< Kutoka 12 >
1 Yahweh akasema na Musa na Aruni katika nchi ya Misri. Alisema,
Yahvé parla à Moïse et à Aaron au pays d'Égypte, et dit:
2 “Kwako wewe, mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi, mwezi wa kwanza wa mwaka kwako.
« Ce mois-ci sera pour vous le commencement des mois. Il sera pour vous le premier mois de l'année.
3 Liambie kusanyiko la Israeli, 'Siku ya kumi mwezi huu kila mtu lazima achukuwe mwana kondoo au mbuzi mdogo wa kwake, kila familia ifanye hivi, mwana kondoo kwa kila nyumba.
Parle à toute l'assemblée d'Israël, et dis: Le dixième jour de ce mois, on prendra chacun un agneau, selon les maisons de ses pères, un agneau par maison;
4 Kama hiyo nyumba ni ndogo sana kwa mwana kondoo, mwanaume na jirani yake wachukuwe mwana kondoo au nyama ya mbuzi mdogo ambayo itatosha watu. Lazima iwe yatosha kwa kila mtu kula, kwaiyo lazima wachukuwe nyama ya kutosha kulisha wote.
et si la maison est trop petite pour un agneau, lui et son voisin de maison en prendront un selon le nombre des âmes. Tu feras ton compte pour l'agneau en fonction de ce que chacun pourra manger.
5 Mwana kondoo wako au mbuzi wako mdogo lazima asiwe na upungufu, dume mwenye mwaka mmoja. Unaweza kuchukuwa mmoja wa kondoo au mbuzi.
Ton agneau sera sans défaut, un mâle d'un an. Tu le prendras parmi les brebis ou parmi les chèvres.
6 Lazima umtunze mpaka siku ya kumi na nne ya huo mwezi. Kisha kusanyiko lote la Israeli lazima liwaue hawa wanyama jioni.
Tu le garderas jusqu'au quatorzième jour du même mois, et toute l'assemblée de la communauté d'Israël l'immolera le soir.
7 Lazima uchukuwe baadhi ya damu na uweke kwenye sehemu mbili za mihimili ya milango na juu ya fremu za milango ambapo utalia hizo nyama.
Ils prendront du sang et en mettront sur les deux montants de la porte et sur le linteau, dans les maisons où ils le mangeront.
8 Lazima ule hizo nyama usiku, baada ya kuchoma kwenye moto. Kula na mkate ulio andaliwa kwa hamira, pamoja na mimea michungu.
Cette nuit-là, ils mangeront la viande rôtie au feu, avec des pains sans levain. Ils la mangeront avec des herbes amères.
9 Usiile mbichi au imechemshwa kwenye maji. Badala yake, choma kwenye moto na kichwa chake, miguu na sehemu za ndani.
Vous ne la mangerez pas crue, ni bouillie à l'eau, mais rôtie au feu, avec sa tête, ses pattes et ses entrailles.
10 Usiache ata kidogo kubaki mpaka asubui. Lazima uchome chochote kilicho baki asubui.
Vous n'en laisserez rien jusqu'au matin; mais ce qui en restera jusqu'au matin, vous le brûlerez au feu.
11 Hivi ndivyo wa paswa kula: ukiwa umefunga mkanda wako, umevaa viatu vyako, na gongo lako mkononi mwako. Lazima ule kwa haraka. Ni Pasaka ya Yahweh.
Voici comment vous le mangerez: votre ceinture à la taille, vos sandales aux pieds et votre bâton à la main, et vous le mangerez en hâte: c'est la Pâque de l'Éternel.
12 Yahweh anasema hili: Nitaenda katika nchi ya Misri usiku na kushambulia wazaliwa wote wa kwanza wa wanadamu na wanyama katika nchi ya Misri. Nitaleta pigo kwa miungu yote ya Misri. Mimi ni Yahweh.
Car cette nuit-là, je traverserai le pays d'Égypte et je frapperai tous les premiers-nés du pays d'Égypte, hommes et animaux. J'exécuterai des jugements contre tous les dieux d'Égypte. Je suis Yahvé.
13 Damu itakuwa ishara kwenye nyumba zenu ya kuja kwangu. Nitakapo ona damu, nitapita nitakapo shambulia nchi ya Misri. Ili pigo halitawajia na kuwaharibu.
Le sang sera pour vous un signe sur les maisons où vous serez. Quand je verrai le sang, je passerai au-dessus de vous, et il n'y aura sur vous aucune plaie qui vous détruise, quand je frapperai le pays d'Égypte.
14 Hii siku itakuwa kumbukumbu kwenu, ambayo lazima muadhimishe kama sherehe ya Yahweh. Itakuwa sheria kwenu pia, kwenye vizazi vyote vya watu wenu, ambayo mwapaswa kuadhimisha leo.
Ce jour sera pour vous un mémorial. Vous le célébrerez comme une fête en l'honneur de Yahvé. Vous le célébrerez comme une fête de génération en génération, par une ordonnance perpétuelle.
15 Utakula mkate bila hamira wakati wa siku saba. Siku ya kwanza utaondoa hamira kwenye nyumba zenu. Yeyote atakaye kula mkate uliyotiwa chachu kwanzia siku ya kwanza mpaka siku ya saba, huyo mtu lazima akatwe kutoka Israeli.
"'Pendant sept jours, vous mangerez des pains sans levain; le premier jour, vous ôterez le levain de vos maisons; car quiconque mangera du pain levé, du premier au septième jour, sera retranché d'Israël.
16 Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko lililo tengwa kwa ajili yangu, na siku ya saba kutakuwa na kusanyiko kama hilo. Hakuna kazi itakayo fanywa hizi siku, zaidi ya kupika kila mmoja ale. Hiyo ndio kazi pekee itakayo fanywa na wewe.
Le premier jour, il y aura pour vous une convocation sainte, et le septième jour, une convocation sainte; on n'y fera aucune espèce de travail, si ce n'est ce que chacun doit manger, et seulement ce qui peut être fait par vous.
17 Lazima uadhimishe hii Sherehe ya Mkate Usiotiwa Chachu kwasababu ni siku hii ambayo nitawaleta watu wako, makundi yaliyo na silaha, kwa makundi yaliyo na silaha, kutoka nchi ya Misri. Lazima uadhimishe hii siku kwa vizazi vyote vya watu wako. Hii itakuwa sheria kwako.
Vous observerez la fête des pains sans levain, car c'est en ce jour que j'ai fait sortir vos armées du pays d'Égypte. C'est pourquoi vous observerez ce jour, de génération en génération, comme une ordonnance perpétuelle.
18 Lazima ule mkate usiotiwa chachu kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza wa mwaka, mpaka jioni ya siku ya ishirini na moja ya mwezi.
Le premier mois, le quatorzième jour du mois, au soir, vous mangerez des pains sans levain, jusqu'au vingt et unième jour du mois, au soir.
19 Wakati wa hizi siku, nyumbani mwenu kusipatikane na hamira. Yeyote atakaye kula mkate ulio andaliwa na hamira lazima akatwe kutoka jamii ya Israeli, huyo mtu awe ni mgeni au mtu aliye zaliwa nchini mwenu.
Il ne se trouvera pas de levure dans vos maisons pendant sept jours, car quiconque mangera du pain levé sera retranché de l'assemblée d'Israël, qu'il soit étranger ou né dans le pays.
20 Hautakula chochote kilicho andaliwa na hamira. Popote utapo ishi, lazima ule mkate usio na hamira.”'
Vous ne mangerez rien de levé. Dans toutes vos habitations, vous mangerez des pains sans levain.'"
21 Kisha Musa akawaita viongozi wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni na mchague mwana kondoo au mbuzi watakao tosha kulisha familia zenu na muue mwana kondoo wa pasaka.
Moïse appela tous les anciens d'Israël, et leur dit: « Sortez, prenez des agneaux selon vos familles, et immolez la Pâque.
22 Kisha chukua jani la hisopu na uchovye kwenye damu itakayo kuwa kwenye beseni. Paka damu iliyo kwenye beseni juu ya fremu ya mlango na kwenye mihimili miwili ya mlango. Hakuna ata mmoja atakaye toka nje ya mlango wake mpaka asubui.
Vous prendrez un bouquet d'hysope, vous le tremperez dans le sang qui sera dans le bassin, et vous frapperez le linteau et les deux montants de la porte avec le sang qui sera dans le bassin. Aucun de vous ne sortira par la porte de sa maison jusqu'au matin.
23 Kwa kuwa Yahweh atapita kushambulia Wamisri. Atakapo ona damu juu ya fremu ya mlango na kwenye mihimili miwili ya mlango, atapita mlango wako na ata ruhusu mharibifu kuja nyumbani kwenu kuwashambulia.
Car l'Éternel passera pour frapper les Égyptiens; et quand il verra le sang sur le linteau et sur les deux montants de la porte, l'Éternel passera par-dessus la porte et ne permettra pas au destructeur d'entrer dans vos maisons pour vous frapper.
24 Lazima uadhimishe hili tukio. Hili litakuwa daima sheria kwako na kwa uzao wenu.
Tu observeras cette chose comme une ordonnance pour toi et pour tes fils, à perpétuité.
25 Utakapo ingia nchi Yahweh atakayo kupa, kama alivyo ahidi kufanya, lazima uadhimishe hili tendo la ibada.
Lorsque vous serez arrivés dans le pays que l'Éternel vous donnera, comme il l'a promis, vous observerez ce service.
26 Watoto wako watakapo kuuliza, 'Hili tendo la ibada lina maana gani?'
Lorsque vos enfants vous demanderont: « Que signifie ce service? »,
27 kisha lazima useme, 'Ni sadaka ya Pasaka ya Yahweh, kwasababu Yahweh kapita nyumba za Waisraeli Misri alipo washambulia Wamisri. Aliweka nyumba zetu huru.”' Kisha watu wakamsujudia Yahweh.
vous répondrez: « C'est le sacrifice de la Pâque de l'Éternel, qui a passé au-dessus des maisons des enfants d'Israël en Égypte, lorsqu'il a frappé les Égyptiens et épargné nos maisons ». Le peuple s'inclina et se prosterna.
28 Waisraeli wakaenda na kufanya kama Yahweh alivyo waamuru Musa na Aruni.
Les enfants d'Israël allèrent et firent ainsi; ils firent ce que Yahvé avait ordonné à Moïse et à Aaron.
29 Ikawa usiku wa manane kuwa Yahweh akawashambulia wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, aliye keti kiti chake cha enzi, mzaliwa wa kwanza wa mtu aliye gerezani na wazaliwa wote wa kwanza wa mifugo.
A minuit, Yahvé frappa tous les premiers-nés du pays d'Egypte, depuis le premier-né de Pharaon assis sur son trône jusqu'au premier-né du captif qui était dans le cachot, et tous les premiers-nés du bétail.
30 Farao akaamka usiku - yeye, watumishi wake, na Wamisri. Palikuwa na kelele za maombolezo Misri, kwa kuwa hakukuwa na nyumba ambayo hamna mtu hakufa.
Pharaon se leva la nuit, lui, tous ses serviteurs et tous les Égyptiens. Il y eut un grand cri en Égypte, car il n'y avait pas une maison où il n'y eût un mort.
31 Farao akamuita Musa na Aruni usiku na kusema, “Inuka, tokeni miongoni mwa watu wangu, nyie pamoja na Waisraeli. Nenda, mmuabudu Yahweh, kama mlivyo sema mnataka kufanya.
Il appela de nuit Moïse et Aaron, et dit: « Lève-toi, sors du milieu de mon peuple, toi et les enfants d'Israël, et va servir Yahvé, comme tu l'as dit!
32 Chukuweni ng'ombe zenu na kondoo zenu, kama mlivyo sema, na muende, na pia mnibariki.”
Prenez vos troupeaux et vos bêtes, comme vous l'avez dit, et partez; et bénissez-moi aussi! ».
33 Wamisri walikuwa na haraka ya kuwa ondoa nchini, kwa kuwa walisema, “Sisi ni watu tuliokufa.”
Les Égyptiens étaient pressés par le peuple, pour l'expulser du pays en toute hâte, car ils disaient: « Nous sommes tous des hommes morts. »
34 Watu wakachukuwa ngano yao pasipo kuongeza hamira yeyote. Bakuli zao zakukandia ngano zilifungiwa kwenye nguo zao na kwenye mabega yao.
Le peuple prit sa pâte avant qu'elle ne soit levée, ses pétrins étant liés dans leurs vêtements sur leurs épaules.
35 Watu Waisraeli walifanya kama Musa alivyo waambia. Waliwaomba Wamisri vitu vya fedha, vitu vya dhahabu, na nguo.
Les enfants d'Israël agirent selon la parole de Moïse; ils demandèrent aux Égyptiens des bijoux d'argent, des bijoux d'or et des vêtements.
36 Yahweh aliwafanya Wamisri na shauku ya kuwapendeza Waisraeli. Hivyo Wamisri waliwapa chochote walicho waomba. Katika hili, Waisraeli waliwachukulia vingi Wamisri.
L'Éternel accorda au peuple la faveur des Égyptiens, qui leur donnèrent ce qu'ils demandaient. Ils pillèrent les Égyptiens.
37 Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesi kwenda Sakothi. Walikuwa na idadi ya wanaume 600, 000 kwa miguu, kuongezea kwa wanawake na watoto.
Les enfants d'Israël firent le voyage de Ramsès à Succoth, environ six cent mille hommes à pied, sans compter les enfants.
38 Mchanganyiko wa kundi la wasio Waisraeli pia walienda nao, pamoja na ng'ombe na kondoo, idadi kumbwa ya mifugo.
Une multitude hétéroclite montait aussi avec eux, avec des troupeaux, des bœufs et même beaucoup de bétail.
39 Walioka mikate na unga wa ngano wenye hamira walio utoa Misri. Ulikuwa hauna hamira kwasababu waliondolewa Misri na hawakuweza chelewa kuandaa chakula.
Ils cuisaient des gâteaux sans levain avec la pâte qu'ils avaient apportée d'Égypte, car elle n'était pas levée, parce qu'ils avaient été poussés hors d'Égypte, qu'ils ne pouvaient pas attendre et qu'ils n'avaient pas préparé de nourriture pour eux.
40 Waisraeli waliishi Misri kwa miaka 430.
Or, le temps que les enfants d'Israël vécurent en Égypte fut de quatre cent trente ans.
41 Baada ya miaka 430, siku hiyo hiyo, majeshi yote ya Yahweh yalio jiami waliondoka kutoka nchi ya Misri.
Au bout de quatre cent trente ans, jour pour jour, toutes les armées de Yahvé sortirent du pays d'Égypte.
42 Huu ulikuwa usiku wakuwa macho, ili Yahweh awatoe kutoka nchi ya Misri. Huu ulikuwa usiku wa Yahweh wa kuadhimishwa na Waisraeli wote na watu wa vizazi vyao vyote.
C'est une nuit à laquelle on rend hommage à l'Éternel pour les avoir fait sortir du pays d'Égypte. C'est la nuit de Yahvé, que tous les enfants d'Israël observeront de génération en génération.
43 Yahweh akamwambia Musa na Aruni, “Hii ni sheria ya Pasaka: hakuna mgeni anaye ruhusiwa kuila.
Yahvé dit à Moïse et à Aaron: « Voici l'ordonnance de la Pâque. Aucun étranger n'en mangera,
44 Walakini, kila mtumwa wa Misraeli, aliye nunuliwa kwa pesa, anaeza kula baada ya kutahiriwa.
mais le serviteur acheté à prix d'argent, quand vous l'aurez circoncis, en mangera.
45 Wageni na watumishi waajiriwa hawapaswi kula chakula chochote.
L'étranger et le mercenaire n'en mangeront pas.
46 Chakula chapaswa kuliwa ndani ya nyumba moja. Hauruhusiwi kubeba nyama yeyote nje ya nyumba, na hauruhusiwi kuvunja mfumba wowote.
La viande doit être mangée dans une seule maison. Tu ne porteras pas de viande en dehors de la maison. Vous ne briserez aucun de ses os.
47 Jamii zote za Israeli za paswa kuadhimisha sherehe.
Toute la congrégation d'Israël l'observera.
48 Kama mgeni anaishi na wewe na anataka kuadhimisha Pasaka kwa Yahweh, ndugu zake wote wa kiume wapaswa kutahiriwa. Kisha anaeza kuja na kuadhimisha. Atakuwa kama watu walio zaliwa kwenye nchi. Walakini, hakuna mtu asiye tahiriwa anaruhusiwa kula chakula chochote.
Lorsqu'un étranger habitera chez vous en tant qu'étranger et qu'il voudra célébrer la Pâque en l'honneur de l'Éternel, que tous ses mâles soient circoncis, puis qu'il s'approche et la célèbre. Il sera comme celui qui est né dans le pays, mais aucun incirconcis n'en mangera.
49 Sheria hii hii itahusika kwa mzaliwa wa asili na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
Une seule loi s'appliquera à celui qui est né dans le pays, et à l'étranger qui vit au milieu de vous comme un étranger. »
50 Waisraeli wote walifanya kama Yahweh alivyo waamuru Musa na Aruni.
Tous les enfants d'Israël firent ainsi. Ils firent ce que Yahvé avait ordonné à Moïse et à Aaron.
51 Ikaja kuwa siku hiyo Yahweh akawaleta Israeli kutoka nchi ya Misri kwa makundi yalio jiami.
Ce même jour, Yahvé fit sortir les enfants d'Israël du pays d'Égypte par leurs armées.