< Kutoka 10 >

1 Yahweh akamwambia Musa, “Nenda kwa Farao, kwa kuwa nimeufanya moyo wake mgumu na moyo wa watumishi wake. Nimefanya hivi kuonyesha hizi ishara za nguvu zangu miongoni mwao.
The Lord told Moses, “Go and see Pharaoh, because it was me who gave him and his officials a stubborn attitude so that I may perform my miracles before them.
2 Pia nimefanya hivi ili muwaambie watoto wenu na wajukuu wenu vitu nilivyo fanya, jinsi nilivyo itendea Misri kwa ukali, na jinsi nilivyo onyesha aina tofauti za ishara za nguvu zangu miongoni mwao. Kwa hili mtajua kuwa mimi ni Yahweh.”
This is so you can tell your children and grandchildren how I made the Egyptians look foolish by doing these miracles among them, and so that you may know that I am the Lord.”
3 Hivyo Musa na Aruni wakaenda kwa Farao na kumwambia, “Yahweh, Mungu wa Waebrania, anasema hivi: 'Kwa muda gani utaendelea kukataa kujinyenyekesha mbele zangu? Acha watu wangu waenda ili wakaniabudu.
Moses and Aaron went to Pharaoh and told him, “This is what the Lord, the God of the Hebrews, says: ‘How long are you going to refuse to humble yourself before me? Let my people go, so that they can worship me.
4 Lakini ukikataa kuwaruhusu watu wangu kwenda, sikiliza, kesho nitaleta nzige kwenye nchi yako.
If you refuse to let my people leave, tomorrow I will send a plague of locusts into your country.
5 Watafunika ardhi ya juu ili kwamba mtu asiweze kuona udongo. Watakula mabaki yote yalio salia kwenye mvua ya barafu ya mawe. Pia watakula kila mti unaokua shambani.
There will be so many of them that they'll cover the ground so no one can see it. They will eat whatever crops were left by the hail, as well as every tree growing in your fields.
6 Watajaza nyumba zenu, zote za watumishi wenu, na zote za Wamisri wote - jambo ambalo baba zenu wala mababu zenu hawakuwai kuona, jambo ambalo halikuwai shuhudiwa toka walipo kuwa duniani hadi leo.”' Kisha Musa akaondoka na kutoka kwa Farao.
They will swarm into your houses and into the houses of all your officials—in fact into the houses of every Egyptian. This is something that none of your forefathers ever saw from the time they arrived in this country.’” Then Moses and Aaron turned and left Pharaoh.
7 Watumishi wa Farao wakamwambia, “Mpaka lini huyu mwanaume ata kuwa msumbufu kwetu? Acha Waisraeli waende wakamuabudu Yahweh Mungu wao. Bado haujatambua kuwa Misri imeharibiwa?”
Pharaoh's officials came to him and asked, “How long are you going to let this man cause us trouble? Let these people go so they can worship the Lord their God. Don't you realize that Egypt has been destroyed?”
8 Musa na Aruni wakaletwa tena kwa Farao, ambaye aliwaambia, “Nendeni amkamuabudu Yahweh Mungu wenu. Lakini watu gani wataenda?”
Moses and Aaron were brought back to see Pharaoh. “Go and worship the Lord your God,” he told them. “But who of you will be going?”
9 Musa akasema, “Tutaondoka na wadogo wetu na wakubwa wetu, pamoja na wana wetu na mabinti zetu. Tutaondoka na ng'ombe na kondoo zetu, maana lazima tufanye siku kuu ya Yahweh.”
“We will all go,” Moses replied. “Young and old, sons and daughters—and we'll take our flocks and herds with us, for we're going to have a religious festival for the Lord.”
10 Farao akawaambia, “Yahweh kwa kweli awe nanyi, kama nitawaacha muende na wadogo zenu waende. Angalia, una uovu kwenye nia.
“The Lord really would have to be with you if I let your children go with you!” Pharaoh answered. “Clearly you're planning some kind of evil trick!
11 Hapana! Nenda, wanaume tu miongoni mwenu, na mmuabudu Yahweh, kwa kuwa hilo ndilo mnalo litaka.” Kisha Musa na Aruni wakaondolewa uweponi mwa Farao.
So no! Only the men can go and worship the Lord, because that's what you've been asking for.” Then he had Moses and Aaron thrown out.
12 Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Nyoosha mkono wako kwenye nchi ya Misri palipo na nzige, ili washambulie nchi ya Misri na kula kila mmea, kila kitu barua ya mawe iliyo acha.”
The Lord told Moses, “Lift up your hand over Egypt, so that the locusts may swarm over it and eat every plant in the country—everything that was left by the hail.”
13 Musa akanyoosha na gongo lake juu ya nchi ya Misri, na Yahweh akaleta upepo wa mashariki juu ya nchi mchana wote na usiku mzima. Palipo kuwa asubui, upepo wa mashariki ulileta nzige.
Moses held out his staff over Egypt, and all through that day and night the Lord sent an east wind blowing over the land. By the time morning came the east wind had brought in the locusts.
14 Nzige wakaenda nchi yote ya Misri na kuharibu sehemu zote. Hapajawai kuwa na kundi kama hilo la nzige juu ya nchi, hakuna kama tena kama hilo litawai kutokea.
The locusts swarmed across the land and settled in every part of the country. There had never been such a swarm of locusts ever before, and there won't be ever again.
15 Walifunika ardhi yote ya juu ikawa giza. Walikula kila mmea na kila tunda la miti ambayo barafu ya mawe ilibakiza. Kila eneo la nchi ya Misri, hakuna mmea wa kijani ulibaki, wala mti au mmea wa shambani.
They covered the ground until it looked black, and they ate up all the plants in the fields and all the fruit on the trees that had been left by the hail. Not a single green leaf was left on any tree or plant anywhere in Egypt.
16 Kisha Farao akawaita Musa na Aruni na kuwaambia, “Nimefanya dhambi dhidi ya Yahweh na dhidi yako.
Pharaoh called urgently for Moses and Aaron and said, “I have sinned against the Lord your God and against you.
17 Kisha sasa, nisamehe dhambi yangu wakati huu, na uombe kwa Yahweh Mungu wako aondoe hichi kifo kwangu.”
So please forgive my sin just this one time and plead with the Lord your God, asking him to at least take away this deathly plague from me.”
18 Musa akaondoka kwa Farao na kumuomba Yahweh.
Moses left Pharaoh and prayed to the Lord.
19 Yahweh akaleta upepo mkali wa magharibi ulio wachukuwa wale nzige na kuwapeleka Bahari ya Shamu; hakuna nzige ata mmoja aliye baki eneo la Misri.
The Lord changed the direction of the wind so that a strong westerly wind blew the locusts into the Red Sea. There wasn't a single locust left anywhere in Egypt.
20 Lakini Yahweh aliufanya moyo wa Farao mgumu, na Farao hakuacha Waisraeli waende.
But the Lord made Pharaoh stubborn, and he would not let the Israelites go.
21 Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Nyoosha mkono wako kuelekea mbingu, ili kuwe na giza nchi yote ya Misri, giza linalo weza kuhisiwa.”
The Lord told Moses, “Lift your hand toward the sky so that darkness will fall over Egypt, darkness so thick that it can be felt.”
22 Musa akanyoosha mkono wake kuelekea mbingu, na kulikuwa na giza nene nchi yote ya Misri kwa siku tatu.
Moses lifted up his hand toward heaven, and the whole of Egypt went completely dark for three days.
23 Hakuna aliye muona mwingine; hakuna aliye toka nyumbani mwake kwa siku tatu. Walakini, Waisraeli wote walikuwa na taa katika sehemu walizo ishi.
No one could see anyone else, and no one moved from where they were for three days. But there was still light where all the Israelites lived.
24 Farao alimuita Musa na kusema, “Nenda umuabudu Yahweh. Ata familia zenu za weza kwenda nanyie, lakini ng'ombe zenu na kondoo zenu zitabaki.”
Eventually Pharaoh called for Moses. “Go and worship the Lord,” he said. “Just leave your flocks and herds here. You can even take your children with you.”
25 Lakini Musa akasema, “Lazima utupe wanyama kwa ajili ya dhabihu na sadaka za kuteketeza ili tuwatoe dhabihu kwa Yahweh Mungu wetu.
But Moses replied, “You must also let us have animals for sacrifices and burnt offerings, so we can offer them to the Lord our God.
26 Mifugo yetu lazima iende na sisi; ata mmoja hawezi kubaki, lazima tuwapeleke wakamuabudu Yahweh Mungu wetu. Kwa kuwa hatujui tutakacho muabudu nacho Yahweh mpaka tufike pale.
Our livestock have to go with us too—not a single animal will be left behind. We'll need some of them to worship the Lord our God, and we won't know how we are to worship the Lord until we get there.”
27 Lakini Yahweh aliufanya moyo wa Farao mgumu, na hakuwaacha waende.
But the Lord made Pharaoh stubborn, and he would not let them go.
28 Farao alimwambia Musa, “Toka kwangu! Kuwa muangalifu na jambo moja, kwamba usinione tena, kwa kuwa siku utakapo uona uso wangu, utakufa.”
Pharaoh shouted at Moses, “Get out of here! I don't want to see you ever again! If I ever do see you again you'll die!”
29 Musa akasema, “Wewe mwenyewe umesema. Sitauona uso wako tena.”
“May it be as you say,” Moses replied. “I won't see you again.”

< Kutoka 10 >