< Kutoka 26 >

1 Lazima ufanye hiyo maskani iwe na mapazia kumi ifanye ya nguo ya kitani nzuri ya kusokota, pamoja na nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, pamoja na makerubi. Kazi ya fundi stadi.
Afterwarde thou shalt make the Tabernacle with tenne curtaines of fine twined linen, and blewe silke, and purple, and skarlet: and in them thou shalt make Cherubims of broydered worke.
2 Urefu wa kila pazia utakuwa dhiraa ishirini na nane, na upana wa kila pazia utakuwa dhiraa nne. Mapazia yote yatakuwa ya kipimo kimoja.
The length of one curtaine shalbe eight and twentie cubites, and the bredth of one curtaine, foure cubites: euery one of the curtaines shall haue one measure.
3 Mapazia matano yataungwa pamoja, na mapazia matano mengine yataungwa pamoja.
Fiue curtaines shalbe coupled one to an other: and the other fiue curtaines shall be coupled one to another.
4 Lazima ufanye tanzi za rangi ya samawati upande wa mwisho wa pazia moja katika ule upindo wa fungu lake. Vivyo hivyo utafanya upande wa mwisho wa ile pazia iliyo, katika fungu la pili.
And thou shalt make stringes of blew silke vpon the edge of the one curtaine, which is in the seluedge of the coupling: and likewise shalt thou make in the edge of the other curtaine in the seluedge, in the second coupling.
5 Fanya matanzi hamsini katika pazia moja, na matanzi hamsini katika upande wa mwisho wa ile pazia iliyo katika kuungana kwa pili.
Fiftie strings shalt thou make in one curtaine, and fiftie stringes shalt thou make in the edge of the curtaine, which is in the second coupling: ye stringes shalbe one right against another.
6 Fanya hivi ili hizo tanzi zielekeana. Kisha ufanye vifungo hamsini vya dhahabu, na kuunganisha hayo mapazia pamoja kwa vile vifungo na hiyo maskani itakuwa ni moja.
Thou shalt make also fiftie taches of gold, and couple the curtaines one to another with the taches, and it shalbe one tabernacle.
7 Lazima ufanye mapazia ya nywele za mbuzi yawe hema juu ya maskani. Lazima ufanye mapazia kumi na moja.
Also thou shalt make curtaines of goates heare, to be a couering vpon the Tabernacle: thou shalt make them to the number of eleuen curtaines.
8 Urefu wa kila pazia utakuwa dhiraa thelathini, na upana wa kila pazia utakuwa dhiraa nne. Hayo mapazia kumi na moja yatakuwa ya kipimo kimoja.
The length of a curtaine shall be thirtie cubites, and the breadth of a curtaine foure cubites: the eleuen curtaines shalbe of one measure.
9 Lazima utaunganisha mapazia matano mbali, na mapazia sita mbali, na lile pazia la sita utalikunja hapo upande wa mbele wa ile hema.
And thou shalt couple fiue curtaynes by themselues, and the sixe curtaines by themselues: but thou shalt double the sixt curtaine vpon the forefront of the couering.
10 Ufanye tanzi hamsini upande wa mwisho wa pazia lile lililo la mwisho katika hayo yaliyounganywa pamoja, na tanzi hamsini upande wa mwisho wa lile pazia lililo nje katika hayo ya pili yaliyounganywa pamoja.
And thou shalt make fifty stringes in the edge of one curtayne, in the seluedge of the coupling, and fifty stringes in the edge of the other curtaine in the second coupling.
11 Kisha ufanye vifungo hamsini vya shaba, na kuvitia vile vifungo katika zile tanzi, na kuiunganya ile hema pamoja, ili iwe hema moja.
Likewise thou shalt make fifty taches of brasse, and fasten them on the strings, and shalt couple the couering together, that it may be one.
12 Kipande kile kilichosalia, kile kiangukacho, cha yale mapazia ya hema, itaanguka huko upande wa nyuma wa maskani.
And the remnant that resteth in ye curtaines of the couering, euen the halfe curtaine that resteth, shalbe left at the backeside of the Tabernacle,
13 Lazima kuwe na dhiraa moja upande mmoja, na ile dhiraa moja upande wa pili - ya urefu wa mapazia ya hema uliosalia, zitaanguka katika ubavu wa maskani upande huu na upande huu, ili kuifunika.
That the cubite on the one side, and the cubite on the other side of that which is left in the legth of the curtaines of ye couering, may remaine on either side of the Tabernacle to couer it.
14 Nawe fanya kifuniko cha ile hema, cha ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
Moreouer, for that couering thou shalt make a couering of rammes skinnes died red, and a couering of badgers skinnes aboue.
15 Nawe lazima ufanye hizo fremu za maskani za mti wa mjohoro.
Also thou shalt make boards for the Tabernacle of Shittim wood to stand vp.
16 Kila fremu utakuwa na urefu wa dhiraa kumi, na upana wake kila ubao utakuwa dhiraa moja na nusu.
Ten cubites shalbe the length of a boarde, and a cubite and an halfe cubite the breadth of one boarde.
17 Kila fremu itakuwa na ndimi mbili, zenye kuunganishwa huu na huu. Ndivyo utakavyozifanya mbao zote za maskani.
Two tenons shalbe in one boarde set in order as the feete of a ladder, one against an other: thus shalt thou make for all the boardes of the Tabernacle.
18 Kisha ufanye zile mbao za maskani, mbao ishirini kwa upande wa kusini kuelekea kusini.
And thou shalt make boardes for the Tabernacle, euen twenty boardes on the South side, euen full South.
19 Lazima nawe ufanye vitako arubaini vya fedha chini ya zile fremu ishirini. Vitako viwili chini ya fremu moja, kupokea zile ndimi zake mbili, na vitako viwili chini ya fremu nyingine kupokea zile ndimi zake mbili.
And thou shalt make fourty sockets of siluer vnder the twentie boardes, two sockets vnder one boarde for his two tenons, and two sockets vnder an other boarde for his two tenons.
20 Kwa upande wa pili wa maskani, upande wa kaskazini, mbao ishirini
In like maner on the other side of the Tabernacle towarde the North side shalbe twentie boardes,
21 na vitako vyake vya fedha arubaini. Lazima kuwe na vitako viwili chini ya fremu moja, na vitako viwili chini ya fremu nyingine.
And their fourtie sockets of siluer, two sockets vnder one boarde, and two sockets vnder another board.
22 Ufanye fremu sita kwa ajili ya upande wa nyuma wa maskani kuelekea magharibi.
And on the side of the Tabernacle, toward the West shalt thou make sixe boards.
23 Tena ufanye fremu mbili kwa ajili ya hizo pembe za maskani zilizo upande wa nyuma.
Also two boardes shalt thou make in the corners of the Tabernacle in the two sides.
24 Hizi fremu zitakuwa zimetengana upande wa chini, lakini zimeshinkana kwa juu ya duara moja.
Also they shalbe ioyned beneath, and likewise they shalbe ioyned aboue to a ring: thus shall it be for them two: they shalbe for ye two corners.
25 Fremu zitakuwa ni nane, na vitako vyake vya fedha. Vitako kumi na sita, vitako viwili chini ya fremu moja, na vitako viwili chini ya ubao wa pili.
So they shalbe eight boardes hauing sockets of siluer, euen sixteene sockets, that is, two sockets vnder one board, and two sockets vnder an other boarde.
26 Lazima ufanye mataruma ya mti wa mshita- mataruma matano kwa ajili ya mbao za upande mmoja wa maskani,
The thou shalt make fiue barres of Shittim wood for the boardes of one side of the Tabernacle,
27 na mataruma matano kwa ajili ya fremu za upande wa pili wa maskani, na mataruma matano kwa ajili ya fremu za upande wa maskani ulio nyuma kuelekea magharibi.
And fiue barres for the boardes of the other side of the Tabernacle: also fiue barres for the boardes of the side of the Tabernacle toward the Westside.
28 Na hilo taruma la katikati lililo katikati ya zile fremu, litapenya toka mwisho huu hata mwisho huu.
And the middle barre shall goe through the middes of the boards, from ende to ende.
29 lazima uzifunuke hizo fremu kwa dhahabu. Nawe lazima ufanye maduara yake ya za dhahabu, kuwa kama vishikizo, na hayo mataruma utayafunika dhahabu.
And thou shalt couer the boards with golde, and make their rings of golde, for places for the barres, and thou shalt couer the barres with golde.
30 Nawe utaisimamisha hiyo maskani sawasawa na mfano wake uliooneshwa mlimani.
So thou shalt reare vp the Tabernacle, according to the facion thereof, which was shewed thee in the mount.
31 Nawe fanya pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na nguo za kitani nzuri zenye kusokotwa, litafumwa na kutiwa makerubi, kazi ya fundi stadi.
Moreouer, thou shalt make a vaile of blewe silke, and purple, and skarlet, and fine twined linen: thou shalt make it of broydred worke with Cherubims.
32 Kisha litungike katika nguzo nne za mti wa mshita zilizofunikwa dhahabu, vifungo vyake vitakuwa vya dhahabu, katika vitako vya fedha vinne.
And thou shalt hang it vpon foure pillars of Shittim wood couered with gold, (whose hookes shalbe of gold) stading vpon foure sockets of siluer.
33 Nawe tungika lile pazia chini ya vile vifungo, nawe lete lile sanduku la ushuhuda. Lile pazia litawagawanyia kati ya patakatifu, na mahali patakatifu sana.
Afterward thou shalt hang the vaile on the hookes, that thou mayest bring in thither, that is (within the vaile) the arke of the Testimonie: and the vaile shall make you a separation betweene the Holy place and the most holy place.
34 Nawe lazima utaweka kiti cha rehema juu ya lile sanduku la ushuhuda ndani ya mahali pale patakatifu sana. Na ile meza utaiweka nje ya pazia.
Also thou shalt put ye Mercy seate vpon the Arke of the testimonie in the most Holy place.
35 Lazima uweke kinara cha taa kuikabili ile meza upande wa maskani wa kuelekea kusini. Lile meza utaiweka upande wa kaskazini.
And thou shalt set the Table without the vaile, and the Candlesticke ouer against the Table on the Southside of the Tabernacle, and thou shalt set the Table on the Northside.
36 Kisha utafanya kisitiri kwa mlango wa hema, cha nyuzi za rangi ya buluu, zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa, kazi ya mshonaji wa taraza.
Also thou shalt make an hanging for the dore of ye Tabernacle of blew silke, and purple, and skarlet, and fine twined linen wrought with needle.
37 Nawe fanya nguzo tano za mti wa mshita kwa kile kisitiri, na kuzifunika dhahabu; kulabu zake zitakuwa za dhahabu. Nawe utasubu vitako vya shaba vitano kwa ajili yake.
And thou shalt make for the hanging fiue pillars of Shittim, and couer them with gold: their heads shalbe of golde, and thou shalt cast fiue sockets of brasse for them.

< Kutoka 26 >