< Kutoka 28 >

1 Umuite Aruni kaka yako na wana wake - Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari - miongoni mwa wana wa Israeli, ili anitumikie katika kazi ya ukuhani.
A ty weźmij do siebie Aarona, brata twego, i syny jego z nim, z pośrodku synów Izraelskich, aby mi urząd kapłański odprawowali, Aaron, Nadab i Abiu, Eleazar, i Itamar, synowie Aaronowi.
2 Nawe utamfanyia Aruni ndugu yako mavazi matakatifu, kwa utukufu na kwa uzuri.
A sprawisz szaty święte Aaronowi, bratu twemu, na cześć i na ozdobę.
3 Nawe utawaambia watu wote wenye moyo wa hekima, niliowajaza na roho ya hekima wamfanyie Aruni mavazi ili kumtakasa anitumikie katika kazi ya ukuhani.
Ty się też rozmówisz z każdym umiejętnym rzemieślnikiem, któregom napełnił Duchem mądrości, aby urobili szaty Aaronowi na poświęcenie jego, aby mi urząd kapłański odprawował.
4 Na mavazi watakayoyafanya ni kifuko cha kifuani, na naivera, na joho, na kanzu ya kazi ya urembo, na kilemba, na mshipi; nao watawafanyia Aruni nduguye, na wanawe, mavazi matakatifu ili anitumikie katika kazi ya ukuhani.
A teć są szaty, które urobią: Napierśnik, i naramiennik, i płaszcz, i suknia haftowana, czapka i pas. I urobią te szaty święte Aaronowi bratu twemu i synom jego, aby mi kapłański urząd sprawowali.
5 Nao wataitwaa dhahabu, na nguo ya rangi ya samawi, na ya rangi ya zambarau, na ya rangi nyekundu.
I nabiorą złota, i hijacyntu, i szarłatu, i karmazynu dwa kroć farbowanego, i jedwabiu białego.
6 Nao waifanye naivera kwa nyuzi za dhahabu, na za samawi, na za zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa kwa kazi ya mstadi.
I uczynią naramiennik ze złota, i z hijacyntu, i z szarłatu, z karmazynu dwa kroć farbowanego, i z jedwabiu białego kręconego, robotą haftarską.
7 Lazima itakuwa na vipande viwili vya mabegani, vilivyoungana kwenye ncha zake mbili; ili ipate kuunganywa.
Dwa zwierzchne kraje zszyte mieć będzie na dwu końcach swych, a tak społu spięte będą.
8 Na mshipi wa kazi ya ustadi ulio juu yake, ili kuifunga mahali pake; utakuwa wa kazi kama ile ya naivera, ya vitu vile vile ya nyuzi za dhahabu, na za rangi ya samawi, na ya zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa.
A przepasanie naramiennika tego, które na nim będzie, podobne będzie robocie jego; będzie także ze złota, z hijacyntu, i z szarłatu, i z karmazynu dwa kroć farbowanego, i z jedwabiu białego kręconego.
9 Nawe utatwaa vito viwili vya shohamu, ya rangi ya chani-kiwiti, nawe utachora juu yake majina ya wana wa Israeli;
I weźmiesz dwa kamienie onychiny, i wyryjesz na nich imiona synów Izraelskich;
10 Majina yao sita katika kito kimoja, na majina sita yaliyosalia katika kile kito cha pili, kwa utaratibu wa kuzaliwa kwao.
Sześć imion ich na jednym kamieniu, a imion sześć drugich na drugim kamieniu, według narodzenia ich.
11 Kwa kazi mtu mwenye kuchora mawe kama vile muhuri ichorwavyo, utavichora hivi vito viwili, sawasawa na majina ya wana wa Israeli, nawe utavitia katika vijalizo vya dhahabu.
Robotą snycerzów, którzy kamienie rzezą, wyryjesz na obu kamieniach imiona synów Izraelskich, i osadzisz je we złote osadzenia.
12 Nawe utavitia vile vito viwili juu ya vipande vya mabegani vya hiyo naivera, viwe vito vya ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli. Naye Aruni atayachukua majina yao mbele za Yahweh juu ya mabega yake mawili ili kuwa ukumbusho.
I położysz te obadwa kamienie na wierzchnich krajach naramiennika, kamienie pamiątki dla synów Izraelskich; i nosić będzie Aaron imiona ich przed Panem na obu ramionach swych na pamiątkę.
13 Nawe fanya vijalizo viwili vya dhahabu
Uczynisz też haczyki złote.
14 na mikufu miwili ya dhahabu safi; utaifanya iwe mfano wa kamba, ya kazi ya kusokotwa; nawe uitie ile mikufu ya kazi ya kusokotwa katika vile vijalizo.
Dwa też łańcuszki ze złota szczerego jednostajne; uczynisz je robotą plecioną, i zawiesisz te łańcuszki plecione na haczykach.
15 Nawe lazima utafanya kifuko cha kifuani cha hukumu, kazi ya fundi stadi; utakifanya kwa kuiandama ile kazi ya hiyo naivera. Fanya nyuzi za dhahabu, na za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na nyekundu, na kitani safi yenye kusokotwa, ndivyo utakavyokifanya.
Uczynisz też napierśnik sądu robotą haftarską, według roboty naramiennika urobisz go; ze złota, z hijacyntu, i z szarłatu, i z karmazynu dwa kroć farbowanego, i z białego jedwabiu kręconego uczynisz go.
16 Kitakuwa mraba, tena cha kukunjwa; urefu wake utakuwa shibiri moja, na upana wake shibiri moja.
Czworograniasty będzie i dwoisty, na piędzi długość jego, i na piędzi szerokość jego.
17 Nawe ukijaze viweko vya vito, safu nne za vito; safu moja itakuwa ni akiki, na yakuti ya rangi ya manjano, na baharamani, hivi vitakuwa safu ya kwanza.
I nasadzisz weń pełno kamienia, cztery rzędy kamienia, tym porządkiem: sardyjusz, topazyjusz i szmaragd w pierwszym rzędzie;
18 Na safu ya pili itakuwa zumaridi, na yakuti samawi, na almasi.
W drugim zasię rzędzie: karbunkuł, szafir, i jaspis.
19 Na safu ya tatu itakuwa hiakintho, na akiki nyekundu, na amethisto.
A w trzecim rzędzie: linkuryjusz, achates, i ametyst.
20 Na safu ya nne itakuwa ni zabarajadi, na shohamu, na yaspi. Vito hivyo vitakazwa ndani ya dhahabu kwa kujaa mahali pake.
A w czwartym rzędzie: chryzolit, onychin i berył; te będą wsadzone w złoto w rzędziech swoich.
21 Na vile vito vitakuwa sawasawa na majina ya wana wa Israeli, kumi na viwili, sawasawa na majina yao. Mfano wa kuchora kwa muhuri kila kimoja sawasawa na jina lake, vitakuwa vya hizo kabila kumi na mbili.
A tych kamieni z imionami synów Izraelskich będzie dwanaście według imion ich; tak jako rzezą pieczęci, każdy według imienia swego będą, dla dwunastu pokoleń.
22 Nawe lazima utie katika kile kifuko cha kifuani mikufu mfano wa kamba, ya kazi ya kusokotwa, ya dhahabu safi.
Uczynisz też do napierśnika łańcuszki jednostajne robotą plecioną ze złota szczerego.
23 Nawe utie maduara mawili ya dhahabu katika kile kifuko cha kifuani, na kuzitia hizo pete mbili katika ncha mbili za kifuko cha kifuani.
Uczynisz też do napierśnika dwa kolce złote, i przyprawisz te dwa kolce do obu krajów napierśnika.
24 Nawe utie hiyo mikufu miwili ya dhahabu iliyosokotwa katika zile pete mbili zilizo katika ncha za kifuko cha kifuani.
I przewleczesz dwa łańcuszki złote przez oba kolce u krajów napierśnika.
25 Na ncha zile nyingine za hiyo mikufu miwili ya kusokotwa utazitia katika vile vijalizo viwili, na kuvitia katika vile vipande vya mabegani vya naivera upande wa mbele.
Drugie zasię dwa kolce dwu łańcuszków zawleczesz na dwa haczyki, i przyprawisz do wierzchnich krajów naramiennika na przodku.
26 Nawe utafanya viduara vili vya dhahabu, uzitie katika hizo ncha mbili za kifuko cha kifuani, katika ukingo wake.
Uczynisz też dwa kolce złote, które przyprawisz do dwu końców napierśnika na kraju jego, który jest od naramiennika ze spodku.
27 Nawe lazima ufanye viduara vili vya dhahabu, na kuzitia katika vile vipande viwili vya mabegani vya ile naivera chini yake, upande wa mbele, karibu na kifungo chake, juu ya huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi.
Do tego uczynisz dwa drugie kolce złote, które przyprawisz na dwie strony naramiennika ze spodku na przeciwko spojeniu jego, z wierzchu nad przepasaniem naramiennika.
28 Nao watakikaza kile kileso kwa vile viduara vyake kwenye viduara za naivera kwa ukanda wa rangi ya samawi, ili kwamba kikae pale juu ya ule mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi, ili kwamba kifuko cha kifuani kisiachane na naivera.
Tak zwiążą napierśnik ten kolce jego z kolcami naramiennika sznurem hijacyntowym, aby był nad przepasaniem naramiennika, żeby nie odstawał napierśnik od naramiennika.
29 Na Aruni atayachukua majina ya wana wa Israeli katika kile kifuko cha kifuani cha hukumu juu ya moyo wake kwa kufanya maamuzi, hapo atakapoingia ndani ya mahali patakatifu, kuwa ukumbusho mbele yaYahweh daima.
I będzie nosił Aaron imiona synów Izraelskich na napierśniku sądu, na piersiach swych, gdy będzie wchodził do świątnicy, na pamiątkę ustawiczną przed Panem.
30 Nawe utie hizo Urimu na Thumimu katika kile kifuko cha kifuani cha hukumu; nazo zitakuwa juu ya moyo wa Aruni, hapo atakapoingia ndani mbele ya Yahweh na Aruni atachukua hukumu ya hao wana wa Israeli juu ya moyo wake mbele ya Yahweh daima.
Położysz też na napierśniku sądu Urim i Tummim, które będą na piersiach Aaronowych, gdy wchodzić będzie przed Pana; i poniesie Aaron sąd synów Izraelskich na piersiach przed Panem ustawicznie.
31 Nawe fanya hiyo joho ya naivera ya rangi ya samawi yote.
Uczynisz też płaszcz pod naramiennik, wszystek z hijacyntu.
32 Nayo itakuwa na tundu katikati yake kwa kupitisha kichwa; itakuwa na utepe wa kazi ya kusokotwa kuzunguka hilo tundu lake, mfano wa tundu lililo katika kanzu ya chuma, ili lisipasuke.
A na wierzchu w pośród jego będzie rozpór, który rozpór obwiedziesz bramą plecioną w pancerzowy wzór, aby się nie rozdzierał.
33 Nawe katika pindo zake utatia makomamanga ya rangi ya samawi, na ya rangi ya zambarau, na ya rangi nyekundu, kuzunguka pindo zake kotekote; na njuga za dhahabu kati ya hayo makomamanga pande zote.
Uczynisz też na podołku jego jabłka granatowe z hijacyntu, i z szarłatu, i z karmazynu dwa kroć farbowanego na podołku jego w około, a dzwonki złote między niemi w około.
34 Kengele ya dhahabu na komamanga, kengele ya dhahabu na komamanga, katika pindo za joho kuizunguka pande zote.
Dzwonek złoty a jabłko granatowe; i zaś dzwonek złoty i jabłko granatowe u podołka płaszcza w około.
35 Nayo itakuwa juu ya Aruni akitumika; na sauti ya hizo kengele itasikilikana hapo aingiapo ndani ya mahali patakatifu mbele ya Yahweh na hapo atokapo nje, ili kwamba asife.
A będzie to miał na sobie Aaron przy posługiwaniu, aby słyszany był dźwięk jego, gdy będzie wchodził do świątnicy przed Pana, i gdy zaś wychodzić będzie, żeby nie umarł.
36 Nawe fanya bamba la dhahabu safi na kuchora juu yake, mfano wa machoro ya muhuri, “Mtakatifu kwa Yahweh.”
Uczynisz też blachę ze złota szczerego, a wyryjesz na niej robotą tych, co pieczęci rzezą: Świętość Panu.
37 Nawe ulitie hilo bamba katika ukanda wa rangi ya samawi, nalo litakuwa katika kile kilemba; litakuwa upande wa mbele wa kile kilemba.
Tę przywiążesz do sznuru hijacyntowego, i będzie na czapce; na przodku na czapce będzie.
38 Nalo litakuwa katika kipaji cha uso cha Aruni, na Aruni atauchukua uovu wa vile vitu vitakatifu, watakavyovitakasa hao wana wa Israeli katika vipawa vyao vyote vitakatifu, nalo litakuwa katika kipaji chake cha uso sikuzote, ili kwamba vipate kukubaliwa mbele za Yahweh.
A ta będzie nad czołem Aaronowem, aby nosił Aaron nieprawość poświęconych rzeczy, które by poświęcali synowie Izraelscy przy wszystkich darach poświęconych rzeczy swych; a będzie nad czołem jego ustawicznie, aby im zjednał łaskę u Pana.
39 Na hiyo kanzu utaifuma ya kitani nzuri ya kazi ya urembo, ufanye na kilemba cha nguo ya kitani nzuri, nawe utafanya mshipi wa kazi ya mwenye kutia taraza.
Sprawisz też szatę z białego jedwabiu dzianą; także uczynisz czapkę z jedwabiu białego, pas też uczynisz robotą haftarską.
40 Kisha utafany kanzu kwa ajili ya wana wa Aruni, nawe wafanyie mishipi, wafanyie na kofia kwa utukufu na uzuri.
Synom także Aaronowym poczynisz szaty; i poczynisz im pasy, i czapki im poczynisz na cześć i na ozdobę.
41 Nawe mvike huyo nduguye Aruni na wanawe nao mavazi hayo; nawe watie mafuta, na kuwaweka kwa kazi takatifu, na kuwatakasa, ili wapate kunitumikia mimi katika kazi ya ukuhani.
A ubierzesz w nie Aarona, brata twego, i syny jego z nim; i pomażesz je, a napełnisz ręce ich, i poświęcisz je, aby mi urząd kapłański sprawowali.
42 Nawe wafanyie suruali za nguo ya kitani, ili kufunika tupu ya miili yao; suruali hizo zitafika tangu kiunoni hata mapajani.
Urobisz im też ubiory lniane, dla zakrycia nagości ciała; od biódr aż do udów będą.
43 Aruni na wanawe watazivaa, hapo watakapoingia katika hema ya kukutania, au hapo watakapoikaribia madhabahu ili watumike katika mahali patakatifu; wasije wakachukua uovu, wakafa; hii itakuwa ni amri ya milele kwake yeye, na kwa wazao wake.
A będą na Aaronie i na synach jego, gdy wchodzić będą do namiotu zgromadzenia, albo gdy będą przystępować do ołtarza, aby służyli w świątnicy, żeby niosąc nieprawość, nie pomarli. Ustawa to wieczna będzie jemu, i nasieniu jego po nim.

< Kutoka 28 >