< Kutoka 18 >

1 Yethro, kuhani wa Midiani, baba mkwe wake Musa, alisikia yote Mungu aliyo fanya kwa Musa na kwa Israeli watu wake. Alisikia Yahweh ametoa Israeli kutoka Misri.
Jethro, the priest of Midian, Moses' father-in-law, heard of all that God had done for Moses and for Israel his people. He heard that Yahweh had brought Israel out of Egypt.
2 Yethro, baba mkwe wake Musa, akamchukuwa Zipora, mke wa Musa, baada ya kumpeleka nyumbani,
Jethro, Moses' father-in-law, took Zipporah, Moses' wife, after he had sent her home,
3 na wana wake wawili; jina mmoja lilikuwa Gershomu, kwa kuwa Musa alisema, “Nimekuwa mgeni katika nchi ya kigeni.”
and her two sons; the name of the one son was Gershom, for Moses had said, “I have been a foreigner in a foreign land.”
4 Jina la mwingine lilikuwa Eliezeri, kwa kuwa Musa alisema, “Mungu wa babu yangu alikuwa msaada wangu. Aliniokoa na mkono wa Farao.”
The name of the other was Eliezer, for Moses had said, “My ancestor's God was my help. He rescued me from Pharaoh's sword.”
5 Yethro, baba mkwe wake Musa, alikuja na watoto wake Musa na mke wake Musa nyikani alipo eka kambi katika mlima wa Mungu.
Jethro, Moses' father-in-law, came with Moses' sons and his wife to Moses in the wilderness where he was camped at the mountain of God.
6 Alimwambia Musa, “Mimi, baba mkwe wako Yethro, nina kuja kwako na mke wako na wanao wawili.”
He said to Moses, “I, your father-in-law Jethro, am coming to you with your wife and her two sons.”
7 Musa alitoka kwenda kukutana na baba mkwe wake, akamwinamia, na kumbusu. Wakajuliana hali na wakaingia ndani ya hema.
Moses went out to meet his father-in-law, bowed down, and kissed him. They asked about each other's welfare and then went into the tent.
8 Musa akamwambia baba mkwe wake yale yote Yahweh aliyo ya fanya kwa Farao na Wamisri kwa ajili ya Waisraeli, magumu yote yaliyo watoke njianim na jinsi Yahweh alivyo waokoa.
Moses told his father-in-law all that Yahweh had done to Pharaoh and the Egyptians for Israel's sake, about all the hardships that had come to them along the way, and how Yahweh had rescued them.
9 Yethro akafurahia yale mema yote Yahweh aliyo watendea Israeli, kwa hilo amewaokoa na mkono wa Wamisri.
Jethro rejoiced over all the good that Yahweh had done for Israel, in that he had rescued them from the hand of the Egyptians.
10 Yethro akasema, “Yahweh atukuzwe, kwa kuwa amekuokoa na mkono wa Wamisri na mkono wa Faraom na kuwatoa watu kwenye mkono wa Wamisri.
Jethro said, “May Yahweh be praised, for he has rescued you from the hand of the Egyptians and from the hand of Pharaoh, and delivered the people from the hand of the Egyptians.
11 Sasa najua Yahweh ni mkuu kuliko miungu yote, kwasababu Wamisri walipo watenda Waisraeli kwa kiburi, Mungu aliwaokoa watu wake.”
Now I know that Yahweh is greater than all the gods, because when the Egyptians treated the Israelites arrogantly, God rescued his people.”
12 Yethro, baba mkwe wake Musa, akaleta sadaka ya kuteketeza na dhabihu kwa Mungu. Aruni na wazee wote wa Israeli wakaja kula chakula mbele za Yahweh na baba mkwe wake Musa.
Jethro, Moses' father-in-law, brought a burnt offering and sacrifices for God. Aaron and all the elders of Israel came to eat a meal before God with Moses' father-in-law.
13 Siku iliyofuata Musa aliketi kuwa hukumu watu. Watu walisimama kumzunguka Musa kwanzia asubui hadi jioni.
On the next day Moses sat down to judge the people. The people stood around him from morning until evening.
14 Baba mkwe wake Musa alipo ona yale yote aliyo yafanya kwa watu, alisema, “Ni nini unachofanya na watu? Kwanini unaketi peke yako na watu wote wamesimama kukuzunguka asubui hadi jioni?”
When Moses' father-in-law saw all that he did for the people, he said, “What is this that you are doing with the people? Why is it that you sit alone and all the people stand about you from morning until evening?”
15 Musa akamwambia baba mkwe wake, “Watu wanakuja kuniuliza muongozo wa Mungu.
Moses said to his father-in-law, “The people come to me to ask for God's direction.
16 Wanapo kuwa na malumbano, wanakuja kwangu. Ninaamua kati ya mtu mmoja na mwingine, na nina wafundisha maagizo na sheria.”
When they have a dispute, they come to me. I decide between one person and another, and I teach them God's statutes and laws.”
17 Baba mkwe wake Musa alimwambia, “Unachofanya sicho kizuri sana.
Moses' father-in-law said to him, “What you are doing is not very good.
18 Hakika utajichosha, wewe na watu waliyopo na wewe. Huu mzigo ni mzito sana kwako. Hauwezi kufanya peke yako.
You will surely wear yourselves out, you and the people who are with you. This burden is too heavy for you. You are not able to do it by yourself.
19 Nisikilize. Nitakupa ushauri, na Mungu ata kuwa na wewe, kwasababu wewe nimwakilishi wa watu kwa Mungu, na una leta malumbano yao kwake.
Listen to me. I will give you advice, and God will be with you, because you are the people's representative to God, and you bring their disputes to him.
20 Lazima uwafundishe maagizo yake na sheria. Lazima uwafundishe njia yakutembea na kazi ya kufanya.
You must teach them his statutes and laws. You must show them the way to walk and the work to do.
21 Mbali zaidi, lazima uchague wanaume wenye uwezo kutoka watu wote, wanaume wanao muheshimu Mungu, wanaume wa kweli wanao chukuia mapato ya ufisadi. Lazima uwaeke juu ya watu, kuwa viongozi wa maelfu, mamia, hamsini, na makumi.
Furthermore, you must choose capable men from all the people, men who honor God, men of truth who hate unjust gain. You must put them over people, to be leaders in charge of thousands, hundreds, fifties, and of tens.
22 Watawa hukumu watu na kesi za kawaida, lakini kesi ngumu wataleta kwako. Kwa kesi ndogo, wanaweza kuhukumu wenyewe. Kwa hivyo itakuwa rahisi kwako, na watabeba mzigo na wewe.
They will judge the people in all routine cases, but the difficult cases they will bring to you. As for all the small cases, they can judge those themselves. In that way it will be easier for you, and they will carry the burden with you.
23 Ukifanya hivi, na kama Mungu akikuamuru kufanya al kadhalika, basi utaweza kuvumilia, na watu wote watarudi nyumbani wameridhika.”
If you do this, and if God commands you to do so, then you will be able to endure, and the entire people will be able to go home satisfied.”
24 Hivyo Musa akasikiliza maneno ya baba mkwe wake na akafanya yale yote aliyo yasema.
So Moses listened to his father-in-law's words and did everything that he had said.
25 Musa alichagua wanaume wenye uwezo kutoka Israeli na kuwa fanya vichwa juu ya watu, viongozi wahusika wa maelfu, mamia, hamsini, na makumi.
Moses chose capable men from all Israel and made them heads over the people, leaders in charge of thousands, hundreds, fifties, and tens.
26 Waliwa hukumu watu katika hali za kawaida. Kesi ngumu walimletea Musa, lakini wao wenyewe wali hukumu kesi ndogo.
They judged the people in normal circumstances. The difficult cases they brought to Moses, but they themselves judged all the small cases.
27 Kisha Musa akamwacha baba mkwe wake kuondoka, na Yethro akarudi kwenye nchi yake.
Then Moses let his father-in-law leave, and Jethro went back into his own land.

< Kutoka 18 >