< Kutoka 20 >
1 Mungu alisema maneno yote haya:
God spoke all these words, saying,
2 Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa katika ardhi Misri, nje ya nyumba ya utumwa.
“I am Yahweh your God, who brought you out of the land of Egypt [Abode of slavery], out of the house of bondage.
3 Msiwe na miungu mingine ila mimi tu.
“You shall have no other elohim ·deities, judges· before me.
4 Msijitengenezee sanamu za kuchonga kufananisha na kitu chochote kilichopo juu ya mbingu, chini ya ardhi, au ndani ya maji.
“You shall not make for yourselves an idol, nor any image of anything that is in the heavens above, or that is in the earth beneath, or that is in the water under the earth:
5 Msipinde na kuabudu sanamu, mimi Yahweh Mungu wenu, ni Mungu mwenye wivu. Nitaadhibu uovu wa mabubu kwa kuleta adhabu juu ya kizazi, cha tatu hadi kizazi cha nne kwa wale wanao nichukia.
you shall not hawa ·bow low, prostrate· yourself down to them, nor abad ·serve· them, for I, Yahweh [He sustains breathing] your God, am El Kana' [Jealous God], visiting the depravity (moral evil) of the fathers on the children, on the third and on the fourth generation of those who hate me,
6 Ila nitaweka agano la uaminifu kwa maelfu watakao nipenda na kushika amri zangu.
and showing chesed ·loving-kindness· to thousands of those who 'ahav ·affectionately love· me and keep my mitzvot ·instructions·.
7 Usilitaje bure jina la Yahweh Mungu wako, sitkuwa na hatia kwa yeyote atakaye taja jina langu bure.
“You shall not use את the name of Yahweh your God worthlessly, for Adonai will not hold him guiltless את who takes את his name in vain.
8 Ikumbuke siku ya Sabato, na kunitengea.
“Remember the Shabath ·Intermission· day, to keep it holy.
9 lazima ufanye kazi zako zote kwa siku sita.
You shall labor six days, and do all your work,
10 Ila siku ya saba ni Sabato kwaajili ya Yahweh Mungu wako. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, au mwana wako, au binti yako, au mtumishi wako wakiume, au mtumishi wako mwanamke, au ng'ombe zako, au mgeni aliye ndani ya malango yako.
but the seventh day is a Shabath ·Intermission· to Adonai your God. You shall not do any work in it, you, nor your son, nor your daughter, your male servant, nor your female servant, nor your livestock, nor your stranger who is within your gates;
11 Kwa siku sita Yahweh aliumba mbingu na nchi, bahari, na vitu vyote vilivyomo, na siku ya saba alipumzika. Kwa hiyo Yahweh aliibariki siku ya Sabato na kuitenga.
for in six days Adonai made heaven and earth, the sea, and all that is in them, and rested the seventh day; therefore Adonai blessed the Shabath ·Intermission· day, and made it holy.
12 Waheshimu baba na mama yako, ili uweze kuishi miaka mingi duniani Yahweh Mungu wako ametoa.
“Honor your father and your mother, so that your days may be long in the land which Adonai your God gives you.
14 Usifanye uasherati (usizini).
“You shall not commit adultery.
15 Usiibe kwa mtu yoyote.
“You shall not steal.
16 Usishuhudie uongo dhidi ya jirani yako.
“You shall not give false witness against your neighbor.
17 Usitaman nyumba ya jirani yako; usitamani mke wa jirani yako, wala mtumishi wake wakiume, mtumishi wake mwanamke, ng'ombe wake, punda wake, au chochote cha jirani yako.
“You shall not covet your neighbor’s house. You shall not covet your neighbor’s wife, nor his male servant, nor his female servant, nor his ox, nor his donkey, nor anything that is your neighbor’s.”
18 Watu wote waliona radi na umeme, na kusikia sauti ya mbiu, na mlima ukitoa moshi. Watu walipoona hivo, walitetemeka na kusimama mbali.
All the people perceived the thunder, the lightnings, the sound of the shofar ·ram horn·, and the mountain smoking. When the people saw it, they trembled, and stayed at a distance.
19 Wakamwambia Musa, ongea na sisi, na tutakusikiliza; lakini usiruhusu Mungu kuongea nasi, ama tutakufa.
They said to Moses [Drawn out], “Speak with us yourself, and we will sh'ma ·hear obey·; but don’t let God speak with us, lest we die.”
20 Musa akawaambia watu, “msiogope, Mungu alikuja kuwajaribu ili heshima yake iwe ndani yenu, kwa hiyo msitende dhambi.”
Moses [Drawn out] said to the people, “Don’t be afraid, for God has come to test you, and that his fear may be before you, that you won’t sin ·err (the standard goal)·.”
21 hivyo watu walisimama mbali, na Musa alikaribia giza nene Mungu alipokuwa.
The people stayed at a distance, and Moses [Drawn out] came near to the thick darkness where God was.
22 Yahweh alimwambia Musa, “Ni lazima uwaambie hili Waisraeli: 'Wewe mwenyewe umeona niliongea na wewe kutoka mbinguni.
Adonai said to Moses [Drawn out], “This is what you shall tell the children of Israel [God prevails]: ‘You yourselves have seen that I have talked with you from heaven.
23 Misjitengenezee miungu mingine pamoja nami, miungu ya fedha au miungu ya dhahabu.
You shall most certainly not make alongside of me deities of silver, or deities of gold for yourselves.
24 Tengenezeni madhabahu ya udongo kwa ajili yangu, na lazima mtoe sadaka ya kuteketeza, sadaka ya ushirika, kondoo, na ng'ombe. kila sehemu ntakapotaka jina langu liheshimiwe, nitakuja kwenu na kuwabariki.
You shall make an altar of earth for me, and shall sacrifice on it your burnt offerings and your peace offerings, your sheep and your cattle. In every place where I record my name I will come to you and I will bless you.
25 Kama mtatengeneza madhabahu ya mawe, msijenge na mawe yaiyokatika, na kama mtatumia vyombo vyenu juu yake, mtaweka unajisi.
If you make me an altar of stone, you shall not build it of cut stones; for if you lift up your tool on it, you have polluted it.
26 msije juu ya madhabahu yangu kwa hatua zenu; hii ni ili msioneshe sehemu zenu za siri.”
You shall not go up by steps to my altar, that your nakedness may not be exposed to it.’