< Kutoka 14 >

1 Yahweh akasema na Musa na kumwambia,
Then spake Yahweh unto Moses, saying:
2 “Waambie Waisraeli wageuke na kueka kambi mbele ya Pi Hahirothi, katikati ya Migdoli na bahari, mbele ya Baali Zefoni. Wapaswa kueka kambi pembenni ya Pi Hahirothi.
Speak unto the sons of Israel, that they turn back and encamp before Pi-hahiroth, between Migdol and the sea, —before Baal-zephon, over against it, shall ye encamp, by the sea.
3 Farao atasema kuhusu Waisraeli, 'Wanaangaika kwenye nchi. Nyikani imewafunika.'
Then will Pharaoh say, of the sons of Israel, Entangled, they are in the land, —the desert hath closed in upon them.
4 Nitaufanya moyo wa Farao mgumu, na yeye ata wakimbiza. Nitapata utukufu kwasababu ya Farao na jeshi lake lote. Wamisri watajua mimi ni Yahweh.” Kisha Waisraeli wakaeka kambi kama walivyo elekezwa.
So will I let the heart of Pharaoh wax bold, and he will pursue them, that I may get me honour over Pharaoh, and over all his forces, and the Egyptians shall know, that I, am Yahweh. And they did so.
5 Mfalme wa Misri alipo ambiwa Waisraeli wametoroka, nia ya Farao na watumishi wake ikageuka dhidi ya watu. Wakasema, “Tumefanya nini kwa kuwaacha Waisraeli waende huru na wasitutumikie?”
And it was told the king of Egypt, that the people had fled, —and the heart of Pharaoh and his servants was turned against the people, and they said—What is this we have done, that we have let Israel go from serving us?
6 Kisha Farao akachukuwa magari yake ya farasi na jeshi lake.
So he yoked his chariot, —and his people, took he with him.
7 Alichukuwa magari ya farasi mia sita imara na magari yote ya farasi ya Misri, pamoja na maafisa wa hayo magari.
And he took six hundred chosen chariots, and all the chariots of Egypt, —with warriors in every one.
8 Yahweh akafanya mgumu moyo wa Farao, mfalme wa Misri, na mfalme akawafukuzia Waisraeli. Sasa Waisraeli waliondoka kwa shangwe.
And Yahweh let the heart of Pharaoh king of Egypt wax bold, and he pursued the sons of Israel, —when the sons of Israel, were going out with a high hand.
9 Lakini Wamisri wali wafukuzia, pamoja na farasi na magari ya farasi, wapanda farasi, na jeshi lake. Walikuta Waisraeli wameeka kambi pembezoni mwa bahari kati ya Pi Hahirothi na Baali Zefoni.
So the Egyptians pursued them and overtook them, encamping by the sea—all the horses and chariots of Pharaoh, and his horsemen, and his forces, —by Pi-hahiroth, before Baal-zephon.
10 Farao alipo karibia, Waisraeli walitaza juu na kushangaa. Wamisri walikuwa wakija kwao, na waliogopa. Waisraeli walimlilia Yahweh.
Now when, Pharaoh, had drawn near, the sons of Israel lifted up their eyes, and lo! the Egyptians, moving along after them and they feared greatly, and the sons of Israel made outcry unto Yahweh.
11 Walimwambia Musa, “Ni kwasababu hakukuwa na makaburi Misri, hadi umetuleta tufe huku nyikani? Kwanini umetutendea hivi, kwa kututoa Misri?
Then said they unto Moses, Was it because there were no graves in Egypt, that thou didst fetch us to die in the desert? What is this thou hast done to us, bringing us forth out of Egypt?
12 Hili si ndilo tulilo kwambia Misri? Tulikwambia, 'Utuache, ili tuwafanyie Wamisri kazi.' Ingekuwa bora kwetu sisi kuwafanyia kazi kuliko kufa nyikani.”
Is not this the word which we spake unto thee in Egypt, saying, Let us alone, that we may serve the Egyptians, —for it is better for us, to serve the Egyptians, than to die in the desert?
13 Musa akawaambia watu, “Msiogope. Simameni imara na muone wokovu Yahweh atakao uleta kwenu leo. Kwa maana hamtawaona tena Wamisri mnao waona leo.
And Moses said unto the people—Do not fear, stand still and see the salvation of Yahweh, which he will work for you to-day, —for as for the Egyptians whom ye have seen to-day, ye shall not again see them any more to times age-abiding.
14 Yahweh ata wapigania, na ninyi mtasima imara.”
Yahweh, will fight for you, —and, ye, shall forbear.
15 Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Kwanini wewe, Musa, unaendelea kuniita mimi? Waambie Waisraeli waendelee mbele.
And Yahweh said unto Moses, What outcry wouldst thou make unto me? Speak unto the sons of Israel, that they go forward;
16 Nyanyua gongo lako juu, nyoosha mkono wako kuelekea baharini na uigawanye sehemu mbili, ili watu wa Israeli wapite baharini kwenye nchi kavu.
and, thou, lift high thy staff and stretch forth thy hand over the sea and cleave it asunder, —that the sons of Israel may enter into the midst of the sea on dry ground;
17 Jitahadharishe kuwa nitafanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu ili wawafuate. Nitapata utukufu kwasababu ya Farao na jeshi lake lote, magari yake ya farasi, na wapanda farasi.
and, I, behold me letting the heart of the Egyptians wax bold, that they may enter after them, —that I may get me honour over Pharaoh and over his forces, over his chariots, and over his horsemen,
18 Kisha Wamisri watajua kuwa mimi ni Yahweh nitakapo pata utukufu kwasababu ya Farao, magari yake ya farasi, na wapanda farasi wake.”
And the Egyptians shall know, that, I, am Yahweh, —when I have gotten me honour over Pharaoh, over his chariots and over his horsemen.
19 Malaika wa Mungu, aliyeenda mbele ya Waisraeli, aliama na kwenda nyuma yao. Nguzo ya wingu ili sogea mbele yao na kwenda kusimama nyumba yao.
And the messenger of God who was going on before the camp of Israel removed, and came on behind them, —and the pillar of cloud removed from before them, and stood behind them;
20 Wingu lilikuja katikati ya kambi ya Misri na kambi ya Israeli. Lilikuwa wingu jeusi kwa Wamisri, lakini liliangaza usiku kwa ajili ya Waisraeli, hivyo upande mmoja haukuweza kuja karibu ya mwingine usiku wote.
so it came in between the camp of the Egyptians and the camp of Israel, so it became a cloud and darkness, and yet lighted up the night, —so that the one came not near unto the other, all the night.
21 Musa akanyoosha mkono wake kuelekea bahari. Yahweh akasogeza bahari nyuma kwa upepo mkali wa mashariki usiku huo wote na kufanya bahari nchi kavu. Kwa namna hii maji yaligawanyika.
And Moses stretched forth his hand over the sea, and Yahweh carried away the sea by a mighty east wind all the night, and turned the sea into dry land, —and the waters were cloven asunder.
22 Waisraeli walienda katikati ya bahari kwa nchi kavu. Maji yaliunda ukuta mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto.
Then went the sons of Israel into the midst of the sea on the dry ground, —and, the waters, to them, were a wall, on their right hand and on their left.
23 Wamisri waka wafukuzia. Wali wafuata hadi katikati ya bahari - farasi wote wa Farao, magari ya farasi, na wapanda farasi.
And the Egyptians pursued, and entered after them—all the horses of Pharaoh his chariots and his horsemen, —into the midst of the sea.
24 Lakini masaa ya mapema ya asubui, Yahweh alitazama chini jeshi la Wamisri kupitia nguzo ya moto na wingu. Alisababisha hofu miongoni mwa Wamisri.
And it came to pass in the morning watch, that Yahweh looked down into the camp of the Egyptians, through the pillar of fire and cloud, and confused the camp of the Egyptians;
25 Magari yao ya farasi yalikuwa yana kwama matairi, na wapanda farasi waliendesha kwa ugumu. Hivyo Wamisri walisema, “Acha tuwakimbie Waisraeli, kwa kuwa Yahweh anawapigania dhidi yetu.”
and he took off the wheels of their chariots, and made them drive heavily, —so that the Egyptians said—We must flee from the face of Israel, for Yahweh, is fighting for them against the Egyptians.
26 Yahweh akamwambia Musa, “Nyoosha mkono kuelekea bahari ili maji yawarudie Wamisri, magari yao ya farasi, na wapanda farasi wao.”
Then said Yahweh unto Moses, Stretch forth thy hand over the sea, —that the waters may return upon the Egyptians, upon their chariots, and upon their horsemen.
27 Hivyo Musa akanyoosha mkono wake kuelekea bahari, na ikarudi kwenye hali yake ya kawaida palipo pambazuka. Wamisri walikimbilia ndani ya bahari, na Yahweh akawaingiza Wamisri katikati ndani yake.
So Moses stretched forth his hand over the sea and the sea returned, towards morning, to its steady flow, when the Egyptians, were fleeing to meet it, —thus Yahweh shook off the Egyptians into the midst of the sea;
28 Maji yakarudi na kufunika magari ya farasi ya Farao, wapanda farasi, na jeshi lake lote lililo fuata magari ya farasi kwenye bahari. Hakuna aliyepona.
thus the waters returned and covered the chariots, and the horsemen, even all the forces of Pharaoh that were entering after them into the sea, —there was not left remaining among them so much as one.
29 Walakini, Waisraeli walitembea kwenye nchi kavu katikati ya bahari. Maji yalikuwa ukuta kwao mkono wa kulia na mkono wa kushoto.
But the sons of Israel, had gone their way on dry ground in the saidst of the sea, —and the waters had been to them a wall, on their right hand and on their left.
30 Hivyo Yahweh akaokoa Israeli hiyo siku kutoka mkono wa Wamisri, na Israeli ikaona maiti za Wamisri ufukweni.
Thus did Yahweh, on that day, save Israel, out of the hand of the Egyptians, —and Israel saw the Egyptians, dead on the shore of the sea.
31 Israeli ilipoona nguvu kubwa Yahweh aliyo itumia dhidi ya Wamisri, watu walimsifu Yahweh, na kumwamini Yahweh na mtumishi wake Musa.
And when Israel saw the mighty hand wherewith Yahweh had wrought against the Egyptians, then did the people revere Yahweh, —and they put their trust in Yahweh, and in Moses, his servant.

< Kutoka 14 >