< Kutoka 15 >

1 Kisha Musa na watu wa Israeli wakaimba hii nyimbo kwa Yahweh. Waliimba, “Nitaimba kwa Yahweh, kwa kuwa ameshinda kwa utukufu; farasi na dereva wake amewatupa kwenye bahari.
Then Moses and the children of Israel made this song to the Lord, and said, I will make a song to the Lord, for he is lifted up in glory: the horse and the horseman he has sent down into the sea.
2 Yahweh ni uweza wangu na nyimbo yangu, na amekuwa wokovu wangu. Huyu ni Mungu wangu, na nitamsifu, Mungu wa baba yangu, nitamtukuza.
The Lord is my strength and my strong helper, he has become my salvation: he is my God and I will give him praise; my father's God and I will give him glory.
3 Yahweh ni shujaa; Yahweh ni jina lake.
The Lord is a man of war: the Lord is his name.
4 Ametupa magari ya farasi ya Farao na jeshi lake kwenye bahari. Maafisa wa Farao hodari walizama kwenye Bahari ya Shamu.
Pharaoh's war-carriages and his army he has sent down into the sea: the best of his captains have gone down into the Red Sea.
5 Kina kiliwafunika; walienda kwenye kina kama jiwe.
They were covered by the deep waters: like a stone they went down under the waves.
6 Mkono wako wakulia, Yahweh, una nguvu ya utukufu; mkono wako, Yahweh, umewavunja adui.
Full of glory, O Lord, is the power of your right hand; by your right hand those who came against you are broken.
7 Kwa utukufu mkubwa umewapindua walio inuka dhidi yako. Umetuma gadhabu; imewateketeza kama karatasi.
When you are lifted up in power, all those who come against you are crushed: when you send out your wrath, they are burned up like dry grass.
8 Kwa pumzi ya pua yako maji yalijaa; maji yanayo tembea yalisimama wima na kujaa juu; maji yalikuwa manene ndani ya kilindi cha bahari.
By your breath the waves were massed together, the flowing waters were lifted up like a pillar; the deep waters became solid in the heart of the sea.
9 Adui alisema, 'Nitakimbiza, nitapita, nitagawa nitakacho chukuwa; tamanio langu litatimizwa kwao; nitavuta upanga wangu; mkono wangu utawaharibu wao.'
Egypt said, I will go after them, I will overtake, I will make division of their goods: my desire will have its way with them; my sword will be uncovered, my hand will send destruction on them.
10 Lakini ulipuliza kwa upepo wako, na bahari ikawafunika wao; walizama kama chuma nzito kwenye maji mengi.
You sent your wind and the sea came over them: they went down like lead into the great waters.
11 Ni nani kama wewe, Yahweh, miongoni mwa miungu? Nani kama wewe, mtakatifu wa utukufu, katika sifa umetukuzwa, anaye fanya miujiza?
Who is like you, O Lord, among the gods? who is like you, in holy glory, to be praised with fear, doing wonders?
12 Ulinyoosha mkono wako wa kulia, na dunia ikawameza.
When your right hand was stretched out, the mouth of the earth was open for them.
13 Katika uaminifu wa agano lako umewaongoza watu ulio waokoa. Katika uweza wako umewaongoza katika sehemu takatifu unayo ishi.
In your mercy you went before the people whom you have made yours; guiding them in your strength to your holy place.
14 Watu watasikia, na watatetemeka; hofu itawakumba wakazi wa Filistia.
Hearing of you the peoples were shaking in fear: the people of Philistia were gripped with pain.
15 Kisha wazee wa Edomu wataogopa; wanajeshi wa Moabu watetemeka; wakazi wote wa Kanani watayayuka.
The chiefs of Edom were troubled in heart; the strong men of Moab were in the grip of fear: all the people of Canaan became like water.
16 Mshituko na hofu vitawaangukia. Kwasababu ya nguvu ya mkono wako, watakuwa kimya kama jiwe hadi watu wako watakapo pita, Yahweh - hadi watu ulio waokoa watakapo pita.
Fear and grief came on them; by the strength of your arm they were turned to stone; till your people went over, O Lord, till the people went over whom you have made yours.
17 Utawaleta na kuwapanda kwenye mlima wa urithi wako, sehemu, Yahweh, ulio jenga ya kuishi, sehemu takatifu, Bwana wetu, mikono yako iliyo jenga.
You will take them in, planting them in the mountain of your heritage, the place, O Lord, where you have made your house, the holy place, O Lord, the building of your hands.
18 Yahweh ata tawala milele na milele.”
The Lord is King for ever and ever.
19 Kwa kuwa farasi wa Farao walienda na magari ya farasi na wapanda farasi kwenye bahari. Yahweh alileta maji ya bahari juu yao. Lakini Waisraeli walienda juu ya nchi kavu katikati ya bahari.
For the horses of Pharaoh, with his war-carriages and his horsemen, went into the sea, and the Lord sent the waters of the sea back over them; but the children of Israel went through the sea on dry land.
20 Miriamu nabii wa kike, dada wa Aruni, akanyanyua tari, na wanawake wote wakatoka na matari, wakicheza nae.
And Miriam, the woman prophet, the sister of Aaron, took an instrument of music in her hand; and all the women went after her with music and dances.
21 Miriamu akawaimbia: “Muimbieni Yahweh, kwa kuwa ameshinda kwa utukufu. Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.
And Miriam, answering, said, Make a song to the Lord, for he is lifted up in glory; the horse and the horseman he has sent into the sea.
22 Kisha Musa akaongoza Israeli mbele kupita Bahari ya Shamu. Walienda nyikani ya Shuri. Walisafiri kwa siku tatu nyikani pasipo kuona maji yeyote.
Then Moses took Israel forward from the Red Sea, and they went out into the waste land of Shur; and for three days they were in the waste land where there was no water.
23 Kisha wakaja Mara, lakini hawakunywa maji ya huko kwasababu yalikuwa machungu. Hivyo wakaita hiyo sehemu Mara.
And when they came to Marah, the water was no good for drinking, for the waters of Marah were bitter, which is why it was named Marah.
24 Hivyo watu wakamlalamikia Musa na kusema, “Nini tunaweza kunywa?”
And the people, crying out against Moses, said, What are we to have for drink?
25 Musa akamlilia Yahweh, na kumonyesha mti. Musa akautupa kwenye maji, na maji yakawa matamu kunywa. Ndio pale Yahweh alipowapa sheria kali, na ndio pale alipo wajaribu.
And in answer to his prayer, the Lord made him see a tree, and when he put it into the water, the water was made sweet. There he gave them a law and an order, testing them;
26 Alisema, “Kama utasikiliza sauti ya Yahweh Mungu wako kwa umakini, na kufanya yalio sahihi machoni pake, na kama utatega sikio kwa amri zake na kutii sheria zake zote - sitawaekea ninyi magonjwa yale niliyo waekea Wamisri, kwa kuwa mimi ni Yahweh ninaye kuponya.”
And he said, If with all your heart you will give attention to the voice of the Lord your God, and do what is right in his eyes, giving ear to his orders and keeping his laws, I will not put on you any of the diseases which I put on the Egyptians: for I am the Lord your life-giver.
27 Kisha watu wakaja Elimu, palipo kuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mtende. Walieka kambi hapo pembeni ya maji.
And they came to Elim where there were twelve water-springs and seventy palm-trees: and they put up their tents there by the waters.

< Kutoka 15 >