< Kutoka 25 >

1 Yahweh akamwambia Musa,
耶和華曉諭摩西說:
2 “Waambie Waisraeli wanitolee sadaka kila mtu nawe utapokea kutoka kwa mtu yeyote atakayetoa kwa moyo mkunjufu. Lazima upokee hizi sadaka kwa ajili yangu.
「你告訴以色列人當為我送禮物來;凡甘心樂意的,你們就可以收下歸我。
3 Hizi ndio sadaka utakazopokea kwao; dhahabu, fedha na shaba,
所要收的禮物:就是金、銀、銅,
4 buluu, zambarau na nyekundu, na nguo za kitani safi, na manyoya ya mbuzi;
藍色、紫色、朱紅色線,細麻,山羊毛,
5 na ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu na ngozi za pomboo, miti ya mjohoro,
染紅的公羊皮,海狗皮,皂莢木,
6 mafuta ya ile taa, na viungo vya manukato kwa yale mafuta ya kupaka na kwa ule uvumba wenye harufu nzuri;
點燈的油並做膏油和香的香料,
7 mawe ya shohamu na mawe mengine ya kutiwa kwa ile naivera na kwa kile kifuko cha kifuani.
紅瑪瑙與別樣的寶石,可以鑲嵌在以弗得和胸牌上。
8 Waache wanifanyie patakatifu ili nipate kukaa kati yao.
又當為我造聖所,使我可以住在他們中間。
9 Lazima ufanye sawa na haya yote nikuoneshayo mfano wa maskani, na vifaa vyake, ndivyo utakavyovifanya.
製造帳幕和其中的一切器具都要照我所指示你的樣式。」
10 Wana paswa wafanye sanduku la mti wa mjohoro. Urefu wake na uwe dhiraa mbili na nusu; na upana wake moja na nusu, na kwenda juu kwake dhiraa moja na nusu.
「要用皂莢木做一櫃,長二肘半,寬一肘半,高一肘半。
11 Lazima ulifunike nadni kwa dhahabu safi, na utie na ukingo wa dhahabu kulizunguka pande zote.
要裏外包上精金,四圍鑲上金牙邊。
12 Nawe uta yayusha katika viduara vinne vya dhahabu, na kuviweka katika miguu yake minne; viduara viwili upande mmoja, na viduara viwili upande wake wa pili.
也要鑄四個金環,安在櫃的四腳上;這邊兩環,那邊兩環。
13 Nawe lazima ufanya miti mirefu ya mshita na kuifunika dhahabu.
要用皂莢木做兩根槓,用金包裹。
14 Nawe lazima uweka hiyo miti katika vile viduara vilivyo katika pande mbili za sanduku ili kulichukua hilo sanduku.
要把槓穿在櫃旁的環內,以便抬櫃。
15 Hiyo miti itakaa katika vile viduara vya sanduku; haitaondolewa.
這槓要常在櫃的環內,不可抽出來。
16 Kisha weka ndani ya sanduku hizo amri nitakazokupa.
必將我所要賜給你的法版放在櫃裏。
17 Nawe lazima utengeneze kifuniko cha dhahabu safi. Urefu wake utakuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu.
要用精金做施恩座 ,長二肘半,寬一肘半。
18 Nawe fanya makerubi mawili ya dhahabu katika hiyo miisho miwili ya kiti cha rehema.
要用金子錘出兩個基路伯來,安在施恩座的兩頭。
19 Weka kerubi moja mwisho mmoja wa kiti cha rehema, na kerubi la pili mwisho wa pili. Lazima hao makerubi wawe kitu kimoja na kiti cha rehema.
這頭做一個基路伯,那頭做一個基路伯,二基路伯要接連一塊,在施恩座的兩頭。
20 Na hao makerubi watainua mabawa yao juu, na kukifunika hicho kiti cha rehema kwa mabawa yao. Nyuso zao makerubi zitaelekeana na zitaelekea kiti cha rehema.
二基路伯要高張翅膀,遮掩施恩座。基路伯要臉對臉,朝着施恩座。
21 Lazima uweke kiti cha rehema juu ya hilo sanduku, kisha uwe hizo amri nitakazokupa ndani ya sanduku.
要將施恩座安在櫃的上邊,又將我所要賜給你的法版放在櫃裏。
22 Nami nitaonana nawe hapo katika sanduku. Nitazungumza nawe pale nilipo juu ya kiti cha rehema. Itakuwa katikati ya hao makerubi mawili waliyo juu ya sanduku la ushuhuda nitakapo zungumza na wewe katika mambo yote nitakayokuagiza kwa ajili ya wana wa Israeli.
我要在那裏與你相會,又要從法櫃施恩座上二基路伯中間,和你說我所要吩咐你傳給以色列人的一切事。」
23 Nawe fanya meza ya mti wa mshiti. Urefu wake utakuwa dhiraa mbili, na upana wake dhiraa moja, na kwenda juu kwake dhiraa moja na nusu.
「要用皂莢木做一張桌子,長二肘,寬一肘,高一肘半。
24 Uifunike dhahabu safi na kuifanyia ukingo wa dhahabu wa kuizunguka pande zote.
要包上精金,四圍鑲上金牙邊。
25 Lazima ufanyie fremu ya kuizunguka pande zote, upana wake utakuwa nyanda nne, ukingo wa dhahabu wa kuuzunguka fremu pande zote.
桌子的四圍各做一掌寬的橫樑,橫樑上鑲着金牙邊。
26 Uifanyie viduara vinne vya dhahabu na kuvitia vile viduara katika pembe zake nne, katika miguu yake minne ilipo kuwa.
要做四個金環,安在桌子的四角上,就是桌子四腳上的四角。
27 Vile viduara na viwe karibu na ile fremu ili viwe mahali pa kutilia ile miti, ya kuichukulia meza.
安環子的地方要挨近橫樑,可以穿槓抬桌子。
28 Fanya ile miti ya mti wa mshita, na kuifunika dhahabu, kwamba ile meza ichukuliwe kwayo.
要用皂莢木做兩根槓,用金包裹,以便抬桌子。
29 Nawe fanya sahani zake, na miiko yake, na makopo yake, na vikombe vyake vya kumiminia. Vifanye vyote vya dhahabu safi.
要做桌子上的盤子、調羹,並奠酒的爵和瓶;這都要用精金製作。
30 Nawe utaiweka mikate ya wonyesho juu ya meza mbele yangu daima.
又要在桌子上,在我面前,常擺陳設餅。」
31 Nawe fanya kinara cha taa cha dhahabu safi; hicho kinara na kifanywe cha kazi ya kufua, kitako chake, na mti wake, vikombe vyake, na matovu yake, na maua yake, vyote vitakuwa vya kitu kimoja nacho.
「要用精金做一個燈臺。燈臺的座和幹與杯、球、花,都要接連一塊錘出來。
32 Nacho kitakuwa na matawi sita yenye kutoka ubavuni mwake - matawi matatu ya kinara upande wake mmoja, na matawi matatu ya kinara upande wake wa pili.
燈臺兩旁要杈出六個枝子:這旁三個,那旁三個。
33 Tawi la kwanza lazima liwe na vikombe vitatu vilivyotengenezwa mfano wa maua ya mlozi katika tawi moja, tovu na ua na vikombe vitatu vilivyofanywa mfano wa maua ya mlozi katika tawi la pili, tovu na ua. Vivyo hivyo hayo matawi yote sita yatokayo katika kile kinara.
這旁每枝上有三個杯,形狀像杏花,有球,有花;那旁每枝上也有三個杯,形狀像杏花,有球,有花。從燈臺杈出來的六個枝子都是如此。
34 Katika hicho kinara, lazima kuwe na vikombe vinne vilivyofanywa mfano wa maua ya mlozi, matovu yake, na maua yake.
燈臺上有四個杯,形狀像杏花,有球,有花。
35 Lazima kuwe na tovu chini ya matawi - mawili la kitu kimoja nacho, na tovu chini ya matawi mawili la kitu kimoja nacho, na tovu chini ya matawi mawili la kitu kimoja nacho, kwa hayo matawi sita yatokayo katika kile kinara.
燈臺每兩個枝子以下有球與枝子接連一塊。燈臺出的六個枝子都是如此。
36 Matovu yake na matawi yake yatakuwa ya kitu kimoja nacho, kiwe chote pia kazi moja ya kufua, ya dhahabu safi.
球和枝子要接連一塊,都是一塊精金錘出來的。
37 Lazima nawe uzifanye hivyo vinara saba na taa zake saba, nao wataziwasha hizo taa zake, zitoe nuru mbele yake.
要做燈臺的七個燈盞。祭司要點這燈,使燈光對照。
38 Na makoleo yake, na visahani vyake, vyote vitakuwa vya dhahabu safi.
燈臺的蠟剪和蠟花盤也是要精金的。
39 Tumia talanta moja ya dhahabu safi, pamoja na vyombo hivi vyote.
做燈臺和這一切的器具要用精金一他連得。
40 Nawe angalia ya kwamba uvifanye kama mfano wake, uliooneshwa mlimani.
要謹慎做這些物件,都要照着在山上指示你的樣式。」

< Kutoka 25 >