< Kutoka 17 >
1 Jamii yote ya Israeli ili safiri kutoka nyikani ya Sinu, wakifuata maelekezo ya Yahweh. Walieka kambi Refidimu, lakini hapakuwa na maji ya watu kunywa.
And all the congregation of the children of Israel departed from the wilderness of Sin, according to their encampments, by the word of the Lord; and they encamped in Raphidin: and there was no water for the people to drink.
2 Hivyo watu wakamlaumu Musa kwa hali yao na kusema, “Tupe maji ya kunywa.” Musa akasema, “Kwanini mnagombana na mimi? Kwanini mnajaribu Yahweh?”
And the people reviled Moses, saying, Give us water, that we may drink; and Moses said to them, Why do you revile me, and why tempt you the Lord?
3 Watu walikuwa na kiu sana, na waka mlalamikia Musa. Wakasema, “Kwanini umetutoa Misri? Ili utuue sisi na watoto wetu na mifugo yetu kwa kiu?”
And the people thirsted there for water, and there the people murmured against Moses, saying, Why is this? have you brought us up out of Egypt to kill us and our children and our cattle with thirst?
4 Kisha Musa akamlilia Yahweh, “Nini ni fanya kwa hawa watu? Wako tayari ata kunipiga mawe.”
And Moses cried to the Lord, saying, What shall I do to this people? yet a little while and they will stone me.
5 Yahweh akamwambia Musa, “Nenda mbele yao, na uchukuwe baadhi ya wazee wa Israeli. Chukuwa gongo ulilo piga nalo mto, na uende.
And the Lord said to Moses, Go before this people, and take to yourself of the elders of the people; and the rod with which you struck the river, take in your hand, and you shall go.
6 Nitasimama mbele yako pale kwenye mwamba wa Horebu, na utaupiga mwamba. Maji yatatoka ya watu kunywa.” Kisha Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Israeli.
Behold, I stand there before you [come], on the rock in Choreb, and you shall strike the rock, and water shall come out from it, and the people shall drink. And Moses did so before the sons of Israel.
7 Aliita ile sehemu Massa na Meriba kwasababu ya malalamishi ya Waisraeli, na kwasababu walimjaribu Bwana kwa kusema, “Je Yahweh yupo miongoni mwetu au hapana?”
And he called the name of that place, Temptation, and Reviling, because of the reviling of the children of Israel, and because they tempted the Lord, saying, Is the Lord among us or not?
8 Kisha jeshi la watu wa Ameleki wakaja na kushambulia Israeli huko Refidimu.
And Amalec came and fought with Israel in Raphidin.
9 Hivyo Musa akamwambia Yoshua, “Chagau wanaume kadha na uende nje. Pigana na Ameleki. Kesho nitasimama juu ya kilima na gongo la Mungu mkononi mwangu.”
And Moses said to Joshua, Choose out for yourself mighty men, and go forth and set the army in array against Amalec to-morrow; and, behold, I [shall] stand on the top of the hill, and the rod of God [will be] in my hand.
10 Hivyo Yoshua akapigana na Ameleki kama Musa alivyo elekeza, wakati Musa, Aruni, na Huri walienda juu ya kilima.
And Joshua did as Moses said to him, and he went out and set the army in array against Amalec, and Moses and Aaron and Or went up to the top of the hill.
11 Wakati Musa alipo kuwa ameshikilia mikono yake juu, Israeli ilikuwa yashinda; alipo acha mikono yake ipumzike, Ameleki alianza kushinda.
And it came to pass, when Moses lifted up his hands, Israel prevailed; and when he let down his hands, Amalec prevailed.
12 Mikono ya Musa alipo kuwa mizito, Aruni na Huri walichukuwa jiwe na kuweka chini yake alikalie. Muda huo huo, Aruni na Huri walinyanyua mikono yake juu, mtu mmoja upande mmoja, na mtu mmoja upande mwingine. Hivyo mikono ya Musa ilishikiliwa tuli mpaka jua lilipo zama.
But the hands of Moses were heavy, and they took a stone and put it under him, and he sat upon it; and Aaron and Or supported his hands one on this side and the other on that, and the hands of Moses were supported till the going down of the sun.
13 Hivyo Yoshua akawashinda watu wa Ameleki kwa upanga.
And Joshua routed Amalec and all his people with the slaughter of the sword.
14 Yahweh akamwambia Musa, “Andika haya kwenye kitabu na umsomee Yoshua, kwasababu nitaondoa kumbukumbu ya Ameleki kutoka chini ya mbingu.”
And the Lord said to Moses, Write this for a memorial in a book, and speak [this] in the ears of Joshua; for I will utterly blot out the memorial of Amalec from under heaven.
15 Kisha Musa akajenga madhabahu na kuiita “Yahweh ni bendera yangu.”
And Moses built an altar to the Lord, and called the name of it, The Lord my Refuge.
16 Alisema, “Kwa kuwa mkono ulinyanyuliwa juu kuelekea kiti cha enzi cha Yahweh - kwamba Yahweh ata fanya vita na Ameleki vizazi na vizazi.”
For with a secret hand the Lord wages war upon Amalec to all generations.