< Esta 2 >

1 Baada ya mambo haya na baada ya hasira ya mfalme Ahusiero kutulia, alifikiri kuhusu Malkia Vashiti na alichokuwa amekifanya na tangazo alilokuwa ameamuru litolewe ya Vashiti kupoteza sifa za kuwa malkia.
After these things, at the ceasing of the fury of King Ahasuerus, he has remembered Vashti, and that which she did, and that which has been decreed concerning her;
2 Kisha vijana waliomtumikia mfalme wakasema, mfalme atafutiwemabikira warembo.
and servants of the king, his ministers, say, “Let them seek for the king young women, virgins, of good appearance,
3 Mfalme na achague wasimamizi katika majimbo yote ya ufalme wake, ili wawakusanye mabikira warembo wote harem katika ikulu ya Susa. Mabikira hawa wawe chini ya usimamizi wa Hegai, msimamizi, ambaye ni mkuu wa wanawake, na wapewe vipodozi vyao vyote.
and the king appoints inspectors in all provinces of his kingdom, and they gather every young woman—virgin, of good appearance—to Shushan the palace, to the house of the women, to the hand of Hegai eunuch of the king, keeper of the women, and to give their purifications,
4 Na binti yule atakaye mfurahisha mfalme ndiye atakaye kuwa Malkia badala ya Vashiti.” Mfalme alupenda ushauri na akafanya kama alivoshauriwa,
and the young woman who is good in the eyes of the king reigns instead of Vashti”; and the thing is good in the eyes of the king, and he does so.
5 Katika mji wa Shushani alikuwepo Myahudi aliyeitwa Modekai mwana wa Jaira mwana wa Shimei mwana wa Kishi, aliye kuwa wa kabila la Benjamini.
A man, a Jew, there has been in Shushan the palace, and his name [is] Mordecai son of Jair, son of Shimei, son of Kish, a Benjamite—
6 Yeye ni miongoni mwa Wayahudi waliochukuliwa pamoja na Yekonia, mfalme wa Yuda kutoka Yerusalemu na kupelekwa uhamishoni na mfalme Nebukadreza.
who had been removed from Jerusalem with the expulsion that was removed with Jeconiah king of Judah, whom Nebuchadnezzar king of Babylon removed—
7 Modekai alikuwa akimlea, Hadasa, yaani Esta, binti wa mjomba wake kwa sababu hakuwa na wazaai wake wote wawili. Modekai alimchukuwa kama binti yake. Esta alikuwa na umbo zuri na uso wa kupendeza.
and he is supporting Hadassah—she [is] Esther—daughter of his uncle, for she has neither father nor mother, and the young woman [is] of beautiful form, and of good appearance, and at the death of her father and her mother Mordecai has taken her to himself for a daughter.
8 Wasichana wengi waliletwa ikulu Shushani, baada ya tangazo na amri ya mfalme kutolewa. Waliwekwa chini ya usimamizi wa Hegai. Esta naye alikuwa ni miongoni mwa wasichana walioletwa na kuwekwa chini ya usimamizi wa Hegai, mwangalizi wa wanawake.
And it comes to pass, in the word of the king, even his law, being heard, and in many young women being gathered to Shushan the palace, to the hand of Hegai, that Esther is taken to the house of the king, to the hand of Hegai, keeper of the women,
9 Esta alimfurahisha, na akapata kibali mbele ya Hegai. Akampa vipodozi na sehemu ya chakula. Akampa wahudumu wa kike saba kutoka katika ikulu ya mfalme, na akampeleka na wahudumu wa kike katika sehemu bora katika nyumba ya wanawake.
and the young woman is good in his eyes, and she receives kindness before him, and he hurries her purifications and her portions—to give to her, and the seven young women who are provided—to give to her, from the house of the king, and he changes her and her young women to a good [place in] the house of the women.
10 Esta hakuwa amemweleza mtu yeyote kuhusu jamaa zake kwa sababu Modekai alikuwa amemzuia.
Esther has not declared her people, and her family, for Mordecai has laid a charge on her that she does not declare [it];
11 kila siku Modekai alienda na kurudi mbele nje ya ua wa nyumba ya wanawake, ili kwamba asikie kuhusu mambo ya Esta na atakachofanyiwa.
and during every day Mordecai is walking up and down before the court of the house of the women to know the welfare of Esther, and what is done with her.
12 Zamu ilipofika ya kila msichana kwenda kwa mfalme Ahusero kwa kufuata maelekezo kwa wanawake, kila msichana alitakiwa kumaliza miezi kumi na miwili ya urembo, miezi sita ya mafuta ya manemane na miezi sita ya vipodozi.
And in the drawing near of the turn of each young woman to come in to King Ahasuerus, at the end of there being to her—according to the law of the women—twelve months, for so they fulfill the days of their purifications; six months with oil of myrrh, and six months with perfumes, and with the purifications of women,
13 wakati msichana alipoenda kwa mfalme, alipewa chochote alichotamani kutoka katika nyumba ya wanawake ili aende nacho katika nyuma ya mfalme.
and with this the young woman has come in to the king, all that she says is given to her to go in with her out of the house of the women to the house of the king;
14 Msichana alipaswa kwenda wakati wa usiku na kurudi katika nyumba ya wanawake, na kwa msimamizi Shaashigazi, msimamizi wa mfalme, ambaye alikuwa mwenye kuwalinda masulia. Msichana hakuruhusiwa kwenda tena kwa mfalme isipokuwa amemfurahiha mfalme na mfalme akaamuru arudi tena.
in the evening she has gone in, and in the morning she has turned back to the second house of the women, to the hand of Shaashgaz eunuch of the king, keeper of the concubines; she does not come in anymore to the king except the king has delighted in her, and she has been called by name.
15 Zamu ya Esta ilipotimia( mwana wa Abihaili, mjomba wa Modekai alikuw amemchukua kama kama binti yake) kwenda mbele ya mfalme, hakutaka kitu chochote isipokuwa vile ambavyo Hegai, msimamizi wa wanawake alimtaka avichukue.
And in the drawing near of the turn of Esther—daughter of Abihail, uncle of Mordecai, whom he had taken to himself for a daughter—to come in to the king, she has not sought a thing except that which Hegai eunuch of the king, keeper of the women, says, and Esther is receiving grace in the eyes of all seeing her.
16 Esta akapata kibali mbele ya kila aliyemwona. Esta akapelekwa kwa Mfalme Ahusiero katika makazi ya kifalme mwezi wa kumi, ambao ni mwezi wa Tabeti, katika mwaka wa saba wa utawala wake.
And Esther is taken to King Ahasuerus, to his royal house, in the tenth month—it [is] the month of Tebeth—in the seventh year of his reign,
17 Mfalme alimpenda Esta zaidi kuliko wanawake wengine, na alipata kibali kuliko na wema mbele zake zaidi kuliko mabikira wengine na hivyo mfalme akamvika taji ya kimalkia badala ya Vashiti.
and the king loves Esther above all the women, and she receives grace and kindness before him above all the virgins, and he sets a royal crown on her head, and causes her to reign instead of Vashti,
18 mfalme akawafanyia karamu kubwa wasimamizi na wahudumu wake wote, karamu ya Esta na akawapa unafuu wa kodi katika majimbo. Pia akawapa zawadi kwa ukarimu.
and the king makes a great banquet to all his heads and his servants—the banquet of Esther—and has made a release to the provinces, and gives gifts as a memorial of the king.
19 Modekai alikuwa ameketi katika lango la mfalme wakati mabikira walipokuwa wamekusanyika kwa mara ya pili.
And in the virgins being gathered a second time, then Mordecai is sitting in the gate of the king;
20 Esta alifuata ushauri Modekai ya kutomwambia mtu yeyote kuhusu jamaa zake. aliendelea kufuata ushauri wa Modekai kama alivyofanya alipokuwa mdogo.
Esther is not declaring her family and her people, as Mordecai has laid a charge on her, and the saying of Mordecai Esther is doing as when she was truly with him.
21 katika siku hizo ambazo Modekai alikuwa ameketi getini kwa mfalme, Bighani na Tereshi, wasimamizi wa mfalme walio linda lando, walikasirika na wakatafuta kumuua mfalme Ahusiero.
In those days, when Mordecai is sitting in the gate of the king, has Bigthan been angry, and Teresh (two of the eunuchs of the king, the keepers of the threshold), and they seek to put forth a hand on King Ahasuerus,
22 Jambo lilipowekwa wazi kwa Modekai, alimtaarifu Malkia Esta na Esta akamweleza kile achoelezwa na Modekai.
and the thing is known to Mordecai, and he declares [it] to Esther the queen, and Esther speaks to the king in the name of Mordecai,
23 Habari hii ilipepelelezwa na kuonekana kuwa kweli na wanaume wawili walinyongwa juu ya mti. Na habari hii ikaandikwa katika kitabu cha taarifa mbele ya mfalme.
and the thing is sought out, and found, and both of them are hanged on a tree, and it is written in the scroll of the Chronicles before the king.

< Esta 2 >