< Kutoka 20 >
1 Mungu alisema maneno yote haya:
And God spoke all these words, saying,
2 Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa katika ardhi Misri, nje ya nyumba ya utumwa.
I am the Lord thy God, who have brought thee out of the land of Egypt, out of the house of slavery.
3 Msiwe na miungu mingine ila mimi tu.
Thou shalt have no other gods before me.
4 Msijitengenezee sanamu za kuchonga kufananisha na kitu chochote kilichopo juu ya mbingu, chini ya ardhi, au ndani ya maji.
Thou shalt not make unto thyself any graven image, or any likeness of any thing that is in heaven above, or that is on the earth beneath, or that is in the water under the earth.
5 Msipinde na kuabudu sanamu, mimi Yahweh Mungu wenu, ni Mungu mwenye wivu. Nitaadhibu uovu wa mabubu kwa kuleta adhabu juu ya kizazi, cha tatu hadi kizazi cha nne kwa wale wanao nichukia.
Thou shalt not bow thyself down to them, nor serve them; for I the Lord thy God am a jealous God, visiting the iniquity of the fathers upon the children, unto the third and fourth generation of them that hate me;
6 Ila nitaweka agano la uaminifu kwa maelfu watakao nipenda na kushika amri zangu.
And showing mercy unto the thousandth generation of them that love me, and keep my commandments.
7 Usilitaje bure jina la Yahweh Mungu wako, sitkuwa na hatia kwa yeyote atakaye taja jina langu bure.
Thou shalt not take the name of the Lord thy God in vain; for the Lord will not hold him guiltless that taketh his name in vain.
8 Ikumbuke siku ya Sabato, na kunitengea.
Remember the sabbath day to keep it holy.
9 lazima ufanye kazi zako zote kwa siku sita.
Six days shalt thou labor, and do all thy work.
10 Ila siku ya saba ni Sabato kwaajili ya Yahweh Mungu wako. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, au mwana wako, au binti yako, au mtumishi wako wakiume, au mtumishi wako mwanamke, au ng'ombe zako, au mgeni aliye ndani ya malango yako.
But the seventh day is the sabbath in honor of the Lord thy God; on it thou shalt not do any work, neither thou, nor thy son, nor thy daughter, thy man-servant, nor thy maid-servant, nor thy cattle, nor thy stranger that is within thy gates;
11 Kwa siku sita Yahweh aliumba mbingu na nchi, bahari, na vitu vyote vilivyomo, na siku ya saba alipumzika. Kwa hiyo Yahweh aliibariki siku ya Sabato na kuitenga.
For in six days the Lord made the heavens and the earth, the sea, and all that is in them, and rested on the seventh day; therefore the Lord blessed the sabbath day, and hallowed it.
12 Waheshimu baba na mama yako, ili uweze kuishi miaka mingi duniani Yahweh Mungu wako ametoa.
Honor thy father and thy mother; in order that thy days may be prolonged upon the land which the Lord thy God giveth thee.
14 Usifanye uasherati (usizini).
Thou shalt not commit adultery.
15 Usiibe kwa mtu yoyote.
Thou shalt not steal.
16 Usishuhudie uongo dhidi ya jirani yako.
Thou shalt not bear false witness against thy neighbor.
17 Usitaman nyumba ya jirani yako; usitamani mke wa jirani yako, wala mtumishi wake wakiume, mtumishi wake mwanamke, ng'ombe wake, punda wake, au chochote cha jirani yako.
Thou shalt not covet thy neighbor's house. Thou shalt not covet thy neighbor's wife, nor his man-servant, nor his maid-servant, nor his ox, nor his ass, nor any thing that is thy neighbor's.
18 Watu wote waliona radi na umeme, na kusikia sauti ya mbiu, na mlima ukitoa moshi. Watu walipoona hivo, walitetemeka na kusimama mbali.
And all the people perceived the thunders, and the lightnings, and the sound of the cornet, and the mountain smoking; and when the people saw it, they removed trembling, and stood afar off.
19 Wakamwambia Musa, ongea na sisi, na tutakusikiliza; lakini usiruhusu Mungu kuongea nasi, ama tutakufa.
And they said unto Moses, Speak thou with us, and we will hear; but let not God speak with us, lest we die.
20 Musa akawaambia watu, “msiogope, Mungu alikuja kuwajaribu ili heshima yake iwe ndani yenu, kwa hiyo msitende dhambi.”
And Moses said unto the people, Fear not; for in order to prove you, did God come, and in order that his fear may be before your faces, that ye sin not.
21 hivyo watu walisimama mbali, na Musa alikaribia giza nene Mungu alipokuwa.
And the people stood afar off, and Moses drew near unto the thick darkness where God was.
22 Yahweh alimwambia Musa, “Ni lazima uwaambie hili Waisraeli: 'Wewe mwenyewe umeona niliongea na wewe kutoka mbinguni.
And the Lord said unto Moses, Thus shalt thou say unto the children of Israel, Ye have seen that from heaven I have spoken with you.
23 Misjitengenezee miungu mingine pamoja nami, miungu ya fedha au miungu ya dhahabu.
Ye shall not make any thing with me; gods of silver, and gods of gold ye shall not make unto yourselves.
24 Tengenezeni madhabahu ya udongo kwa ajili yangu, na lazima mtoe sadaka ya kuteketeza, sadaka ya ushirika, kondoo, na ng'ombe. kila sehemu ntakapotaka jina langu liheshimiwe, nitakuja kwenu na kuwabariki.
An altar of earth shalt thou make unto me, and shalt sacrifice thereon thy burnt-offerings, and thy peace-offerings, thy sheep, and thy oxen; in every place where I shall permit my name to be mentioned, I will come unto thee, and I will bless thee.
25 Kama mtatengeneza madhabahu ya mawe, msijenge na mawe yaiyokatika, na kama mtatumia vyombo vyenu juu yake, mtaweka unajisi.
And if thou wilt make me an altar of stone, thou shalt not build it of hewn stone; for if thou lift up thy tool upon it, thou hast polluted it.
26 msije juu ya madhabahu yangu kwa hatua zenu; hii ni ili msioneshe sehemu zenu za siri.”
Neither shalt thou go up by steps upon my altar, that thy nakedness be not laid open thereon.