< Waefeso 4 >

1 Kwa hiyo, kama mfungwa kwa ajili ya Bwana, nawasihi mtembee sawasawa na wito ambao Mungu aliwaita.
Je vous prie donc, moi qui suis prisonnier pour le Seigneur, de vous conduire d'une manière digne de la vocation à laquelle vous êtes appelés;
2 Muishi kwa unyenyekevu mkuu na upole na uvumilivu. Mkichukuliana katika upendo.
Avec toute humilité et douceur, avec un esprit patient, vous supportant l'un l'autre en charité;
3 Fanyeni bidii kuutunza umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
Etant soigneux de garder l'unité de l'Esprit par le lien de la paix.
4 Kuna mwili mmoja na Roho moja, kama ambavyo pia mlikuwa mmeitwa katika uhakika wa taraja moja la wito wenu.
[Il y a] un seul corps, un seul Esprit, comme aussi vous êtes appelés à une seule espérance de votre vocation.
5 Na kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja,
[Il y a] un seul Seigneur, une seule foi, un seul Baptême;
6 na Mungu mmoja na Baba wa wote. Yeye yuko juu ya yote, na katika yote na ndani ya yote.
Un seul Dieu et Père de tous, qui est sur tous, parmi tous, et en vous tous.
7 Kwa kila mmoja wetu amepewa kipawa kulingana na kipimo cha kipawa cha Kristo.
Mais la grâce est donnée à chacun de nous, selon la mesure du don de Christ.
8 Ni kama maandiko yasemavyo: “Alipopaa juu sana, aliongoza mateka katika utumwa. Akatoa vipawa kwa watu.”
C'est pourquoi il [est] dit: étant monté en haut il a amené captive une grande multitude de captifs, et il a donné des dons aux hommes.
9 Ni nini maana ya, “Alipaa,” isipokuwa kwamba alishuka pia pande za chini za dunia?
Or ce qu'il est monté, qu'est-ce [autre chose] sinon que premièrement il était descendu dans les parties les plus basses de la terre?
10 Yeye ambaye alishuka ni mtu yuleyule ambae pia alipaa mbali juu ya mbingu zote. Alifanya hivi ili uwepo wake uwe katika vitu vyote.
Celui qui est descendu, c'est le même qui est monté au-dessus de tous les Cieux, afin qu'il remplît toutes choses.
11 Kristo alitoa vipawa kama hivi: mitume, manabii, wainjilisti, wachungaji, na waalimu.
Lui-même donc a donné les uns [pour être] Apôtres, les autres [pour être] Prophètes, les autres [pour être] Evangélistes, les autres [pour être] Pasteurs et Docteurs.
12 Alifanya hivi kuwawezesha waumini kwa ajili ya kazi ya huduma, kwa ajili ya kuujenga mwili wa Kristo.
Pour [travailler] à la perfection des Saints, pour l’œuvre du ministère, pour l'édification du corps de Christ.
13 Anafanya hivi hadi sisi sote tufikie umoja wa imani na maarifa ya mwana wa Mungu. Anafanya hivi hadi tuweze kukomaa kama wale waliofikia kimo kamili cha Kristo.
Jusqu'à ce que nous nous rencontrions tous dans l'unité de la foi, et de la connaissance du Fils de Dieu, dans l'état d'un homme parfait, dans la mesure de la parfaite stature de Christ;
14 Hii ni ili kwamba tusiwe tena kama watoto, tusirushwerushwe huku na huko. Ili kwamba tusichukuliwe na kila aina ya upepo wa fundisho, kwa hila za watu katika ujanja wa udanganyifu uliopotoka.
Afin que nous ne soyons plus des enfants flottants, et emportés çà et là à tous vents de doctrine, par la tromperie des hommes, et par leur ruse à séduire artificieusement.
15 Badala yake, tutaongea ukweli katika upendo na kukua zaidi katika njia zote ndani yake ambaye ndiye kichwa, Kristo.
Mais afin que suivant la vérité avec la charité, nous croissions en toutes choses en celui qui est le Chef, [c'est-à-dire], Christ.
16 Kristo ameunganisha, kwa pamoja, mwili wote wa waumini. Umeungamanishwa pamoja na kila kiungo ili kwamba mwili wote ukue na kujijenga wenyewe katika upendo.
Duquel tout le corps bien ajusté et serré ensemble par toutes les jointures du fournissement, prend l'accroissement du corps, selon la vigueur qui est dans la mesure de chaque partie, pour l'édification de soi-même, en charité.
17 Kwa hiyo, nasema hili, na nawasihi katika Bwana: Msitembee tena kama watu wa mataifa wanavyotembea katika ubatili wa akili zao.
Je vous dis donc, et je vous conjure de la part du Seigneur, de ne vous conduire plus comme le reste des Gentils, qui suivent la vanité de leurs pensées;
18 Wametiwa giza katika mawazo yao. Wamefukuzwa kutoka katika uzima wa Mungu kwa ujinga ulio ndani yao kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao.
Ayant leur entendement obscurci de ténèbres, et étant éloignés de la vie de Dieu, à cause de l'ignorance qui est en eux par l'endurcissement de leur cœur.
19 Hawajisikii aibu. Wamejikabidhi wenyewe kwa ufisadi katika matendo machafu, katika kila aina ya uchoyo.
Lesquels ayant perdu tout sentiment, se sont abandonnés à la dissolution, pour commettre toute souillure, à qui en ferait pis.
20 Lakini, hivi sivyo mlivyojifunza kuhusu Kristo.
Mais vous n'avez pas ainsi appris Christ;
21 Nadhani kwamba mmesikia kuhusu yeye. Nadhani kwamba mmekuwa mkifundishwa katika yeye, kama tu ukweli ulivyo ndani ya Yesu.
Si toutefois vous l'avez écouté, et si vous avez été enseignés par lui, selon que la vérité est en Jésus;
22 Lazima mvue mambo yote yanayoendana na mwenendo wenu wa zamani, utu wa zamani. Ni utu wa zamani unaooza kwa sababu ya tamaa za udanganyifu.
[Savoir] que vous dépouilliez le vieil homme, quant à la conversation précédente, lequel se corrompt par les convoitises qui séduisent;
23 Vueni utu wenu wa zamani ili kwamba mfanywe upya katika roho ya akili zenu.
Et que vous soyez renouvelés dans l'esprit de votre entendement.
24 Fanyeni hivi ili muweze kuvaa utu mpya, unaoendana na Mungu. Umeumbwa katika haki na utakatifu wa kweli.
Et que vous soyez revêtus du nouvel homme, créé selon Dieu en justice et en vraie sainteté.
25 Kwa hiyo, weka mbali udanganyifu. “Ongeeni ukweli, kila mmoja na jirani yake,” kwa sababu tu washirika kwa kila mmoja kwa mwenzake.
C'est pourquoi ayant dépouillé le mensonge, parlez en vérité chacun avec son prochain; car nous sommes les membres les uns des autres.
26 Mwe na hasira, lakini msitende dhambi.” Jua lisizame mkiwa katika hasira zenu.
Si vous vous mettez en colère, ne péchez point. Que le soleil ne se couche point sur votre colère.
27 Msimpe Ibilisi nafasi.
Et ne donnez point lieu au Démon [de vous perdre].
28 Yeyote aibaye lazima asiibe tena. Badala yake ni lazima afanye kazi. Afanye kazi yenye manufaa kwa mikono yake, ili kwamba aweze kumhudumia mtu aliye na hitaji.
Que celui qui dérobait, ne dérobe plus; mais que plutôt il travaille en faisant de ses mains ce qui est bon; afin qu'il ait de quoi donner à celui qui en a besoin.
29 Kauli mbaya isitoke kinywani mwenu. Badala yake, maneno lazima yatoke katika vinywa vyenu yafaayo kwa mahitaji, kuwapa faida wale wanaosikiliza.
Qu'aucun discours malhonnête ne sorte de votre bouche, mais [seulement] celui qui est propre à édifier, afin qu'il soit agréable à ceux qui l'écoutent.
30 Na msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu. Ni kwa Yeye kwamba mmewekewa muhuri kwa ajili ya siku ya ukombozi.
Et n'attristez point le Saint-Esprit de Dieu, par lequel vous avez été scellés pour le jour de la Rédemption.
31 Lazima muweke mbali uchungu wote, ghadhabu, hasira, ugomvi, na matusi, pamoja na kila aina ya uovu. Iweni wema ninyi kwa ninyi.
Que toute amertume, colère, irritation, crierie, et médisance, soient ôtées du milieu de vous, avec toute malice.
32 Mwe na huruma. Msameheane ninyi kwa ninyi, kama vile Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.
Mais soyez doux les uns envers les autres, pleins de compassion, et vous pardonnant les uns aux autres, ainsi que Dieu vous a pardonné par Christ.

< Waefeso 4 >