< Waefeso 5 >
1 Kwa hiyo muwe watu wa kumfuata Mungu, kama watoto wake wapendwao.
SED, pues, imitadores de Dios como hijos amados:
2 Mtembee katika pendo, vilevile kama Kristo alivyotupenda sisi, alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu. Yeye alikuwa sadaka na dhabihu, kuwa harufu nzuri ya kumfurahisha Mungu.
Y andad en amor, como tambien Cristo nos amó, y se entregó á sí mismo por nosotros, [como] ofrenda y sacrificio á Dios en olor suave.
3 Zinaa au uchafu wowote na tamaa mbaya lazima visitajwe kati yenu, kama inavyotakiwa kwa waaminio,
Pero fornicacion y toda inmundicia, ó avaricia, ni aun se nombre entre vosotros como conviene á santos:
4 wala machukizo yasitajwe, mazungumzo ya kipumbavu, au mizaha ya udhalilishaji, ambayo siyo sawa, badala yake iwepo shukrani.
Ni palabras torpes, ni necedades, ni truhanerías, que no convienen; sino ántes bien acciones de gracias.
5 Mnaweza kuwa na uhakika ya kwamba kuna zinaa, uchafu, wala atamaniye, huyo nimwabudu sanamu, hana urithi wowote katika ufalme wa Kristo na Mungu.
Porque sabeis esto, que ningun fornicario, ó inmundo, ó avaro, que [tambien] es servidor de ídolos, tiene herencia en el reino de Cristo, y de Dios.
6 Mtu yote asikudanganye kwa maneno matupu, kwa sababu ya mambo haya hasira ya Mungu inakuja juu ya wana wasiotii.
Nadie os engañe con palabras vanas; porque por estas cosas viene la ira de Dios sobre los hijos de desobediencia.
7 Hivyo usishiriki pamoja nao.
No seais pues aparceros con ellos.
8 Kwa kuwa ninyi mwanzo mlikuwa giza, lakini sasa mmekuwa nuru katika Bwana. Hivyo tembeeni kama watoto wa nuru.
Porque en otro tiempo erais tinieblas; mas ahora [sois] luz en el Señor: andad como hijos de luz,
9 Kwa kuwa matunda ya nuru yanajumuisha uzuri wote, haki na ukweli.
(Porque el fruto del Espíritu [es] en toda bondad, y justicia, y verdad; )
10 Tafuta kile kinacho furahisha kwa Bwana.
Aprobando lo que es agradable al Señor.
11 Usiwepo ushiriki katika kazi za giza zisizo na matunda, badala yake ziweke wazi.
Y no comuniqueis con las obras infructuosas de las tinieblas; sino ántes bien redargüidlas.
12 Kwa sababu mambo yanayofanywa na wao sirini ni aibu sana hata kuyaelezea.
Porque torpe cosa es aun hablar de lo que ellos hacen en oculto.
13 Mambo yote, yanapofichuliwa na nuru, huwa wazi,
Mas todas las cosas cuando son redargüidas, son manifestadas por la luz porque lo que manifiesta todo, la luz es.
14 kwa kuwa Kila kitu kilichofichuliwa kinakuwa nuruni. Hivyo husema hivi, “Amka, wewe uliyelala, na inuka kutoka wafu na Kristo atang'aa juu yako.”
Por lo cual dice: Despiértate tú que duermes, y levántate de los muertos, y te alumbrará Cristo.
15 Hivyo iweni makini jinsi mtembeavyo, siyo kama watu wasio werevu bali kama werevu.
Mirad, pues, cómo andeis avisadamente; no como necios, mas como sabios,
16 Ukomboeni muda kwa kuwa siku ni za uovu.
Redimiendo el tiempo, porque los dias son malos.
17 Msiwe wajinga, badala yake, fahamuni nini mapenzi ya Bwana.
Por tanto no seais imprudentes sino entendidos de cual sea la voluntad del Señor.
18 Msilewe kwa mvinyo, huongoza kwenye uharibifu, badala yake mjazwe na Roho Mtakatifu.
Y no os embriagueis de vino, en lo cual hay disolucion; mas sed llenos de Espíritu:
19 Zungumzeni na kila mmoja wenu kwa zaburi, na sifa, na nyimbo za rohoni. Imbeni na sifuni kwa moyo kwa Bwana.
Hablando entre vosotros con salmos, y con himnos, y canciones espirituales, cantando y alabando al Señor en vuestros corazones:
20 Daima toa shukrani kwa mambo yote katika jina la Kristo Yesu Bwana wetu kwa Mungu Baba.
Dando gracias siempre de todo al Dios y Padre en el nombre de nuestro Señor Jesu-Cristo;
21 Jitoeni wenyewe kila mmoja kwa mwingine kwa heshima ya Kristo.
Sujetados los unos á los otros en el temor de Dios.
22 Wake, jitoeni kwa waume zenu, kama kwa Bwana.
Las casadas estén sujetas á sus propios maridos, como al Señor.
23 Kwa sababu mume ni kichwa cha mke, kama Kristo alivyo kichwa cha kanisa. Ni mwokozi wa mwili.
Porque el marido es cabeza de la mujer, así como Cristo es cabeza de la iglesia; y él es el que da la salud al cuerpo.
24 Lakini kama kanisa lilivyo chini ya Kristo, vilevile wake lazima wafanye hivyo kwa waume zao katika kila jambo.
Así que como la iglesia está sujeta á Cristo, así tambien las casadas [lo estén] á sus maridos en todo.
25 Waume, wapendeni wake zenu kama vile Kristo alivyolipenda kanisa na akajitoa mwenyewe kwa ajili yake.
Maridos, amad á vuestras mujeres así como Cristo amó á la iglesia, y se entregó á sí mismo por ella,
26 Alifanya hivyo ili liwe takatifu. Alilitakasa kwa kuliosha na maji katika neno.
Para santificarla limpiándola en el lavacro del agua por la palabra,
27 Alifanya hivi ili kwamba aweze kujiwasilishia mwenyewe kanisa tukufu, pasipo na doa wala waa au kitu kifananacho na haya, badala yake ni takatifu lisilo na kosa.
Para presentársela gloriosa para sí, una iglesia que no tuviese mancha ni arruga, ni cosa semejante; sino que fuese santa y sin mancha.
28 Kwa njia ile ile, waume wanatakiwa kuwapenda wake zao kama miili yao. Yule ampendae mke wake anajipenda mwenyewe.
Así tambien los maridos deben amar á sus mujeres, como á sus [mismos] cuerpos. El que ama á su mujer, á sí mismo ama.
29 Hakuna hata mmoja anayechukia mwili wake. Badala yake, huurutubisha na kuupenda, kama Kristo pia alivyolipenda kanisa.
Porque ninguno aborreció jamás su propia carne; ántes la sustenta y regala, como tambien Cristo á la iglesia.
30 Kwa kuwa sisi ni washiriki wa mwili wake.
Porque somos miembros de su cuerpo, de su carne, y de sus huesos.
31 “Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na ataungana na mke wake, na hao wawili watakuwa mwili mmoja”.
Por esto dejará el hombre á su padre y á su madre, y se allegará á su mujer, y serán dos en una carne.
32 huu ulikuwa umefichika. Lakini ninasema kuhusu Kristo na kanisa.
Este misterio grande es: mas yo digo [esto] con respecto á Cristo y á la iglesia.
33 Walakini, kila mmoja wenu lazima ampende mke wake kama mwenyewe, na mke lazima amheshimu mumewe.
Cada uno empero de vosotros, de por sí, ame tambien á su mujer como á sí mismo; y la mujer reverencie á [su] marido.