< Kutoka 27 >

1 Nawe fanya madhabahu ya mti wa mshita, urefu wake utakuwa ni dhiraa tano na upana wake dhiraa tano. Hiyo madhabahu itakuwa mraba na kwenda juu kwake kutakuwa dhiraa tatu.
Tu feras encore un autel de bois de sétim, qui aura cinq coudées en longueur et autant en largeur, c’est-à-dire carré, et trois coudées en hauteur.
2 Nawe fanya pembe nne kama mfano wa pembe za ng'ombe. Hizo pembe zitakuwa za kitu kimoja na madhabahu, nawe utayafunika kwa shaba.
Mais les cornes en sortiront aux quatre angles; et tu le couvriras d’airain.
3 Lazima vyombo vyake vya kuyaondoa majivu yake utavifanya, na majembe yake, na mabakuli yake, na uma zake, na meko yake. Vyombo vyake vyote utavifanya vya shaba.
Et tu feras à son usage des chaudières pour recevoir les cendres, des pincettes, des fourchettes et des brasiers; tu feras tous ces instruments en airain.
4 Nawe uifanyie hiyo madhabahu wavu wa shaba. Kisha utie pete nne za shaba katika hizo pembe nne za ule wavu.
Tu feras encore une grille d’airain en forme de rets: à ses quatre angles seront des anneaux d’airain,
5 Nawe lazima uweke huo wavu chini ya kizingo kiizungukacho madhabahu upande wa chini.
Que tu mettras au-dessous du foyer de l’autel: et la grille viendra jusqu’au milieu de l’autel.
6 Nawe fanya miti kwa ajili ya madhabahu, miti ya mshita, na kuifunika shaba.
Tu feras aussi deux leviers d’autel de bois de sétim, que tu couvriras de lames d’airain:
7 Na hiyo miti itatiwa katika viduara, na ile miti itakuwa katika pande mbili za madhabahu, wakati wa kuichukua.
Et tu les passeras dans les anneaux; et ils seront des deux côtés de l’autel pour le porter.
8 Uifanye ya mbao, yenye mvungu ndani yake kama ulivyooneshwa mlimani.
Tu ne feras point l’autel solide, mais vide et creux au dedans, comme il t’a été montré sur la montagne.
9 Nawe ufanye ua wa maskani. Upande wa kusini wa kuelekea kusini kutakuwa na chandarua ya nguo ya kitani nzuri yenye kusokotwa, kwa huo ua, urefu wake upande mmoja utakuwa ni dhiraa mia moja.
Tu feras aussi le parvis du tabernacle au côté austral duquel seront contre le midi des rideaux de fin lin retors: un seul côté tiendra cent coudées en longueur.
10 Na nguzo zake zitakuwa nguzo ishirini, na vitako vyake ishirini, vitako vyake vitakuwa vya shaba kulabu za zile nguzo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha.
Et tu y poseras vingt colonnes avec autant de soubassements d’airain, lesquelles auront leurs chapiteaux avec leurs ornements d’argent.
11 Ni vivyo hivyo upande wa kaskazini, urefu wake hiyo chandarua utakuwa ni dhiraa mia moja, na nguzo zake ishirini, na vitako vyake ishirini vitakuwa vya shaba, kulabu za zile nguzo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha.
De même aussi du côté de l’aquilon il y aura des rideaux de cent coudées de long, vingt colonnes et des soubassements d’airain de même nombre; leurs chapiteaux avec leurs ornements seront d’argent.
12 Na upande wa magharibi, upana wa ua kutakuwa na chandarua ya dhiraa hamsini; nguzo zake kumi, na vitako vyake kumi.
Mais dans la largeur du parvis qui regarde l’occident il y aura dans l’espace de cinquante coudées des rideaux, dix colonnes et autant de soubassements.
13 Na upana wa ule ua upande wa mashariki kuelekea mashariki utakuwa ni dhiraa hamsini.
De même, dans la largeur du parvis, laquelle regarde l’orient, il y aura cinquante coudées,
14 Chandarua upande mmoja wa lango itakuwa dhiraa kumi na tano upana wake. Lazima nguzo zake zitakuwa tatu na vitako vyake vitatu.
Dans lesquelles seront affectés à un côté des rideaux de quinze coudées, trois colonnes et autant de soubassements:
15 Upande wa pili ni vivyo hivyo chandarua ya dhiraa kumi na tano; nguzo zake tatu, na vitako vyake vitatu.
Et de l’autre côté seront des rideaux ayant quinze coudées, trois colonnes et autant de soubassements.
16 Na kwa lile lango la ua patakuwa na kisitiri cha dhiraa ishirini, kitakuwa cha nguo ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa, kazi ya mshonaji taraza; nguzo zake zitakuwa nne, na vitako vyake vinne.
Mais à l’entrée du parvis on fera un rideau de vingt coudées d’hyacinthe, de pourpre, d’écarlate deux fois teinte et d’un fin lin retors, en ouvrage de brodeur: cette entrée aura quatre colonnes et autant de soubassements.
17 Nguzo zote za ule ua ziuzungukao pande zote zitakuwa na vitanzi vya fedha; kulabu zake za fedha, na vitako vyake vya shaba.
Toutes les colonnes du parvis seront revêtues tout autour de lames d’argent; elles auront des chapiteaux d’argent et des soubassements d’airain.
18 Urefu wa huo ua utakuwa dhiraa mia moja, na upana wake utakuwa dhiraa hamsini kotekote, na kwenda juu kwake dhiraa tano; yawe ya nguo ya kitani nzuri, na vitako vyake vitakuwa vya shaba.
En longueur le parvis aura cent coudées, en largeur cinquante; sa hauteur sera de cinq coudées; et il sera fait de fin lin retors, et il aura des soubassements d’airain.
19 Vyombo vyote vya maskani vitumiwavyo katika utumishi wake wote, na vigingi vyake vyote, na vigingi vyote vya ule ua, vitakuwa vya shaba.
Tous les vases du tabernacle destinés à tous les usages et à toutes les cérémonies, tant ses pieux que ceux du parvis, tu les feras d’airain.
20 awe waamuru wana wa Israeli wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya nuru, ili kufanya ile taa kuwaka daima.
Ordonne aux enfants d’Israël qu’ils t’apportent de l’huile d’oliviers très pure, et pilée au mortier, afin qu’une lampe brûle toujours.
21 Ndani ya ile hema ya kukutania, nje ya hilo pazia, lililo mbele ya huo ushuhuda, Haruni na wanawe wataitengeza tangu jioni hadi asubuhi mbele ya BWANA; itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyao vyote kwa ajili ya wana wa Israeli.
Dans le tabernacle de témoignage en dehors du voile qui est suspendu devant le témoignage. Et Aaron et ses fils la placeront, afin qu’elle éclaire jusqu’au matin devant le Seigneur. Ce sera un culte perpétuel durant leurs successions parmi les enfants d’Israël.

< Kutoka 27 >