< Kutoka 15 >

1 Kisha Musa na watu wa Israeli wakaimba hii nyimbo kwa Yahweh. Waliimba, “Nitaimba kwa Yahweh, kwa kuwa ameshinda kwa utukufu; farasi na dereva wake amewatupa kwenye bahari.
Then sang Moses and the children of Israel this song to the LORD, and spoke, saying, I will sing to the LORD, for he has triumphed gloriously: the horse and his rider has he thrown into the sea.
2 Yahweh ni uweza wangu na nyimbo yangu, na amekuwa wokovu wangu. Huyu ni Mungu wangu, na nitamsifu, Mungu wa baba yangu, nitamtukuza.
The LORD is my strength and song, and he is become my salvation: he is my God, and I will prepare him an habitation; my father’s God, and I will exalt him.
3 Yahweh ni shujaa; Yahweh ni jina lake.
The LORD is a man of war: the LORD is his name.
4 Ametupa magari ya farasi ya Farao na jeshi lake kwenye bahari. Maafisa wa Farao hodari walizama kwenye Bahari ya Shamu.
Pharaoh’s chariots and his host has he cast into the sea: his chosen captains also are drowned in the Red sea.
5 Kina kiliwafunika; walienda kwenye kina kama jiwe.
The depths have covered them: they sank into the bottom as a stone.
6 Mkono wako wakulia, Yahweh, una nguvu ya utukufu; mkono wako, Yahweh, umewavunja adui.
Your right hand, O LORD, is become glorious in power: your right hand, O LORD, has dashed in pieces the enemy.
7 Kwa utukufu mkubwa umewapindua walio inuka dhidi yako. Umetuma gadhabu; imewateketeza kama karatasi.
And in the greatness of your excellency you have overthrown them that rose up against you: you sent forth your wrath, which consumed them as stubble.
8 Kwa pumzi ya pua yako maji yalijaa; maji yanayo tembea yalisimama wima na kujaa juu; maji yalikuwa manene ndani ya kilindi cha bahari.
And with the blast of your nostrils the waters were gathered together, the floods stood upright as an heap, and the depths were congealed in the heart of the sea.
9 Adui alisema, 'Nitakimbiza, nitapita, nitagawa nitakacho chukuwa; tamanio langu litatimizwa kwao; nitavuta upanga wangu; mkono wangu utawaharibu wao.'
The enemy said, I will pursue, I will overtake, I will divide the spoil; my lust shall be satisfied on them; I will draw my sword, my hand shall destroy them.
10 Lakini ulipuliza kwa upepo wako, na bahari ikawafunika wao; walizama kama chuma nzito kwenye maji mengi.
You did blow with your wind, the sea covered them: they sank as lead in the mighty waters.
11 Ni nani kama wewe, Yahweh, miongoni mwa miungu? Nani kama wewe, mtakatifu wa utukufu, katika sifa umetukuzwa, anaye fanya miujiza?
Who is like to you, O LORD, among the gods? who is like you, glorious in holiness, fearful in praises, doing wonders?
12 Ulinyoosha mkono wako wa kulia, na dunia ikawameza.
You stretched out your right hand, the earth swallowed them.
13 Katika uaminifu wa agano lako umewaongoza watu ulio waokoa. Katika uweza wako umewaongoza katika sehemu takatifu unayo ishi.
You in your mercy have led forth the people which you have redeemed: you have guided them in your strength to your holy habitation.
14 Watu watasikia, na watatetemeka; hofu itawakumba wakazi wa Filistia.
The people shall hear, and be afraid: sorrow shall take hold on the inhabitants of Palestina.
15 Kisha wazee wa Edomu wataogopa; wanajeshi wa Moabu watetemeka; wakazi wote wa Kanani watayayuka.
Then the dukes of Edom shall be amazed; the mighty men of Moab, trembling shall take hold on them; all the inhabitants of Canaan shall melt away.
16 Mshituko na hofu vitawaangukia. Kwasababu ya nguvu ya mkono wako, watakuwa kimya kama jiwe hadi watu wako watakapo pita, Yahweh - hadi watu ulio waokoa watakapo pita.
Fear and dread shall fall on them; by the greatness of your arm they shall be as still as a stone; till your people pass over, O LORD, till the people pass over, which you have purchased.
17 Utawaleta na kuwapanda kwenye mlima wa urithi wako, sehemu, Yahweh, ulio jenga ya kuishi, sehemu takatifu, Bwana wetu, mikono yako iliyo jenga.
You shall bring them in, and plant them in the mountain of your inheritance, in the place, O LORD, which you have made for you to dwell in, in the Sanctuary, O LORD, which your hands have established.
18 Yahweh ata tawala milele na milele.”
The LORD shall reign for ever and ever.
19 Kwa kuwa farasi wa Farao walienda na magari ya farasi na wapanda farasi kwenye bahari. Yahweh alileta maji ya bahari juu yao. Lakini Waisraeli walienda juu ya nchi kavu katikati ya bahari.
For the horse of Pharaoh went in with his chariots and with his horsemen into the sea, and the LORD brought again the waters of the sea on them; but the children of Israel went on dry land in the middle of the sea.
20 Miriamu nabii wa kike, dada wa Aruni, akanyanyua tari, na wanawake wote wakatoka na matari, wakicheza nae.
And Miriam the prophetess, the sister of Aaron, took a tambourine in her hand; and all the women went out after her with tambourines and with dances.
21 Miriamu akawaimbia: “Muimbieni Yahweh, kwa kuwa ameshinda kwa utukufu. Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.
And Miriam answered them, Sing you to the LORD, for he has triumphed gloriously; the horse and his rider has he thrown into the sea.
22 Kisha Musa akaongoza Israeli mbele kupita Bahari ya Shamu. Walienda nyikani ya Shuri. Walisafiri kwa siku tatu nyikani pasipo kuona maji yeyote.
So Moses brought Israel from the Red sea, and they went out into the wilderness of Shur; and they went three days in the wilderness, and found no water.
23 Kisha wakaja Mara, lakini hawakunywa maji ya huko kwasababu yalikuwa machungu. Hivyo wakaita hiyo sehemu Mara.
And when they came to Marah, they could not drink of the waters of Marah, for they were bitter: therefore the name of it was called Marah.
24 Hivyo watu wakamlalamikia Musa na kusema, “Nini tunaweza kunywa?”
And the people murmured against Moses, saying, What shall we drink?
25 Musa akamlilia Yahweh, na kumonyesha mti. Musa akautupa kwenye maji, na maji yakawa matamu kunywa. Ndio pale Yahweh alipowapa sheria kali, na ndio pale alipo wajaribu.
And he cried to the LORD; and the LORD showed him a tree, which when he had cast into the waters, the waters were made sweet: there he made for them a statute and an ordinance, and there he proved them,
26 Alisema, “Kama utasikiliza sauti ya Yahweh Mungu wako kwa umakini, na kufanya yalio sahihi machoni pake, na kama utatega sikio kwa amri zake na kutii sheria zake zote - sitawaekea ninyi magonjwa yale niliyo waekea Wamisri, kwa kuwa mimi ni Yahweh ninaye kuponya.”
And said, If you will diligently listen to the voice of the LORD your God, and will do that which is right in his sight, and will give ear to his commandments, and keep all his statutes, I will put none of these diseases on you, which I have brought on the Egyptians: for I am the LORD that heals you.
27 Kisha watu wakaja Elimu, palipo kuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mtende. Walieka kambi hapo pembeni ya maji.
And they came to Elim, where were twelve wells of water, and three score and ten palm trees: and they encamped there by the waters.

< Kutoka 15 >