< Esta 5 >

1 Baada ya siku tatu, Esta akajivika mavazi yake ya kimalkia na akasimama sehemu ya ndani ya ua wa ikulu ya mfalme, mbele ya nyumba ya mfalme. mfalme alikuwa ameketi katika kiti chake cha enzi na akitazama mlango wa kuingilia.
Le troisième jour, Esther mit ses vêtements royaux et se tint dans la cour intérieure de la maison du roi, à côté de la maison du roi. Le roi était assis sur son trône royal dans la maison royale, à côté de l'entrée de la maison.
2 Mfalme alipomwona malkia Esta alipata kibali kwa mfalme. Alimpa fimbo ya dhahabu mikononi mwa Esta. Hivyo Esta akamsogelea mfalme na kuishika fimbo ya utawala.
Lorsque le roi vit la reine Esther debout dans la cour, elle obtint grâce à ses yeux; et le roi tendit à Esther le sceptre d'or qui était dans sa main. Esther s'approcha et toucha le sommet du sceptre.
3 Kisha mfalme akamwambia Malkia Esta, “Unahitaji upewe nini? Ombi lako ni lipi? Hata nusu ya ufalme wangu utapewa.”
Alors le roi lui demanda: « Que veux-tu, reine Esther? Quelle est ta demande? Il te sera donné jusqu'à la moitié du royaume. »
4 Malkia Esta akamwambia mfalme, kama nimepata kibali machoni pako, naomba wewe na Hamani muhudhurie leo katika karamu niliyoiandaa kwa ajili yake.”
Esther dit: « Si le roi le trouve bon, que le roi et Haman viennent aujourd'hui au banquet que j'ai préparé pour lui. »
5 Mfalme akasema, “Mleteni haraka Hamani sawa sawa na matakwa ya Malkia Esta.” Mfalme pamoja na Hamani wakahuduria katika karamu aliyoandaa malkia Esta.
Alors le roi dit: « Amène vite Haman, afin qu'il soit fait comme Esther l'a dit. » Le roi et Haman arrivèrent donc au banquet qu'Esther avait préparé.
6 Mvinyo ulipohudumiwa katika karamu, mfalme akamuuliza Malkia Esta hitaji lako ni nini? Na ombi lako ni lipi? Utapewa hata nusu ya ufalme.”
Le roi dit à Esther, lors du banquet du vin: « Quelle est ta demande? Elle te sera accordée. Quelle est ta demande? Elle sera exécutée jusqu'à la moitié du royaume. »
7 Esta akajibu mfalme, “Hitaji na ombi langu ni hili,
Alors Esther répondit et dit: Voici ma requête et ma demande.
8 kama ikikupendeza mfalme, kwa kunipa haja yangu na kuheshimu ombi langu, wewe na Hamani muhudhurie tena katika karamu nitakayoiandaa kesho na hapo ndipo nitakapo kuambia haja yangu.
Si j'ai trouvé grâce aux yeux du roi, et s'il plaît au roi d'accéder à ma requête et d'exécuter ma demande, que le roi et Haman viennent au banquet que je leur préparerai, et je ferai demain ce que le roi a dit. »
9 Hamani akaenda nyumbani kwakwe huku akiwa amejawa na furaha moyoni mwake. Lakini alipomwona Modekai katika lango la mfalme, modekai hasimami wala kutetemeka mbele zake, alijawa na ghadhabu kwa ajili ya Modekai.
Haman sortit ce jour-là, joyeux et le cœur content. Mais quand Haman vit Mardochée à la porte du roi, qui ne se levait pas et ne bougeait pas pour lui, il fut rempli de colère contre Mardochée.
10 Lakini akajizuia na akaenda nyumbani kwake. Akawaarika marafiki zake wakakusanyika pamoja na Zereshi, mkewe.
Haman se retint néanmoins et rentra chez lui. Là, il fit appeler ses amis et Zéresh, sa femme.
11 Hamani akawaeleza juu ya utukufu wa mali na idadi ya watoto aliokuwa nao, na vile alivyo juu kuliko wasimamizi na watumishi wote wa mfalme.
Haman leur raconta la gloire de ses richesses, la multitude de ses enfants, toutes les choses dans lesquelles le roi l'avait promu, et comment il l'avait élevé au-dessus des princes et des serviteurs du roi.
12 Hamani akawambia, “Hata jana Malkia Esta aliandaa karamu kwa ajili ya mfalme na ni mimi tu na mfalme tulio hudhuria katika karamu aliyoiandaa Malkia Esta. Na hata kesho tuna mwaliko mwingine pamoja na mfalme.
Haman dit aussi: « Oui, la reine Esther n'a laissé entrer personne d'autre que moi au banquet qu'elle a préparé avec le roi, et demain elle m'invitera aussi avec le roi.
13 Lakini haya yote sio kitu kama Modekai ataendelea kukaa katika lango la mfalme.
Mais tout cela ne me sert à rien, tant que je vois le Juif Mardochée assis à la porte du roi. »
14 Kisha Zereshi, mkewe Hamani akamwambia Mmewe na rafiki zake wote, “Andaeni mti wenye urefu wa futi hamsini. Na wakati wa ahsubuhi ongea na mfalme ili Modekai atundikwe katika mti huo. Kisha nenda kwa furaha na mfalme katika karamu aliyoiandaa Malkia.
Alors Zéresh, sa femme, et tous ses amis lui dirent: « Qu'on fasse une potence de cinquante coudées de haut, et demain matin, tu parleras au roi pour qu'il y pende Mardochée. Puis tu iras joyeusement avec le roi au banquet. » Cela plut à Haman, et il fit fabriquer la potence.

< Esta 5 >