< Esta 5 >
1 Baada ya siku tatu, Esta akajivika mavazi yake ya kimalkia na akasimama sehemu ya ndani ya ua wa ikulu ya mfalme, mbele ya nyumba ya mfalme. mfalme alikuwa ameketi katika kiti chake cha enzi na akitazama mlango wa kuingilia.
And on the third day Ester put on her royal apparel, and stood in the court of the Kings palace within, ouer against the Kings house: and the King sate vpon his royal throne in the Kings palace ouer against the gate of the house.
2 Mfalme alipomwona malkia Esta alipata kibali kwa mfalme. Alimpa fimbo ya dhahabu mikononi mwa Esta. Hivyo Esta akamsogelea mfalme na kuishika fimbo ya utawala.
And when the King saw Ester the Queene standing in the court, shee founde fauour in his sight: and the King held out the golden scepter that was in his hand: so Ester drewe neere, and touched the toppe of the scepter.
3 Kisha mfalme akamwambia Malkia Esta, “Unahitaji upewe nini? Ombi lako ni lipi? Hata nusu ya ufalme wangu utapewa.”
Then saide the King vnto her, What wilt thou, Queene Ester? and what is thy request? it shall be euen giuen thee to the halfe of ye kingdome.
4 Malkia Esta akamwambia mfalme, kama nimepata kibali machoni pako, naomba wewe na Hamani muhudhurie leo katika karamu niliyoiandaa kwa ajili yake.”
Then saide Ester, If it please the King, let the King and Haman come this day vnto the banket, that I haue prepared for him.
5 Mfalme akasema, “Mleteni haraka Hamani sawa sawa na matakwa ya Malkia Esta.” Mfalme pamoja na Hamani wakahuduria katika karamu aliyoandaa malkia Esta.
And the King sayd, Cause Haman to make haste that he may doe as Ester hath sayde. So the King and Haman came to the banket that Ester had prepared.
6 Mvinyo ulipohudumiwa katika karamu, mfalme akamuuliza Malkia Esta hitaji lako ni nini? Na ombi lako ni lipi? Utapewa hata nusu ya ufalme.”
And the King sayd vnto Ester at the banket of wine, What is thy petition, that it may be giuen thee? and what is thy request? it shall euen be performed vnto the halfe of the kingdome.
7 Esta akajibu mfalme, “Hitaji na ombi langu ni hili,
Then answered Ester, and sayd, My petition and my request is,
8 kama ikikupendeza mfalme, kwa kunipa haja yangu na kuheshimu ombi langu, wewe na Hamani muhudhurie tena katika karamu nitakayoiandaa kesho na hapo ndipo nitakapo kuambia haja yangu.
If I haue found fauour in the sight of the King, and if it please the King to giue me my petition, and to perfourme my request, let the King and Haman come to the banket that I shall prepare for them, and I will doe to morowe according to the Kings saying.
9 Hamani akaenda nyumbani kwakwe huku akiwa amejawa na furaha moyoni mwake. Lakini alipomwona Modekai katika lango la mfalme, modekai hasimami wala kutetemeka mbele zake, alijawa na ghadhabu kwa ajili ya Modekai.
Then went Haman forth the same day ioyfull and with a glad heart. But when Haman sawe Mordecai in the Kings gate, that he stoode not vp, nor moued for him, then was Haman full of indignation at Mordecai.
10 Lakini akajizuia na akaenda nyumbani kwake. Akawaarika marafiki zake wakakusanyika pamoja na Zereshi, mkewe.
Neuerthelesse Haman refrayned himselfe: and when he came home, he sent, and called for his friends, and Zeresh his wife.
11 Hamani akawaeleza juu ya utukufu wa mali na idadi ya watoto aliokuwa nao, na vile alivyo juu kuliko wasimamizi na watumishi wote wa mfalme.
And Haman tolde them of the glory of his riches, and the multitude of his children, and all the things wherein the King had promoted him, and how that he had set him aboue the princes and seruants of the King.
12 Hamani akawambia, “Hata jana Malkia Esta aliandaa karamu kwa ajili ya mfalme na ni mimi tu na mfalme tulio hudhuria katika karamu aliyoiandaa Malkia Esta. Na hata kesho tuna mwaliko mwingine pamoja na mfalme.
Haman sayde moreouer, Yea, Ester the Queene did let no man come in with the King to the banket that she had prepared, saue me: and to morowe am I bidden vnto her also with the King.
13 Lakini haya yote sio kitu kama Modekai ataendelea kukaa katika lango la mfalme.
But al this doth nothing auaile me, as long as I see Mordecai ye Iewe sitting at ye Kings gate.
14 Kisha Zereshi, mkewe Hamani akamwambia Mmewe na rafiki zake wote, “Andaeni mti wenye urefu wa futi hamsini. Na wakati wa ahsubuhi ongea na mfalme ili Modekai atundikwe katika mti huo. Kisha nenda kwa furaha na mfalme katika karamu aliyoiandaa Malkia.
Then sayde Zeresh his wife and all his friends vnto him, Let them make a tree of fiftie cubites hie, and to morowe speake thou vnto the King, that Mordecai may be hanged thereon: then shalt thou goe ioyfully with the King vnto the banket. And the thing pleased Haman, and he caused to make the tree.