< Esta 4 >

1 Modeka aliposikia kilichokuwa kimepangwa dhidi yao, alirarua mavazi yake na kuvaa maguni na majivu. Akaenda katikati mwa mji na kulia kwa sauti na uchungu mwingi.
When Mordecai found out about those [letters, he was so anguished that] he tore his clothes and put on [rough] sackcloth and [threw] ashes over himself. Then he went into the city, crying very loudly.
2 Akaenda hadi langoni mwa mfalme; kwa sababu hakuna aliye ruhusiwa kuingia akiwa amevaa magunia.
He stood outside the gate of the palace, because no one who was wearing sackcloth was allowed to enter the palace.
3 Amri hii ilipofika katika kila jimbo, kulikuwa na kilio kikubwa kwa Wayahudi, na kufunga, kulia na maombolezo. Wengi wao walilala katika magunia na majivu.
In every province [of the empire], when the letter from the king was read to the Jewish people, they cried and mourned. They (fasted/abstained from eating food), and wailed loudly. Many of them also put on sackcloth and threw ashes on themselves and lay [on the ground].
4 Malkia Esta alipopata habari kutoka kwa wahudumu wake, alipatwa na majonzi. Akatuma watu wampelekee nguo Modekai ili avue magunia na kuvaa nguo nzuri, lakini Modekai hakukubali.
When Esther’s maids and other officials came to her and told her what Mordecai had done, she was very distressed. So she sent to Mordecai [some good] clothes to wear instead of the sackcloth, but he refused to take them.
5 kisha Esta akamwita Hathaki, mmoja wa wasimamizi wa mfalme, ambaye alikuwa amepewa wajibu wa kumuhudumia. Akamwagiza kwenda kwa Modekai ili afahamu kwa nini Modekai ameamua kufanya hivyo.
Then Esther summoned Hathach, one of the king’s officials whom he had appointed to help take care of Esther. She told him to go [out and talk] to Mordecai to find out what was distressing him and why [he was wearing sackcloth to show] that he was grieving.
6 Hivyo Hathaki akaenda kwa Modekai katika mji mbele ya lango la mfalme.
Hathach went to Mordecai, who was in the plaza in front of the palace gate.
7 Modekai akamweleza Hathaki mambo yote kuhusu maangamizi ya Wayahudi yaliyo pangwa na kiasi cha fedha ambacho Hamani ameahidi kuwapa wahazini wa mfalme, ili kuwaua Wayahudi.
Mordecai told him everything that had happened. He told him how much money Haman had promised to give to the government if the king commanded that all the Jews be killed.
8 Na kisha akampa nakala ya mbiu ambayo ilitolewa Shushani kwa uangamivu wa Wayahudi. Alifanya hiivyo ili kwamba Hathaki amwambie Esta achukue jukumu la kwenda na kumuomba mfalme na kumsihi kwa niaba ya Wayahudi.
Mordecai also gave to Hathach a copy of the decree that had been read in Susa, [in which it was stated] that all the Jews must be killed. He told Hathach to show the copy to Esther. He told Hathach to explain to Esther what (it meant/would happen). Then he told him to urge her to go to the king and request the king to act mercifully to her people.
9 Hivyo, Hathaki akaenda na kumweleza Esta kile alicho ambiwa na Modekai.
So Hathach returned to Esther and told her what Mordecai said.
10 Esta akaongea na Hathaki na akamwambia arudi kwa Modekai.
Then Esther told Hathach to [return to] Mordecai [and] tell this [to him]:
11 Esta akamwambia Hathaki, “Watumishi wote wa mfalme na watu wote katika majimbo yote wanafahamu kuwa mtu yeyote aingiae kwa mfalme bila kibali anapaswa kufa isipokuwa yule ambaye mfalme atamunyoshea fimbo yake ya dhahabu. Ni siku thelathini sasa sijaenda mbele ya mfalme.
“There is a law [about people going to talk to the king]. All the king’s officials and all the people in the empire know this law. [In that law it states that] anyone who goes to the king in his inner court without having been summoned by the king must be executed. Only those to whom the king has extended his scepter/staff will not be executed. And a month has passed since the king has summoned me, [so what will happen to me if I try to see him and he doesn’t want to see me?]”
12 Hathaki akamwambia Modekai maneno aliyoambiwa na Esta.
So Hathach [went back to] Mordecai [and] told [him] what Esther had said.
13 Modekai akarudisha ujumbe: “usifikiri kwamba wewe utasalimika kuliko Wayahudi wote.
Mordecai replied, “[Go back and] tell this to Esther: 'Do not think that just because you live there in the palace, you will escape when all the other Jews [are killed].
14 Kama ukikaa kimya kwa wakati huu, Mungu ataleta wokovu kwa njia nyingine, lakini wewe na nyumba ya baba yako mtaangamia. Ni nani ajuaye umekuja katika nafasi hii kwa wakati muafaka kama huu.
If you say nothing now, someone from some other place will rescue [many of] us Jews, but you and your relatives will be killed. Furthermore, (perhaps [God]/who knows if [God]) has put you here [as queen] (for a situation like this/to prevent this from happening to us)!'” [RHQ]
15 Kisha Esta akatuma ujumbe kwa Modekai,
Then [after Hathach told this to] Esther, [she] told him to return to Mordecai and say this to him:
16 “Nenda, uwakusanyea Wayahudi wote wanaoishi katika mji wa Shushani, na wafunge kwa ajili yangu. Wasile wala kunywa kwa muda wa siku tatu. Mimi na watumishi watumishi wangu wa kike tutafunga kwa siku hizo. Na kisha nitaenda mbele ya mfalme kinyume cha sheria. Na kama nitakufa na nife.
“Gather together all the Jews here in Susa, and tell them to (fast/abstain from food) for my sake. Tell them to not eat or drink anything for three days and nights. My maids and I will also fast. Then, I will go to talk to the king. Even if (I am executed/they execute me) for disobeying the law [by seeing him when he does not hold out the scepter/staff toward me, I am willing for that to happen”].
17 Modekai akaenda na akafanya yote ambayo Esta aliyo mwagiza kufanya.
So [after Hathach told this to Mordecai, ] Mordecai went and did what Esther told him to do.

< Esta 4 >