< Kutoka 11 >

1 Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Bado kuna pigo moja nitalo lileta kwa Farao na Misri. Baada ya hilo, atakuacha uondoke hapa. Atakapo kuachia uende, ata kuondoa kabisa.
And Jehovah saith unto Moses, 'One plague more I do bring in on Pharaoh, and on Egypt, afterwards he doth send you away from this; when he is sending you away, he surely casteth you out altogether from this [place];
2 Waelekeze watu kwamba kila mwanaume na mwanamke amuulizie jirani yake vitu vya fedha na vitu vya dhahabu.”
speak, I pray thee, in the ears of the people, and they ask — each man from his neighbour, and each woman from her neighbour, vessels of silver, and vessels of gold.'
3 Sasa Yahweh aliwafanya Wamisri kuwa na shauku ya kuwapendeza Waisraeli. Aidha, Musa alikuwa wakuvutia sana machoni pa watumishi wa Farao na watu wa Misri.
And Jehovah giveth the grace of the people in the eyes of the Egyptians; also the man Moses [is] very great in the land of Egypt, in the eyes of the servants of Pharaoh, and in the eyes of the people.
4 Musa akasema, “Yahweh asema hivi: 'Wakati wa usiku wa manane nitaenda Misri yote.
And Moses saith, 'Thus said Jehovah, About midnight I am going out into the midst of Egypt,
5 Wazaliwa wa kwanza wote wa nchi ya Misri watakufa, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, anaye keti kiti chake cha enzi, mpaka mzaliwa wa kwanza wa misichana mtumwa anaye saga mbegu, na kwa wazaliwa wa kwanza wa mifugo.
and every first-born in the land of Egypt hath died, from the first-born of Pharaoh who is sitting on his throne, unto the first-born of the maid-servant who [is] behind the millstones, and all the first-born of beasts;
6 Kisha kutakuwa na kilio kikubwa nchi yote ya Misri, kama ambacho hakijawai wala hakitatokea tena.
and there hath been a great cry in all the land of Egypt, such as there hath not been, and such as there is not again.
7 Lakini ata mbwa hata bweka kwa watu wa Israeli, dhidi ya mtu au mnyama. Kwa hili utajuwa kuwa nina watendea Wamisri na Waisraeli tofauti.'
'And against all the sons of Israel a dog sharpeneth not its tongue, from man even unto beast, so that ye know that Jehovah doth make a separation between the Egyptians and Israel;
8 Watumishi wote hawa wako, Farao, watakuja chini yangu na kunisujudu mimi. Watasema, 'Nenda, wewe na watu wote wanao kufuata!' Baada ya hapo nitaondoka.” Kisha akaondoka mbele ya Farao kwa hasira kubwa.
and all these thy servants have come down unto me, and bowed themselves to me, saying, Go out, thou and all the people who [are] at thy feet; and afterwards I do go out;' — and he goeth out from Pharaoh in the heat of anger.
9 Yahweh akamwambia Musa, Farao hatakusikiliza. Hii ni ili nifanye mambo ya ajabu katika nchi ya Misri.”
And Jehovah saith unto Moses, 'Pharaoh doth not hearken unto you, so as to multiply My wonders in the land of Egypt;'
10 Musa na Aruni wakafanya mambo haya ya kushangaza mbele za Farao. Lakini Yahweh aliufanya moyo wa Farao mgumu, na Farao hakuwaacha watu wa Israeli kuondoka katika nchi yake.
and Moses and Aaron have done all these wonders before Pharaoh, and Jehovah strengtheneth Pharaoh's heart, and he hath not sent the sons of Israel out of his land.

< Kutoka 11 >