< Kutoka 28 >

1 Umuite Aruni kaka yako na wana wake - Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari - miongoni mwa wana wa Israeli, ili anitumikie katika kazi ya ukuhani.
« Fais venir auprès de toi Aaron, ton frère, et ses fils avec lui, du milieu des enfants d'Israël, afin qu'il soit à mon service dans le sacerdoce: Aaron, avec Nadab, Abihu, Éléazar et Ithamar, fils d'Aaron.
2 Nawe utamfanyia Aruni ndugu yako mavazi matakatifu, kwa utukufu na kwa uzuri.
Tu feras à Aaron, ton frère, des vêtements sacrés, pour sa gloire et sa beauté.
3 Nawe utawaambia watu wote wenye moyo wa hekima, niliowajaza na roho ya hekima wamfanyie Aruni mavazi ili kumtakasa anitumikie katika kazi ya ukuhani.
Tu parleras à tous ceux qui ont le cœur sage, que j'ai remplis de l'esprit de sagesse, pour qu'ils fassent les vêtements d'Aaron afin de le sanctifier, pour qu'il soit à mon service dans le sacerdoce.
4 Na mavazi watakayoyafanya ni kifuko cha kifuani, na naivera, na joho, na kanzu ya kazi ya urembo, na kilemba, na mshipi; nao watawafanyia Aruni nduguye, na wanawe, mavazi matakatifu ili anitumikie katika kazi ya ukuhani.
Voici les vêtements qu'ils feront: un pectoral, un éphod, une robe, une tunique ajustée, un turban et une ceinture. Ils feront des vêtements sacrés pour Aaron, ton frère, et pour ses fils, afin qu'ils soient à mon service dans le sacerdoce.
5 Nao wataitwaa dhahabu, na nguo ya rangi ya samawi, na ya rangi ya zambarau, na ya rangi nyekundu.
Ils utiliseront l'or, le bleu, le pourpre, l'écarlate et le lin fin.
6 Nao waifanye naivera kwa nyuzi za dhahabu, na za samawi, na za zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa kwa kazi ya mstadi.
« On fera l'éphod d'or, de bleu, de pourpre, d'écarlate et de fin lin retors, ouvrage d'un habile ouvrier.
7 Lazima itakuwa na vipande viwili vya mabegani, vilivyoungana kwenye ncha zake mbili; ili ipate kuunganywa.
Il aura deux bretelles attachées à ses deux extrémités, afin qu'on puisse le joindre.
8 Na mshipi wa kazi ya ustadi ulio juu yake, ili kuifunga mahali pake; utakuwa wa kazi kama ile ya naivera, ya vitu vile vile ya nyuzi za dhahabu, na za rangi ya samawi, na ya zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa.
La ceinture qui l'entourera sera semblable à son ouvrage et de la même pièce, en or, en bleu, en pourpre, en cramoisi et en fin lin retors.
9 Nawe utatwaa vito viwili vya shohamu, ya rangi ya chani-kiwiti, nawe utachora juu yake majina ya wana wa Israeli;
Tu prendras deux pierres d'onyx, et tu graveras sur elles les noms des enfants d'Israël.
10 Majina yao sita katika kito kimoja, na majina sita yaliyosalia katika kile kito cha pili, kwa utaratibu wa kuzaliwa kwao.
Six de leurs noms sur l'une des pierres, et les noms des six autres sur l'autre pierre, dans l'ordre de leur naissance.
11 Kwa kazi mtu mwenye kuchora mawe kama vile muhuri ichorwavyo, utavichora hivi vito viwili, sawasawa na majina ya wana wa Israeli, nawe utavitia katika vijalizo vya dhahabu.
Avec le travail d'un graveur sur pierre, comme les gravures d'un sceau, tu graveras les deux pierres, selon les noms des enfants d'Israël. Tu les feras enfermer dans des montures d'or.
12 Nawe utavitia vile vito viwili juu ya vipande vya mabegani vya hiyo naivera, viwe vito vya ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli. Naye Aruni atayachukua majina yao mbele za Yahweh juu ya mabega yake mawili ili kuwa ukumbusho.
Tu mettras les deux pierres sur les bretelles de l'éphod, comme pierres de souvenir pour les enfants d'Israël. Aaron portera leurs noms devant Yahvé sur ses deux épaules, en souvenir.
13 Nawe fanya vijalizo viwili vya dhahabu
Tu feras des montures d'or,
14 na mikufu miwili ya dhahabu safi; utaifanya iwe mfano wa kamba, ya kazi ya kusokotwa; nawe uitie ile mikufu ya kazi ya kusokotwa katika vile vijalizo.
et deux chaînettes d'or pur; tu les feras comme des cordons tressés. Tu mettras les chaînettes tressées sur les montures.
15 Nawe lazima utafanya kifuko cha kifuani cha hukumu, kazi ya fundi stadi; utakifanya kwa kuiandama ile kazi ya hiyo naivera. Fanya nyuzi za dhahabu, na za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na nyekundu, na kitani safi yenye kusokotwa, ndivyo utakavyokifanya.
« Tu feras un pectoral de jugement, ouvrage d'un habile ouvrier; tu le feras comme l'ouvrage de l'éphod; tu le feras d'or, de bleu, de pourpre, d'écarlate, et de fin lin retors.
16 Kitakuwa mraba, tena cha kukunjwa; urefu wake utakuwa shibiri moja, na upana wake shibiri moja.
Il sera carré et plié en deux; sa longueur sera d'un empan, et sa largeur d'un empan.
17 Nawe ukijaze viweko vya vito, safu nne za vito; safu moja itakuwa ni akiki, na yakuti ya rangi ya manjano, na baharamani, hivi vitakuwa safu ya kwanza.
Tu y sertiras des pierres, quatre rangées de pierres: une rangée de rubis, de topaze et de béryl pour la première rangée;
18 Na safu ya pili itakuwa zumaridi, na yakuti samawi, na almasi.
une deuxième rangée de turquoise, de saphir et d'émeraude;
19 Na safu ya tatu itakuwa hiakintho, na akiki nyekundu, na amethisto.
une troisième rangée de jacinthe, d'agate et d'améthyste;
20 Na safu ya nne itakuwa ni zabarajadi, na shohamu, na yaspi. Vito hivyo vitakazwa ndani ya dhahabu kwa kujaa mahali pake.
une quatrième rangée de chrysolithe, d'onyx et de jaspe. Ils seront entourés d'or dans leurs montures.
21 Na vile vito vitakuwa sawasawa na majina ya wana wa Israeli, kumi na viwili, sawasawa na majina yao. Mfano wa kuchora kwa muhuri kila kimoja sawasawa na jina lake, vitakuwa vya hizo kabila kumi na mbili.
Les pierres seront selon les noms des enfants d'Israël, douze, selon leurs noms; comme les gravures d'un cachet, chacun selon son nom, elles seront pour les douze tribus.
22 Nawe lazima utie katika kile kifuko cha kifuani mikufu mfano wa kamba, ya kazi ya kusokotwa, ya dhahabu safi.
Tu feras sur le pectoral des chaînettes semblables à des cordons, tressées d'or pur.
23 Nawe utie maduara mawili ya dhahabu katika kile kifuko cha kifuani, na kuzitia hizo pete mbili katika ncha mbili za kifuko cha kifuani.
Tu feras sur le pectoral deux anneaux d'or, et tu mettras les deux anneaux aux deux extrémités du pectoral.
24 Nawe utie hiyo mikufu miwili ya dhahabu iliyosokotwa katika zile pete mbili zilizo katika ncha za kifuko cha kifuani.
Tu mettras les deux chaînes d'or tressées dans les deux anneaux, aux extrémités du pectoral.
25 Na ncha zile nyingine za hiyo mikufu miwili ya kusokotwa utazitia katika vile vijalizo viwili, na kuvitia katika vile vipande vya mabegani vya naivera upande wa mbele.
Tu mettras les deux autres extrémités des deux chaînettes tressées sur les deux montures, et tu les mettras sur les bretelles de l'éphod dans sa partie antérieure.
26 Nawe utafanya viduara vili vya dhahabu, uzitie katika hizo ncha mbili za kifuko cha kifuani, katika ukingo wake.
Tu feras deux anneaux d'or, et tu les mettras aux deux extrémités du pectoral, sur son bord, qui est du côté de l'éphod, vers l'intérieur.
27 Nawe lazima ufanye viduara vili vya dhahabu, na kuzitia katika vile vipande viwili vya mabegani vya ile naivera chini yake, upande wa mbele, karibu na kifungo chake, juu ya huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi.
Tu feras deux anneaux d'or, et tu les mettras sur les deux bretelles de l'éphod, en dessous, dans sa partie antérieure, près de son attache, au-dessus de la bande habilement tissée de l'éphod.
28 Nao watakikaza kile kileso kwa vile viduara vyake kwenye viduara za naivera kwa ukanda wa rangi ya samawi, ili kwamba kikae pale juu ya ule mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi, ili kwamba kifuko cha kifuani kisiachane na naivera.
On attachera le pectoral par ses anneaux aux anneaux de l'éphod, avec un lacet bleu, pour qu'il soit sur la ceinture de l'éphod et que le pectoral ne se détache pas de l'éphod.
29 Na Aruni atayachukua majina ya wana wa Israeli katika kile kifuko cha kifuani cha hukumu juu ya moyo wake kwa kufanya maamuzi, hapo atakapoingia ndani ya mahali patakatifu, kuwa ukumbusho mbele yaYahweh daima.
Aaron portera sur son cœur les noms des enfants d'Israël dans le pectoral du jugement, lorsqu'il entrera dans le sanctuaire, en souvenir permanent devant l'Éternel.
30 Nawe utie hizo Urimu na Thumimu katika kile kifuko cha kifuani cha hukumu; nazo zitakuwa juu ya moyo wa Aruni, hapo atakapoingia ndani mbele ya Yahweh na Aruni atachukua hukumu ya hao wana wa Israeli juu ya moyo wake mbele ya Yahweh daima.
Tu mettras dans le pectoral du jugement l'urim et le thummim, et ils seront sur le cœur d'Aaron, lorsqu'il entrera devant l'Éternel. Aaron portera sur son cœur le jugement des enfants d'Israël, devant Yahvé, en permanence.
31 Nawe fanya hiyo joho ya naivera ya rangi ya samawi yote.
« Tu feras la robe de l'éphod toute bleue.
32 Nayo itakuwa na tundu katikati yake kwa kupitisha kichwa; itakuwa na utepe wa kazi ya kusokotwa kuzunguka hilo tundu lake, mfano wa tundu lililo katika kanzu ya chuma, ili lisipasuke.
Elle sera percée en son milieu d'un trou pour la tête. Il sera entouré d'une bordure tissée, comme le trou d'une cotte de mailles, afin qu'il ne se déchire pas.
33 Nawe katika pindo zake utatia makomamanga ya rangi ya samawi, na ya rangi ya zambarau, na ya rangi nyekundu, kuzunguka pindo zake kotekote; na njuga za dhahabu kati ya hayo makomamanga pande zote.
Sur son ourlet, tu feras des grenades bleues, pourpres et écarlates, tout autour de l'ourlet, avec des clochettes d'or entre elles et autour d'elles:
34 Kengele ya dhahabu na komamanga, kengele ya dhahabu na komamanga, katika pindo za joho kuizunguka pande zote.
une clochette d'or et une grenade, une clochette d'or et une grenade, autour du bord de la robe.
35 Nayo itakuwa juu ya Aruni akitumika; na sauti ya hizo kengele itasikilikana hapo aingiapo ndani ya mahali patakatifu mbele ya Yahweh na hapo atokapo nje, ili kwamba asife.
Elle sera sur Aaron pour le service; on en entendra le son quand il entrera dans le sanctuaire devant l'Éternel et quand il en sortira, afin qu'il ne meure pas.
36 Nawe fanya bamba la dhahabu safi na kuchora juu yake, mfano wa machoro ya muhuri, “Mtakatifu kwa Yahweh.”
Tu feras une plaque d'or pur, et tu graveras dessus, comme on grave un cachet: « Sainteté à Yahvé ».
37 Nawe ulitie hilo bamba katika ukanda wa rangi ya samawi, nalo litakuwa katika kile kilemba; litakuwa upande wa mbele wa kile kilemba.
Tu la mettras sur un lacet bleu, et elle sera sur la ceinture. Elle sera sur le devant de la ceinture.
38 Nalo litakuwa katika kipaji cha uso cha Aruni, na Aruni atauchukua uovu wa vile vitu vitakatifu, watakavyovitakasa hao wana wa Israeli katika vipawa vyao vyote vitakatifu, nalo litakuwa katika kipaji chake cha uso sikuzote, ili kwamba vipate kukubaliwa mbele za Yahweh.
Elle sera sur le front d'Aaron; Aaron portera l'iniquité des choses saintes que les enfants d'Israël sanctifieront dans tous leurs dons sacrés; elle sera toujours sur son front, afin qu'ils soient agréés devant l'Éternel.
39 Na hiyo kanzu utaifuma ya kitani nzuri ya kazi ya urembo, ufanye na kilemba cha nguo ya kitani nzuri, nawe utafanya mshipi wa kazi ya mwenye kutia taraza.
Tu tisseras la tunique avec du lin fin. Tu feras un turban de fin lin. Tu feras une ceinture, ouvrage du brodeur.
40 Kisha utafany kanzu kwa ajili ya wana wa Aruni, nawe wafanyie mishipi, wafanyie na kofia kwa utukufu na uzuri.
« Tu feras des tuniques pour les fils d'Aaron. Tu leur feras des ceintures. Tu leur feras des bandeaux, pour leur gloire et leur beauté.
41 Nawe mvike huyo nduguye Aruni na wanawe nao mavazi hayo; nawe watie mafuta, na kuwaweka kwa kazi takatifu, na kuwatakasa, ili wapate kunitumikia mimi katika kazi ya ukuhani.
Tu les mettras sur Aaron, ton frère, et sur ses fils avec lui; tu les oindras, tu les consacreras et tu les sanctifieras, afin qu'ils puissent exercer mon ministère dans le cadre du sacerdoce.
42 Nawe wafanyie suruali za nguo ya kitani, ili kufunika tupu ya miili yao; suruali hizo zitafika tangu kiunoni hata mapajani.
Tu leur feras un pantalon de lin pour couvrir leur chair nue. Il ira de la taille jusqu'aux cuisses.
43 Aruni na wanawe watazivaa, hapo watakapoingia katika hema ya kukutania, au hapo watakapoikaribia madhabahu ili watumike katika mahali patakatifu; wasije wakachukua uovu, wakafa; hii itakuwa ni amri ya milele kwake yeye, na kwa wazao wake.
Ils seront sur Aaron et sur ses fils, lorsqu'ils entreront dans la tente de la Rencontre ou lorsqu'ils s'approcheront de l'autel pour faire le service dans le lieu saint, afin qu'ils ne portent pas l'iniquité et ne meurent pas. Ce sera une loi pour lui et pour sa descendance après lui, pour toujours.

< Kutoka 28 >