< Esta 9 >
1 Sasa katika mwezi wa kumi na mbili, siku ya kumi na tatu ambayo ni siku ya Adari, siku ambayo adui wa Wayahudi walitarajia kutekeleza sheria ya mfalme na kupata nguvu dhidi ya Wayahudi. Badala yake Wayahudi wakapata nguvu dhidi ya adui zao.
And in the twelfth month, that is, the month Adar, on the thirteenth day thereof, when the king's commandment and his decree drew near to be put in execution, in the day that the enemies of the Jews hoped to have power over them (but it was turned to the contrary, that the Jews had power over them that hated them),
2 Wayahudi wote wakakusanyika katika miji yao katika majimbo yote ya Mfalme Ahusiero, kutia mikono juu ya wale waliokusudia ubaya. Hakuna aliye kuwa tayari kusimama zao kwa sababu hofu yao ilikuwa imewaangukia watu wote.
the Jews gathered themselves together in their cities throughout the provinces of king Ahasuerus, to lay hand on such as sought their hurt. And no man could withstand them; for the fear of them had fallen upon all the peoples.
3 Wakuu wote wa majimbo, maakida na magavana, na watawala wa mfalme, waliwasaidia Wayahudi kwa kuwa hofu ya Modekai ilikuwa imewaangukia.
And all the princes of the provinces, and the satraps, and the governors and officers of the king, helped the Jews; for the fear of Mordecai had fallen upon them.
4 Kwa kuwa Modekai alikuwa mkuu katika nyumba ya mfalme, na umaarufu wake ukasambaa katika majimbo yote, kwa kuwa Modekai alikuwa akifanyika mkuu.
For Mordecai was great in the king's house, and his fame went forth throughout the provinces; for the man Mordecai became continually greater.
5 Wayahudi wakawavamia maadi zao kwa upanga, wakiwatenda vibaya kama walivyokuwa wamekusudiwa mabaya dhidi yao Wakawatenda kama walivyo ona vyema machoni pao.
And the Jews smote all their enemies with the stroke of the sword and slaughter and destruction, and did what they would to those that hated them.
6 Katika ngome ya mji wa Shushani pekee jumla ya maadui waliouawa na na kuharibiwa na Wayahudi ni wanaume mia tano.
And in Shushan the fortress the Jews slew and destroyed five hundred men.
7 Miongoni mwa waliouawa ni pamoja na Parishandatha, Dalphoni, Aspatha,
And Parshandatha, and Dalphon, and Aspatha,
8 Poratha, Adalia, Aridatha,
and Poratha, and Adalia, and Aridatha,
9 Parimashita, Arisai, Aridai, Vaizatha,
and Parmashta, and Arisai, and Aridai, and Vajezatha,
10 na wana kumi wa Hamani, mwana wa Hammedatha, adui wa Wayahudi. Lakini hawakuchua mateka yoyote.
the ten sons of Haman the son of Hammedatha, the oppressor of the Jews, they slew; but they laid not their hands on the prey.
11 Idadi ya wale waliouawa siku hiyo katika mji wa Shushani, ilifikishwa kwa Mfalme Ahusiero.
On that day the number of those that were slain in Shushan the fortress was brought before the king.
12 Mfalme akamwambia malkia Esta. Mfalme akamwambia Malkia Esta, “Wayahudi wameua wanaume mia tano katika mji wa Shushani, wakiwemo wana kumi wa Hamani adui wa Wayahudi. Je wamefanya nini katika majimbo mengine? Na sasa haja yako ni nini? Utapewa. Ombi lako ni nini?”
And the king said to Esther the queen, The Jews have slain and destroyed five hundred men in Shushan the fortress, and the ten sons of Haman; what have they done in the rest of the king's provinces? And what is thy petition? and it shall be granted thee; and what is thy request further? and it shall be done.
13 Esta akamjibu, “Mfalme kama ikikupendeza, ruhusu Wayuadi walio katika mji wa Shushani wapige mbiu hii na kesho, na miili ya watoto wa Hamani itundikwe juu ya miti.”
And Esther said, If it please the king, let it be granted to the Jews that are in Shushan to do to-morrow also according to this day's decree, and let Haman's ten sons be hanged upon the gallows.
14 Mfalme akaamuru ombi la Esta litekelezwe. Mbiu ilipigwa katika mji wa Shushani, na wana kumi wa Hamani wakatundikwa juu ya miti.
And the king commanded it so to be done: and the decree was given at Shushan; and they hanged Haman's ten sons.
15 Wayahudi katika mji wa Shushani walisanyika pamoja siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, na kuwaua maadui zao mia tatu katika mji wa Shushani, lakini hawakugusa nyara zao.
And the Jews that were in Shushan gathered themselves together on the fourteenth day also of the month Adar, and slew three hundred men at Shushan; but they laid not their hand on the prey.
16 Na Wayahudi katika majimbo mengine wakakusanyika ili kujilinda na wakapata faraja kutoka kwa maadui na wakawaua maadui zao elfu sabini na tano, lakini hawakugusa mikono yao kwa vitu vya thamani wale waliouwawa.
And the other Jews that were in the king's provinces gathered themselves together, and stood for their life, and had rest from their enemies; and they slew of them that hated them seventy-five thousand (but they laid not their hand on the prey),
17 Katika siku ya kumi na tatu ya mwezi wa Adari, Wayahudi wakapumzika katika siku ya kumi na nne, wakapumzika siku hiyo ya karamu na furaha.
on the thirteenth day of the month Adar; and on the fourteenth of the same they rested, and made it a day of feasting and joy.
18 Lakini Wayahudi walioishi katika mji wa Shushani wakaja pamoja siku ya kumi na tatu na ya kumi na nne. Na siku ya kumi na tano wakapumzika na wafanya karamu na kufurahia.
But the Jews that were at Shushan gathered themselves together on the thirteenth [day] thereof, and on the fourteenth thereof; and on the fifteenth of the same they rested, and made it a day of feasting and joy.
19 Hii ndiyo sababu Wayahudi wa vijijini, wanaishi maeneo ya vijijini, huadhimisha siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari kama siku ya furaha na karamu na siku ambayo hutumiana zawadi kwa kila mmoja.
Therefore the Jews of the villages that dwell in the country towns make the fourteenth of the month Adar a day of joy and feasting, and a good day, and on which they send portions one to another.
20 Modekai akaweka mambo haya na akatuma nyaraka kwa Wayahudi wote waliokuwa katika utawala wa Mfalme Ahusiero,
And Mordecai wrote these things, and sent letters to all the Jews near and far that were in all the provinces of king Ahasuerus,
21 akiwataka kuazimisha siku ya kumi na nne na kumi na tano ya mwezi wa Adari kila mwaka.
to establish [this] among them, that they should keep the fourteenth day of the month Adar, and the fifteenth day of the same, yearly,
22 Hizi zilikuwa ndizo siku ambazo Wahudi walipata faraja kutoka kwa maadui zao na wakati huu ndio wakati ambao huzuni ya Wayahudi iligeuzwa kuwa furaha, na kutoka kwa maombolezo hadi kwenye pumziko. Walipaswa kuzifanya siku za karamu na furaha, na kutumiana zawadi ya chakula, na zawadi kwa masikini.
as the days on which the Jews rested from their enemies, and the month that was turned to them from sorrow to joy, and from mourning into a good day; that they should make them days of feasting and joy, and of sending portions one to another, and gifts to the poor.
23 Wayahudi wakaendelea na maadhimisho wakifanya kile ambacho Modekai alikuwa amewaandikia.
And the Jews undertook to do as they had begun, and as Mordecai had written to them.
24 Na wakati huo Modekai mwana wa Hammedatha mwagagi, adui wa Wayahudi aliyekuwa amepanga njama ya kuwaangamiza Wayahudi, na kwa kupiga Puri (yaani akapiga kura) ili kuwaangamiza kabisa.
For Haman the son of Hammedatha the Agagite, the oppressor of all the Jews, had devised against the Jews to destroy them, and had cast Pur, that is, the lot, to consume them and to destroy them;
25 Lakini Mfalme Ahusiero alipopata taarifa ya mpango mbaya huu alioupanga Modekai dhidi ya Wayahudi, aliagiza kwa nyaraka afanyiwe Modekai mwenyewe, na kwamba yeye na wana wake wanyongwe juu ya miti.
and when [Esther] came before the king, he commanded by letters that his wicked device, which he had devised against the Jews, should return upon his own head; and they hanged him and his sons on the gallows.
26 Hivyo Wayahudi wakaziita siku hizi Purimu, kutokana na jina Puri. Kwa sababu ya mambo yote yaliyo kuwa yameandika katika barua, na mambo yote ambayo walikuwa wameyaona kwa macho yao, na yale yalikuwa yamewapata,
Therefore they called these days Purim after the name of Pur. Therefore, according to all the words of this letter, and for what they had seen concerning this matter and what had happened to them,
27 Wayahudi wakapokea jukumu na desturi mpya. Desturi hii iwe kwa ajili yao, watoto wao, na kila ambaye aliyeungana nao. Na itakuwa kwamba maadhimisho haya watayafanya kwa kila mwaka. Wataadhimisha kwa namna fulani na nyakati hizo hizo kila mwaka.
the Jews ordained and took upon them, and upon their seed, and upon all such as joined themselves to them, so that it should not fail, that they would observe these two days according to their writing and according to their fixed time, every year;
28 Siku hizi zilipaswa kuadhimishwa katika kila kizazi, kila familia, kila jimbo na kwa kila mji. Wayahudi hawa na watoto wao hawakuacha kuadhimisha siku hizi za Purimu, ili kwamba wasizisahau.
and that these days should be remembered and observed throughout every generation, in every family, every province, and every city, and that these days of Purim should not fail from among the Jews, nor the memorial of them cease from among their seed.
29 Malkia Esta na Modekai wakaandika kwa mamlaka yote na kuthibitisha barua hii ya pili kuhusu Purimu.
And queen Esther the daughter of Abihail, and Mordecai the Jew, wrote with all authority to confirm this second letter of Purim.
30 Barua zilipelekwa katika majimbo 127 ya mfalme Ahusiero, zikiwatakia Wayahudi wote amani na kweli.
And he sent letters to all the Jews, to the hundred and twenty-seven provinces of the kingdom of Ahasuerus, words of peace and truth,
31 Na kuthibitisha siku za Purimu sawa sawa na maelekezo ya Modekai na Esta yaliyowataka Wayahudi waadhimishe. Wayahudi wakatii maagizo kwa ajili yao na uzao wao, kama walivyotii siku za kufunga na kuomboleza.
to confirm these days of Purim in their fixed times, according as Mordecai the Jew and queen Esther had enjoined them, and as they had decreed for themselves and for their seed, as to the matters of the fastings and their cry.
32 Agizo la Esta likahakikisha sheria hizi kuhusu Purimu, na ikaandikwa katika kitabu.
And the decree of Esther confirmed these matters of Purim; and it was written in the book.