< Waefeso 4 >

1 Kwa hiyo, kama mfungwa kwa ajili ya Bwana, nawasihi mtembee sawasawa na wito ambao Mungu aliwaita.
I therefore, the prisoner in the Lord, beg you to walk worthily of the calling with which you were called,
2 Muishi kwa unyenyekevu mkuu na upole na uvumilivu. Mkichukuliana katika upendo.
with all lowliness and humility, with patience, bearing with one another in love,
3 Fanyeni bidii kuutunza umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
being eager to keep the unity of the Spirit in the bond of peace.
4 Kuna mwili mmoja na Roho moja, kama ambavyo pia mlikuwa mmeitwa katika uhakika wa taraja moja la wito wenu.
There is one body and one Spirit, even as you also were called in one hope of your calling,
5 Na kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja,
one Lord, one faith, one baptism,
6 na Mungu mmoja na Baba wa wote. Yeye yuko juu ya yote, na katika yote na ndani ya yote.
one God and Father of all, who is over all and through all and in us all.
7 Kwa kila mmoja wetu amepewa kipawa kulingana na kipimo cha kipawa cha Kristo.
But to each one of us, the grace was given according to the measure of the gift of Christ.
8 Ni kama maandiko yasemavyo: “Alipopaa juu sana, aliongoza mateka katika utumwa. Akatoa vipawa kwa watu.”
Therefore he says, “When he ascended on high, he led captivity captive, and gave gifts to people.”
9 Ni nini maana ya, “Alipaa,” isipokuwa kwamba alishuka pia pande za chini za dunia?
Now this, “He ascended”, what is it but that he also first descended into the lower parts of the earth?
10 Yeye ambaye alishuka ni mtu yuleyule ambae pia alipaa mbali juu ya mbingu zote. Alifanya hivi ili uwepo wake uwe katika vitu vyote.
He who descended is the one who also ascended far above all the heavens, that he might fill all things.
11 Kristo alitoa vipawa kama hivi: mitume, manabii, wainjilisti, wachungaji, na waalimu.
He gave some to be apostles; and some, prophets; and some, evangelists; and some, shepherds and teachers;
12 Alifanya hivi kuwawezesha waumini kwa ajili ya kazi ya huduma, kwa ajili ya kuujenga mwili wa Kristo.
for the perfecting of the saints, to the work of serving, to the building up of the body of Christ,
13 Anafanya hivi hadi sisi sote tufikie umoja wa imani na maarifa ya mwana wa Mungu. Anafanya hivi hadi tuweze kukomaa kama wale waliofikia kimo kamili cha Kristo.
until we all attain to the unity of the faith and of the knowledge of the Son of God, to a full grown man, to the measure of the stature of the fullness of Christ,
14 Hii ni ili kwamba tusiwe tena kama watoto, tusirushwerushwe huku na huko. Ili kwamba tusichukuliwe na kila aina ya upepo wa fundisho, kwa hila za watu katika ujanja wa udanganyifu uliopotoka.
that we may no longer be children, tossed back and forth and carried about with every wind of doctrine, by the trickery of men, in craftiness, after the wiles of error;
15 Badala yake, tutaongea ukweli katika upendo na kukua zaidi katika njia zote ndani yake ambaye ndiye kichwa, Kristo.
but speaking truth in love, we may grow up in all things into him who is the head, Christ,
16 Kristo ameunganisha, kwa pamoja, mwili wote wa waumini. Umeungamanishwa pamoja na kila kiungo ili kwamba mwili wote ukue na kujijenga wenyewe katika upendo.
from whom all the body, being fitted and knit together through that which every joint supplies, according to the working in measure of each individual part, makes the body increase to the building up of itself in love.
17 Kwa hiyo, nasema hili, na nawasihi katika Bwana: Msitembee tena kama watu wa mataifa wanavyotembea katika ubatili wa akili zao.
This I say therefore, and testify in the Lord, that you no longer walk as the rest of the Gentiles also walk, in the futility of their mind,
18 Wametiwa giza katika mawazo yao. Wamefukuzwa kutoka katika uzima wa Mungu kwa ujinga ulio ndani yao kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao.
being darkened in their understanding, alienated from the life of God because of the ignorance that is in them, because of the hardening of their hearts.
19 Hawajisikii aibu. Wamejikabidhi wenyewe kwa ufisadi katika matendo machafu, katika kila aina ya uchoyo.
They, having become callous, gave themselves up to lust, to work all uncleanness with greediness.
20 Lakini, hivi sivyo mlivyojifunza kuhusu Kristo.
But you did not learn Christ that way,
21 Nadhani kwamba mmesikia kuhusu yeye. Nadhani kwamba mmekuwa mkifundishwa katika yeye, kama tu ukweli ulivyo ndani ya Yesu.
if indeed you heard him and were taught in him, even as truth is in Jesus:
22 Lazima mvue mambo yote yanayoendana na mwenendo wenu wa zamani, utu wa zamani. Ni utu wa zamani unaooza kwa sababu ya tamaa za udanganyifu.
that you put away, as concerning your former way of life, the old man that grows corrupt after the lusts of deceit,
23 Vueni utu wenu wa zamani ili kwamba mfanywe upya katika roho ya akili zenu.
and that you be renewed in the spirit of your mind,
24 Fanyeni hivi ili muweze kuvaa utu mpya, unaoendana na Mungu. Umeumbwa katika haki na utakatifu wa kweli.
and put on the new man, who in the likeness of God has been created in righteousness and holiness of truth.
25 Kwa hiyo, weka mbali udanganyifu. “Ongeeni ukweli, kila mmoja na jirani yake,” kwa sababu tu washirika kwa kila mmoja kwa mwenzake.
Therefore, putting away falsehood, speak truth each one with his neighbor, for we are members of one another.
26 Mwe na hasira, lakini msitende dhambi.” Jua lisizame mkiwa katika hasira zenu.
“Be angry, and do not sin.” Do not let the sun go down on your wrath,
27 Msimpe Ibilisi nafasi.
and do not give place to the devil.
28 Yeyote aibaye lazima asiibe tena. Badala yake ni lazima afanye kazi. Afanye kazi yenye manufaa kwa mikono yake, ili kwamba aweze kumhudumia mtu aliye na hitaji.
Let him who stole steal no more; but rather let him labor, producing with his hands something that is good, that he may have something to give to him who has need.
29 Kauli mbaya isitoke kinywani mwenu. Badala yake, maneno lazima yatoke katika vinywa vyenu yafaayo kwa mahitaji, kuwapa faida wale wanaosikiliza.
Let no corrupt speech proceed out of your mouth, but only what is good for building others up as the need may be, that it may give grace to those who hear.
30 Na msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu. Ni kwa Yeye kwamba mmewekewa muhuri kwa ajili ya siku ya ukombozi.
Do not grieve the Holy Spirit of God, in whom you were sealed for the day of redemption.
31 Lazima muweke mbali uchungu wote, ghadhabu, hasira, ugomvi, na matusi, pamoja na kila aina ya uovu. Iweni wema ninyi kwa ninyi.
Let all bitterness, wrath, anger, outcry, and slander be put away from you, with all malice.
32 Mwe na huruma. Msameheane ninyi kwa ninyi, kama vile Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.
And be kind to one another, tender hearted, forgiving each other, just as God also in Christ forgave you.

< Waefeso 4 >