< Kutoka 27 >
1 Nawe fanya madhabahu ya mti wa mshita, urefu wake utakuwa ni dhiraa tano na upana wake dhiraa tano. Hiyo madhabahu itakuwa mraba na kwenda juu kwake kutakuwa dhiraa tatu.
And you will make the altar wood of acacia five cubits length and five cubits breadth square it will be the altar and [will be] three cubits height its.
2 Nawe fanya pembe nne kama mfano wa pembe za ng'ombe. Hizo pembe zitakuwa za kitu kimoja na madhabahu, nawe utayafunika kwa shaba.
And you will make horns its on [the] four corners its from it they will be horns its and you will overlay it bronze.
3 Lazima vyombo vyake vya kuyaondoa majivu yake utavifanya, na majembe yake, na mabakuli yake, na uma zake, na meko yake. Vyombo vyake vyote utavifanya vya shaba.
And you will make pots its to take away ashes its and shovels its and bowls its and forks its and fire-pans its to all articles its you will make bronze.
4 Nawe uifanyie hiyo madhabahu wavu wa shaba. Kisha utie pete nne za shaba katika hizo pembe nne za ule wavu.
And you will make for it a grating a work of a net of bronze and you will make on the net four rings of bronze on four extremities its.
5 Nawe lazima uweke huo wavu chini ya kizingo kiizungukacho madhabahu upande wa chini.
And you will put it under [the] ledge of the altar from to downwards and it will be the net to [the] middle of the altar.
6 Nawe fanya miti kwa ajili ya madhabahu, miti ya mshita, na kuifunika shaba.
And you will make poles for the altar poles of wood of acacia and you will overlay them bronze.
7 Na hiyo miti itatiwa katika viduara, na ile miti itakuwa katika pande mbili za madhabahu, wakati wa kuichukua.
And it will be put poles its in the rings and they will be the poles on [the] two [the] sides of the altar when carry it.
8 Uifanye ya mbao, yenye mvungu ndani yake kama ulivyooneshwa mlimani.
Hollow of boards you will make it just as he showed you on the mountain so they will do.
9 Nawe ufanye ua wa maskani. Upande wa kusini wa kuelekea kusini kutakuwa na chandarua ya nguo ya kitani nzuri yenye kusokotwa, kwa huo ua, urefu wake upande mmoja utakuwa ni dhiraa mia moja.
And you will make [the] courtyard of the tabernacle for [the] side of [the] south south-ward curtains for the courtyard fine linen twisted [will be] one hundred by the cubit [the] length of the side one.
10 Na nguzo zake zitakuwa nguzo ishirini, na vitako vyake ishirini, vitako vyake vitakuwa vya shaba kulabu za zile nguzo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha.
And pillars its twenty and bases their twenty [will be] bronze [the] hooks of the pillars and bands their [will be] silver.
11 Ni vivyo hivyo upande wa kaskazini, urefu wake hiyo chandarua utakuwa ni dhiraa mia moja, na nguzo zake ishirini, na vitako vyake ishirini vitakuwa vya shaba, kulabu za zile nguzo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha.
And thus for [the] side of [the] north in the length curtains [will be] one hundred length (and pillars its *Q(K)*) twenty and bases their twenty [will be] bronze [the] hooks of the pillars and bands their [will be] silver.
12 Na upande wa magharibi, upana wa ua kutakuwa na chandarua ya dhiraa hamsini; nguzo zake kumi, na vitako vyake kumi.
And [the] breadth of the courtyard to [the] side of [the] west curtains fifty cubit[s] pillars their ten and bases their ten.
13 Na upana wa ule ua upande wa mashariki kuelekea mashariki utakuwa ni dhiraa hamsini.
And [the] breadth of the courtyard to [the] side of east-ward east-ward [will be] fifty cubit[s].
14 Chandarua upande mmoja wa lango itakuwa dhiraa kumi na tano upana wake. Lazima nguzo zake zitakuwa tatu na vitako vyake vitatu.
And [will be] fif-teen cubit[s] curtains for the side pillars their three and bases their three.
15 Upande wa pili ni vivyo hivyo chandarua ya dhiraa kumi na tano; nguzo zake tatu, na vitako vyake vitatu.
And for the side second fif-ten curtains pillars their three and bases their three.
16 Na kwa lile lango la ua patakuwa na kisitiri cha dhiraa ishirini, kitakuwa cha nguo ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa, kazi ya mshonaji taraza; nguzo zake zitakuwa nne, na vitako vyake vinne.
And for [the] gate of the courtyard a screen - twenty cubit[s] violet stuff and purple and scarlet stuff of scarlet and fine linen twisted [the] work of a worker in colors pillars their four and bases their four.
17 Nguzo zote za ule ua ziuzungukao pande zote zitakuwa na vitanzi vya fedha; kulabu zake za fedha, na vitako vyake vya shaba.
All [the] pillars of the courtyard all around [will be] furnished with bands silver hooks their [will be] silver and bases their [will be] bronze.
18 Urefu wa huo ua utakuwa dhiraa mia moja, na upana wake utakuwa dhiraa hamsini kotekote, na kwenda juu kwake dhiraa tano; yawe ya nguo ya kitani nzuri, na vitako vyake vitakuwa vya shaba.
[the] length of The courtyard [will be] one hundred by the cubit and [the] breadth - [will be] fifty on fifty and [the] height [will be] five cubits fine linen twisted and bases their [will be] bronze.
19 Vyombo vyote vya maskani vitumiwavyo katika utumishi wake wote, na vigingi vyake vyote, na vigingi vyote vya ule ua, vitakuwa vya shaba.
To all [the] articles of the tabernacle in all service its and all tent pegs its and all [the] tent pegs of the courtyard [will be] bronze.
20 awe waamuru wana wa Israeli wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya nuru, ili kufanya ile taa kuwaka daima.
And you you will command - [the] people of Israel so they may bring to you oil of olive pure pressed for the light to lift up a lamp continually.
21 Ndani ya ile hema ya kukutania, nje ya hilo pazia, lililo mbele ya huo ushuhuda, Haruni na wanawe wataitengeza tangu jioni hadi asubuhi mbele ya BWANA; itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyao vyote kwa ajili ya wana wa Israeli.
In [the] tent of meeting from [the] outside of the curtain which [is] on the testimony he will arrange it Aaron and sons his from evening until morning before Yahweh a statute of perpetuity to generations their from with [the] people of Israel.