< Kutoka 26 >

1 Lazima ufanye hiyo maskani iwe na mapazia kumi ifanye ya nguo ya kitani nzuri ya kusokota, pamoja na nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, pamoja na makerubi. Kazi ya fundi stadi.
Tabernaklet skall du göra af tio tapeter, af hvitt tvinnadt silke, af gult silke, af skarlakan och rosenrödt; Cherubim skall du göra deruppå konsteliga.
2 Urefu wa kila pazia utakuwa dhiraa ishirini na nane, na upana wa kila pazia utakuwa dhiraa nne. Mapazia yote yatakuwa ya kipimo kimoja.
Längden på hvart tapetet skall vara åtta och tjugu alnar, bredden fyra alnar; och skola alla tio vara ens;
3 Mapazia matano yataungwa pamoja, na mapazia matano mengine yataungwa pamoja.
Och skola ju vara fem tillhopafogd, det ena vid det andra.
4 Lazima ufanye tanzi za rangi ya samawati upande wa mwisho wa pazia moja katika ule upindo wa fungu lake. Vivyo hivyo utafanya upande wa mwisho wa ile pazia iliyo, katika fungu la pili.
Och du skall göra lyckor af gult silke, allestädes på stadet på tapeten, att de måga tillhopafogas, att ju tu och tu på sitt stad kunna tillsammanfästas;
5 Fanya matanzi hamsini katika pazia moja, na matanzi hamsini katika upande wa mwisho wa ile pazia iliyo katika kuungana kwa pili.
Femtio lyckor på hvart tapetet, att det ena må fästas vid det andra.
6 Fanya hivi ili hizo tanzi zielekeana. Kisha ufanye vifungo hamsini vya dhahabu, na kuunganisha hayo mapazia pamoja kwa vile vifungo na hiyo maskani itakuwa ni moja.
Och du skall göra femtio gyldene häkte, der man de tapeter med tillsammanknäpper, det ena vid det andra, tilldess det blifver ett tabernakel.
7 Lazima ufanye mapazia ya nywele za mbuzi yawe hema juu ya maskani. Lazima ufanye mapazia kumi na moja.
Du skall ock göra ellofva tapeter af getahår, till öfvertäckelse öfver tabernaklet.
8 Urefu wa kila pazia utakuwa dhiraa thelathini, na upana wa kila pazia utakuwa dhiraa nne. Hayo mapazia kumi na moja yatakuwa ya kipimo kimoja.
Längden af hvart tapetet skall vara tretio alnar, bredden fyra alnar; och skola alla ellofva vara lika stor.
9 Lazima utaunganisha mapazia matano mbali, na mapazia sita mbali, na lile pazia la sita utalikunja hapo upande wa mbele wa ile hema.
Fem skall du med hvartannat tillhopafoga, och sedan sex tillhopa med hvartannat, så att du gör det sjette tapetet dubbelt frammanför tabernaklet.
10 Ufanye tanzi hamsini upande wa mwisho wa pazia lile lililo la mwisho katika hayo yaliyounganywa pamoja, na tanzi hamsini upande wa mwisho wa lile pazia lililo nje katika hayo ya pili yaliyounganywa pamoja.
Och du skall göra femtio lyckor på stadet, af hvart tapetet, att de måga tillhopaknäppas med hvartannat.
11 Kisha ufanye vifungo hamsini vya shaba, na kuvitia vile vifungo katika zile tanzi, na kuiunganya ile hema pamoja, ili iwe hema moja.
Och skall du göra femtio kopparhäkte, och knäppa häkten in uti lyckorna, att tapeten tillsammanfogas, och varda en täckelse.
12 Kipande kile kilichosalia, kile kiangukacho, cha yale mapazia ya hema, itaanguka huko upande wa nyuma wa maskani.
Men det öfver är, i längdene af tapeten på tabernaklet, skall du hälftena låta hänga utöfver tabernaklet,
13 Lazima kuwe na dhiraa moja upande mmoja, na ile dhiraa moja upande wa pili - ya urefu wa mapazia ya hema uliosalia, zitaanguka katika ubavu wa maskani upande huu na upande huu, ili kuifunika.
På båda sidor en aln långt; så att det öfver är, blifver på sidomen af tabernaklet, och betäcker det på båda sidor.
14 Nawe fanya kifuniko cha ile hema, cha ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
Utöfver denna täckelse skall du göra en annor öfvertäckelse af rödlett vädurskinn; och dertill en öfvertäckelse af tackskinn.
15 Nawe lazima ufanye hizo fremu za maskani za mti wa mjohoro.
Du skall ock göra bräder till tabernaklet, af furoträ, hvilka stå skola.
16 Kila fremu utakuwa na urefu wa dhiraa kumi, na upana wake kila ubao utakuwa dhiraa moja na nusu.
Tio alnar långt skall hvart brädet vara, och halfannor aln bredt.
17 Kila fremu itakuwa na ndimi mbili, zenye kuunganishwa huu na huu. Ndivyo utakavyozifanya mbao zote za maskani.
Två nåckor skall hvart brädet hafva, så att det ena må sättas vid det andra; alltså skall du göra all bräden till tabernaklet.
18 Kisha ufanye zile mbao za maskani, mbao ishirini kwa upande wa kusini kuelekea kusini.
Tjugu af dem skola stå söder.
19 Lazima nawe ufanye vitako arubaini vya fedha chini ya zile fremu ishirini. Vitako viwili chini ya fremu moja, kupokea zile ndimi zake mbili, na vitako viwili chini ya fremu nyingine kupokea zile ndimi zake mbili.
De skola hafva fyratio silfverfötter nedan under, ju två fötter under hvart brädet på sina två nåckor.
20 Kwa upande wa pili wa maskani, upande wa kaskazini, mbao ishirini
Sammalunda på den andra sidone, norrut, skola ock stå tjugu bräder;
21 na vitako vyake vya fedha arubaini. Lazima kuwe na vitako viwili chini ya fremu moja, na vitako viwili chini ya fremu nyingine.
Och fyratio silfverfötter, ju två fötter under hvart brädet.
22 Ufanye fremu sita kwa ajili ya upande wa nyuma wa maskani kuelekea magharibi.
Men bak i tabernaklet, vesterut, skall du göra sex bräder;
23 Tena ufanye fremu mbili kwa ajili ya hizo pembe za maskani zilizo upande wa nyuma.
Dertill tu bräder bak i de tu hörnen af tabernaklet;
24 Hizi fremu zitakuwa zimetengana upande wa chini, lakini zimeshinkana kwa juu ya duara moja.
Så att hvartdera af de tu bräden lagar sig med sitt hörnebräde ifrå nedan allt uppåt, och komma ofvan tillika tillhopa med en krampo;
25 Fremu zitakuwa ni nane, na vitako vyake vya fedha. Vitako kumi na sita, vitako viwili chini ya fremu moja, na vitako viwili chini ya ubao wa pili.
Så att det äro åtta bräder med deras silfverfötter, hvilke skola vara sexton; ju två under ett bräde.
26 Lazima ufanye mataruma ya mti wa mshita- mataruma matano kwa ajili ya mbao za upande mmoja wa maskani,
Och du skall göra skottstänger af furoträ, fem till de bräden, som äro på den ena sidone i tabernaklet;
27 na mataruma matano kwa ajili ya fremu za upande wa pili wa maskani, na mataruma matano kwa ajili ya fremu za upande wa maskani ulio nyuma kuelekea magharibi.
Och fem till de bräden, som äro på den andra sidone i tabernaklet; och fem till de bräden bak i tabernaklet, vesterut.
28 Na hilo taruma la katikati lililo katikati ya zile fremu, litapenya toka mwisho huu hata mwisho huu.
Och du skall skjuta medelstången midt öfver bräden utåt, och fatta dem alla tillhopa ifrå den ena ändan till den andra.
29 lazima uzifunuke hizo fremu kwa dhahabu. Nawe lazima ufanye maduara yake ya za dhahabu, kuwa kama vishikizo, na hayo mataruma utayafunika dhahabu.
Och skall du bedraga bräden med guld, och ringarna på dem göra af guld, att man skjuter stängerna derin; och stängerna skall du bedraga med guld.
30 Nawe utaisimamisha hiyo maskani sawasawa na mfano wake uliooneshwa mlimani.
Och så skall du nu göra tabernaklet, efter det sättet, som du sett hafver på bergena.
31 Nawe fanya pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na nguo za kitani nzuri zenye kusokotwa, litafumwa na kutiwa makerubi, kazi ya fundi stadi.
Och du skall göra en förlåt af gult silke, skarlakan, och rosenrödt, och tvinnadt hvitt silke; och du skall göra Cherubim deruppå konsteliga.
32 Kisha litungike katika nguzo nne za mti wa mshita zilizofunikwa dhahabu, vifungo vyake vitakuwa vya dhahabu, katika vitako vya fedha vinne.
Och du skall hänga det på fyra stolpar af furoträ, de som bedragne äro med guld, och hafva gyldene knappar, och fyra silfverfötter.
33 Nawe tungika lile pazia chini ya vile vifungo, nawe lete lile sanduku la ushuhuda. Lile pazia litawagawanyia kati ya patakatifu, na mahali patakatifu sana.
Och skall du knäppa förlåten derintill med häkter, och sätta vittnesbördsens ark innanför förlåten, att han är eder en åtskilnad emellan det helga och det aldrahelgasta.
34 Nawe lazima utaweka kiti cha rehema juu ya lile sanduku la ushuhuda ndani ya mahali pale patakatifu sana. Na ile meza utaiweka nje ya pazia.
Och du skall sätta nådastolen på vittnesbördsens ark, uti det aldrahelgasta.
35 Lazima uweke kinara cha taa kuikabili ile meza upande wa maskani wa kuelekea kusini. Lile meza utaiweka upande wa kaskazini.
Men bordet sätt utanför förlåten, och ljusastakan tvärtöfver emot bordet, söderut i tabernaklet, så att bordet står norrut.
36 Kisha utafanya kisitiri kwa mlango wa hema, cha nyuzi za rangi ya buluu, zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa, kazi ya mshonaji wa taraza.
Och skall du göra ett kläde i tabernaklets dörr, virkadt med gult silke, rosenrödt, skarlakan, och hvitt tvinnadt silke.
37 Nawe fanya nguzo tano za mti wa mshita kwa kile kisitiri, na kuzifunika dhahabu; kulabu zake zitakuwa za dhahabu. Nawe utasubu vitako vya shaba vitano kwa ajili yake.
Och skall du göra fem stolpar till det samma klädet af furoträ, öfverdragna med guld, med gyldene knappar; och du skall gjuta dem fem kopparfötter.

< Kutoka 26 >