< Kutoka 15 >

1 Kisha Musa na watu wa Israeli wakaimba hii nyimbo kwa Yahweh. Waliimba, “Nitaimba kwa Yahweh, kwa kuwa ameshinda kwa utukufu; farasi na dereva wake amewatupa kwenye bahari.
Then Moses and the sons of Israel sang this song to the Lord, and they said: “Let us sing to the Lord, for he has been gloriously magnified: the horse and the rider he has cast into the sea.
2 Yahweh ni uweza wangu na nyimbo yangu, na amekuwa wokovu wangu. Huyu ni Mungu wangu, na nitamsifu, Mungu wa baba yangu, nitamtukuza.
The Lord is my strength and my praise, and he has become my salvation. He is my God, and I shall glorify him. He is the God of my father, and I shall exalt him.
3 Yahweh ni shujaa; Yahweh ni jina lake.
The Lord is like a fighting man. Almighty is his name.
4 Ametupa magari ya farasi ya Farao na jeshi lake kwenye bahari. Maafisa wa Farao hodari walizama kwenye Bahari ya Shamu.
The chariots of Pharaoh, and his army, he has cast into the sea; his elect leaders have been submerged in the Red Sea.
5 Kina kiliwafunika; walienda kwenye kina kama jiwe.
The abyss has covered them. They descended into the depths like a stone.
6 Mkono wako wakulia, Yahweh, una nguvu ya utukufu; mkono wako, Yahweh, umewavunja adui.
Your right hand, O Lord, has been magnified in strength. Your right hand, O Lord, has struck down the enemy.
7 Kwa utukufu mkubwa umewapindua walio inuka dhidi yako. Umetuma gadhabu; imewateketeza kama karatasi.
And in the multitude of your glory you have put down your adversaries. You sent out your wrath, which devoured them like stubble.
8 Kwa pumzi ya pua yako maji yalijaa; maji yanayo tembea yalisimama wima na kujaa juu; maji yalikuwa manene ndani ya kilindi cha bahari.
And by the breath of your fury, the waters were gathered together. The flowing waves stood still. The abyss was gathered into the midst of the sea.
9 Adui alisema, 'Nitakimbiza, nitapita, nitagawa nitakacho chukuwa; tamanio langu litatimizwa kwao; nitavuta upanga wangu; mkono wangu utawaharibu wao.'
The enemy said: ‘I will pursue and overtake them. I will divide the spoils. My soul will be filled. I will unsheathe my sword. My hand will put them to death.’
10 Lakini ulipuliza kwa upepo wako, na bahari ikawafunika wao; walizama kama chuma nzito kwenye maji mengi.
Your breath blew, and the sea covered them. They were submerged like lead into the mighty waters.
11 Ni nani kama wewe, Yahweh, miongoni mwa miungu? Nani kama wewe, mtakatifu wa utukufu, katika sifa umetukuzwa, anaye fanya miujiza?
Who is like you in strength, O Lord? Who is like you: magnificent in sanctity, terrible and yet praiseworthy, accomplishing miracles?
12 Ulinyoosha mkono wako wa kulia, na dunia ikawameza.
You extended your hand, and the earth devoured them.
13 Katika uaminifu wa agano lako umewaongoza watu ulio waokoa. Katika uweza wako umewaongoza katika sehemu takatifu unayo ishi.
In your mercy, you have been a leader to the people whom you have redeemed. And in your strength, you have carried them to your holy dwelling place.
14 Watu watasikia, na watatetemeka; hofu itawakumba wakazi wa Filistia.
Peoples rose up and became angry. Sorrows took hold of the inhabitants of Philistia.
15 Kisha wazee wa Edomu wataogopa; wanajeshi wa Moabu watetemeka; wakazi wote wa Kanani watayayuka.
Then the leaders of Edom were stirred up, and trembling took hold of the robust of Moab. All the inhabitants of Canaan were petrified.
16 Mshituko na hofu vitawaangukia. Kwasababu ya nguvu ya mkono wako, watakuwa kimya kama jiwe hadi watu wako watakapo pita, Yahweh - hadi watu ulio waokoa watakapo pita.
Let fear and dread fall upon them, by the magnitude of your arm. Let them become immobilized like stone, until your people cross through, O Lord, until this, your people whom you possess, cross through.
17 Utawaleta na kuwapanda kwenye mlima wa urithi wako, sehemu, Yahweh, ulio jenga ya kuishi, sehemu takatifu, Bwana wetu, mikono yako iliyo jenga.
You shall lead them in and plant them, on the mountain of your inheritance, in your most firm dwelling place, which you have formed, O Lord, your sanctuary, O Lord, which your hands have made firm.
18 Yahweh ata tawala milele na milele.”
The Lord will reign in eternity and beyond.
19 Kwa kuwa farasi wa Farao walienda na magari ya farasi na wapanda farasi kwenye bahari. Yahweh alileta maji ya bahari juu yao. Lakini Waisraeli walienda juu ya nchi kavu katikati ya bahari.
For the rider Pharaoh, with his chariots and horsemen, was brought into the sea. And the Lord brought back upon them the waters of the sea. But the sons of Israel walked across dry ground in its midst.”
20 Miriamu nabii wa kike, dada wa Aruni, akanyanyua tari, na wanawake wote wakatoka na matari, wakicheza nae.
And so Miriam, the prophetess, the sister of Aaron, took up a timbrel in her hand. And all the women followed her with timbrels and dancing.
21 Miriamu akawaimbia: “Muimbieni Yahweh, kwa kuwa ameshinda kwa utukufu. Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.
And she prophesied, saying: “Let us sing to the Lord, for he has been gloriously magnified. The horse and its rider, he has thrown into the sea.”
22 Kisha Musa akaongoza Israeli mbele kupita Bahari ya Shamu. Walienda nyikani ya Shuri. Walisafiri kwa siku tatu nyikani pasipo kuona maji yeyote.
Then Moses took Israel from the Red Sea, and they went forth into the desert of Shur. And they wandered for three days through the wilderness, and they found no water.
23 Kisha wakaja Mara, lakini hawakunywa maji ya huko kwasababu yalikuwa machungu. Hivyo wakaita hiyo sehemu Mara.
And they arrived at Marah. They were unable to drink the waters of Marah because they were bitter. Therefore, he also established a name befitting the place, calling it ‘Marah,’ that is, bitterness.
24 Hivyo watu wakamlalamikia Musa na kusema, “Nini tunaweza kunywa?”
And the people murmured against Moses, saying: “What shall we drink?”
25 Musa akamlilia Yahweh, na kumonyesha mti. Musa akautupa kwenye maji, na maji yakawa matamu kunywa. Ndio pale Yahweh alipowapa sheria kali, na ndio pale alipo wajaribu.
So he cried out to the Lord, who showed him a tree. And when he had cast it into the waters, they were turned into sweetness. In that place, he established instructions for him, and also judgments. And he tested him there,
26 Alisema, “Kama utasikiliza sauti ya Yahweh Mungu wako kwa umakini, na kufanya yalio sahihi machoni pake, na kama utatega sikio kwa amri zake na kutii sheria zake zote - sitawaekea ninyi magonjwa yale niliyo waekea Wamisri, kwa kuwa mimi ni Yahweh ninaye kuponya.”
saying: “If you will listen to the voice of the Lord your God, and do what is right in his sight, and obey his commands, and keep all his precepts, I will not bring upon you any of the distress that I imposed on Egypt. For I am the Lord, your healer.”
27 Kisha watu wakaja Elimu, palipo kuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mtende. Walieka kambi hapo pembeni ya maji.
Then the sons of Israel arrived in Elim, where there were twelve fountains of water and seventy palm trees. And they camped next to the waters.

< Kutoka 15 >