< Esta 5 >
1 Baada ya siku tatu, Esta akajivika mavazi yake ya kimalkia na akasimama sehemu ya ndani ya ua wa ikulu ya mfalme, mbele ya nyumba ya mfalme. mfalme alikuwa ameketi katika kiti chake cha enzi na akitazama mlango wa kuingilia.
On the third day, Esther put on her regalia and stood in the inner court of the royal palace opposite the king’s house. The king was sitting on his throne in the palace, opposite the entrance.
2 Mfalme alipomwona malkia Esta alipata kibali kwa mfalme. Alimpa fimbo ya dhahabu mikononi mwa Esta. Hivyo Esta akamsogelea mfalme na kuishika fimbo ya utawala.
When he saw Esther the queen standing in the court, she won his favor, and he held out to her the golden sceptre that was in his hand. So Esther approached and touched the top of the sceptre.
3 Kisha mfalme akamwambia Malkia Esta, “Unahitaji upewe nini? Ombi lako ni lipi? Hata nusu ya ufalme wangu utapewa.”
Then the king said to her, “What is it, Queen Esther? Whatever your request is, it will be granted, even if it is the half of the kingdom.”
4 Malkia Esta akamwambia mfalme, kama nimepata kibali machoni pako, naomba wewe na Hamani muhudhurie leo katika karamu niliyoiandaa kwa ajili yake.”
“If it seems best to the king,” Esther said, “let the king and Haman come today to the banquet that I have prepared for him.”
5 Mfalme akasema, “Mleteni haraka Hamani sawa sawa na matakwa ya Malkia Esta.” Mfalme pamoja na Hamani wakahuduria katika karamu aliyoandaa malkia Esta.
Then the king ordered, “Bring Haman quickly, so that Esther’s wish may be gratified.” So the king and Haman went to the banquet that Esther had prepared.
6 Mvinyo ulipohudumiwa katika karamu, mfalme akamuuliza Malkia Esta hitaji lako ni nini? Na ombi lako ni lipi? Utapewa hata nusu ya ufalme.”
While they were drinking wine, the king said to Esther, “Whatever your petition is, it will be granted. Your request, it will be done – even if it takes half of my kingdom.”
7 Esta akajibu mfalme, “Hitaji na ombi langu ni hili,
Esther answered,
8 kama ikikupendeza mfalme, kwa kunipa haja yangu na kuheshimu ombi langu, wewe na Hamani muhudhurie tena katika karamu nitakayoiandaa kesho na hapo ndipo nitakapo kuambia haja yangu.
“If I have won the king’s favor and if it seems best to the king to grant my petition and to accede to my request, my petition and my request are that the king and Haman come to the banquet which I will prepare for them. Tomorrow I will answer the king’s question as he wishes.”
9 Hamani akaenda nyumbani kwakwe huku akiwa amejawa na furaha moyoni mwake. Lakini alipomwona Modekai katika lango la mfalme, modekai hasimami wala kutetemeka mbele zake, alijawa na ghadhabu kwa ajili ya Modekai.
Haman went out that day joyful and elated, but when he saw Mordecai in the king’s gate and noticed that he neither stood up nor moved for him, he was furiously angry with Mordecai.
10 Lakini akajizuia na akaenda nyumbani kwake. Akawaarika marafiki zake wakakusanyika pamoja na Zereshi, mkewe.
Nevertheless Haman restrained himself and went home. He called together his friends and Zeresh his wife
11 Hamani akawaeleza juu ya utukufu wa mali na idadi ya watoto aliokuwa nao, na vile alivyo juu kuliko wasimamizi na watumishi wote wa mfalme.
and recounted to them the greatness of his wealth, how many children he had, and all the ways in which the king had honored him, and how he had promoted him above the officials and the royal courtiers.
12 Hamani akawambia, “Hata jana Malkia Esta aliandaa karamu kwa ajili ya mfalme na ni mimi tu na mfalme tulio hudhuria katika karamu aliyoiandaa Malkia Esta. Na hata kesho tuna mwaliko mwingine pamoja na mfalme.
“What is more,” Haman said, “Queen Esther brought no one in with the king to the banquet which she had prepared except me, and tomorrow also I am invited by her along with the king.
13 Lakini haya yote sio kitu kama Modekai ataendelea kukaa katika lango la mfalme.
Yet all this does not satisfy me as long as I see Mordecai the Jew sitting at the king’s gate.”
14 Kisha Zereshi, mkewe Hamani akamwambia Mmewe na rafiki zake wote, “Andaeni mti wenye urefu wa futi hamsini. Na wakati wa ahsubuhi ongea na mfalme ili Modekai atundikwe katika mti huo. Kisha nenda kwa furaha na mfalme katika karamu aliyoiandaa Malkia.
Then Zeresh his wife and all his friends said to him, “Let a gallows seventy-five feet high be erected, and in the morning speak to the king and let Mordecai be hanged on it. Then go merrily with the king to the banquet.” The advice pleased Haman, and so he had the gallows erected.