< Kutoka 15 >

1 Kisha Musa na watu wa Israeli wakaimba hii nyimbo kwa Yahweh. Waliimba, “Nitaimba kwa Yahweh, kwa kuwa ameshinda kwa utukufu; farasi na dereva wake amewatupa kwenye bahari.
Then sang Moses and the children of Israel this song vnto the Lord, and sayd in this maner, I will sing vnto the Lord: for he hath triumphed gloriously: the horse and him that rode vpon him hath he ouerthrowen in the Sea.
2 Yahweh ni uweza wangu na nyimbo yangu, na amekuwa wokovu wangu. Huyu ni Mungu wangu, na nitamsifu, Mungu wa baba yangu, nitamtukuza.
The Lord is my strength and praise, and he is become my saluation. He is my God, and I will prepare him a tabernacle. he is my fathers God, and I will exalt him.
3 Yahweh ni shujaa; Yahweh ni jina lake.
The Lord is a man of warre, his Name is Iehouah.
4 Ametupa magari ya farasi ya Farao na jeshi lake kwenye bahari. Maafisa wa Farao hodari walizama kwenye Bahari ya Shamu.
Pharaohs charets and his host hath he cast into the Sea: his chosen captaines also were drowned in the red Sea.
5 Kina kiliwafunika; walienda kwenye kina kama jiwe.
The depths haue couered them, they sanke to the bottome as a stone.
6 Mkono wako wakulia, Yahweh, una nguvu ya utukufu; mkono wako, Yahweh, umewavunja adui.
Thy right hande, O Lord, is glorious in power: thy right hand, O Lord, hath brused the enemie.
7 Kwa utukufu mkubwa umewapindua walio inuka dhidi yako. Umetuma gadhabu; imewateketeza kama karatasi.
And in thy great glorie thou hast ouerthrowen them that rose against thee: thou sentest forth thy wrath, which consumed them as the stubble.
8 Kwa pumzi ya pua yako maji yalijaa; maji yanayo tembea yalisimama wima na kujaa juu; maji yalikuwa manene ndani ya kilindi cha bahari.
And by the blast of thy nostrels the waters were gathered, the floods stoode still as an heape, the depthes congealed together in the heart of the Sea.
9 Adui alisema, 'Nitakimbiza, nitapita, nitagawa nitakacho chukuwa; tamanio langu litatimizwa kwao; nitavuta upanga wangu; mkono wangu utawaharibu wao.'
The enemie sayd, I wil pursue, I wil ouertake them, I will deuide the spoyle, my lust shall bee satisfied vpon them, I will drawe my sworde, mine hand shall destroy them.
10 Lakini ulipuliza kwa upepo wako, na bahari ikawafunika wao; walizama kama chuma nzito kwenye maji mengi.
Thou blewest with thy winde, the Sea couered them, they sanke as leade in the mightie waters.
11 Ni nani kama wewe, Yahweh, miongoni mwa miungu? Nani kama wewe, mtakatifu wa utukufu, katika sifa umetukuzwa, anaye fanya miujiza?
Who is like vnto thee, O Lord, among the Gods! who is like thee so glorious in holinesse, fearefull in prayses, doing wonders!
12 Ulinyoosha mkono wako wa kulia, na dunia ikawameza.
Thou stretchedst out thy right hande, the earth swallowed them.
13 Katika uaminifu wa agano lako umewaongoza watu ulio waokoa. Katika uweza wako umewaongoza katika sehemu takatifu unayo ishi.
Thou wilt by thy mercie cary this people, which thou deliueredst: thou wilt bring them in thy strength vnto thine holy habitation.
14 Watu watasikia, na watatetemeka; hofu itawakumba wakazi wa Filistia.
The people shall heare and be afraide: sorow shall come vpon the inhabitants of Palestina.
15 Kisha wazee wa Edomu wataogopa; wanajeshi wa Moabu watetemeka; wakazi wote wa Kanani watayayuka.
Then the dukes of Edom shalbe amased, and trembling shall come vpon the great men of Moab: all the inhabitantes of Canaan shall waxe faint hearted.
16 Mshituko na hofu vitawaangukia. Kwasababu ya nguvu ya mkono wako, watakuwa kimya kama jiwe hadi watu wako watakapo pita, Yahweh - hadi watu ulio waokoa watakapo pita.
Feare and dread shall fall vpon them: because of the greatnesse of thine arme, they shalbe stil as a stone, till thy people passe, O Lord: til this people passe, which thou hast purchased.
17 Utawaleta na kuwapanda kwenye mlima wa urithi wako, sehemu, Yahweh, ulio jenga ya kuishi, sehemu takatifu, Bwana wetu, mikono yako iliyo jenga.
Thou shalt bring them in, and plant them in the mountaine of thine inheritance, which is the place that thou hast prepared, O Lord, for to dwell in, euen the sanctuarie, O Lord, which thine hands shall establish.
18 Yahweh ata tawala milele na milele.”
The Lord shall reigne for euer and euer.
19 Kwa kuwa farasi wa Farao walienda na magari ya farasi na wapanda farasi kwenye bahari. Yahweh alileta maji ya bahari juu yao. Lakini Waisraeli walienda juu ya nchi kavu katikati ya bahari.
For Pharaohs horses went with his charets and horsemen into the Sea, and the Lord brought the waters of the Sea vpon them: but the children of Israel went on drie land in the middes of the Sea.
20 Miriamu nabii wa kike, dada wa Aruni, akanyanyua tari, na wanawake wote wakatoka na matari, wakicheza nae.
And Miriam the prophetesse, sister of Aaron tooke a timbrell in her hande, and all the women came out after her with timbrels and daunces.
21 Miriamu akawaimbia: “Muimbieni Yahweh, kwa kuwa ameshinda kwa utukufu. Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.
And Miriam answered the men, Sing yee vnto the Lord: for he hath triumphed gloriously: the horse and his rider hath hee ouerthrowen in the Sea.
22 Kisha Musa akaongoza Israeli mbele kupita Bahari ya Shamu. Walienda nyikani ya Shuri. Walisafiri kwa siku tatu nyikani pasipo kuona maji yeyote.
Then Moses brought Israel from the redde Sea, and they went out into the wildernesse of Shur: and they went three dayes in the wildernesse, and found no waters.
23 Kisha wakaja Mara, lakini hawakunywa maji ya huko kwasababu yalikuwa machungu. Hivyo wakaita hiyo sehemu Mara.
And whe they came to Marah, they could not drinke of the waters of Marah, for they were bitter: therefore the name of the place was called Marah.
24 Hivyo watu wakamlalamikia Musa na kusema, “Nini tunaweza kunywa?”
Then the people murmured against Moses, saying, What shall we drinke?
25 Musa akamlilia Yahweh, na kumonyesha mti. Musa akautupa kwenye maji, na maji yakawa matamu kunywa. Ndio pale Yahweh alipowapa sheria kali, na ndio pale alipo wajaribu.
And he cried vnto the Lord, and the Lord shewed him a tree, which when he had cast into the waters, the waters were sweete: there he made them an ordinance and a law, and there he proued them,
26 Alisema, “Kama utasikiliza sauti ya Yahweh Mungu wako kwa umakini, na kufanya yalio sahihi machoni pake, na kama utatega sikio kwa amri zake na kutii sheria zake zote - sitawaekea ninyi magonjwa yale niliyo waekea Wamisri, kwa kuwa mimi ni Yahweh ninaye kuponya.”
And sayd, if thou wilt diligently hearken, O Israel, vnto the voyce of the Lord thy God, and wilt do that, which is right in his sight, and wilt giue eare vnto his commandements, and keepe all his ordinances, then will I put none of these diseases vpon thee, which I brought vpon the Egyptians: for I am the Lord that healeth thee.
27 Kisha watu wakaja Elimu, palipo kuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mtende. Walieka kambi hapo pembeni ya maji.
And they came to Elim, where were twelue fountaines of water, and seuentie palme trees, and they camped thereby the waters.

< Kutoka 15 >