa kazi takatifu, na kukitikisa-tikisa kiwe sadaka ya kutikiswa mbele za Yahwe nacho kitakuwa ni sehemu yako.
Likewise thou shalt take the brest of the ram of the consecration, which is for Aaron, and shalt shake it to and from before the Lord and it shalbe thy part.
27 Nawe kitakase kile kidari cha ile sadaka ya kutikiswa, na lile paja la sadaka ya kuinuliwa, lililotikiswa, na lililoinuliwa juu, vya yule kondoo wa kuwekwa kwa kazi takatifu, huyo aliyekuwa kwa ajili ya Aruni na wanawe.
And thou shalt sanctifie the brest of the shaken offering, and the shoulder of the heaue offering, which was shaken to and from, and which was heaued vp of the ramme of the consecration, which was for Aaron, and which was for his sonnes.
28 Navyo vitakuwa vya Haruni na wanawe posho ya lazima sikuzote itokayo kwa hao wana wa Israeli; kwa kuwa ni sadaka ya kuinuliwa; nayo itakuwa ni sadaka ya kuinuliwa itokayo kwa hao wana wa Israeli katika dhabihu zao za sadaka za amani, ni sadaka yao ya kuinuliwa kwa ajili ya Yahweh.
And Aaron and his sonnes shall haue it by a statute for euer, of the children of Israel: for it is an heaue offering, and it shall be an heaue offering of the children of Israel, of their peace offerings, euen their heaue offering to the Lord.
29 Na hayo mavazi matakatifu ya Aruni yatakuwa ya wanawe baada yake, wayavae watakapotiwa mafuta, na watakapowekwa kwa kazi takatifu.
And the holy garmets, which appertaine to Aaron, shall bee his sonnes after him, to bee anoynted therein, and to bee consecrate therein.
30 Huyo mwanawe atakayekuwa kuhani badala yake atayavaa muda wa siku saba, hapo atakapoingia ndani ya hiyo hema ya kukutania, ili atumike ndani ya mahali patakatifu.
That sonne that shalbe Priest in his steade, shall put them on seuen dayes, when he commeth into the Tabernacle of the Congregation to minister in the holy place.
31 Nawe twaa huyo kondoo mume aliyekuwa wa kuwekwa kwa kazi takatifu, na kuitokosa nyama yake katika mahali patakatifu.
So thou shalt take the ram of the consecration, and seeth his flesh in the holy place.
32 Na Aruni na wanawe wataila ile nyama ya kondoo, na mikate iliyo katika kile kikapu, hapo mbele ya mlango wa hema ya kukutania.
And Aaron and his sonnes shall eate the flesh of the ram, and the bread that is in the basket, at the doore of ye Tabernacle of ye Congregation.
33 Nao watakula vile vitu ambavyo upatanisho ulifanywa kwa hivyo, ili kuwaweka kwa kazi takatifu na kuwatakasa; lakini mgeni asivile, maana, ni vitu vitakatifu.
So they shall eate these thinges, whereby their attonement was made, to consecrate them, and to sanctifie them: but a stranger shall not eate thereof, because they are holy things.
34 Na kwamba kitu cho chote cha ile nyama, iliyo kwa ajili ya kuweka kwa kazi takatifu, au cho chote cha hiyo mikate, kikisalia hata asubuhi, ndipo utavichoma kwa moto hivyo vilivyosalia; havitaliwa, maana, ni vitu vitakatifu
Now if ought of the flesh of the consecration, or of the bread remaine vnto the morning, then thou shalt burne the rest with fire: it shall not be eaten, because it is an holie thing.
35 Ni hivyo utakavyowatendea Aruni na wanawe kama nilivyo kuagiza. Utawaweka kwa kazi takatifu siku saba.
Therefore shalt thou doe thus vnto Aaron and vnto his sonnes, according to all things, which I haue commanded thee: seuen dayes shalt thou consecrate them,
36 Kila siku utamtoa ng’ombe wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho; nawe utaisafisha hiyo madhabahu, hapo utakapofanya upatanisho kwa ajili ya hiyo madhabahu; nawe utaitia mafuta, ili kuitakasa.
And shalt offer euery day a calfe for a sinne offring, for reconciliation: and thou shalt cleanse the altar, when thou hast offred vpon it for reconciliation, and shalt annoynt it, to sanctifie it.
37 Utafanya upatanisho kwa ajili ya hiyo madhabahu muda wa siku saba, na kuitakasa; ndipo madhabahu itakapokuwa takatifu sana; kila kitu kiigusacho madhabahu kitakuwa kitakatifu.
Seuen dayes shalt thou cleanse the altar, and sanctifie it, so the altar shalbe most holy: and whatsoeuer toucheth the altar, shalbe holy.
38 Lazima utoe kwenye madhabahu wana-kondoo wa mwaka mmoja wawili siku baada ya siku
Nowe this is that which thou shalt present vpon the altar: euen two lambes of one yere olde, day by day continually.
39 daima. Mwana-kondoo mmoja utamchinja asubuhi; na mwana-kondoo wa pili utamchinja jioni
The one lambe thou shalt present in the morning, and the other lambe thou shalt present at euen.
40 Pamoja na mwana-kondoo mmoja utatoa vibaba vitatu vya unga mzuri uliochanganyika na mafuta yenye kupondwa, kiasi cha kibaba na robo kibaba; na divai kiasi cha kibaba na robo kibaba, iwe sadaka ya kinywaji.
And with the one lambe, a tenth part of fine floure mingled with the fourth part of an Hin of beaten oyle, and the fourth part of an Hin of wine, for a drinke offring.
41 Na huyo mwana-kondoo wa pili utamchinja wakati wa jioni. Nawe utamfanyia vivyo kama ile sadaka ya unga ya asubuhi, na kama ile sadaka yake ya kinywaji. Hii itatoa harufu nzuri, ni dhabihu ya kusongezwa kwangu kwa njia ya moto.
And the other lambe thou shalt present at euen: thou shalt doe thereto according to the offring of the morning, and according to the drinke offring thereof, to be a burnt offring for a sweete sauour vnto, the Lord.
42 Itakuwa ni sadaka ya kuteketezwa milele katika vizazi vyenu vyote mlangoni pa ile hema ya kukutania mbele ya Yahweh, hapo nitakapokutana nanyi, ili niseme na wewe hapo.
This shalbe a continuall burnt offring in your generations at the doore of the Tabernacle of the Congregation before the Lord, where I wil make appoyntment with you, to speake there vnto thee.
43 Nami nitakutana na wana wa Israeli hapo; na hiyo hema itafanywa takatifu na utukufu wangu. Nami nitaitakasa hiyo hema ya kukutania, na hiyo madhabahu.
There I will appoynt with the children of Israel, and the place shall bee sanctified by my glorie.
44 Pia Aruni na wanawe nitawatakasa, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
And I will sanctifie the Tabernacle of the Congregation and the altar: I will sanctifie also Aaron and his sonnes to be my Priests,
45 Na mimi nitakaa kati ya wana wa Israeli, nami nitakuwa Mungu wao.
And I will dwell among the children of Israel, and will bee their God.
46 Nao watanijua kuwa mimi ndimi Yahweh, Mungu wao, niliyewaleta watoke katika nchi ya Misri, nipate kukaa kati yao. Ni mimi Yahweh, Mungu wao.
Then shall they knowe that I am ye Lord their God, that brought them out of the lande of Egypt, that I might dwell among them: I am the Lord their God.